Kwanini Majaji wanaapa mbele ya Rais na sio Jaji Mkuu?

Kwanini Majaji wanaapa mbele ya Rais na sio Jaji Mkuu?

Kenya wenzetu wameondokana na hizi teuzi kwa kiasi kikubwa sana!
Nafasi nyingi hutangazwa kisha watu huomba!
Nafasi kama IGP n.k wanafanya kuomba na usaili wa wazi kufanyika kumpata anaestahili!
Wenzetu walishaona mapungufu makubwa yaliyopo kwenye teuzi wakaamua kuondokana nazo !


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba nikujibu kwa msingi ya utawala na sio kisheria.
Tanzania kama ilivyo Marekani, Rais ana-play role ya mkuu wa nchi. Kwa kofia ya Ukuu wa nchi, anakua na madaraka ya kuteua na kuongoza kiapo cha utii kwa majaji.

Uingereza (The United Kingdom) majaji wanateuliwa na Malkia au Mfalime. Waziri mkuu (amabe ni mkuu wa serikali) anawajibika kumshauri Malkia nani wa kumteua akishirikiana na tume ya utumishi wa mahakama.

Ujerumani, jaji mkuu anakula kiapo mbela ya Rais wa Germany Federation (na sio Chancellor ambae ni mkuu wa serikali)

Israeli pia, majina ya majaji wanapendekezwa na tume ya kijaji (Judicial Nomination Committee). Anaewateua na Rais wa Israel ambae ni mkuu wa nchi.

Kwa kifupi sana, Tanzania, Rais kwa kofia yake ya Ukuu wa Nchi, katiba inampa nguvu ya kisheria na kiutawala kuchagua/kuteua majaji na kuwaongoza kula kiapo cha utii kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Niko tarari kukosolewa na kupata ufahamu zaidi toka kwa "wasomi na mawakili"
leo TUNAJIFANANISHA NA WALE TUNAOWAITA MABEBERU.
baniani mbaya.kiatu chake dawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rais ndie huteua Majaji,Majaji hawateuliwi Na Jaji Mkuu huteuliwa Na Rais

Hivyo ni sahihi Rais kuwaapisha kwa Kuwa Yeye ndie kawateua!
Labda tuhoji Kwanini Majaji wa Mahakama kuu Na ya Rufaa huteuliwa Na Rais badala ya Jaji Mkuu kwa kushauriwa Na Mamlaka husika?

Haiingi akilini Jaji Mkuu kuapisha Mtu ambae hajamteua
Kwa RC kumuapisha DC anafanya hivyo kwa Kuwa amekasimiwa hayo majukumu ya Mkoa Na Rais Mwenyewe kwa hiyo anawaapisha ma DC kwa niaba ya Rais

Hata Kwenye Majeshi ngazi Za Juu Za Maafisa wanadhimu wa Majeshi wanateuliwa Na kuapishwa Na Rais sio Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi

Rais wa Nchi Ana kofia Mbili Za Ngazi ya Utawala

1) Mkuu wa Serikali ( Head of Executive)
2) Mkuu wa Dola ( Head of state)

Akiteua Mkurugenzi wa Halmshauri Au WaZiri hapo inakuwa Kama Mkuu wa Serikal

Lakin akiteua Jaji Mkuu Au Katibu wa Bunge hapo anafanya kazi Kama Mkuu wa Dola ( Head of state)

Head of state maana yake Ana simamia Nchi Na mihimili yake yote mitatu ndio sababu ana Mamlaka ya Kuvunja Bunge Na Hata kufukuza Jaji Mkuu japo kwa Jaji kumewekwa Urasimu kidogo ili kutofautisha Na wateule wengine
 
HATA ILI UWA LINANIACHA NA MASWALI MENGI.JAJI MKUU ANAMUAPISHA RAIS NA RAIS NDIYE ANAMTEUA JAJI MKUU.IKITOKEA KWA WAKATI MMOJA NAFASI ZOTE ZIKO WAZI.HAPO ITAKUWAJE MAANA ILI UWE RAIS LAZIMA UAPE KWANZA NA JE KAMA NAFASI YA JAJI MKUU IKO WAZI,HAPO JE

Sent using Jamii Forums mobile app

Kaimu Jaji Mkuu atamuapisha Rais wa Jamhuri then Rais wa Jamhuri anaweza kumthibitisha Jaji Mkuu au kuteua Mwingine kwa nafasi hiyo
 
Naomba nikujibu kwa msingi ya utawala na sio kisheria.
Tanzania kama ilivyo Marekani, Rais ana-play role ya mkuu wa nchi. Kwa kofia ya Ukuu wa nchi, anakua na madaraka ya kuteua na kuongoza kiapo cha utii kwa majaji.

