Kwanini magari aina ya Nissan yanasumbua mafundi kwenye matengenezo?

Kwanini magari aina ya Nissan yanasumbua mafundi kwenye matengenezo?

Hahahaha gar za Nissan hazina shida kabisa wala sio sumbufu kama watu wanavyozisema, gari ni maintanance, sasa linapokuja kwa wakina fundi wa mitaan hua ni wababaishaji wamezoea kufanya kazi kwa mazoea hawataki kujifunza mambo mapya.

Na kuhusu Nissan nazani hua hawana spear sub standard ndo maana bei za spea hua juu kidogo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tokea yametengenezwa ina maana yanabadilika mifumo kila kukicha
Hapana mifumo haibadiliki sana, ila ukiangalia magari ya toyota yaliyokuwa yanaingia nchini miaka ya nyuma, yalikuwa hayana mifumo mingi ya umeme kama Magari Nissana. Kwa mfano Injini ya Rav 4 Masawe ile 3s, haina sensors nyingi kama injini ya Xtrail...

Kwa mfano Xtrail inaweza kuzingua sensor ya accelerator,fundi anatoa macho...yeye ameshazoea accelerator ya 3s ni ya cable..

Kwa hiyo mafundi wanaaza kusema hayo magari ni mabovu, kumbe ndiyo marahisi kwa sababu unaweka tu mashine, inakupa code...unabadilisha sensor unaendelea na mwendo.
 
Spare za nissan ni bei lakini wanaofanya ziwe bei ni hao hao wauza spare. Ukiwatajia tu nissan kosa kubwa. Fungua kifaa kilichoharibika nenda nacho ukawaambie naomba spare kama hii. Bei haitakuwa kubwa
 
Siyo wavivu mkuu,imagine mtu ameishia darasa la saba halafu hajawahi kwenda VETA wala chuo chochote kile cha ufundi ni amejifunzia tu garage za mitaani huko halafu anakuja kukutana na magari ya siku hizi ambayo ni computerized, mambo ya decoding of codes!😁😁😁
Ngumbaru
 
Hata siwaelewi kitu gani fundi anaweza kushindwa kutengeneza kwenye hizo Nissan zilizopo mnazosema ni mpya...Maana Nissan nyingi ni ngumu kidogo au ninyi ndio mnachelewa kutengeneza gari ikihitaji matengenezo haraka maana gari huwa inaongea inapokua na tatizo kwa mtu wa magari hata Kama sio fundi utajua unaanzia wapi...
 
Hata siwaelewi kitu gani fundi anaweza kushindwa kutengeneza kwenye hizo Nissan zilizopo mnazosema ni mpya...Maana Nissan nyingi ni ngumu kidogo au ninyi ndio mnachelewa kutengeneza gari ikihitaji matengenezo haraka maana gari huwa inaongea inapokua na tatizo kwa mtu wa magari hata Kama sio fundi utajua unaanzia wapi...
X-trail Gari ya wanyonge
 
Mafundi wetu bado saana..
Juzi mwezi Februari gari lilileta shida..
Radiator fan ilikuwa ikifunguka, haizimi na inazunguka kwa kasi isiyo ya kawaida..
Injini ikawa inapandisha joto..

Nikafanya diagnosis hapakuonekana code yoyote..

Wapiga ramli hao wakasema swichi ya fan ya radiator ndiyo imekufa...Wakaja mafundi kama watatu wakasema swichi imekufa hivyo ikihisi joto la injini inafungua fan na inashindwa kuzima..

Niakanunua Swichi nyingine, tatizo likawa pale pale...
Nikawaambia huenda thermostat imekufa, wabisha sana wakasema havina uhusiano..

Nikarudi home, nikawasha gari tena nikaacha lipate moto, fan ikawaka, nikashika hose inayotoa maji kwenye inji kuja kweny radiator, ilikuwa ya moto sana kiasi cha kutokushikika..

