Kwanini magari aina ya Nissan yanasumbua mafundi kwenye matengenezo?

Kwanini magari aina ya Nissan yanasumbua mafundi kwenye matengenezo?

Nissan ni mzigo ndugu yangu!
ni matunzo mkuu , japo ni kweli huwezi linganisha na toyota .... mimi niliunguza kwa uzembe wangu nina option ya kupeleka engeneering waipeleke standard thrn kufanya overall nikikosa half engine ...
 
mnapigwa parefu sana na service mnazofanya kwenye dealerships (stealerships). I pity you.
Kwahiyo unatushauri service tufanye chini ya miembe?
Bora niingie gharama sehemu ya uhakika kuliko kuingia hasara maradufu chini miembe
 
Kwahiyo unatushauri service tufanye chini ya miembe?
Bora niingie gharama sehemu ya uhakika kuliko kuingia hasara maradufu chini miembe
nunua vipuri, fluids, oil, n.k. maduka yenye kuaminika, au kama unaweza agiza. tafuta mafundi wenye historia nzuri, wanaojua nini wanafanya. wapo.
 
nunua vipuri, fluids, oil, n.k. maduka yenye kuaminika, au kama unaweza agiza. tafuta mafundi wenye historia nzuri, wanaojua nini wanafanya. wapo.
Ungesema hivyo sasa
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Basi unakosea mkuu, kama vipi anza mtindo mtindo wa kupunguza bolts kwenye chuma yako cause hata ikipelea bolt moja au mbili life litasonga...

Anzia kwenye matairi kisha nenda mpaka kwenye steering wheel , shock absorber /spring na kwingine kote...

Then utanipa majibu...
Jamaa katili wewe..[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kama uliilaza garage lazima wameshaiba..
Unaweza kupata kwa kuagiza kati ta laki 6 mpaka laki 8.

Au upate gari lililopata ajali wakuuzie kisela...
Ni kweli mkuu ila asante sana nimefanikiwa kupata kingine sasa hivi nimebaki na tatizo moja ambalo bado linanichanganya kidogo nilikuwa nikikimbia speed ikifika 120 gari ina vibrate sana pia nikishika brake napata iyo vibration hadi sterling inavibrate sasa mara ya kwanza nilidhani labda ni mountain zimekufa nimebadilisha zoote lakini tatizo bado lipo sasa sijui shida itakuwa ni nini
 
Ni kweli mkuu ila asante sana nimefanikiwa kupata kingine sasa hivi nimebaki na tatizo moja ambalo bado linanichanganya kidogo nilikuwa nikikimbia speed ikifika 120 gari ina vibrate sana pia nikishika brake napata iyo vibration hadi sterling inavibrate sasa mara ya kwanza nilidhani labda ni mountain zimekufa nimebadilisha zoote lakini tatizo bado lipo sasa sijui shida itakuwa ni nini
Gari kuvibrate kuna mambo mengi..
Yawezekana mifumo ya suspension haijakaa vizuri..
Wakati mwingine hata tairi bovu linaweza kusababisha tatizo hilo..mfano kama matairi yamevimba vimba..

Kama umeshaweka mounts zote mpya, anza kukagua suspension parts moja baada ya nyingine na matairi..

Kama vipo sawa, ishu inaweza kuwa nyingine
 
Gari kuvibrate kuna mambo mengi..
Yawezekana mifumo ya suspension haijakaa vizuri..
Wakati mwingine hata tairi bovu linaweza kusababisha tatizo hilo..mfano kama matairi yamevimba vimba..

Kama umeshaweka mounts zote mpya, anza kukagua suspension parts moja baada ya nyingine na matairi..

Kama vipo sawa, ishu inaweza kuwa nyingine
Asante mkuu nitalifanyia kazi nimeona mahali pia wanasema muda mwingine inaweza kuwa inasababishwa na kufa kwa u joint hivo ntafania kazi yote haya nione kama tatizo bado litakuwepo
 
Gari za nissan ni gari ambazo zinataka technical knowledge ya kisasa. Hawa mafundi wetu wengi ni watu wa experience na kubahatisha. Sio watu wa kujifunza na kujiongeza.

Kuhusu hizi gari nimeshakutana na mafundi wengi na kuwabana maswali utasikia anamalizia sentence kwakusema zile sio gari za kununua, nunua toyota.


Kimsingi gari mbovu huwa hazidumu barabarani. Sasa unapishana na nissan namba B au A halafu unasema ni gari mbovu?!

