Kwanini kijana hutakiwi kutoa mahari kwa karne hii

Kwanini kijana hutakiwi kutoa mahari kwa karne hii

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Nafahamu mada hii ni ngumu, na haitakuwa nzuri sana kwa sababu ya mazoea na desturi za jamii zetu nyingi ambazo kimsingi bado zipo gizani. Lakini hiyo haitazuia kuijadili na hapa tutajadiliana kwa hoja. Wale wenye hisia na mihemko ya kimbuzimbuzi tayari nilishawafikiria hivyo najua nitadili nao vipi.

Elewa kuwa Mahari ni utaratibu wa zamani ambao ulihusisha kumtoa binti kwenda/kuhamia familia au ukoo mwingine. Yaani Mwanamke kumilikiwa na familia au ukoo mwingine. Unapozungumzia umiliki unazungumzia vitu, wazo au wanyama au rasilimali zingine isipokuwa Watu.

Kiasili, kisheria, Kihaki, na kiukweli, na kiakili Mtu HAMILIKIWI. Hakuna sheria popote pale ya kummiliki MTU.

Hata Mungu muumbaji hakumiliki na hana hatimiliki yako wewe kama Mtu. Hii ni kwa sababu ya utu ulio ndani ya mtu mwenyewe. UTASHI ndio kitu kipekee ambacho kinamfanya Mtu asimilikiwe na yeyote yule hata yule aliyemuumba.

Mtu anahaki ya kuchagua chochote atakacho, kumchagua yoyote amtakaye na ikiwezekana kumuacha wakati wowote autakao bila kuzuiwa na yeyote. Mtu amepewa uwezo wa kumchagua au kumkataa hata muumba wake. Hii ni kwa sababu ndani ya mtu kuna Uungu ndani yake, huo Uungu ndio unaitwa UTU.

Zamani, wanawake na baadhi ya makundi ya binadamu hawakuchukuliwa kama Watu. Hata juzijuzi tuu hapa kulikuwa na biashara ya utumwa. Watumwa hawachukuliwi kama Watu na ndio maana huuzwa, na kutumikishwa pasipo haki yoyote ya kujiamulia (UTASHI).

Zamani ili umiliki mwanamke (sio mtu) ni lazima umnunue. Ili awe kwenye ukoo au familia yenu.
Mwanamke kwa vile hakuwa mtu, aliweza kuuzwa hata pasipo kushirikishwa kuwa anauzwa kwa nani bila kujali anampenda mtu huyo au laa. Ulikuwa ni ukatili wa kuogofya. Binti yangu kamwe sitokufanyia jambo hili.

Katika kuuza Mwanamke ambaye baadaye ataitwa mke(kumbe sio kweli isipokuwa mtumwa fulani) kinachofuata ni kumfanya yule mke mtumwa na kijakazi lakini pia Inakuwa kama mashine ya ngono na kuzalisha watoto.

Wanawake hawakuzingatiwa kihisia, kiakili, kiroho wala kimwili. Sio ajabu Mwanamke asipozaa mtoto kwa zama zile ilikuwa Kimbembe. Sio ajabu pia kukuta wanawake wameolewa kimafungu kwa makumi kwa kile kiitwacho ndoa za Mitala.

Hii itategemea na uwezo wa Mwanamke kununua Wanawake kama ng'ombe. Ukiweza kununua wanawake ishirini zamani ungewanunua na kuwaweka sehemu moja na wasifanye kitu kwa sababu hawakuwa Watu bali waliathiriwa na mifumo ya kijinga na kuwageuza kuwa wanyama. Ndio maana walinunuliwa.

Mwanamke hakuweza kurithi chochote kwa sababu alinunuliwa tuu, na anaweza kuuzwa muda wowote. Ilikuwa ni bidhaa. Kwa kweli Taikon ingawaje sieleweki na wengi lakini naandika mambo haya kwa huzuni.