Uingereza (The United Kingdom) majaji wanateuliwa na Malkia au Mfalime. Waziri mkuu (amabe ni mkuu wa serikali) anawajibika kumshauri Malkia nani wa kumteua akishirikiana na tume ya utumishi wa mahakama.

Ujerumani, jaji mkuu anakula kiapo mbela ya Rais wa Germany Federation (na sio Chancellor ambae ni mkuu wa serikali)

Israeli pia, majina ya majaji wanapendekezwa na tume ya kijaji (Judicial Nomination Committee). Anaewateua na Rais wa Israel ambae ni mkuu wa nchi.

Kwa kifupi sana, Tanzania, Rais kwa kofia yake ya Ukuu wa Nchi, katiba inampa nguvu ya kisheria na kiutawala kuchagua/kuteua majaji na kuwaongoza kula kiapo cha utii kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Niko tarari kukosolewa na kupata ufahamu zaidi toka kwa "wasomi na mawakili"
Asante mkuu
 
Hapo hata mimi sielewi.Jaji anaapishwa na Rais wakati huohuo Rais akishachaguliwa anaapishwa na jaji hivi hii imekaaje.wataalam tupeni taaluma zenu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio hapo watu waelewe,sio hizi kelele za mihimili sijui upuuzi gani huko.
 
Wanabodi kuuliza si ujinga nataka kupata kufahamu tu. Najua kuna Mihimili mitatu kwa Maana ya Bunge , Mahakama na Serikali.

Na naambiwa mihimili hii ina Nguvu sawa na kujitegemea.

Nimeona wateule wa Serikali wanateuliwa na Rais na kuapa kwa Rais.

Naona Wabunge wanaochaguliwa na wananchi wanaapa kwa Spika wa Bunge.

Swali sasa kwa nini majaji wateuliwe na Rais? Je kwa nini waape kwa Rais, wakati wapo kwenye Muhimili wa Mahakama?

Je huku si kusema kuwa ni Bunge pekee ambalo labda liko huru kidogo maana wabunge hawapaswi kuapa mbele ya Rais.?

Je, huku ni kusema kuwa Mahakama haiko huru maana Watendaji wake wanateuliwa na Rais na kuapa kwa Rais?

Nauliza tu waungwana maana hii inanichanganya?View attachment 1008124
Ama kweli Roma ina nguvu sna aisee japo nnatoka nje ya mada lakini hawa majaji kuvaa kama mapadri wa kiroma au wasaidizi wao ndo imenifanya nianze kulichukulia tofauti kabisa hili kanisa la Roma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kenya ukilinganisha
Kenya wenzetu wameondokana na hizi teuzi kwa kiasi kikubwa sana!
Nafasi nyingi hutangazwa kisha watu huomba!
Nafasi kama IGP n.k wanafanya kuomba na usaili wa wazi kufanyika kumpata anaestahili!
Wenzetu walishaona mapungufu makubwa yaliyopo kwenye teuzi wakaamua kuondokana nazo !


Sent using Jamii Forums mobile app
Kenya hawana demokrasia komavu kama Marekani.
Ni kweli mfumo wao wa sasa Jaji mkuu anaomba kazi na kupitia katika mikono ya usaili toka kwa manguli wa sheria. Pamoja na hayo, bado mfumo huo una mapungufu mengi hasa ukikuta Jaji Mkuu ana msimamo mkali ambao hauzingatii matakwa ya maslahi mapana ya Taifa.
Fikiria kitendo cha mahakama kufuta uchaguzi mkuu wa Kenya mwaka jana. Hakuna anaepinga gharama za demokrasia na utawala wa sheria. Mwisho wa siku uchaguzi umerudiwa na fedha nyingi zimetumika, na alieshinda ni yule yule Uhuru Kenyatta.