Hizi gari zinahitaji ufahamu kuzihandle. Vifaa vyake kutokana na short supply kwenye soko vilikuwa very expensive ila kwasasa vinaanza kushuka sababu supply inaongezeka mdogo mdogo.

Kuwa makini sana na uulize mara mbili mbili mafundi kabla haujawapelekea gari.
 
Hata siwaelewi kitu gani fundi anaweza kushindwa kutengeneza kwenye hizo Nissan zilizopo mnazosema ni mpya...Maana Nissan nyingi ni ngumu kidogo au ninyi ndio mnachelewa kutengeneza gari ikihitaji matengenezo haraka maana gari huwa inaongea inapokua na tatizo kwa mtu wa magari hata Kama sio fundi utajua unaanzia wapi...
Nitakupa mfano kuna nissan ya bi dada m'moja ilikuwa imewasha taa ya ABS. Shida ilikuwa mguu wa upande wa dereva mbele.

Wakafanya wheels alignment, taa bado, wakafungua ile kitu inashika break pads, taa bado, akafumua miguu na kuicheki wapi.

Dada akanunulishwa vifaa hata ambavyo havina shida patupu taa bado. Fundi akataka kudisable mfumo wa sensor sasa kama bahati, mimi nikakutana nae bi dada before zoezi hakijafanyika.

Nikamuuliza uliifanyia gari yako diagnosis kabla ya yote haya, akasema hapana. Ikabidi nimpatie namba ya kijana ambaye anafanya hizo vitu.

Akaenda wakakuta issue ilitakiwa tu kureset taarifa na changamoto ilikuwa ni rotation ya tairi zilikuwa zinapishana so sensor ilisoma na kutoa taarifa.

Ila gari ilirekebishwa na mfumo kuwa reset.
 
Mafundi wetu bado saana..
Juzi mwezi Februari gari lilileta shida..
Radiator fan ilikuwa ikifunguka, haizimi na inazunguka kwa kasi isiyo ya kawaida..
Injini ikawa inapandisha joto..

Nikafanya diagnosis hapakuonekana code yoyote..

Wapiga ramli hao wakasema swichi ya fan ya radiator ndiyo imekufa...Wakaja mafundi kama watatu wakasema swichi imekufa hivyo ikihisi joto la injini inafungua fan na inashindwa kuzima..

Niakanunua Swichi nyingine, tatizo likawa pale pale...
Nikawaambia huenda thermostat imekufa, wabisha sana wakasema havina uhusiano..

Nikarudi home, nikawasha gari tena nikaacha lipate moto, fan ikawaka, nikashika hose inayotoa maji kwenye inji kuja kweny radiator, ilikuwa ya moto sana kiasi cha kutokushikika..

Hose ya chini inayotoa maji kwenye radiator kwenda kwenye injini ni ya baridi kabisa...Kati ya hose ya chini na injini, ndipo thermostat ya gari langu ilipo....Nikagundua thermostat imekufa kwa mtindo unaoitwa Stuck closed...hivyo maji ya radiaotor hayaingii kwenye injini..

Yale yaliyopo kwenye injini yanachemka sana na ile swichi (sensor) ya kufanya fan iwake , ikawa haizimi kwa sababu maji ya ndani ya inji hayapungu joto.

Nikatoa thermalsta mwenyewe, nikaitest kwa kuichensha jikoni, inafunguka kwa shida sana na kuwa wakati haifunguki..

Baada ya kuitoa tatizo likaisha, joto la injini likipanda fan inawaka na likishuka inazima kama kawaida.

Kwa sasa nataka ninunue thermostat mpya niweke.

Mafundi wetu hawa, mmh...

Binafsi nimeamua kuwa fundi wa gari langu mwenyewe...
Mafundi huwa nawapelekea zile sehemu za kimakanika zaidi, mfano bearing, shockup nk
Safi. Na katika kitu watu hawajui ni kuwa thermostat zina kipindi maalumu cha kutumia. Ni vema gari nyingi zinazokuja hasa hizi mileage imefika 50,000 + zikabadilishwa thermostat maana inakuwa imeshakaa sana.