Haya, Mwanamke kwa vile sio mtu na alinunuliwa basi hana haki na watoto aliowabeba yeye mwenyewe katika tumbo lake kwa miezi tisa, kwa taabu. Akizaa inakuwa tena shida kama amezaa mtoto aliyekinyume na matarajio ya mumewe au ukoo alionunuliwa. Mwanamke hakuwa na haki ya watoto na wakati mwingine mpaka jina lake huweza kubadilishwa kwa sababu alinunuliwa, sio Mtu.

Ni kama wazungu walivyokuja Afrika, walibadisha majina ya wale wote waliotaka kuwa na uhusiano nao(wazungu).

Kimsingi mimi kama Mtibeli halisi nilishasema kuwa sitotoa mahari na kamwe sitofanya jambo hilo kwa sababu ninajua ni ujinga, kosa na kinyume na haki, upendo, akili na Ukweli.

Sasa Kwa nini kijana wa sasa hutakiwi kutoa Mahari? Sababu zifuatazo zinahusika;

1. Mwanamke ni mtu kama wewe, huwezi kumnunua/kummiliki
Unaweza ukajidanganya umemnunua lakini kimsingi hujafanya hivyo zaidi ya kuwa umemdhalilisha na atakuzalilisha tuu. Sio ajabu baada ya kumnunua bado atataka kwenda kwao jambo ambalo kwa zamani ukishamnunua Mwanamke hana uwezo wa kufikiri jambo kama hilo.

Huwezi kumnunua/kummiliki kwa sababu siku yoyote akitaka kukuacha atakuacha tuu na hakuna chochote utafanya na huna pakulalamika hata kwa Mungu muumbaji. Kwa sababu hata Mungu mwenyewe hawezi kummiliki/kumnunua mtu.

2. Haki sawa
Wewe na Mwanamke mnahaki sawa kwa sababu nyote ni Watu ila wewe mwanaume kwa upeo wako mdogo au ubinafsi ndio ulitaka kumgeuza mwenzako kama Bidhaa au kifaa fulani hivi. Sio ajabu sikú mkiachana licha ya kuwa ulimnunua (tolea mahari) hautalipwa chochote zaidi ya kugawana mali ikiwezekana na watoto kwenda na mama yao.

Wakati zamani ukitoa Mahari (ukinunua Mwanamke) unammiliki (kwa sababu sio mtu) na hamuwezi kuwa na haki sawa. Hata akizingua hana popote pakwenda na hata akiondoka bado hataondoka na chochote hata watoto aliowazaa na hakuna wa kumsikiliza kwa sababu yeye sio mtu na alinunuliwa. Ni kama ng'ombe tuu.

3. Huna mamlaka naye licha ya kumnunua
Zamani ukimnunua Mwanamke unakuwa na Mamlaka naye na kumuamulia chochote.
Lakini siku hizi kwa vile wanawake wameshajitambua na kuwa Watu, huwezi kuwa na Mamlaka nao ingawaje watakulaghai au utalaghaiwa na familia au jamii kuwa ni mkeo na unamamlaka naye lakini huo ni uongo tuu.

Labda ni kwa sababu siku hizi Mahari au biashara ya kuuza wanawake siku hizi sio kwa jumla jumla bali unakodishiwa tuu.

Elewa kuwa licha ya kuwa utamuoa binti wa Watu kwa kumnunua lakini bado Mamlaka itakuwa juu yake mwenyewe na wazazi wake au ukoo wake. Hivyo hukuwa na sababu ya kumnunua wakati ungeweza kumchukua kwa hiyari ili Muishi maisha ya Hiyari pasipo Unafiki.

4. Mwanamke anahaki ya kuondoka na watoto na usifanye chochote
Zamani jambo hili lisingewezekana kwa sababu tayari ulishamnunua na kumtolea mahari. Nina kesi nyingi za wanaume wanaonipigia simu wakiomba ushauri wa namna ya kuwachukua watoto waliochukuliwa na Mama zao licha ya kuwa walifuata taratibu zote za kimila ikiwemo utaratibu wa kumnunua huyo Mwanamke.

5. Mtoto anahaki ya kumchagua mama yake na kukukataa wewe hata kama ulimnunua mama yake
Zamani hilo lisingewezekana, mtoto hana uwezo wa kumchagua mama yake hata angekua mkubwa kwani mfumo tayari ulikuwa unatambua biashara ya kuuza binadamu ikiwemo kuuza Wanawake.

