Kwanini injili ya Barnabas iliteketezwa?

Kwanini injili ya Barnabas iliteketezwa?

Mkuu tatizo sio nani kaandika ni bali nini kaandika?

Unaposema alisafiri kwa meli/mashua sehemu ambayo ni nchi kavu tu kama Dar kwenda Morogoro utasema huyo mtu anaongea ukweli?

Mimi nimekufafanulia huo mfano mmoja tu, wewe nenda karudie kapitie hoja zote zaidi ya 8 alizozitoa mdau Che mittoga pale juuu.
Nimekuuliza ukigundua makosa kwenye kitabu kingine katika biblia yako nacho utakikataa? hapo ndipo penye hoja
 
Waislamu huwa ukataa utume wa Paulo kwa kigezo kwamba " Paulo hakuwa miongoni mwa wale wanafunzi 12 wa Yesu ". Kutokuwa moja wa wale thenashara inamfanya Paulo asiwe mtume, na kama si mtume maandiko yake si sahihi kwa maana hakuwa na hiyo mamlaka ya kiutume kuandika hivyo vitabu vikawekwa kwenye Biblia.

Barnaba hakuwa miongoni mwa wanafunzi kumi na mbili, na alikuwa rafiki yake Paulo, kila sehemu alipokwenda Paulo, Baranaba alikuwepo, lakini Waislam kwa akili zao kubwa kupita kiasi wanaona kuwa Barnaba ni mtume na maandishi yake wanapaswa kutumia hadi na Waislamu. Huwa ninajiuliza, kwanini Paulo ambaye hakuwa miongoni mwa thenashara asiwe mtume, na Barnaba ambaye pia hakuwa mmoja wa thenashara ( wanafunzi 12 ) amekuwa mtume hadi anaaandika kitabu kinachopendwa na Waislamu?????. Barnaba ana kitu gani cha ziada????.

Kwa watu wenye akili hawawezi kuamini kile Waislamu wanachokiita "Injili ya Barnaba" kwa sababu Barnaba, mtume Mkristo, hakufundisha vitu vingine vilivyokuwa vinatofautiana na mitume wengine kama akina Paulo, Petro, Yohana n.k. nitatoa ushaudi wa kwamba Barnaba hawezi kufundisha kitu tofauti na Mtume Paulo ( asiyekuwa mtume kwa Waislamu ) ambaye waliongozana kwenda kuhubiri katika miji ya wayunani na pia kubishana na wayahudi wenye imani kali.

1. Paulo alipoongoka kwa mara ya kwanza, alikwenda kanisani Yerusalemu ambapo waumini wote walimkimbia, lakini BARNABA alimchukua akampeleka kwa mitume ( Petro, Yakobo na Yohana )huko huko Yerusalemu. ( Matendo ya Mitume 9:26-27).

2. Kanisa huko Yerusalemu waliposikia ya kwamba mataifa wanaliamini neno la Mungu wakamtuma BARNABA aende Antiokia kuiona hiyo neema, lakini Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Sauli ( Paulo ) akamleta Antiokia, wakakaa wakihubiri na kulifundisha pamoja kwa mwaka mmoja. ( Matendo ya mitume 11:19-26).

3. BARNABA na Paulo walibishana na wayahudi waliokuwa wanataka kuwapotosha wakristo. Mtazamo wa Baranaba na Paulo ulikuwa ni mmoja kuhusu kile walichokuwa wanakiamini ( Matendo ya Mitume 15: 2 ).

4. Paulo analiambia kanisa la Galatia kwamba "Paulo na BARNABA walipokwenda Yerusalemu kwa mitume Petro, Yakobo na Yohana, mitume hawa waliwapa mkono wa kiume wa shirika ili waende kwa mataifa na hao mitume wabaki kwa Wayahudi ( Wagalatia 2:9-10)

5. Baraza la kwanza la mitume wote lilipokaa Yerusalemu, wakapitisha baadhi ya sheria kwa watu wa mataifa, waliwapa Paulo na BARNABA hizo nyaraka wazisambaze kwa makanisa mbalimbali. ( Matendo ya mitume 15:1-35 ).

Kwa mifano hiyo hiyo ni dhahiri kabisa kuwa BARNABA hawezi kuja na injili inayopingana na mafundisho yaliyoko kwenye nyaraka za Paulo, Yakobo, Petro na Yohana. Hiyo Injili ya Barnabas imeandikwa baada ya miaka mingi kupita wakati huo Barnaba alikuwa ameshakufa. Injili ya Barnaba inasadikika kuandikwa mwaka 120 AD, wakati Mtume wa mwisho kufa alikuwa Yohana aliyekufa mwaka 100AD.