Kumbuka kile kifaa kinapitisha maji muda wote sometimes kuna uchafu ule wa kwenye Radiator unaifanya ina nasa na kuachia so zoezi hili hutokea kimya kimya sana mtu anaweza kutojua nini kinaendelea.
 
nikushauri, kama hiyo gari ni la petroli, na ni automatic, na unalitumia mkoa wenye joto la wastani, achana na thermostat. maana with or without thermostat joto litapanda tu hadi kufikia optimum (magari mengi naona temp. gauge huwa ni katikati ya cool na hot). muhimu hakikisha coolant ipo.

baada ya hayo, niseme "Toyota All The Way".
Thermostat haina cha mkoa wala inchi. Kile kifaa kazi yake ni kuregulate joto la engine na flow ya coolant.

Sasa ukikitoa inamaana unaondoa mfumo wa regulation ya temperature ya engine na hii ni mbaya kwa system ya gari especially za kisasa. Kumbuka hizi gari zinafanya kazi kwa kutumia centralized system ya taarifa ya computer. Unapotoa kifaa muhimu kama thermostat ina maana unaiambia computer system ya gari isifuatilie maswala ya temperature ya engine ya gari, something which is very wrong.

So usije ukathubutu kutoa thermostat, umuhimu wake ni mkubwa sana zaidi ya unavyofikiria. Inasaidiana na oil kuoperate moderate temperature ya gari.

Unajua ukitoa thermostat kinachotokea asubuhi au usiku kwenye engine hakina tofauti na kuweka wrong oil....?!
 
Nashukuru sana kwa ushauri mkuu

Binafsi nitapenda kuirudishia ila lazima iwe genuine...
Japo sina haraka sana..

Itoshe tu kusema "Nissan all the way."[emoji3][emoji119][emoji119][emoji3]
Kabisa... Nissan all the way.
 
ni kweli ina kazi nyingi, ila kwa utashi wangu naona kama kitu kikikosekana na maisha yanaenda basi hicho kitu sio lazima kiwepo.

kwenye ulaji wa mafuta sijaona tofauti kwangu.
Hebu acha uongo. Hakuna kifaa unakiona kwenye gari kisiwe na kazi yake na ukakitoa gari ikawa haina mushkeli katika kuitumia.

Wewe sema haujui kazi ya kitu ulichotoa sio useme hakina kazi.
 
Nishawahi tumia xtrail. Mnyonge haiwezi, itamfia.
Unapokuwa na gari ambayo parts zake ni expensive then usidundulize matatizo. Umesikia inagonga haraka shughulikia tatizo.

Kawaida ya wabongo gari itagonga miguu anauchuna, hadi ianze kuashia na taa za check engine ndio aende gereji. Akifika huko wanamletea msululu wa matatizo kuyatibu inakuwa gharama anaanza oooh toyota sijui nafuu.

Sio kweli. Wewe pay attention na gari yako. Hakikisha unaihudumia on the spot inapokohoa au kupiga chafya. Yaani usilale na tatizo zaidi ya wiki.
 
wakuu nissan dualis inasauti mbaya kama exahaust ina tundu lakini nilifungua nikakuta yale masega hayapo je hii inaweza kuwa sababu na naweza pata wapi masega
Ha ha ha ha ha ha dah watu wana roho mbaya sana. Wameshakuibia catalyst converter. Hizo zinapatikana unaagizia na unaifunga fresh ila next time kuwa makini usiache gari gereji, usiilaze sehemu za ajabu ajabu. Vibaka wanaziiba sana hizo.
 
na nilifanya engine diagnosis gari haina shida yoyote natafuta fundi mzuri a fix hili tatizo la sauti msaaada wadau gari mpya haina 3 month
Hizo zinapatikana unaagiza na unaletewa inafungwa safi tu....
 
nimeshaanza. stabilizer ilikuwa inaleta mambo meusi, ikarekebishwa mara ya kwanza, ya pili muda mfupi tu baadaye, nikaona ukiazi huu. nikaitoa, sai iko store.

nafanya hivyo kwenye non-essential parts tu.
Haupo serious.... Hebu tukaushie basi.
 
Ni kweli mkuu ila asante sana nimefanikiwa kupata kingine sasa hivi nimebaki na tatizo moja ambalo bado linanichanganya kidogo nilikuwa nikikimbia speed ikifika 120 gari ina vibrate sana pia nikishika brake napata iyo vibration hadi sterling inavibrate sasa mara ya kwanza nilidhani labda ni mountain zimekufa nimebadilisha zoote lakini tatizo bado lipo sasa sijui shida itakuwa ni nini
Unatumia gari gani hiyo?! Taa ya Gani inawaka kwenye dashboard?!

Umefanya wheel alignment check?!
 
Back
Top Bottom