Yaani unamnunua Mwanamke kwa kile kiitwacho mahari, unamzalisha, unalea watoto kwa nguvu zako alafu mwisho wa siku Mwanamke anaomba talaka, kisha huyo na watoto wanamchagua yeye wewe unabaki huna lolote zaidi ya kulialia kama lijinga na kusema wanawake ni mashetani. Wewe ndio shetani ambaye ulifanyika biashara ya kununua binadamu.

Hutafanya chochote hata uende mahakamani hakuna utakachokipata kwa sababu Mahakama zinatambua Mkeo na watoto wako ni Watu na wana uhuru wa kuchagua. Usije ukaleta upuuzi wako kuwa sijui ulimnunua (ulitoa mahari), sijui uliwalea hiyo haitahesabika chochote.

6. Unaweza kutoa Mahari na ukamfumania mkeo na mwanaume mwingine na mkeo akawa upande wa huyo mwanaume uliyemfumania naye na hutafanya chochote zaidi ya uhalifu kama ulivyomnunua.

Hakunga kesi mahakamani ya kuibiwa Mke. Mke haibiwi kijana. Mke ni mtu anahiyari na uhuru wa kutumia mawazo yake, mwili wake atakavyo na yeyote ilimradi wamepatana.

Kama wewe unavyoweza kuwa na Mwanamke yeyote ndio vivyohivyo.

Sasa wanaume wengi tukiona wake zetu wanatumia uhuru wao katika miili yao roho zinatutoka na hii ni kutokana na ile kasumba mbaya ya kujua tunamiliki wake zetu na zaidi tumewanunua na kugharamika kwa mengi. Acheni uzwazwa vijana. Mtakufa siku sio zenu. Huwezi miliki mtu yeyote dunia hii hata mtoto uliyemzaa huwezi kummiliki. Mbuzi Wewe.

Taikon Master ninakushauri, Usitoe mahari(usimnunue Mwanamke), Kama umempenda Mwanamke au kama wewe ni binti unakijana anakupenda.

Kwa heshima tuu, zungumzeni, wekeni mambo yenu Sawa. Nendeni kwa Wazazi wenu pande Mbili.
Kama wanataka mahari waambieni hatuna mahari ya kutoa au binti sema sitaki kutolewa mahari.

Sio ajabu mtu akishatoa mahari hataki tena ukaribu na Familia ya Mwanamke. Pia familia ya Mwanamke haina uhuru wa kwenda kwa binti yao kusalimia. Huo ni ubinafsi. Lakini kwa upande mwingine ni haki kwa sababu binti yenu nilishamnunua, nilimalizana na nyie kwa nini kunifuatafuata.

Watibeli hatutoa mahari wala binti zetu hawatolewi Mahari. Familia zinaunganishwa kwa upendo na sio biashara za kijinga. Wazazi wa mwanamke ni wazazi wetu na wazazi wa mwanaume ni wazazi wa Wake zetu.

Mama mkwe au baba mkwe wangu anahaki ya kunichukulia kama kijana wake na mimi namchukulia kama mzazi wangu kwa sababu tumeunganishwa na upendo. Sikununua binti yao na wao hawakuniuzia binti yao. Wanahaki ya kunionya kama kijana wao.

Lakini mniuzie binti yenu tena kwa kushusha shusha bei kama nguo za karume. Ati ku-bargain kutoka milioni saba mpaka tatu alafu leo mjifanye kuniita mtoto wenu. Pumbavu labda sio Mimi Mtibeli na wala sio Watibeli. Watibeli hatunaga unafiki.

Au ati umeshachukua mahari ya watu, umemuuza binti yako hivi kuna upendo tena hapo. Ndio ile hata kwenda kumsalimia binti yako mpaka ujiulizeulize, unaona aibu kama jinga fulani.

Sio ajabu ndoa inaonekana ngumu kwa sababu kuna mambo mengi ya kijinga ambayo Watu wanayaona kabisa lakini wanashindwa nini chakufanya wakati uwezo wanao. Waliochukizwa Poleni

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Unanikumbusha kwenye filamu ya Apocalypto, wanawake watumwa waliuzwa, walikaguliwa rangi ya meno na uimara wa matiti.
 
