Kwanini Magufuli anachukiwa na CCM, Chadema, ACT, CUF na wasomi wengi ila anapendwa na wanyonge?

Kwanini Magufuli anachukiwa na CCM, Chadema, ACT, CUF na wasomi wengi ila anapendwa na wanyonge?

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Lipo wazi CCM wengi hawampendi Magufuli, ila wanajitahidi kutomshambulia moja kwa moja sababu alikuwa kiongozi wao waliomuunga mkono alipokuwa kiongozi, CHADEMA ndiyo hawampendi kabisa, ACT ndiyo kabisaa.

Wasomi wengi pia hawamkubali Magufuli, ukiwauliza tu ukiwa nao wengi wanamponda, baadhi walikuwa wakimsifia tu kipindi kile sababu ya woga au kutaka cheo ila wanyonge, kama alivyopenda kuwaita Watanzania wa kawaida, hili ndio kundi kubwa la watu na linamkubali sana, utaona comments zao Facebook na Instagram wakimfagilia, ila hutawaona sana Twitter na hapa JF, hawapendi sana hii mitandao.

Najiuliza ni kwa nini? Magufuli alikuwa akiwaeleza watu Tanzania ni tajiri, miradi mingi tunaifanya kwa fedha zetu, akawaeleza pia yeye siyo miongoni mwa kundi la elites ndani ya CCM walioifisadi nchi.

Pia alisikika akisema mtu katika utawala wa nyuma masikini aliweza kufanywa chochote na tajiri ila katika utawala wake tajiri anaweza kufanyiwa chochote, aliruhusu pia wafanyabishara ndogondogo kufanya biashara popote na kusema yeye ni mkombozi wao.

Alikuwa akiwafokea, kuwatukana na kuwafukuza maafisa wa Serikali waliokuwa wakilalamikiwa na wananchi mbele ya hadhara, na mara nyingi alisimama kusikiliza matatizo binafsi ya wananchi kama vile mirathi.

Haya na mengine mengi yaliwafurahisha sana watu wa tabaka la chini ambalo liliamini shida zao zinatokana na kuonewa na viongozi wa serikali na matajiri

Sasa kwa nini wasomi na wanasiasa wengi wasimpende? Kwa haraka haraka mtu ukitazama uongozi wa Magufuli utaona ni uongozi wa kuleta maendeleo na kuondoa rushwa, kuwapa haki wanyonge dhidi ya matajiri na mabwanyenye na kuipaisha nchi kiuchumi.

Mtu huwezi kusema unaondoa rushwa huku ukiua uwazi, unafunga na kuua wanaokosoa, ukifungia na kuvitisha vyombo vya habari, huwezi kusema utakuza uchumi na kipato cha watu huku unakandamiza sekta binafsi kwa kuvuruga biashara, huwezi kusema hubagui watu kwa vyama huku ukiwaambia mmechagua upinzani maendeleo siwapi, huwezi kusema upo against na mabwanyeye huku ukiwajengea mahekalu wastaafu, na kuteua watoto wao na wake zao kwenye vyeo vya kisiasa badala ya watu wa kawaida.

Huwezi kusema umerudisha nidhamu kwa watendaji wa serikali huku wateule wako wakiingia benki na kupora mchana kweupe, kuvamia vituo vya habari na walinzi wa ikulu, Polisi wakiua na kubambikiza watu kesi, watu wenye uelewa hawawezi kukuelewa kamwe.

Samia kwenye moja ya mahojiano yake, alisema anataka legacy yake iwe ni kuwafanya watanzania kujitambua hasa kwenye mambo ya siasa na uraia, nafikiri ameona watanzania wengi hawajui wana uelewa mdogo sana kwenye siasa na ni rahisi sana kuwalaghai.
 
Sasa inakuwaje watu hai wapambane na maiti?
Maana yake kuna shida kwenye vichwa vyetu yana tuendelee kupambana na maiti?
kujadili legacy ya rais aliyepita ni kupambana na maiti? tunapojadili legacy ya Nyerere ni kupambana na maiti? Mtu akishakuwa kiongozi wa nchi ni sehemu ya historia, atajadiliwa lazima..
 
