Kwanini Magufuli anachukiwa na CCM, Chadema, ACT, CUF na wasomi wengi ila anapendwa na wanyonge?

Kwanini Magufuli anachukiwa na CCM, Chadema, ACT, CUF na wasomi wengi ila anapendwa na wanyonge?

Nitamkumbuka daima Rais Magufuli kwa kuwa alikuwa mtu mwenye maamuzi na maamuzi mengi yaliwakilisha asilimia 80 ya Wananchi wa Tanzania.
 
Awamu ya fulani nimeisahau jina,Waziri Mkuu alikwenda nchi fulani akakuta vigari vidogo vingi,viswift,visuzuki akaambiwa hivi vigari ndio wanatumia Mawaziri,Waziri Mkuu wetu alishangaa,akaishia kusema kule kwetu basi tu sijui kama inawezekana,Waziri Mkuu lakini alikuwa hana maamuzi🤔
 
Awamu fulani nimeisahau jina Rais aliletewa list ya Mafisadi papa akaishia kusema awa wakiguswa nchi itatikisika.
 
Rais Magufuli alikuwa anasimama anasema Serikali inahamia Dodoma na mara moja ofisi zinaanza kujengwa na Serikali inahamia Dodoma,hakuna longolongo.
 
kujadili legacy ya rais aliyepita ni kupambana na maiti? tunapojadili legacy ya Nyerere ni kupambana na maiti? Mtu akishakuwa kiongozi wa nchi ni sehemu ya historia, atajadiliwa lazima..
Katika kupambana mfano wako hauna maana

Mnapojadili legacy ya Magufuli mnaambiwa mnapambana sababu mnazungumza negatively

Mkizungumzia Nyerere hampambani sababu mnazungumza positively
 
Katika kupambana mfano wako hauna maana

Mnapojadili legacy ya Magufuli mnaambiwa mnapambana sababu mnazungumza negatively

Mkizungumzia Nyerere hampambani sababu mnazungumza positively

Wote nyungu moja , Nyerere aliuwa watu kwa maelfu huku Zanzibar, Rest all in Hell
 
Katika kupambana mfano wako hauna maana

Mnapojadili legacy ya Magufuli mnaambiwa mnapambana sababu mnazungumza negatively

Mkizungumzia Nyerere hampambani sababu mnazungumza positively
Sasa kwani legacy lazima iwe positive? So wanapojadiliwa akina Hitler ni kuwa wanapambana na maiti?
 
Hata kwenye dini wanyonge hatawaingia kwenye ufalme wabinguni
Ndugu yangu, hao wanaoitwa 'wanyonge' na wengi wao kwa kutotambua haki zao za msingi, wataendelea kukumbatia umaskini na kukosekana kwa maendeleo makini kwa nchi zao, kwa miaka mingi ijayo.....that's bitter truth'.
 
Magufuli kama wanyonge wake walikuwa ni majuha na washamba

Wote yeye na wanyonge wenzie walikuwa na akili ya kimasikini,husda na ujima

Waliamini ili maskini aendelee basi tajiri ni lazima ashushwe
Utajiri mwingi Tz ni lazima ufanye figisufigisu, ukwepe kodi, utoe na rushwa !! Ndio utajiri unaochukiwa !! Na sio kweli kwamba matajiri wote Tz wanachukiwa !! Yapo mengi aliyafanya JPM watu wenye akili wakamkubali sana lakini yapo pia mengine alikosea sana !! Binadamu sio malaika ! Hawezi kuwa 100% Perfect !! Mabaya yaachwe mema yaendelezwe !! Haiwezekani ukawa na utajiri unotokana na deals haramu na biashara zingine haramu halafu watu wakupende !! Never !! Watakuwa wanakudanganya tu mbele yako ili wapate wanachokitaka lakini mioyoni wanakuchukia !! That's it !!
 
02205298110509.jpg
 
Lipo wazi CCM wengi hawampendi Magufuli, ila wanajitahidi kutomshambulia moja kwa moja sababu alikuwa kiongozi wao waliomuunga mkono alipokuwa kiongozi, CHADEMA ndiyo hawampendi kabisa, ACT ndiyo kabisaa.

Wasomi wengi pia hawamkubali Magufuli, ukiwauliza tu ukiwa nao wengi wanamponda, baadhi walikuwa wakimsifia tu kipindi kile sababu ya woga au kutaka cheo ila wanyonge, kama alivyopenda kuwaita Watanzania wa kawaida, hili ndio kundi kubwa la watu na linamkubali sana, utaona comments zao Facebook na Instagram wakimfagilia, ila hutawaona sana Twitter na hapa JF, hawapendi sana hii mitandao.

