Kwanini kujenga nyumba imekuwa ni fashion kwa Watanzania?

Kwanini kujenga nyumba imekuwa ni fashion kwa Watanzania?

Hujamuelewa mleta uzi hatakataa kujenga ila jenga ukiwa ushazungusha hela yako mara kadhaa yaani kama una biashara tayari ushazungusha faida hata mara kumi ndo uanze kujenga ili kukuza mtaji.
Kichwa cha habari cha huu uzi kinajieleza. Kama kujenga nyumba ni fasheni basi ni fasheni nzuri sana.
 
Hata kama unafanya biashara kumiliki ardhi na kujenga ni muhimu sana. Wajanja wote kwenye biashara wako mstari wa mbele kumiliki ardhi na kujenga.
Kumiliki ardhi ni jambo la msingi ila kuanza kujenga ni risk Sana itakayokufanya usiishi maisha bora na usifikie kufikia ndoto zako kwa wakati Mimi ni kijana chini ya miaka 30 nimfanyabiahara ninamiliki ardhi na nimeona umuhimu wakumiliki ardhi lakini kujenga ni risk Sana pale ambapo hauna msingi wa kujenga nashauri Sana kwanini usianze kujenga vyumba kazaa
 
Hufikirii gharama anazokwepa za kuama na kodi zitatumika kuongeza mapato?
 
Wabongo wanapenda sana kujenga, kwao kujenga ndo mafanikio...kuna ndugu yangu majuzi ananishauri nijenge hata chumba na sebule, nikajisemea huyu mzima kweli ..sina kitega uchumi chochote cha maana naanzaje kujenga?
Majuzi zaidi ya 20m nimewekeza kwenye buashara ila ndo hivyo hata kiwanja sina [emoji3].

Sent from my CPH2219 using JamiiForums mobile app
Jambo jema Ila ungefanya mpango wa kumiliki ardhi tu ardhi inapanda thamani kila miaka kazaa

Mtu akiona ana mtaji wa huo anaona kashatoboa kumbe mtaji mdogo ambao hautakiwi kufanya shughuli nyingine mtu ana kata mill 7 anaanza kuporomosha jengo mwisho biashara huwa haidanganyi bidhaa dukani zinaanza kuadimika wateja wanakukimbia na ndio inakuwa mwanzo wa biashara yako kufa ndio chanzo cha kuwa masikini huku umejenga
 
Sasa unataka tusijenge tuishi kama manyani kwenye miti? Unajua kero za Kodi wewe? Hivi ukitokea msiba na wewe mpangaji umefiwa utakaa wapi? Masuala mengine sio ya kuyaandika mbele za watu dogo.
Kwani hao ambao sasa hivi wanapanga hawapati misiba? Ulipopanga ndio kwako kwa kipindi uluchopanga iwe msiba au sherehe unafanyia hapo hapo.
 
Imekuwa ni jambo la kushangaza kwa watanzania wengi kuamua kujenga na kuendelea kuishi maisha yale yale

Unakutana fundi fenicha aliyefanya kazi miaka 15 anakuambia anamalizia ujenzi ukiangalia ufanyaji kazi bado wa kusubiri hela advance kwa mteja hafikirii kabisa kuwa na store kubwa utakayotoa faida kubwa zaidi kwa haraka zaidi kutokana na uzoefu wake.

Unakutana na dereva yeye miaka na miaka anaendesha gari za watu anakuja na habari njema amejenga ni vyema lakini kwanini asikilie kumiliki gari yake.

Unakutana na kijana kinyozi ana uzoefu wa miaka saba anakuambia nimejenga vyumba vitatu nataka nihamie kwangu ni jambo jema lakini hafikirii kama pesa hizo kama angetumia kufungua barbershop kubwa ambayo ingempa faida maradufu
Bro unaishi TZ hii hiii?
Kuna mfalme mmoja alipewa taarifa kwamba wananchi wanaandamana,hawana chakula,mikate ya kula,mfalme akashangaa akawaambie wasaidizi wake kama hawana mikate,wapeni keki!!!
Huyu alikua juha kweli kweli,watu walikuwa hawana mikate,maisha ni magumu,mfslme akafikiri watu wameichoka mikate hakujua hali halisi ya maisha ya ufukara ya watu.
 
Watu wengi wamempinga mleta maada sababu hawakutaka kushughurisha akili zao. Kiukweli kujenga nyumba while bado huna sehemu ya kukuingizia kipato, mfano biashara ni uoga wa maisha. Hili nilikuja kulielewa tayari nimeshachelewa acha tuishi humo humo. Ila kumbuka nyumba ya kuishi si Assets Otherwise ujenge upangishe
 
Imekuwa ni jambo la kushangaza kwa watanzania wengi kuamua kujenga na kuendelea kuishi maisha yale yale

Unakutana fundi fenicha aliyefanya kazi miaka 15 anakuambia anamalizia ujenzi ukiangalia ufanyaji kazi bado wa kusubiri hela advance kwa mteja hafikirii kabisa kuwa na store kubwa utakayotoa faida kubwa zaidi kwa haraka zaidi kutokana na uzoefu wake.

Unakutana na dereva yeye miaka na miaka anaendesha gari za watu anakuja na habari njema amejenga ni vyema lakini kwanini asikilie kumiliki gari yake.

Unakutana na kijana kinyozi ana uzoefu wa miaka saba anakuambia nimejenga vyumba vitatu nataka nihamie kwangu ni jambo jema lakini hafikirii kama pesa hizo kama angetumia kufungua barbershop kubwa ambayo ingempa faida maradufu
Risk ya biashara hapa kwetu ni kubwa kuliko kujenga nyumba..

biashara hazitabiriki hapa nchini so bora ujenge tu ujue pesa umeizika..
 
Watu wengi wamempinga mleta maada sababu hawakutaka kushughurisha akili zao. Kiukweli kujenga nyumba while bado huna sehemu ya kukuingizia kipato, mfano biashara ni uoga wa maisha. Hili nilikuja kulielewa tayari nimeshachelewa acha tuishi humo humo. Ila kumbuka nyumba ya kuishi si Assets Otherwise ujenge upangishe
Akili za kushindwa hizi.



Sent from my 2201117SG using JamiiForums mobile app
 
Imekuwa ni jambo la kushangaza kwa watanzania wengi kuamua kujenga na kuendelea kuishi maisha yale yale

Unakutana fundi fenicha aliyefanya kazi miaka 15 anakuambia anamalizia ujenzi ukiangalia ufanyaji kazi bado wa kusubiri hela advance kwa mteja hafikirii kabisa kuwa na store kubwa utakayotoa faida kubwa zaidi kwa haraka zaidi kutokana na uzoefu wake.

Unakutana na dereva yeye miaka na miaka anaendesha gari za watu anakuja na habari njema amejenga ni vyema lakini kwanini asikilie kumiliki gari yake.

Unakutana na kijana kinyozi ana uzoefu wa miaka saba anakuambia nimejenga vyumba vitatu nataka nihamie kwangu ni jambo jema lakini hafikirii kama pesa hizo kama angetumia kufungua barbershop kubwa ambayo ingempa faida maradufu

Na wanao panga nyumba kwann wasifikirie kumiliki nyumba zao?

Au ni sawa dereva amiliki gari yake na kinyozi salon yake lakini wapangaji wasimiliki nyumba zao?
 
Kama ulishawahi kukaa nyumba za kupanga,ukakutana na adha za wenye nyumba, lazima ukipata vihela uvikimbize kwenye ujenzi wa nyumba ya kuishi...
 
Back
Top Bottom