Kwanini Mangungu lazima akae pembeni?

Kwanini Mangungu lazima akae pembeni?

inaonekana wewe kama sio mshirikina basi unaamini sana ushirikina.
Dunia nzima bila kujali taifa, dini wala bara inaamini kwenye ushirikina. Ushirikina ndio mtaji mkubwa wa viongozi wa dini duniani. Mafundisho na mahubiri yao yote ni kuhusu shetani, uchawi, husuda, mikosi, freemason, na majini zaidi kuliko Mungu. Uchawi na ushirikina ndio mtaji wao. Jamii zetu zote zinaamini kwenye uchawi na ushirikana; hebu fuatilia miziki, maigizo, filamu, ngoma na maisha ya watu duniani yote yanazunguukwa na uchawina ushirikina.

Siku imani ya uchawi, ushirikina na majini ikiisha kwenye vichwa vya watu utakuwa ndio mwisho wa dini zetu zote.
 
Mangungu yupo kuitumia Simba kama daraja la kupatia ubunge. Wanachama wenzetu waliomchagua huyu mtu wametukosea sana wana Simba.
Huyu ni mtu wa karibu sana na JK na tunajua kuwa JK ni mwana Yanga lialia na JK huyu ana ushawishi mkubwa ndani ya uongozi wa juu wa CCM,sasa kwa tamaa ya Mangungu kupata ubunge hashindwi kuiuza timu ili kufikia malengo na matamanio yake ya kisiasa.
 
Watu wanajitoa ufahamu tu, Simba majuzi kati alienda South Africa dhidi ya Orlanda Pirates na akaenda kuroga uwanjani kabla ya mechi wakati wa warm up, FIFA sijui CAF wakaitwanga faini Simba milioni takribani 20 au 40 kwa kitendo kile.

Simba na mambo ya ulozi huwezi kuvitenganisha toka uwanja ufanyiwe ukarabati, Simba wamekuwa hoi saana.
Mimi nayachukia na kuyadharau sana mambo ya uchawi kwenye mpira ni ushamba. Ila ukweli timu zote hizi mbili Simba na Yanga wanashiriki sana haya mambo,ni upuuzi na kujidhalilisha mbele ya dunia.
 
Basi nikuibie siri unamkumbuka yule sultan Mangungo wa msovera ambaye aliingia mikataba ya ulaghai na wazungu? Basi ni mpwa wake na huyo Sultan Mangungu wa simba AKA Mangungu bay na kichwa chake kile kama parachichi me ananiudhi
kwa kutumia uchawi wake aliwaaminisha wanasimba kuwa wakimpa uongozi ataifunga Yanga milele nje ndani. Hata wanasimba wanamjua kuwa Mangungu ni mchawi au anatoka kwenye familia ya kichawi au anawafahamu wachawi.
 
Mangungu ni Master Mind tu kufuatia u mbumbumbu wa mashabiki na Wana chama mfano kwenye mkutano mkuu wa klab kuletewa Manzoki n.k kwenye ushirikina Simba ni jadi Yao kabla ata Mangungu.
Alikuwepo Mwenyekiti wa Simba marehemu Amir Bamchawi, uyu jamaa kipindi Cha uongozi wake Alifanya ulozi wa kufuru mbaya, Si kumbuki kwa hivi karibuni kama Kuna Kiongozi aliye wahi kufikia au kukaribia uwezo wake wa kichawi/ fitina pale msimbazi.

Uyu jamaa kwenye fainali ya 1993 kabla mpira hauja anza alitangaza njia ambazo watapita na kombe lao ili kulifikisha pale klabuni msimbazi.
Bahati mbaya Kiongozi mwenzake alimzidi akili na timu ikapoteza mechi.

Uyu Amiri Bamchawi anaweza kuwa the Greatest of all time in witchcraft based on football pale Msimbazi.

Jamaa ilikua siku inayo cheza Simba na ikatokea mvua imenyesha kabla ya mechi basi mara nyingi Simba ilishinda na yeye ni kama mu asisi wa Simba na mvua.

Kule Angola wakati Simba inakwenda kucheza nusu fainali ya pili ya kombe la CAF/ Abiola cup, mvua ilikua haijawahi kunyesha kwenye eneo lile kwa miaka kadhaa lakini siku ya mechi ya Simba dhidi ya Petro Atletico Aviacao kule Angola mvua kubwa ili mwagika.
Simba ikapata suluhu ya bila goli na kutinga fainali.
Kumbuka mechi ya Awali pale shamba la bibi mechi ili Isha kwa ushindi wa Simba wa goli 3- 1
Yes mkuu upo sahihi sana. Bamchawi alikuwa habari nyingine.

