Kwanini Ikulu hawapokei simu zinazopigwa kwenye line walizotuwekea?

Kama hawapokei kwanini usiende kabisa mwenyewe pale getini? Ninaamini watakupokea na kukupa huduma nzuri kabisa, amini au usiamini
 
Nchi hii ya kifala sana yaani 1960 mpaka leo watu hawana umeme na maji ya uhakika!!
 
Kuna mdau kashauri nifunge safari hadi getini Ikulu.

Dunia hii ya kidijitali nisafiri toka Kamachumu hadi getini Chamwino kwa tatizo linalomalizwa kwa mtu kuinua tu mkono kupokea simu!

Kwanini huyo anayekaidi kupokea simu za wananchi asiwajibishwe na wakubwa wake kazini?

Nafahamu wanasoma haya tunayoandika, wabadilike.
 
Tuma hiyo no mkuu tuwe nayo wengi , maana mtaani kuna URASIMU na RUSHWA nyingi
 
Wanapewa maelekezo na wazee waliosoma Cuba na Urusi.

Ikulu haipaswi kulalamikiwa kuhusu mawasiliano. Ina maana kuna tatizo la perfomance appraisal ambapo hawaangalii tija bali amri kutoka juu bila kuzingatia agony ya walio chini

Fanya hivi. Ingia kwenye email ya ikulu andika kisha nenda kwenye twitter au insta account ya mama weka link ya huu uzi.
 
we kama unatatizo la msingi sana na unahitaji majibu ya haraka mcheki huyo maza kwenye dm ya ig yake anaweza kujibu japo sio kila mara ila uwezekano wa kupata majibu au suluhu ya jambo lako ni kubwa
 
Watumishi wa Umma wengi Waporipori.
Mimi nimemwandikia barua Rais kupitia email ya Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi tangu mwezi mei mwaka huu,haijajibiwa.Ila wakati wa JPM walikuwa wanajibu.
 
we kama unatatizo la msingi sana na unahitaji majibu ya haraka mcheki huyo maza kwenye dm ya ig yake anaweza kujibu japo sio kila mara ila uwezekano wa kupata majibu au suluhu ya jambo lako ni kubwa
Fafanua kidogo, hiyo dm na ig sijaielewa.
 
 
Ila MCT wanapokea sikuhizi... Ma Chief wako makini sasa
 
Namba za simu na emails kwenye taasisi za bongo ni mapambo tu, hakuna hata moja inayojibiwa. Bongo ukipewa cheo unakua Mungu mtu badala ya kutumikia wananchi.
 
Monica Lewinsky alifanya mazoezi kwa vitendo Ikulu ya Marekani, uliwahi kulisikia hilo?

Post #1 nimeandika kuwa Ikulu ya Marekani wanapokea simu, kwanini hawa wakwetu hawawezi kupokea? Au Ikulu yetu ina unyeti zaidi ya White house!

Hawataki kitokee kitu kinachofanana au kitu chochote kibaya ndani ya nyumba hiyo jinsi ilivyotokea kwa Monica kule White house. 🤣
 


Kama wanashindwa kupokea e mails na cm zilizoko mezani kwao je muda wa "kujisomea" na kutekeleza hiki tunachoandika watatoa wapi??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…