Hii injili ya Barnabas iliandikwa na Waislamu wenyewe ili waitumie kupotosha Wakristo wasiojielimisha.
Unaweza kuthibitisha ni muislamu gani aliandika injili ya barnaba? unajua tatizo lenu WAKRISTO mnajaribu kuikosoa injili ya barnaba sio kwa hoja nzito ila tu kwa vile waislamu wanaisoma injili hiyo, kosoa injili ya barnaba kwa hoja bila kuwatupia lawama zako waislamu sawa sawa
 
Injili iliyofichwa sio ya barinaba tu hata ya Yesu mwenyewe aliyo andika kwa mkono wake imefichwa haiwezekani Mungu ampe Yesu injili alafu iandikwe na wengine yeye mwenyewe asiandika
Kuna andiko moja Yesu anasema
TUBUNI NA KUIAMINI INJILI HII hivyo inaonyesha yake aliandika mwenyewe ila imefichwa ili kuwapoteza watu
Hata hii iliandikwa kuna vitu vimeachwa kwa makusudi sasa nashangaa kwanini wanamnyooshea barnaba vidole wakati hata ishara za Yesu waandishi waliamua kuzitupilia mbali wasiziandike, vipi kama barnaba kaandika yale wengine waliamua kutoyaandika?
YOHANA 20:30
" Basi kuna ishara nyingine nyingi, alizozifanya Yesu mbele ya wanafunzi wake ZISIZOANDIKWA katika kitabu hiki";

sasa kama kwenye kitabu hiki azijaandikwa , sasa zimeandikwa wapi? ili swali uenda barnaba amelijibu kwakumiletea yale mliyoyaacha kuyaandika ,sasa badala ya kumshukuru mnaanza kumpopoa
 
Nilibahatika kusoma nakala ya injili hiyo na kwa kiasi kikubwa inakubaliana na mafunzo ya Quran. Huenda ni kwa sababu hiyo ndo ikazuiwa isisomwe ili watu wasijewakaona hakuna kupingana katika mafunzo ya imani mbili hizi.
Wachangiaji wengi wanaipinga kwa kule kushabihiana na QURAN , lakini bado sijaona hoja ya msingi
 
Alikaimisha Mamlaka yake kwaKanisa [emoji117] View attachment 894731 umenielewa?
Kama alikaminisha mamlaka kwa kanisa ebu tuambie Nani alimwambia Yohana ASIANDIKE baadhi ya ishara za Yesu na kwanini?
YOHANA 20:30
";Basi kuna ishara nyingine nyingi, alizozifanya Yesu mbele ya wanafunzi wake ZISIZOANDIKWA katika kitabu hiki";
 
Tofautisha yudas msaliti na Yuda Muinjili [emoji117] View attachment 894775[emoji117] View attachment 894776 Ukristo una Wenyewe sio mnakuwa waongo na kudhania tu [emoji117] View attachment 894783 [emoji53] [emoji12]
Ni kweli kabisa QURAN imeweka wazi dhana ni jambo baya kwa mfano mimi sijui wana wa ZATU walikuwa wangapi kati ya hawa?
EZRA 2:8
" Wana wa ZATU , mia kenda arobaini na watano (945)
NEHEMIA 7:13
" Wana wa ZATU mia nane arobaini na watano"(845)

haya tuambie kwasababu DHANA ni mbaya sasa kati ya EZRA au NEHEMIA nani ametaja idadi sahihi ya wana wa ZATU waliotoka utumwani babiloni kurudi Yerusalem? tutoe hofu tupe jibu sahihi maana nasikia wewe unaongozwa na roho mtakatifu
 
Usianze kutoa malalamiko nimekuuliza , makosa akiandika barnaba ndio unakataa injili yake, vip tukikuonyesha makosa mengine ndani ya biblia utakataa pia kama ulivyoikataa injili ya barnaba? rahisi tu kipi ujanielewa
Nawewe uwe unaelewa.
Chapisho lolote kitaalamu au niite kisomi halikataliwi sababu limeandikwa na nani.
Linakataliwa au kukanushwa sababu ya uhalali au ukweli au ualisia wa kilichoandikwa na/au kukinzana kwa mambo ya kitakwimu, au kijiografia, kifizikia, kihistoria, kikemia au kifalsafa n.k.
Au kutokuwa consistency and conclusive kwa kuzingatia timeline of events.
 
