Kwanini mafunzo ya mgambo yasiwe "compulsory" kwa wanafunzi wote waliohitimu kidato cha sita ambao hawakubahatika kuchaguliwa kujiunga na mafunzo JKT?

Kwanini mafunzo ya mgambo yasiwe "compulsory" kwa wanafunzi wote waliohitimu kidato cha sita ambao hawakubahatika kuchaguliwa kujiunga na mafunzo JKT?

We jamaa una maisha ya kimasikini sana.

Yani badala ya kuhamasisha vijana wajifunze hata ku-code au wajifunze soft skills za kuwafanya wa-cope na utandawazi unaleta hadithi za kufagia uwanja.

Dunia ya sasa haihitaji migambo wala wafagia uwanja. Inahitaji watu smart vichwani.
 
Umemaliza kila kitu mkuu,kila mwenye akili kubwa hapa atakuwa amekuelewa.
Mkuu wazo lako zuri ila Kwa dunia ya sasa tunaitaji vijana wenye technical skills ili waweze kujiajiri na kuzalisha sio ukakamavu tena dunia unaenda mbio saizi hakuna kulima na jembe la ng'ombe au kusukuma mizigo kuna Conveyor belt .

Ilo Jambo la ukakamavu lirudishwe shule za msingi na sekondari Kwa kuweka program za michezo walau mara 2 Kwa wiki na mazoezi ya viungo kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma kulikuwa na mbio za mchakamchaka,Umiseta na Umitashunta.

Sasa tupo kwenye zama za science na technology serikali inabidi ikubali vijana wanaohitimu au walio mitaani wapate technical skills ili waweze kukitegemea na kujiajiri. Mfano huo muda wa kukimbia mgambo kisha urudi kitaa ni bora watu wakusanywe wilayani kisha waitwe wauzaji wa Maroli ya kichina ya Faw,Howo,Beiben,Dayun,Foton na Shacman Kwa muda wa mwezi watoe training kwa watu wanaojifunza ufundi upepo,brake system, umeme, mechanical na rangi hapo kila kijana akitoka anatoka na skills ambayo itamsaidia vivyo hivyo kwenye simu,pikipiki na boti.
 
Kumpeleka mtoto JKT ni kumwandaa kuwa fukara maisha yake yote ,kwasababu

1.Hatakuwa na akili za ubunifu tena zaidi ya kusubiri command tu
2.Unaanda watu ambao hawana mawazo mbadala zaidi ya kutumia nguvu tuu
3.Litakuwa liCcm la kudumu

Hio number 3 umeweka kwa kusisitiza litakuwa liCcm la kudumu 🤣🤣🤣
 
Israel bado inathamini mafunzo ya ukakamavu sio kwa ajili ya kuwafanya vijana waweze kujitegema ni kwa sababu ya vita zake na majirani zake wakati ikiwa na raia wachache hivyo inahitaji jeshi la akiba la uhakika kwa muda wote.
Ndio maana baada ya kutoka mafunzo ya ukakamavu sasa wanaenda chuoni kupata mafunzo hayo ambayo wewe unayaita kuwa ni "technical skills"

Hata nchi zilizoendelea kama Israel bado wanathamini sana mafunzo ya ukakamavu wa mwili na akili kwa vijana wao...
 
Nchi nyingine yenye mambo kama hayo ni Eritrea,Korea ya Kaskazini na Kusini ila nchi nyingi zilizoendelea hazina hayo mambo.
Ndio maana baada ya kutoka mafunzo ya ukakamavu sasa wanaenda chuoni kupata mafunzo hayo ambayo wewe unayaita kuwa ni "technical skills"

Hata nchi zilizoendelea kama Israel bado wanathamini sana mafunzo ya ukakamavu wa mwili na akili kwa vijana wao...
 
Hili wazo lake la kijima sana
We jamaa una maisha ya kimasikini sana.

Yani badala ya kuhamasisha vijana wajifunze hata ku-code au wajifunze soft skills za kuwafanya wa-cope na utandawazi unaleta hadithi za kufagia uwanja.

Dunia ya sasa haihitaji migambo wala wafagia uwanja. Inahitaji watu smart vichwani.
 
Hii ni idea nzuri sana ya kufanywa na wakuu wa Wilaya pamoja na viongozi wengine kwa ngazi zao lakini sio mbadala wa kupeleka vijana wetu JKT pamoja na mgambo.

Sasa kama mtu hana ukakamavu atawezaje kufanya kazi za ufundi wa mikono kama vile rangi, welding pamoja na automobile mechanics?
Mkuu dunia inaenda mbio sana huku sisi tunatembea wenzetu wakombio. Achana na fikra kuwa mekanika lazima awe na mwili kama Mwarabu fighter. Hizo skills hata watoto wa sekondari wakipewa wanafanya haiitaji kuwa na miili au ukakamavu.

Kwenye rangi siku hizi tunatumia gun spray haihitaji mtu mrefu, mekanika nayo haihitaji nguvu nyingi sasa kuna mashine kibao za kurahisisha kazi stadi za nati ya roli hata binti wa miaka 16 anaweza akafungua kwa kutumia mashine,kuna winch, pressing mashine na vifaa kibao na sasa ni zama za electric kila mahali.