Mwanamke akitembea na wanaume wengi na mwanaume akitembea na wanawake wengi anayetukanwa ni mwanamke huku mwanaume akipewa sifa

Mwanamke na mwanaume wakizaa mtoto kisha wakaachana anayetukanwa ni mwanamke na kuitwa single mother ilihali mwanaume yeye wala haitwi single father

Mwanamke akichelewa kurudi nyumbani ni kosa na anaonekana malaya ila mwanaume akichelewa kurudi nyumbani ni kawaida na hatakiwi kuulizwa

Sasa kwa mitazamo hii iliyoko kwenye jamii kwa wazazi wenye watoto wote wa kiume na wa kike unadhani kwenye suala la malezi watatilia mkazo kwa jinsia gani

Mimi siongei kwa hisia bali uhalisia fuatilia familia nyingi utaona mtoto wa kiume na wa kike hawalelewi kwa usawa ndio maana tunaona tabia mbovu kama hizo kwa wanaume kuliko kwa wanawake
Umenena vema ingawa kwa kuangalia upande mmoja pekee. Jamii ulea watoto wote [me&ke] wawe wema na waweze kumudu majukumu yao hapo ukubwani.

Watoto wa kike kuna masuala yao yanatiliwa mkazo katika malezi na makuzi yao kama ulivo yaanisha hapa. Lakini umesahau kuweka ya wanaume pia.

Angalia ya wanaume sasa. Mimi nimeandaliwa kuwa baba. Nimepatiwa elimu huku nikisisitizwa kutojilinganisha na dada zangu maana mimi ni mtoto wa kiume, familia yangu hapo baadae itaishi kwa kupata mahitaji yote kutoka kwangu. Leo nina uwezo wa kuoa na kuhudumia familia yangu ipasavyo.

SWALI

1. Wazee wangu hawasitahiri kupata zawadi kutoka familia ya binti ili hali wameniandaa vema niweze kumudu kumtunza binti yao?

2. Uoni kwamba, mtoa mada ana hoja nzito?
 
Umenena vema ingawa kwa kuangalia upande mmoja pekee. Jamii ulea watoto wote [me&ke] wawe wema na waweze kumudu majukumu yao hapo ukubwani.

Watoto wa kike kuna masuala yao yanatiliwa mkazo katika malezi na makuzi yao kama ulivo yaanisha hapa. Lakini umesahau kuweka ya wanaume pia.

Angalia ya wanaume sasa. Mimi nimeandaliwa kuwa baba. Nimepatiwa elimu huku nikisisitizwa kutojilinganisha na dada zangu maana mimi ni mtoto wa kiume, familia yangu hapo baadae itaishi kwa kupata mahitaji yote kutoka kwangu. Leo nina uwezo wa kuoa na kuhudumia familia yangu ipasavyo.

SWALI

1. Wazee wangu hawasitahiri kupata zawadi kutoka familia ya binti ili hali wameniandaa vema niweze kumudu kumtunza binti yao?

2. Uoni kwamba, mtoa mada ana hoja nzito?
Well sidhani kama unaweza kufananisha malezi anayopewa mtoto wa kike kulingana na majukumu yake na malezi anayopewa mtoto wa kiume kulingana na majukumu yake, malezi ya mtoto wa kike ni practical kwa maana kwamba anatakiwa aanze kujua kupika, kuosha vyombo, kufua, kusafisha nyumba, tangu akiwa nyumbani, malezi ya mtoto wa kiume ni theoretical yeye ataambiwa tu kwamba atatakiwa afanye kazi au biashara na anachopata ahakikishe anahudumia mkewe na watoto

Ndio maana mtoto wa kike kuolewa hawaangalii kama mwanaume tayari ana pesa na mali au hana, mwanaume hata akiwa masikini akitoa mahari atapewa tu mke wakiamini kwamba mafanikio yatakuja huko huko ndoani maana pesa haziji tu zinatafutwa, lakini wewe uliona wapi mtoto wa kike anaenda kujifunzia kazi za nyumbani akiwa tayari kwenye ndoa kama hajarudishwa kwao siku ya pili tu kwa maana anatakiwa aende kwenye ndoa akiwa tayari anajua hizo kazi

