Kwanini kodi ikatwe mara mbili kwa kipato hicho hicho kimoja?

Kwanini kodi ikatwe mara mbili kwa kipato hicho hicho kimoja?

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Sio kwamba hatutaki kutozwa kodi.
Swali la msingi la kujiuliza ni kwanini makato yawe zaidi ya mara moja kwa kipato kimoja?

Mshahara unakatwa kodi (PAYE), bank husika wanakata service charge. Wakati wa kutoa unakatwa salio la kutolea. Na bado serikali ikate tena tozo. Huu ni uonevu.

Tumevumilia kwenye tozo za miamala ya simu, ila hili la bank HAPANA!
NI UONEVU! Hata kama kiasi ni kidogo ila kwanini kitozwe zaidi ya mara moja?

Kama nchi inapitia wakati mgumu, kwanini wasiuze magari ya serikali na kupunguza ziara na misafara isiyo na ulazima? Mbona hatuoni jitihada za makusudi za kubana matumizi ya serikali kwa kuondoa vikao na mikutano ya ana kwa ana na kufanya kwa njia isiyo ya ana kwa ana (zoom, video conference) ili kubana matumizi?

Ina maana njia pekee ya kukusanya mapato ni kupitia tozo?

Ni nani amewaambia kuwa wananchi wana fedha nyingi? Ilihali mfumuko wa bei uko juu! Gharama za maisha ziko juu. Wananchi wanalalamika kila iitwapo leo.

Tozo na kodi mara mbili kwa kipato hichohicho kimoja, ni uonevu!
 
IMG_5344.jpg
 
Wakate hata Mara 1000 Watanzania hamlipe Kodi hasa nyie mnao jiona wanyonge.Nchi haiwezi piga hatua ya maendeleo pasipo kulipa Kodi au kama una njia tofauti ya kuishauri serikali kuleta maendeleo pasi kulipa Kodi iseme?
 
Ifike muda Watanzania tuamke.
Nani alituroga sisi?
Tulitakiwa kuuwasha moto mkali Nchi nzima japo kwa siku moja tu.
Kwa upole huu tulionao, sidhani kama tutafika popote.
Lakini saa inakuja ambapo Watanzania wote kwa umoja wetu tutaimba wimbo mmoja bila kujali tofauti zetu za Dini, Rangi, Kabila, Kanda, Jinsi, Rika, Hali na hata Vyama vyetu.
Huo ndio utakaokuwa mwanzo wa ukombozi wa Nchi hii teule.
 
Wanajua kama sisi ni mang'ombe, tutapiga kelele mitandaoni kisha tutakaa kimya, maisha yataemdelea.
 
Makofia matisheti wali wa siku moja elfu tano tano...kupakiwa bure kwenye malori kunyweshwa mapipa ya mapuya bure.....Nabado mpaka vumbi litimke kwenye meno....
 
Back
Top Bottom