Kwanini huyu bondia Mtanzania aliyeshinda Uingereza anajiita Hassan Mwakinyo?

Kwanini huyu bondia Mtanzania aliyeshinda Uingereza anajiita Hassan Mwakinyo?

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
20,137
Reaction score
26,189
Wanandugu leo katika pita pita zangu nikasema ngoja niangalie boxing records za huyu ndugu yetu Hassan Mwakinyo lakini cha ajabu nikakuta anaitwa Halfan Hythan Hamza, sasa nimeshindwa kuelewa hilo jina la Hassan Mwakinyo amelitolea wapi? Au anatumia cheti cha mtu maana anadai ana miaka 23 lakini ukimuangalia sura inaonesha kabisa yupo kwenye 30+ huko.


Ila kingine ninachomkubali huyu ninja amewachana wale wote wanaojifanya wanamjua jua na kujifanya watu wake wa karibu wakati alipata shida hata namna kusafiri ili akapambane aliwekewa kila aina ya vigingi lakini Mungu akamsaidia akafanikisha safari na akaenda kufanya alichokifuata kule Uingereza.


Miongoni mwa watu waliojifanya wanamjua jua sana Mwakinyo ni pamoja na waziri Mwakyembe ambaye bila aibu anadai kuwa wanafahamiana siku nyingi jambo ambalo sio la kweli bali ni unafiki mtupu.

Hassan atapanda tena ulingoni mwezi october kupambana na Wanik Awdijan raia wa Ujerumani.



Swali linabaki pale pale jina la Hassan Mwakinyo limetoka wapi wakati jina lake ni Halfan Hamza , kama angekuwa na jina la kikristo kidogo isingekuwa kuwa tabu maana tungejua huenda amebadili dini na kuwa muislamu , sasa shida ni kwamba majina yote ni ya kiislamu, ambao mnamjua huyu bondia embu toleeni ufafanuzi kidogo suala hili.View attachment 866189
20180914_165742.jpg
 
Hatumtii nuksi tunataka kujua hilo jina la Halfani Hamza
na Hassan Mwakinyo yanaingiliana vipi?
Baada ya Hapo ...

Maana hicho sio cheti mseme amegushi labda hapana ...

Yule kampa mtu vitasa ... Yaani ngumi tena za maana na nyie mmeona wenyewe kwa Macho yenu kwenye vyombo vya habari ...

Sasa je inawezekana mtu akagushi ngumi?

Jina sisi linatuhusu nini hapa ... afu ukisha lijua then what ... !!!!
 
Back
Top Bottom