Fedha zile zingeweza kufanya miradi ya kugusa wananchi moja kwa moja kama vile maji, huduma ya afya, mikopo inayoibua ajira endelevu kwa vijana na mambo kama hayo
 
Hapo hata mimi sielewi.Jaji anaapishwa na Rais wakati huohuo Rais akishachaguliwa anaapishwa na jaji hivi hii imekaaje.wataalam tupeni taaluma zenu

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii ni takwa la kisheria na katiba.
Katiba imeainisha wazi kuwa Rais akichakuchaguliwa na wananchi na matokeo kutangazwa na Tume ya Taifa ya uchaguzi, Rais atakula kiapo mbele ya jaji mkuu.
Hata Marekani ambao ni magwiji wa Kidemokrasia, Rais wao nae anakula kiapo mbele ya Jaji Mkuu.

Katiba iko online. Unaweza kui-download na soma Ibara ya 42, kifungu cha kwanza mpaka cha tano kuna maeliezo mazuri ya kujibu hoja yako
 
Ni katiba ndo inasema hivyo.

Halafu kusema kuna mihimili mitatu naona ni geresha tu. Mi naona kuna mhimili mmoja (serikali) na matawi yake mawili (mahakama na bunge)
 
Eti mihimili mitatu. hapa kwetu hiyo ni geresha tu. watu ni wezi wanaogopa siku hiyo mihimili ikifanya kazi yake vyema watu wataumbuka. tunapelekana hivyo hivyo siku zinaenda. Haki haiwezi kutendeka kwa katiba tuliyo nayo
 
Wanabodi kuuliza si ujinga nataka kupata kufahamu tu. Najua kuna Mihimili mitatu kwa Maana ya Bunge , Mahakama na Serikali.

Na naambiwa mihimili hii ina Nguvu sawa na kujitegemea.

Nimeona wateule wa Serikali wanateuliwa na Rais na kuapa kwa Rais.

Naona Wabunge wanaochaguliwa na wananchi wanaapa kwa Spika wa Bunge.

Swali sasa kwa nini majaji wateuliwe na Rais? Je kwa nini waape kwa Rais, wakati wapo kwenye Muhimili wa Mahakama?

Je huku si kusema kuwa ni Bunge pekee ambalo labda liko huru kidogo maana wabunge hawapaswi kuapa mbele ya Rais.?

Je, huku ni kusema kuwa Mahakama haiko huru maana Watendaji wake wanateuliwa na Rais na kuapa kwa Rais?

Nauliza tu waungwana maana hii inanichanganya?View attachment 1008124
Na nani anamwapisha Rais? Jibu ni Jaji Mkuu. Kwa hiyo ngoma sawa
 
Naomba nikujibu kwa msingi ya utawala na sio kisheria.
Tanzania kama ilivyo Marekani, Rais ana-play role ya mkuu wa nchi. Kwa kofia ya Ukuu wa nchi, anakua na madaraka ya kuteua na kuongoza kiapo cha utii kwa majaji.

Uingereza (The United Kingdom) majaji wanateuliwa na Malkia au Mfalime. Waziri mkuu (amabe ni mkuu wa serikali) anawajibika kumshauri Malkia nani wa kumteua akishirikiana na tume ya utumishi wa mahakama.

Ujerumani, jaji mkuu anakula kiapo mbela ya Rais wa Germany Federation (na sio Chancellor ambae ni mkuu wa serikali)

Israeli pia, majina ya majaji wanapendekezwa na tume ya kijaji (Judicial Nomination Committee). Anaewateua na Rais wa Israel ambae ni mkuu wa nchi.

Kwa kifupi sana, Tanzania, Rais kwa kofia yake ya Ukuu wa Nchi, katiba inampa nguvu ya kisheria na kiutawala kuchagua/kuteua majaji na kuwaongoza kula kiapo cha utii kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Niko tarari kukosolewa na kupata ufahamu zaidi toka kwa "wasomi na mawakili"
Kwa maelezo yako hayo yanadhihirisha kuwa rais wa nchi ndiye bosi wa majaji wote, na hivyo akiwapa maelekezo bila shaka watatumia kila wawezalo ili kuyatekeleza. Na hapo ndipo watu wanatia shaka ya kweli kabisa juu ya uhuru wa mahakama zetu hasa pale kesi itakapokuwa inayagusa maslahi ya utawala.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
alafu rais anaapa mbele ya jaji mkuu

1548853980300.png
 
Back
Top Bottom