Najiuliza ni kwa nini? Magufuli alikuwa akiwaeleza watu Tanzania ni tajiri, miradi mingi tunaifanya kwa fedha zetu, akawaeleza pia yeye siyo miongoni mwa kundi la elites ndani ya CCM walioifisadi nchi.

Pia alisikika akisema mtu katika utawala wa nyuma masikini aliweza kufanywa chochote na tajiri ila katika utawala wake tajiri anaweza kufanyiwa chochote, aliruhusu pia wafanyabishara ndogondogo kufanya biashara popote na kusema yeye ni mkombozi wao.

Alikuwa akiwafokea, kuwatukana na kuwafukuza maafisa wa Serikali waliokuwa wakilalamikiwa na wananchi mbele ya hadhara, na mara nyingi alisimama kusikiliza matatizo binafsi ya wananchi kama vile mirathi.

Haya na mengine mengi yaliwafurahisha sana watu wa tabaka la chini ambalo liliamini shida zao zinatokana na kuonewa na viongozi wa serikali na matajiri

Sasa kwa nini wasomi na wanasiasa wengi wasimpende? Kwa haraka haraka mtu ukitazama uongozi wa Magufuli utaona ni uongozi wa kuleta maendeleo na kuondoa rushwa, kuwapa haki wanyonge dhidi ya matajiri na mabwanyenye na kuipaisha nchi kiuchumi.

Mtu huwezi kusema unaondoa rushwa huku ukiua uwazi, unafunga na kuua wanaokosoa, ukifungia na kuvitisha vyombo vya habari, huwezi kusema utakuza uchumi na kipato cha watu huku unakandamiza sekta binafsi kwa kuvuruga biashara, huwezi kusema hubagui watu kwa vyama huku ukiwaambia mmechagua upinzani maendeleo siwapi, huwezi kusema upo against na mabwanyeye huku ukiwajengea mahekalu wastaafu, na kuteua watoto wao na wake zao kwenye vyeo vya kisiasa badala ya watu wa kawaida.

Huwezi kusema umerudisha nidhamu kwa watendaji wa serikali huku wateule wako wakiingia benki na kupora mchana kweupe, kuvamia vituo vya habari na walinzi wa ikulu, Polisi wakiua na kubambikiza watu kesi, watu wenye uelewa hawawezi kukuelewa kamwe.

Samia kwenye moja ya mahojiano yake, alisema anataka legacy yake iwe ni kuwafanya watanzania kujitambua hasa kwenye mambo ya siasa na uraia, nafikiri ameona watanzania wengi hawajui wana uelewa mdogo sana kwenye siasa na ni rahisi sana kuwalaghai.
Wajinga ndiyo waliwao.
 
Asilimia kubwa ya wanaomchukia JPM wapo humu JF, cha ajabu asilimia kubwa mitaani watu wanamkubali na kumkumbuka sana.

Yawezekana kuna watu wachache walioteseka na utawala wake hasa wale wapiga dili wameamua kuunda magenge ya machawa na ID fake nyingi humu kuonyesha chuki zao kwa mwendazake.

Kwahiyo ndugu yangu hakuna namna ni kuwazoea tu na kuwachukulia poa na chuki zao. Sitoshangaa nikiona mda sio mrefu wanaishambulia hii comment na kuniita sukuma gang ingawa ni kijana muungwana kabisa wa kisiwani mafia. Ni hayo tu...
 
Wewe kenge, kwanza kuitwa mnyonge ni matusi!
Mnyonge ni mtu wa namna gani kwanza?
Yule alikuwa anawapumbaza tu na kichwani hakuwa vyema!
Tukatae kabisa tunapomuona mtu anawaita wengine wanyonge!
 
Asilimia kubwa ya wanaomchukia JPM wapo humu JF, cha ajabu asilimia kubwa mitaani watu wanamkubali na kumkumbuka sana.

Yawezekana kuna watu wachache walioteseka na utawala wake hasa wale wapiga dili wameamua kuunda magenge ya machawa na ID fake nyingi humu kuonyesha chuki zao kwa mwendazake.

Kwahiyo ndugu yangu hakuna namna ni kuwazoea tu na kuwachukulia poa na chuki zao. Sitoshangaa nikiona mda sio mrefu wanaishambulia hii comment na kuniita sukuma gang ingawa ni kijana muungwana kabisa wa kisiwani mafia. Ni hayo tu...

Ilikuwaje kwenye uchaguzi akalitumia jeshi, Polisi, Usalama kuiba kura Na kuuwa watu ili kubaki madarakani? Kama watu wanampenda?
 
Back
Top Bottom