Halafu kingine hiyo ya kusema mahari ni shukurani kwa familia ya mke kwa kumlea binti ni minor reason tu ile major reason yenyewe huwa mnaifumbia macho, sababu kubwa ya kutoa mahari ni kutoa fidia kwa familia ya mke sababu mwanamke anapoolewa familia yake inahesabu imelose while ya mwanaume imegain, kwa maana kwamba mke na watoto wataenda kutumia majina ya upande wa mwanaume sasa kwa kuzingatia hilo mnataka familia ya mwanaume ipewe mahari kwa sababu zipi
 
Father wake kakataa katukatu, kasema kama nimeshindwa nimwachie binti yake pale...

Namimi stress siweezi

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Mtoa mada nakushauri ufwatilie alianzisha ndoa ni nani na utaratibu wa kutoa mahali ulianza ln na kwanini,vinginevyo unazungumzia mada yaliyokuzidi uwezo
 
Hujajibu baadhi ya hoja za mtibeli. Vipi kuhusu:-
1. Mwanamke kubadilishwa jina?
2. Mwanamke kunyang'anywa watoto endapo ndoa itavunjika?
3. Watoto wote kuitwa kwa ukoo wa mwanaume na siyo mwanamke?
4. Mwanamke kutopata mgawo wowote endapo ndoa itavunjika?

Haya yote ni sehemu ya mila za kiafrika. Je, ni sahihi ama potofu?
1. Mwanamke huwa habadili jina ila huwa anabadili ubini wake au jina la ukoo kwasababu anahama ukoo wake na kuingia ukoo mwingine. Kubadili jina ni ishara ya kuhama ukoo wake na kuwa sehemu ya huo ukoo mpya.

2. Si mara zote mwanamke ananyang'anywa watoto. Ila kitendo cha watoto kuchukuliwa itategemea na sababu na sababu zipo nyingi. Inaweza kuwa sio mlezi mzuri wa watoto, watoto huwa wanafuata paternal clan sababu ndio uzao wao na asili yao inapotokea. Sasa sijui hapa unataka ufafanuzi upi zaidi.

3. Watoto kuitwa ukoo wa mwanaume ni ishara ya uongozi. Paternal clan ndio ina mamlaka juu ya watoto sababu ndio ukoo unaotakiwa kutoa malezi ya mbegu yao ya watoto na sio upande wa mama. Tazama koo ambazo watoto hupewa majina ya mama na kulelewa upande wa mama namna zinavyotoa wanaume dhaifu na wanawake majeuri.

4. Hiyo sio tamaduni na mila za africa nzima bali ni baadhi ya makabila na wanazo sababu za kufanya hivyo mojawapo ikiwa mali zinapokuwa mikononi mwa mwanamke akija mwanaume mwingine atazimiliki kama zake na hivyo jasho la mume na urithi wa watoto unaweza potea.

Kuna kisa kimoja za bibi kuwa na ali rithisha ng'ombe zake karibu 3000 kwa binti yake badala ya vijana wake, binti akaanza mahusiano na mwanaume akatapeliwa ng'ombe wote 3000 na huyo mwanaume. Kaka zake walienda kuwagomboa kwa kuwaiba na kurejea nao miaka kadhaa baadae ingawa hawakurejea ng'ombe wote 3000.
 
Mtoa mada nakushauri ufwatilie alianzisha ndoa ni nani na utaratibu wa kutoa mahali ulianza ln na kwanini,vinginevyo unazungumzia mada yaliyokuzidi uwezo

Aliyeanzisha Ndoa NI Nani?
Wahusika wakwanza kuingia kwèñye Ndoa NI kina Nani?
Je walitoa Mahari?
Kama walitoa Mahari, Nani aliyetoa Mahari? Mwanaume au mwanamke? Au huyo aliyeanzisha hiyo Ndoa ndiye aliyetoa Mahari?

Aliyetoa Mahari alimpa Nani?
 
