Kwanini magari aina ya Nissan yanasumbua mafundi kwenye matengenezo?

Kwanini magari aina ya Nissan yanasumbua mafundi kwenye matengenezo?

Ni nini kinakufa mkuu mimi ndio hapo nataka kujua...
Sensors ikifa angalia na mashine yenye updated software, nunua sensor original, gari isiwe ya mikono mingi, oil service kwa wakati, hakikisha haichemshi, zingatia coolant engine inapinda block kirahisi ila zinauzwa cheap.
 
Nissan Terano lipo linadunda tu miaka zaidi ya kumi,fundi wake ni mzee mmoja mstaafu wa Sub Scania.
Kuna kipindi ilisumbua sana Cylinder head mzee akakagua mfumo wa cooling system aliporekebisha mfumo wa cooling na tatizo la cylinder head likaisha.
 
nikushauri, kama hiyo gari ni la petroli, na ni automatic, na unalitumia mkoa wenye joto la wastani, achana na thermostat. maana with or without thermostat joto litapanda tu hadi kufikia optimum (magari mengi naona temp. gauge huwa ni katikati ya cool na hot). muhimu hakikisha coolant ipo.

baada ya hayo, niseme "Toyota All The Way".
Lakini walioweka thermostat walifanya research ya kutosha. Ndiyo maana hata magari yatokayo UAE, pamoja na joto la kule, bado yanakuwa na thermostat.

Nina uzoefu wa kuondoa thermostat, na simshauri mmiliki wa gari kutoa. Miaka kama kumi iliyopita nilipata breakdown ya gari, tena Toyota nikiwa Ruvu darajani, fan clutch ilikufa, na gari ikaanza kuchemsha. Nikaiendesha mdogomdogo mpata chalinze. Pale hawa mafundi wetu wakaibana fan, lakini wakanishawishi niitoe thermostat wakidai huku kwetu haina haja ya kuwemo kwenye engine.

Kwa shingo upande, nikakubali kuitoa thermostat lakini sikuwaachia. Nikaanza tena safari kuelekea Mbeya, ila sikufika Iringa. Kila nilipotaka kukanyagia, temperature ilipanda. Nikapumzika comfort motel (enzi zile), baada ya engine kupoa, nikapanda kitonga kwa shida mpaka Iringa.

Pale Iringa nikatafuta Fundi akarudishia thermostat yangu, nikaanza tena safari kwenda Mbeya. Nikakanyagia mashine kwa hasira, haikupandisha temperature kabisa na gari nipo nayo mpaka leo na thermostat sijaitoa.

Kwa uzoefu huu, Mimi simshauri mtu yeyote kuondoa thermostat kwenye engine ya gari yake, labda iwe imekufa, lakini ikifa pia, mpya zipo, una replace tu.
 
Sensors ikifa angalia na mashine yenye updated software, nunua sensor original, gari isiwe ya mikono mingi, oil service kwa wakati, hakikisha haichemshi, zingatia coolant engine inapinda block kirahisi ila zinauzwa cheap.
Ok hii kanuni ni kwa gari zote Mkuu ndio nilitaka kujua hii Nissan ina utofauti upi na magari mengine maana kama Nissan ya kawaida tuu tunalia jee Rover au Benz hizi za kisasa tutaziweza kweli...
 
Ok hii kanuni ni kwa gari zote Mkuu ndio nilitaka kujua hii Nissan ina utofauti upi na magari mengine maana kama Nissan ya kawaida tuu tunalia jee Rover au Benz hizi za kisasa tutaziweza kweli...
Nissan haitakusumbua sana ukifata hizo kanuni. Toyota mfano rav 4 old hata usipofat hizo kanuni inavumilia,ukifata kanuni inaishi milele ndo watu wanazilinganisha hapo. Rover,BM na Benz hutaziweza kama nissan unalia lia kuihudumia.
 
nissanxtrail2021.jpg

Xtrail new shape
 
Nissan haitakusumbua sana ukifata hizo kanuni. Toyota mfano rav 4 old hata usipofat hizo kanuni inavumilia,ukifata kanuni inaishi milele ndo watu wanazilinganisha hapo. Rover,BM na Benz hutaziweza kama nissan unalia lia kuihudumia.
Mkuu mimi nilikua nauliza kujua hayo magari yanawasumbua nini zaidi ila sipo kwenye hayo sasa hivi nishatoka huko kitambo kidogo...
 