Hapa tupindue meza ile stadi za kazi ya shule za msingi baada ya kufundisha watoto kushona vitambaa na mkeka wafindishwe hata kufungua kompyuta,pikipiki, bodaboda, baiskeli na vifaa ambavyo katika Maisha ya kila siku watatumia au kukutana navyo.
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania eti;

Kwanini mafunzo ya mgambo yasiwe "compulsory" kwa wanafunzi wote waliohitimu kidato cha sita ambao hawakuchaguliwa kujiunga na mafunzo ya J.K.T?

View attachment 1610352


Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba, inafahamika vema na watanzania wengi ya kuwa lengo la kuwapeleka hawa wadogo wetu JKT ni kuwajengea uzalendo, ukakamavu pamoja na mentality ya kujitegemea.

Ninafahamu fika ya kuwa serikali haiwezi kupeleka graduates wote wa kidato cha sita kwenda mafunzo ya JKT kutokana na ufinyu wa budget, lakini inapaswa kukumbuka pia kwa kutokufanya hivyo inakuwa imetengeneza kundi lingine kuwa la vijana waliokosa fursa adhimu ya kupata mafunzo ya ukakamavu na uzalendo huko vyuoni na mtaani.

View attachment 1610365

Kuna mtoto mmoja wa mama yangu mdogo yeye hakubahatika kupata nafasi ya kuchaguliwa kwenda huko sasa kwa namna anavyogombana na baba yake kila siku ilikuwa mpaka kero.

Kijana mdogo wa kiume yeye akilala usiku kuja kuamka kesho yake basi ni saa nne au tano asubuhi. Mtoto hajui kufagia uwanja wala kufuta madirisha ya nyumbani kwao mpaka huwa ninajiuliza sasa watoto kama hao ambao ndio tunategemea watakuja kuwa taifa la kesho ndio wanakuwa lelemama kiasi hiki sijui Tanzania ya mwaka 2050 itakuwa na watu wazima wa aina gani?

ANGALIZO: Mimi Infantry Soldier sio askari jeshi wala mtumishi wa ofisi yoyote ya serikali bali ni raia mwema ninayeipenda sana Tanzania. Hili jina nilijpa tu kutokana na changamoto kadhaa nzito nilizowahi kuzipitia katika maisha yangu. Hakika umasikini ni m-baya.

View attachment 1610364

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Kwa msisitizo tu ni kwamba kijana yoyote ambae ni raia wa kuzaliwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambae amemaliza kidato cha sita anapaswa kujiunga JKT kwa mujibu wa sheria.

Hiyo haijalishi umemaliza Mzizima, Al Haramain au Feza boys au Girls.

Iwe ni kwa mujibu kwa sheria ya JMT.

Na hata iwe kwa sababu mbalimbali kijana huyo hakuweza kujiunga huo basi iwe ni deni na atumukie kwa muda utakaofaa.

Nchi kama Israeli, Korea Kusini, Kazakhstan na zingine wanafanya hivyo.

Hii yaondoa matatizo kama kutokuwa mzalendo, uzembe wa kufikiri na ushawishi wa kujiunga na makundi kama yale ya kule Kibiti.

Enzi zetu sisi kaka na dada zenu tulikuwa tukikutana pamoja JKT na bila kujali tajiri au maskini au mtoto wa mkulima wote tulinyoa nywele na kuwa na madenge sawa.

JKT ndipo ndipo misingi ya umoja, amani na upendo baina ya wana wa nchi inapojengwa.

Wengine wanaobadilika kama tunaowaona leo hii na wamepitia JKT ni kwa kudanganywa na vijienti vya hapa na pale.
 
Uongo
Kwa msisitizo tu ni kwamba kijana yoyote ambae ni raia wa kuzaliwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambae amemaliza kidato cha sita anapaswa kujiunga JKT kwa mujibu wa sheria.

Hiyo haijalishi umemaliza Mzizima, Al Haramain au Feza boys au Girls.

Iwe ni kwa mujibu kwa sheria ya JMT.

Na hata iwe kwa sababu mbalimbali kijana huyo hakuweza kujiunga huo basi iwe ni deni na atumukie kwa muda utakaofaa.

Nchi kama Israeli, Korea Kusini, Kazakhstan na zingine wanafanya hivyo.

Hii yaondoa matatizo kama kutokuwa mzalendo, uzembe wa kufikiri na ushawishi wa kujiunga na makundi kama yale ya kule Kibiti.

Enzi zetu sisi kaka na dada zenu tulikuwa tukikutana pamoja JKT na bila kujali tajiri au maskini au mtoto wa mkulima wote tulinyoa nywele na kuwa na madenge sawa.

JKT ndipo ndipo misingi ya umoja, amani na upendo baina ya wana wa nchi inapojengwa.

Wengine wanaobadilika kama tunaowaona leo hii na wamepitia JKT ni kwa kudanganywa na vijienti vya hapa na pale.
 
Naunga mkono hoja.
Dunia ya sasa haiendeshwi kwa njia primitive kama zamani.
Achilia mbali mitaani hata hao maaskari wa nchi za wenzetu vitani hawapigani kwa kutumia miguvu kama zamani ni akili tu na teknolojia.
Mtu yupo Korea analipua marekani
Physical presence katika Vita bado itaendelea kuhitajika. Ni kweli waweza kuilipua Montana ukiwa Tarime, Mannheim, au Bergamo na kinyume chake. Lakini huwezi kuteka nchi kwa kutumia makombora ya masafa marefu, drones nk. Hivyo infantry soldiers wana umuhimu mkubwa na ndio huteka au hukomboa nchi. Bottom line is Kila Askari regardless uko jeshi gani ukakamavu Ni lazima.
 
Back
Top Bottom