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Nafahamu mada hii ni ngumu, na haitakuwa nzuri sana kwa sababu ya mazoea na desturi za jamii zetu nyingi ambazo kimsingi bado zipo gizani. Lakini hiyo haitazuia kuijadili na hapa tutajadiliana kwa hoja. Wale wenye hisia na mihemko ya kimbuzimbuzi tayari nilishawafikiria hivyo najua nitadili nao vipi.

Elewa kuwa Mahari ni utaratibu wa zamani ambao ulihusisha kumtoa binti kwenda/kuhamia familia au ukoo mwingine. Yaani Mwanamke kumilikiwa na familia au ukoo mwingine. Unapozungumzia umiliki unazungumzia vitu, wazo au wanyama au rasilimali zingine isipokuwa Watu.

Kiasili, kisheria, Kihaki, na kiukweli, na kiakili Mtu HAMILIKIWI. Hakuna sheria popote pale ya kummiliki MTU.

Hata Mungu muumbaji hakumiliki na hana hatimiliki yako wewe kama Mtu. Hii ni kwa sababu ya utu ulio ndani ya mtu mwenyewe. UTASHI ndio kitu kipekee ambacho kinamfanya Mtu asimilikiwe na yeyote yule hata yule aliyemuumba.

Mtu anahaki ya kuchagua chochote atakacho, kumchagua yoyote amtakaye na ikiwezekana kumuacha wakati wowote autakao bila kuzuiwa na yeyote. Mtu amepewa uwezo wa kumchagua au kumkataa hata muumba wake. Hii ni kwa sababu ndani ya mtu kuna Uungu ndani yake, huo Uungu ndio unaitwa UTU.

Zamani, wanawake na baadhi ya makundi ya binadamu hawakuchukuliwa kama Watu. Hata juzijuzi tuu hapa kulikuwa na biashara ya utumwa. Watumwa hawachukuliwi kama Watu na ndio maana huuzwa, na kutumikishwa pasipo haki yoyote ya kujiamulia (UTASHI).

Zamani ili umiliki mwanamke (sio mtu) ni lazima umnunue. Ili awe kwenye ukoo au familia yenu.
Mwanamke kwa vile hakuwa mtu, aliweza kuuzwa hata pasipo kushirikishwa kuwa anauzwa kwa nani bila kujali anampenda mtu huyo au laa. Ulikuwa ni ukatili wa kuogofya. Binti yangu kamwe sitokufanyia jambo hili.

Katika kuuza Mwanamke ambaye baadaye ataitwa mke(kumbe sio kweli isipokuwa mtumwa fulani) kinachofuata ni kumfanya yule mke mtumwa na kijakazi lakini pia Inakuwa kama mashine ya ngono na kuzalisha watoto.

Wanawake hawakuzingatiwa kihisia, kiakili, kiroho wala kimwili. Sio ajabu Mwanamke asipozaa mtoto kwa zama zile ilikuwa Kimbembe. Sio ajabu pia kukuta wanawake wameolewa kimafungu kwa makumi kwa kile kiitwacho ndoa za Mitala.

Hii itategemea na uwezo wa Mwanamke kununua Wanawake kama ng'ombe. Ukiweza kununua wanawake ishirini zamani ungewanunua na kuwaweka sehemu moja na wasifanye kitu kwa sababu hawakuwa Watu bali waliathiriwa na mifumo ya kijinga na kuwageuza kuwa wanyama. Ndio maana walinunuliwa.

Mwanamke hakuweza kurithi chochote kwa sababu alinunuliwa tuu, na anaweza kuuzwa muda wowote. Ilikuwa ni bidhaa. Kwa kweli Taikon ingawaje sieleweki na wengi lakini naandika mambo haya kwa huzuni.

Haya, Mwanamke kwa vile sio mtu na alinunuliwa basi hana haki na watoto aliowabeba yeye mwenyewe katika tumbo lake kwa miezi tisa, kwa taabu. Akizaa inakuwa tena shida kama amezaa mtoto aliyekinyume na matarajio ya mumewe au ukoo alionunuliwa. Mwanamke hakuwa na haki ya watoto na wakati mwingine mpaka jina lake huweza kubadilishwa kwa sababu alinunuliwa, sio Mtu.

