Kwanini Hospitali ya St. Benedict, Ndanda, Mtwara huuliza wateja dini zao?

Kwanini Hospitali ya St. Benedict, Ndanda, Mtwara huuliza wateja dini zao?

Salaam wanajamvi!

Sitaki kuwapotezea muda kwa kuwa nami sipendi kupoteza muda wangu, najielekeza moja kwa moja kwenye mada lengwa karibuni.

Jana nilienda hospitali ya Rufaa ya Mt. Benedikto (St. Benedict, Ndanda, Mtwara) kwa ajili ya matibabu. Nakiri hii ni katika hospitali bora kabisa kwa huku Kusini mwa Tanzania.

Hata hivyo, katika mchakato wa Usajili nilipata ukakasi baada ya kuulizwa dini yangu. Ilinichukua sekunde takribani 20 kutafakari na kujibu swali kwakuwa sikuona haja na hoja ya msingi kwa mteja kuulizwa swali hilo.

Niliamua kumuhoji mhudumu wa mapokezi kuhusu umuhimu wa kuwatambua wateja kwa dini zao, alijibu kuwa yeye hafahamu chochote kuhusu mantiki ya hilo bali anachofahamu hilo ni hitaji la lazima la usajili na mfumo wa usajili hauendelei kama kitarukwa kipengele cha dini.

Kwakuwa jamii Forums ni chaka la magwiji, majagina na maguru naomba kwa yeyote mwenye ujuzi anijuze iwapo ipo hoja na haja ya Mamlaka ya Hospitali hii ya Wakatoliki kuuliza dini za wateja.

Naomba kuwasilisha.View attachment 3251613
Siyo Ndanda tu ni hospitali zote Ni lazima tujue dini yako. Kuna magonjwa yapo common kwa dini fulani. Mfano wakristo kwasababu wanakula kitimoto wana uwezekano wa kuwa na ugonjwa wa nguruwe tineasisi. Wakati waislam siyo sana. Lakini kuna dini ambazo wao hawaongezwi damu mfano mashahidi wa yehova.

Wakristo kutairi ni optional wakati waislam ni lazima. So kuna magonjwa common kwa dini fulani pia.
 
hawaombi sadaka za magonjwa?? Kila siku sadaka mpya zinaibuka saiv kuna sadaka inaitwa sadaka ya saa100
 
Pumbavu unafikiri kwa kutumia kinyeo chako

Ndanda ukifika hakuna mtu atakayekuambia kuwa umefika kwenye ngome ya wakristo

Hospital ni ya kikristo (japo serikali ina mkono)

Kuna chuo Cha manesi Cha kikristo hata ukiwa muislamu lazima uende kanisani

Kuna chuo Cha masister na ma brother
Duuuuuuuuuuuh😳
 
Kujua zaidi hapo inabidi uende na mshikaji wako, mtaje ugonjwa mmoja, ila dini zenu tofauti, hiyo ni hatua ya kwanza.
 
Back
Top Bottom