Ni kweli kabisa QURAN imeweka wazi dhana ni jambo baya kwa mfano mimi sijui wana wa ZATU walikuwa wangapi kati ya hawa?
EZRA 2:8
" Wana wa ZATU , mia kenda arobaini na watano (945)
NEHEMIA 7:13
" Wana wa ZATU mia nane arobaini na watano"(845)

haya tuambie kwasababu DHANA ni mbaya sasa kati ya EZRA au NEHEMIA nani ametaja idadi sahihi ya wana wa ZATU waliotoka utumwani babiloni kurudi Yerusalem? tutoe hofu tupe jibu sahihi maana nasikia wewe unaongozwa na roho mtakatifu
Hivi ndivyo unavyopaswa kujenga hoja na kukosoa.
Sio ile unashikilia sababu ya jina la mtu.
 
Nawewe uwe unaelewa.
Chapisho lolote kitaalamu au niite kisomi halikataliwi sababu limeandikwa na nani.
Linakataliwa au kukanushwa sababu ya uhalali au ukweli au ualisia wa kilichoandikwa na/au kukinzana kwa mambo ya kitakwimu, au kijiografia, kifizikia, kihistoria, kikemia au kifalsafa n.k.
Au kutokuwa consistency and conclusive kwa kuzingatia timeline of events.
Ndio hoja yangu hicho unachotumia kuitoa uhalali injili ya barnaba , mbona utumii kuvitoa uhalali vitabu vingine vyenye changamoto hizo ulizo andika hapo mfano KUKINZANA KWA MAMBO YA KITAKWIMU
baada ya wayahudi kuachiwa mateka huko babiloni walirudi Yerusalem sasa takwimu za EZRA kwa wana wa ZATU ni hizo
EZRA 2:8
" Wana wa ZATU , mia kenda arobaini na watano(945)

lakini NEHEMIA yeye takwimu zake kuhusu huyo huyo ZATU zikawa tofauti
NEHEMIA7:13
" Wana wa ZATU, mia nane arobaini na watano(845)
hapo utaona kabisa kuna kosa la KITAKWIMU sasa kwakosa hili maana yake mmoja kati ya hawa ni muongo kabisaa au wote ni waongo lakini hawawezi kuwa wakweli wote
 
[emoji23][emoji23][emoji23] Me napenda maelezo yako huwezi kutoa nusu/mkato siku zote!..
Haaahaaa mkuu We sio mtu mzuri kabisa kuna mtu umemkimbiza Jf intelligence cku hizi hapost wala comment!! 😀😀
 
Nina uzoefu mkubwa wa kujenga hoja , mara zote sijengi hoja bila kuangalia msemaji anasema kitu gani
Wewe mshahara unaitaka Injiri gani ?
Hebu tuweke wazi kwanza naona unatumia nguvu nyingi sana kwenye hii hoja.
Nakuuliza tena, ni Injiri gani unayoipenda na kuiamini ?
 
Wewe mshahara unaitaka Injiri gani ?
Hebu tuweke wazi kwanza naona unatumia nguvu nyingi sana kwenye hii hoja.
Nakuuliza tena, ni Injiri gani unayoipenda na kuiamini ?
Mkuu mbona unakuwa mkali mimi najadili kilichopo mezani, ukubwa wa nguvu ninayotumia labda unijuze umetumia kipimo gani?
 
Samahani mkuu,
hapa katika kitabu cha kutoka Mungu alimwambia Musa aandike andiko gani ?
Kama hajahusika kabisa na kuandika chochote kwenye Agano la Kale ?

Kutoka 34 : 27-28
27 BWANA akamwambia Musa, Andika maneno haya; kwa kuwa mimi nimefanya agano nawe, na pamoja na Israeli, kwa mujibu wa maneno haya.
28 Naye alikuwa huko pamoja na BWANA siku arobaini na masiku yake; hakula chakula, wala hakunywa maji. Naye akaandika katika hizo mbao, hayo maneno ya maagano, hizo amri kumi.
29 Hata ikawa, Musa aliposhuka katika mlima Sinai, na zile mbao mbili za ushuhuda zilikuwa mkononi mwa Musa, hapo aliposhuka katika mlima, Musa hakujua ya kuwa ngozi ya uso wake iling’aa kwa sababu amesema naye.