Ni kama wazungu walivyokuja Afrika, walibadisha majina ya wale wote waliotaka kuwa na uhusiano nao(wazungu).

Kimsingi mimi kama Mtibeli halisi nilishasema kuwa sitotoa mahari na kamwe sitofanya jambo hilo kwa sababu ninajua ni ujinga, kosa na kinyume na haki, upendo, akili na Ukweli.

Sasa Kwa nini kijana wa sasa hutakiwi kutoa Mahari? Sababu zifuatazo zinahusika;

1. Mwanamke ni mtu kama wewe, huwezi kumnunua/kummiliki
Unaweza ukajidanganya umemnunua lakini kimsingi hujafanya hivyo zaidi ya kuwa umemdhalilisha na atakuzalilisha tuu. Sio ajabu baada ya kumnunua bado atataka kwenda kwao jambo ambalo kwa zamani ukishamnunua Mwanamke hana uwezo wa kufikiri jambo kama hilo.

Huwezi kumnunua/kummiliki kwa sababu siku yoyote akitaka kukuacha atakuacha tuu na hakuna chochote utafanya na huna pakulalamika hata kwa Mungu muumbaji. Kwa sababu hata Mungu mwenyewe hawezi kummiliki/kumnunua mtu.

2. Haki sawa
Wewe na Mwanamke mnahaki sawa kwa sababu nyote ni Watu ila wewe mwanaume kwa upeo wako mdogo au ubinafsi ndio ulitaka kumgeuza mwenzako kama Bidhaa au kifaa fulani hivi. Sio ajabu sikú mkiachana licha ya kuwa ulimnunua (tolea mahari) hautalipwa chochote zaidi ya kugawana mali ikiwezekana na watoto kwenda na mama yao.

Wakati zamani ukitoa Mahari (ukinunua Mwanamke) unammiliki (kwa sababu sio mtu) na hamuwezi kuwa na haki sawa. Hata akizingua hana popote pakwenda na hata akiondoka bado hataondoka na chochote hata watoto aliowazaa na hakuna wa kumsikiliza kwa sababu yeye sio mtu na alinunuliwa. Ni kama ng'ombe tuu.

3. Huna mamlaka naye licha ya kumnunua
Zamani ukimnunua Mwanamke unakuwa na Mamlaka naye na kumuamulia chochote.
Lakini siku hizi kwa vile wanawake wameshajitambua na kuwa Watu, huwezi kuwa na Mamlaka nao ingawaje watakulaghai au utalaghaiwa na familia au jamii kuwa ni mkeo na unamamlaka naye lakini huo ni uongo tuu.

Labda ni kwa sababu siku hizi Mahari au biashara ya kuuza wanawake siku hizi sio kwa jumla jumla bali unakodishiwa tuu.

Elewa kuwa licha ya kuwa utamuoa binti wa Watu kwa kumnunua lakini bado Mamlaka itakuwa juu yake mwenyewe na wazazi wake au ukoo wake. Hivyo hukuwa na sababu ya kumnunua wakati ungeweza kumchukua kwa hiyari ili Muishi maisha ya Hiyari pasipo Unafiki.

4. Mwanamke anahaki ya kuondoka na watoto na usifanye chochote
Zamani jambo hili lisingewezekana kwa sababu tayari ulishamnunua na kumtolea mahari. Nina kesi nyingi za wanaume wanaonipigia simu wakiomba ushauri wa namna ya kuwachukua watoto waliochukuliwa na Mama zao licha ya kuwa walifuata taratibu zote za kimila ikiwemo utaratibu wa kumnunua huyo Mwanamke.

5. Mtoto anahaki ya kumchagua mama yake na kukukataa wewe hata kama ulimnunua mama yake
Zamani hilo lisingewezekana, mtoto hana uwezo wa kumchagua mama yake hata angekua mkubwa kwani mfumo tayari ulikuwa unatambua biashara ya kuuza binadamu ikiwemo kuuza Wanawake.