Wengi wao waganga njaa tu sasa mtu anajiita fundi umeme ama fundi waya hana lolote anahangaika kuchuna nyaya na kuunganisha kitesta sijui kimechoooka anaungaunga hajui A wala B, mwisho anakwambia sensor imekufa lete laki tano Mxiuuuuuuuuu , kuna mmoja nilimtandika makofi hana hamu.
 
Shida mafundi wetu wanapiga ramli, gari ni kama binadamu lazima diagnosis ifanyike. Unaweza kununulishwa vifaa na gari isipone
Kuna jamaa gari ilizingua kina Fundi Maiko wakamnunulisha pump na makolokolo ya karibia 700k na haikupona.

Akampa jamaa yangu mmoja k/koo , akabadili plugs tu mwendo mdundo[emoji1][emoji1]
 
Si bure una idea za ufundi au umeendesha gari bovu mda mrefu huko nyuma[emoji1787]
Mafundi wetu bado saana..
Juzi mwezi Februari gari lilileta shida..
Radiator fan ilikuwa ikifunguka, haizimi na inazunguka kwa kasi isiyo ya kawaida..
Injini ikawa inapandisha joto..

Nikafanya diagnosis hapakuonekana code yoyote..

Wapiga ramli hao wakasema swichi ya fan ya radiator ndiyo imekufa...Wakaja mafundi kama watatu wakasema swichi imekufa hivyo ikihisi joto la injini inafungua fan na inashindwa kuzima..

Niakanunua Swichi nyingine, tatizo likawa pale pale...
Nikawaambia huenda thermostat imekufa, wabisha sana wakasema havina uhusiano..

Nikarudi home, nikawasha gari tena nikaacha lipate moto, fan ikawaka, nikashika hose inayotoa maji kwenye inji kuja kweny radiator, ilikuwa ya moto sana kiasi cha kutokushikika..

Hose ya chini inayotoa maji kwenye radiator kwenda kwenye injini ni ya baridi kabisa...Kati ya hose ya chini na injini, ndipo thermostat ya gari langu ilipo....Nikagundua thermostat imekufa kwa mtindo unaoitwa Stuck closed...hivyo maji ya radiaotor hayaingii kwenye injini..

Yale yaliyopo kwenye injini yanachemka sana na ile swichi (sensor) ya kufanya fan iwake , ikawa haizimi kwa sababu maji ya ndani ya inji hayapungu joto.

Nikatoa thermalsta mwenyewe, nikaitest kwa kuichensha jikoni, inafunguka kwa shida sana na kuwa wakati haifunguki..

Baada ya kuitoa tatizo likaisha, joto la injini likipanda fan inawaka na likishuka inazima kama kawaida.

Kwa sasa nataka ninunue thermostat mpya niweke.

Mafundi wetu hawa, mmh...

Binafsi nimeamua kuwa fundi wa gari langu mwenyewe...
Mafundi huwa nawapelekea zile sehemu za kimakanika zaidi, mfano bearing, shockup nk
 
wakuu nissan dualis inasauti mbaya kama exahaust ina tundu lakini nilifungua nikakuta yale masega hayapo je hii inaweza kuwa sababu na naweza pata wapi masega
 
na nilifanya engine diagnosis gari haina shida yoyote natafuta fundi mzuri a fix hili tatizo la sauti msaaada wadau gari mpya haina 3 month
 
Back
Top Bottom