Mimi kwa uelewa wangu nilifikiri hapo Musa hapo anambiwa na Mungu aandike kitu fulani kwenye Agano la Kale.
Mkuu labda nirudie tena.... Musa hakuandika kitabu cha Mwanzo bali aliandika "makabrasha" na nyaraka kadhaa kama memoir,sheria za torati na amri kumi za Mungu. Ila hakuandika kitabu chochote maana kitabu cha mwanzo hadi Yoshua kwa ushahidi wa kitheolojia na kisayansi unaonyesha kuwa vitabu hivyo viliandikwa miaka 600 kabla ya kristo ilihali musa alikufa zaidi ya miaka 1000 kabla ya kristo.

Kama unafahamu kitabu alichoandika Musa unaweza kutusaidia hapa je ni kipi na alikiandika lini.... Utakuwa umetusaidia sana.
 
Haaahaaa mkuu We sio mtu mzuri kabisa kuna mtu umemkimbiza Jf intelligence cku hizi hapost wala comment!! 😀😀
[emoji23][emoji23] sasa kweli akaogopa kamtu kama Wick. Ila akili za wabongo mada zake basi ndio wanaona big news kuliko hizi wanazotaka zitoke kwenye bible pekee.
 
Mkuu mbona unakuwa mkali mimi najadili kilichopo mezani, ukubwa wa nguvu ninayotumia labda unijuze umetumia kipimo gani?
Hapana mkuu.
Mi nakufuatilia na kuona unavyochangia.
Naona tu unasema Injiri fulani imekosewa.
Ndio maana makuuliza,
Wewe umeisoma Injiri ipi ambayo ipo sahihi ?
Kama hujawahi kuiona injiri sahihi basi sema tu ili tujue mtazamo wako.
Kwakuwa huwezi kuikosoa injiri fulani bila kuijua injiri ya kweli.
Ndio maana nakuambia kuwa wewe kwa hekima yako unaikubali Injiri gani ?
 
Mkuu labda nirudie tena.... Musa hakuandika kitabu cha Mwanzo bali aliandika "makabrasha" na nyaraka kadhaa kama memoir,sheria za torati na amri kumi za Mungu. Ila hakuandika kitabu chochote maana kitabu cha mwanzo hadi Yoshua kwa ushahidi wa kitheolojia na kisayansi unaonyesha kuwa vitabu hivyo viliandikwa miaka 600 kabla ya kristo ilihali musa alikufa zaidi ya miaka 1000 kabla ya kristo.

Kama unafahamu kitabu alichoandika Musa unaweza kutusaidia hapa je ni kipi na alikiandika lini.... Utakuwa umetusaidia sana.
Mkuu.
Katika Kutoka 34, Mungu anamwambia Musa aandike maneno ya Agano lake na Wana wa Israeli.
Nawe unatuambia kuwa Musa aliandika Sheria za Torati na Amri kumi, wakati Torati yenyewe iliandikwa, 600 kabla ya Kristo na Musa alikufa yapata miaka 1000 kabla ya Kristo.
Kwa manano yako Musa alikufa zamani zaidi yaani miaka 1000kk na Torati ikaja kuandikwa baadae miaka 600kk.
Naina jambo hili linafanana tu na walioandika Injiri na nyaraka nyingine za Agano jipya, kwamba wanafunzi na mitume waliandika Injiri ya Yesu Kristo baada ya Yesu mwenyewe kwenda mbinguni.
Huu ukweli unaweza kututhibitishia kuwa Musa alishaandika Agano la Kale ambalo tunaweza kuliita Torati, miaka 600 kabla ya Kristo, kama alivyoagizwa na Mungu katika Kutoka 34, kwa kuwa Sheria za Torati na Amri Kumi alizo andika Musa, ndio Torati yenyewe.
Manabii na Mitume wengine wakaja kuiandika kitaaluma zaidi, kwamba katika kuiandika na kuihifadhi katika vitabu vya kisasa, miaka 400 baadae.
Ndivyo ninavyo elewa kwa mtazamo wangu.
 
Kama alikaminisha mamlaka kwa kanisa ebu tuambie Nani alimwambia Yohana ASIANDIKE baadhi ya ishara za Yesu na kwanini?
YOHANA 20:30
";Basi kuna ishara nyingine nyingi, alizozifanya Yesu mbele ya wanafunzi wake ZISIZOANDIKWA katika kitabu hiki";

hayo yaliyo Andikwa Yanatosha KUAMINI NA KUFUZU [emoji123] [emoji123] [emoji106] [emoji117]
IMG_20181012_071533_818.jpg
 
Back
Top Bottom