Yaani unamnunua Mwanamke kwa kile kiitwacho mahari, unamzalisha, unalea watoto kwa nguvu zako alafu mwisho wa siku Mwanamke anaomba talaka, kisha huyo na watoto wanamchagua yeye wewe unabaki huna lolote zaidi ya kulialia kama lijinga na kusema wanawake ni mashetani. Wewe ndio shetani ambaye ulifanyika biashara ya kununua binadamu.

Hutafanya chochote hata uende mahakamani hakuna utakachokipata kwa sababu Mahakama zinatambua Mkeo na watoto wako ni Watu na wana uhuru wa kuchagua. Usije ukaleta upuuzi wako kuwa sijui ulimnunua (ulitoa mahari), sijui uliwalea hiyo haitahesabika chochote.

6. Unaweza kutoa Mahari na ukamfumania mkeo na mwanaume mwingine na mkeo akawa upande wa huyo mwanaume uliyemfumania naye na hutafanya chochote zaidi ya uhalifu kama ulivyomnunua.

Hakunga kesi mahakamani ya kuibiwa Mke. Mke haibiwi kijana. Mke ni mtu anahiyari na uhuru wa kutumia mawazo yake, mwili wake atakavyo na yeyote ilimradi wamepatana.

Kama wewe unavyoweza kuwa na Mwanamke yeyote ndio vivyohivyo.

Sasa wanaume wengi tukiona wake zetu wanatumia uhuru wao katika miili yao roho zinatutoka na hii ni kutokana na ile kasumba mbaya ya kujua tunamiliki wake zetu na zaidi tumewanunua na kugharamika kwa mengi. Acheni uzwazwa vijana. Mtakufa siku sio zenu. Huwezi miliki mtu yeyote dunia hii hata mtoto uliyemzaa huwezi kummiliki. Mbuzi Wewe.

Taikon Master ninakushauri, Usitoe mahari(usimnunue Mwanamke), Kama umempenda Mwanamke au kama wewe ni binti unakijana anakupenda.

Kwa heshima tuu, zungumzeni, wekeni mambo yenu Sawa. Nendeni kwa Wazazi wenu pande Mbili.
Kama wanataka mahari waambieni hatuna mahari ya kutoa au binti sema sitaki kutolewa mahari.

Sio ajabu mtu akishatoa mahari hataki tena ukaribu na Familia ya Mwanamke. Pia familia ya Mwanamke haina uhuru wa kwenda kwa binti yao kusalimia. Huo ni ubinafsi. Lakini kwa upande mwingine ni haki kwa sababu binti yenu nilishamnunua, nilimalizana na nyie kwa nini kunifuatafuata.

Watibeli hatutoa mahari wala binti zetu hawatolewi Mahari. Familia zinaunganishwa kwa upendo na sio biashara za kijinga. Wazazi wa mwanamke ni wazazi wetu na wazazi wa mwanaume ni wazazi wa Wake zetu.

Mama mkwe au baba mkwe wangu anahaki ya kunichukulia kama kijana wake na mimi namchukulia kama mzazi wangu kwa sababu tumeunganishwa na upendo. Sikununua binti yao na wao hawakuniuzia binti yao. Wanahaki ya kunionya kama kijana wao.

Lakini mniuzie binti yenu tena kwa kushusha shusha bei kama nguo za karume. Ati ku-bargain kutoka milioni saba mpaka tatu alafu leo mjifanye kuniita mtoto wenu. Pumbavu labda sio Mimi Mtibeli na wala sio Watibeli. Watibeli hatunaga unafiki.

Au ati umeshachukua mahari ya watu, umemuuza binti yako hivi kuna upendo tena hapo. Ndio ile hata kwenda kumsalimia binti yako mpaka ujiulizeulize, unaona aibu kama jinga fulani.

Sio ajabu ndoa inaonekana ngumu kwa sababu kuna mambo mengi ya kijinga ambayo Watu wanayaona kabisa lakini wanashindwa nini chakufanya wakati uwezo wanao. Waliochukizwa Poleni

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Una mawazo ya ajabu sana. Na pia hio ni mtazamo wako kuhusu mahari,
 
Back
Top Bottom