Lipo wazi CCM wengi hawampendi Magufuli , ila wanajitahidi kuto mshambulia moja kwa moja sababu alikuwa kiongozi wao waliomuunga mkono alipokuwa kiongozi, CHADEMA ndio hawampendi kabisa, ACT ndio kabisaa.

Wasomi wengi pia hawamkubali Magufuli, ukiwauliza tu ukiwa nao wengi wanamponda, baadhi walikuwa wakimsifia tu kipindi kile sababu ya woga au kutaka cheo il wanyonge, kama alivyopenda kuwaita watanzania wa kawaida, hili ndio kundi kubwa la watu na linamkubali sana, utaona comments zao Facebook na Instagrma wakimfagilia, ila hutawaona sana Twitter na hapa JF, hawapendi sana hii mitandao.

Najiuliza ni kwa nini? Magufuli alikuwa akiwaeleza watu Tanzania ni tajiri, miradi mingi tunaifanya kwa fedha zetu, akawaeleza pia yeye sio miongoni mwa kundi la elites ndani ya CCM walioifisadi nchi.

Pia alisikika akisema mtu katika utawala wa nyuma masikini aliweza kufanywa chochote na tajiri ila katika utawala wake tajiri anaweza kufanyiwa chochote, aliruhusu pia wafanyabishara ndogondogo kufanya biashara popote na kusema yeye ni mkombozi wao.

alikuwa akiwafokea, kuwatukana na kuwafukuza maafisa wa serikali waliokuwa wakilalamikiwa na wananchi mbele ya hadhara, na mara nyingi alisimama kusikiliza matatizo binafsi ya wananchi kama vile mirathi.

Haya na mengine mengi yaliwafurahisha sana watu wa tabaka la chini ambalo liliamini shida zao zinatokana na kuonewa na viongozi wa serikali na matajiri

Sasa kwa nini wasomi na wanasiasa wengi wasimpende? kwa haraka haraka mtu ukitazama uongozi wa Magufuli utaona ni uongozi wa kuleta maendeleo na kuondoa rushwa, kuwapa haki wanyonge dhidi ya matajiri na mabwanyenye na kuipaisha nchi kiuchumi.

Mtu huwezi kusema unaondoa rushwa huku ukiua uwazi, unafunga na kuua wanaokosoa, ukifungia na kuvitisha vyombo vya habari, huwezi kusema utakuza uchumi na kipato cha watu huku unakandamiza sekta binafsi kwa kuvuruga biashara, huwezi kusema hubagui watu kwa vyama huku ukiwaambia mmechagua upinzani maendeleo siwapi, huwezi kusema upo against na mabwanyeye huku ukiwajengea mahekalu wastaafu, na kuteua watoto wao na wake zao kwenye vyeo vya kisiasa badala ya watu wa kawaida.

Huwezi kusema umerudisha nidhamu kwa watendaji wa serikali huku wateule wako wakiingia benki na kupora mchana kweupe, kuvamia vituo vya habari na walinzi wa ikulu, Polisi wakiua na kubambikiza watu kesi, Watu wenye uelewa hawawezi kukuelewa kamwe.

Samia kwenye moja ya mahojiano yake, alisema anataka legacy yake iwe ni kuwafanya watanzania kujitambua hasa kwenye mambo ya siasa na uraia, nafikiri ameona watanzania wengi hawajui wana uelewa mdogo sana kwenye siasa na ni rahisi sana kuwalaghai.
Wacha ulevi wako wa kimpumu kutuletea hapa jamvini.

Wanyonge gani unao wazungumzia wewe?
 
Jiulize swali dogo sana halafu labda utapata jibu la swali lako, uliona wapi Dunia hii Vyama vya Upinzani vinakosa chochote cha kuikosoa Serikali iliyo madarakani ? Utawala wa sasa na Upinzani ni wamoja na wametoka mbali wote wanalipwa na kutumika na George Soros, na ndo maana Mbowe kaenda Kenya huko ndio makao makuu ya George Soros kwa Afrika Mashariki.

George Soros huyo bosi wao wote na ndo maana so called upinzani hawawezi kukosoa chochote, wote wana one master huyo hapo chini!
1648889148365.jpeg
 
Back
Top Bottom