Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 20,137
- 26,189
Wanandugu leo katika pita pita zangu nikasema ngoja niangalie boxing records za huyu ndugu yetu Hassan Mwakinyo lakini cha ajabu nikakuta anaitwa Halfan Hythan Hamza, sasa nimeshindwa kuelewa hilo jina la Hassan Mwakinyo amelitolea wapi? Au anatumia cheti cha mtu maana anadai ana miaka 23 lakini ukimuangalia sura inaonesha kabisa yupo kwenye 30+ huko.
Ila kingine ninachomkubali huyu ninja amewachana wale wote wanaojifanya wanamjua jua na kujifanya watu wake wa karibu wakati alipata shida hata namna kusafiri ili akapambane aliwekewa kila aina ya vigingi lakini Mungu akamsaidia akafanikisha safari na akaenda kufanya alichokifuata kule Uingereza.
Miongoni mwa watu waliojifanya wanamjua jua sana Mwakinyo ni pamoja na waziri Mwakyembe ambaye bila aibu anadai kuwa wanafahamiana siku nyingi jambo ambalo sio la kweli bali ni unafiki mtupu.
Hassan atapanda tena ulingoni mwezi october kupambana na Wanik Awdijan raia wa Ujerumani.
Swali linabaki pale pale jina la Hassan Mwakinyo limetoka wapi wakati jina lake ni Halfan Hamza , kama angekuwa na jina la kikristo kidogo isingekuwa kuwa tabu maana tungejua huenda amebadili dini na kuwa muislamu , sasa shida ni kwamba majina yote ni ya kiislamu, ambao mnamjua huyu bondia embu toleeni ufafanuzi kidogo suala hili.View attachment 866189
Ila kingine ninachomkubali huyu ninja amewachana wale wote wanaojifanya wanamjua jua na kujifanya watu wake wa karibu wakati alipata shida hata namna kusafiri ili akapambane aliwekewa kila aina ya vigingi lakini Mungu akamsaidia akafanikisha safari na akaenda kufanya alichokifuata kule Uingereza.
Miongoni mwa watu waliojifanya wanamjua jua sana Mwakinyo ni pamoja na waziri Mwakyembe ambaye bila aibu anadai kuwa wanafahamiana siku nyingi jambo ambalo sio la kweli bali ni unafiki mtupu.
Hassan atapanda tena ulingoni mwezi october kupambana na Wanik Awdijan raia wa Ujerumani.
Swali linabaki pale pale jina la Hassan Mwakinyo limetoka wapi wakati jina lake ni Halfan Hamza , kama angekuwa na jina la kikristo kidogo isingekuwa kuwa tabu maana tungejua huenda amebadili dini na kuwa muislamu , sasa shida ni kwamba majina yote ni ya kiislamu, ambao mnamjua huyu bondia embu toleeni ufafanuzi kidogo suala hili.View attachment 866189