Kwanini magari aina ya Nissan yanasumbua mafundi kwenye matengenezo?

Kwanini magari aina ya Nissan yanasumbua mafundi kwenye matengenezo?

Lakini walioweka thermostat walifanya research ya kutosha. Ndiyo maana hata magari yatokayo UAE, pamoja na joto la kule, bado yanakuwa na thermostat.

Nina uzoefu wa kuondoa thermostat, na simshauri mmiliki wa gari kutoa. Miaka kama kumi iliyopita nilipata breakdown ya gari, tena Toyota nikiwa Ruvu darajani, fan clutch ilikufa, na gari ikaanza kuchemsha. Nikaiendesha mdogomdogo mpata chalinze. Pale hawa mafundi wetu wakaibana fan, lakini wakanishawishi niitoe thermostat wakidai huku kwetu haina haja ya kuwemo kwenye engine.

Kwa shingo upande, nikakubali kuitoa thermostat lakini sikuwaachia. Nikaanza tena safari kuelekea Mbeya, ila sikufika Iringa. Kila nilipotaka kukanyagia, temperature ilipanda. Nikapumzika comfort motel (enzi zile), baada ya engine kupoa, nikapanda kitonga kwa shida mpaka Iringa.

Pale Iringa nikatafuta Fundi akarudishia thermostat yangu, nikaanza tena safari kwenda Mbeya. Nikakanyagia mashine kwa hasira, haikupandisha temperature kabisa na gari nipo nayo mpaka leo na thermostat sijaitoa.

Kwa uzoefu huu, Mimi simshauri mtu yeyote kuondoa thermostat kwenye engine ya gari yake, labda iwe imekufa, lakini ikifa pia, mpya zipo, una replace tu.
Swali!! Thermostat kazi yake ni nn kwenye engine inafanyaje kazi ,, na iweje ukitoa gari inachemsha ikirudi haichemki
 
Vipi umewahi kubadili oil ya gear box..?
Kama ndiyo, uliweka oil ya aina gani..? tuanzie hapo kwanza
Tayari tena ilifunguliwa gear box yote. Nikaweka ya aina yake ambayo namba zake ziko kwenye stick ya gear box oil. Kuna mtu kashauri gearbox mounting na niweke tena oil. Nitajaribu hayo mapendekezo. Ila tukubali mafundi wa Nissan ni wachache mjini Dar. Kuwapata sasa!
 
Back
Top Bottom