Mkuu,ebu nieleweshe kidogo.
-JWTZ haina mahakama na wanasheria?
-Je,unakubaiana na mimi,mwanajeshi awapo kazini,analindwa na sheria za jeshi siyo za kiraia!
-Jeshi lina sero zake au linaombaga hifadhi vituo vya polisi?Anyway,huenda una uelewa,ila nachojua,mahakama ya jeshi inafuata katiba na wakati kesi ikiendelea,raia wanaruhusiwa kufatilia kesi mahakama ya jeshi.
Raia anayetakiwa kuwa na nidhamu namba moja na isiyotiliwa shaka nchini ni askari wa JWTZ kutokana na kubanwa kwake na sheria zote za kiraia na kijeshi mtawalia.
Askari ama ofisa afanyapo kosa kambini hukabiliwa na mashitaka ya kijeshi , kuna summary trial kwa askari wadogo na kuna court martial kwa wote, askari na maofisa wao pamoja na raia kwa ujumla wake.
Summary trial huendeshwa na wakuu wa vikosi kwa makosa madogo madogo kwa askari, lakini Court martial huendeshwa na wanasheria wa kijeshi ambao huitwa mawakili (advocates).
Hawa mawakili hufanya kazi zote za kuendesha mashitaka na kutoa miongozo ya hukumu kwa mujibu wa sheria katika mahakama za kijeshi.
Afisa, askari ama raia anaweza kushitakiwa katika mahakama hii kutokana na kosa atalokabiliwa nalo.
Kuhusu mwanajeshi kuwajibika na sheria za kiraia, ni kwamba: mwanajeshi awapo nje ya kazi za kijeshi, mfano kupiga raia, wizi, ujambazi, mauaji nk nk, atakamatwa na kisha mkuu wa kikosi chake ataarifiwa na kama atatenda kosa uraiani na kukimbilia kambini, basi vyombo vya sheria (civ Police) wataomba kibali cha kumkamata kwa mkuu wake wa kikosi na MPs watumika kumkamata na kumkabidhi kwa Polisi.
Mwenendo wa mashitaka unatakiwa ufuatiliwe na Adjutant wa kikosi na kutoa ripoti kwa mkuu wa Kikosi namna mwenendo wa kesi unavyokwenda mpaka siku ya hukumu.
Kama mshitakiwa atapatikana na hatia atahukumiwa na kutumikia adhabu yake kama mwananchi mwingine yeyote.
Yapo maelezo mengi kuhusujambo hilo, ila haya maelezo mafupi waweza kupata mwanga.
Huwa hakuna sheria wala muhali kumlinda mwanajeshi anayefanya makosa ama uhalifu.
Ndomaana nikasema anatakiwa kuwa mnyenyekevu sana kwa sababu amelengwa na 'mishale' mingi.