Hose ya chini inayotoa maji kwenye radiator kwenda kwenye injini ni ya baridi kabisa...Kati ya hose ya chini na injini, ndipo thermostat ya gari langu ilipo....Nikagundua thermostat imekufa kwa mtindo unaoitwa Stuck closed...hivyo maji ya radiaotor hayaingii kwenye injini..

Yale yaliyopo kwenye injini yanachemka sana na ile swichi (sensor) ya kufanya fan iwake , ikawa haizimi kwa sababu maji ya ndani ya inji hayapungu joto.

Nikatoa thermalsta mwenyewe, nikaitest kwa kuichensha jikoni, inafunguka kwa shida sana na kuwa wakati haifunguki..

Baada ya kuitoa tatizo likaisha, joto la injini likipanda fan inawaka na likishuka inazima kama kawaida.

Kwa sasa nataka ninunue thermostat mpya niweke.

Mafundi wetu hawa, mmh...

Binafsi nimeamua kuwa fundi wa gari langu mwenyewe...
Mafundi huwa nawapelekea zile sehemu za kimakanika zaidi, mfano bearing, shockup nk
 
Radiator fan switch ya Nissan,

Mafundi ndiyo walinipigia ramli kuwa imekufa,
Mafundi buana..[emoji3][emoji3][emoji119][emoji119][emoji119][emoji3][emoji3]
images%20(30).jpg
 
Mafundi wetu bado saana..
Juzi mwezi Februari gari lilileta shida..
Radiator fan ilikuwa ikifunguka, haizimi na inazunguka kwa kasi isiyo ya kawaida..
Injini ikawa inapandisha joto..

Nikafanya diagnosis hapakuonekana code yoyote..

Wapiga ramli hao wakasema swichi ya fan ya radiator ndiyo imekufa...Wakaja mafundi kama watatu wakasema swichi imekufa hivyo ikihisi joto la injini inafungua fan na inashindwa kuzima..

Niakanunua Swichi nyingine, tatizo likawa pale pale...
Nikawaambia huenda thermostat imekufa, wabisha sana wakasema havina uhusiano..

Nikarudi home, nikawasha gari tena nikaacha lipate moto, fan ikawaka, nikashika hose inayotoa maji kwenye inji kuja kweny radiator, ilikuwa ya moto sana kiasi cha kutokushikika..

Hose ya chini inayotoa maji kwenye radiator kwenda kwenye injini ni ya baridi kabisa...Kati ya hose ya chini na injini, ndipo thermostat ya gari langu ilipo....Nikagundua thermostat imekufa kwa mtindo unaoitwa Stuck closed...hivyo maji ya radiaotor hayaingii kwenye injini..

Yale yaliyopo kwenye injini yanachemka sana na ile swichi (sensor) ya kufanya fan iwake , ikawa haizimi kwa sababu maji ya ndani ya inji hayapungu joto.

Nikatoa thermalsta mwenyewe, nikaitest kwa kuichensha jikoni, inafunguka kwa shida sana na kuwa wakati haifunguki..

Baada ya kuitoa tatizo likaisha, joto la injini likipanda fan inawaka na likishuka inazima kama kawaida.

Kwa sasa nataka ninunue thermostat mpya niweke.

Mafundi wetu hawa, mmh...

Binafsi nimeamua kuwa fundi wa gari langu mwenyewe...
Mafundi huwa nawapelekea zile sehemu za kimakanika zaidi, mfano bearing, shockup nk
nikushauri, kama hiyo gari ni la petroli, na ni automatic, na unalitumia mkoa wenye joto la wastani, achana na thermostat. maana with or without thermostat joto litapanda tu hadi kufikia optimum (magari mengi naona temp. gauge huwa ni katikati ya cool na hot). muhimu hakikisha coolant ipo.

baada ya hayo, niseme "Toyota All The Way".
 
Back
Top Bottom