Mechi ya Simba na Stella Abidjan hakuzidiwa ujanja na mtu yoyote ila yeye mwenyewe ndio ali ihujumu hiyo mechi baada ya kupewa mtee mkubwa na Kassim Dewji.


Alicho kifanya ni kutoa maelekezo kwa benchi la ufundi kwamba Simba wajikite zaidi kwenye dua, maombi na matambiko kuliko mazoezi.


Wiki yote kabla ya mechi ilikuwa ni duwa maombi ( ya kilokole)visomo na matambiko.

Siku moja kabla ya mechi timu ilikuwa zanzibar.


Kuanzia asubuhi hadi saa tisa usiku ilikuwa ni dua maombi visomo na matambiko wachezaji hakuna kupumzika.


Atakuja kiongozi anasema kuna sheikh anakuja kufanya dua, dua inafanyika masaa 4 mfululizo. Then baada ya kupumzika kama lisaa limoja analetwa mchungaji anapiga maombi masaa mawili then anakuja ostaz kisomo masaa manne then anakuja sangoma tambiko masaa ma5. Watu wamelala saa kumi alfajiri, Dar wameingia saa 6 mchana kwanini usifungwe.

Wachezaji wamecheza na usingizi na uchovu.
 
Mimi nayachukia na kuyadharau sana mambo ya uchawi kwenye mpira ni ushamba. Ila ukweli timu zote hizi mbili Simba na Yanga wanashiriki sana haya mambo,ni upuuzi na kujidhalilisha mbele ya dunia.
Uchawi kwenye mpira unasaidia kuboresha fikira na saikologia za wachezaji uwanjani ili kucheza kwa nguvu wakijua kuwa wanayo nguvu za ziada (uchawi). Uchawi ulisaidia kinjekitile kuwahamasisha watu wapigane na Mjerumani vita ya majimaji kwa kuwaaminisha kuwa risasi za adui zitageuka maji, lakini ukweli risasi hazikugeuka maji waliuawa wengi. Uchawi unaongeza morali ya wachezaji uwanjani, lakini ili ufanyekazi lazima upate wachezaji wanaoamini uchawi na timu pinzani inayoamini na kutegemea uchawi pia. Uchawi haufanyi kazi kama ukiwa na wachezaji na kocha wasioamini uchawi kwenye mpira.
 
ha
Yes mkuu upo sahihi sana. Bamchawi alikuwa habari nyingine.

Mechi ya Simba na Stella Abidjan hakuzidiwa ujanja na mtu yoyote ila yeye mwenyewe ndio ali ihujumu hiyo mechi baada ya kupewa mtee mkubwa na Kassim Dewji.


Alicho kifanya ni kutoa maelekezo kwa benchi la ufundi kwamba Simba wajikite zaidi kwenye dua, maombi na matambiko kuliko mazoezi.


Wiki yote kabla ya mechi ilikuwa ni duwa maombi ( ya kilokole)visomo na matambiko.

Siku moja kabla ya mechi timu ilikuwa zanzibar.


Kuanzia asubuhi hadi saa tisa usiku ilikuwa ni dua maombi visomo na matambiko wachezaji hakuna kupumzika.


Atakuja kiongozi anasema kuna sheikh anakuja kufanya dua, dua inafanyika masaa 4 mfululizo. Then baada ya kupumzika kama lisaa limoja analetwa mchungaji anapiga maombi masaa mawili then anakuja ostaz kisomo masaa manne then anakuja sangoma tambiko masaa ma5. Watu wamelala saa kumi alfajiri, Dar wameingia saa 6 mchana kwanini usifungwe.

Wachezaji wamecheza na usingizi na uchovu.
hahaha!!
 
Uchawi kwenye mpira unasaidia kuboresha fikira na saikologia za wachezaji uwanjani ili kucheza kwa nguvu wakijua kuwa wanayo nguvu za ziada (uchawi). Uchawi ulisaidia kinjekitile kuwahamasisha watu wapigane na Mjerumani vita ya majimaji kwa kuwaaminisha kuwa risasi za adui zitageuka maji, lakini ukweli risasi hazikugeuka maji waliuawa wengi. Uchawi unaongeza morali ya wachezaji uwanjani, lakini ili ufanyekazi lazima upate wachezaji wanaoamini uchawi na timu pinzani inayoamini na kutegemea uchawi pia. Uchawi haufanyi kazi kama ukiwa na wachezaji na kocha wasioamini uchawi kwenye mpira.
Mbona pamoja na hamasa ya uchawi bado wanakandwa? Haya mambo ni ya kupigwa vita kabisa,yanadumaza fikra.
 
Mangungu ni Master Mind tu kufuatia u mbumbumbu wa mashabiki na Wana chama mfano kwenye mkutano mkuu wa klab kuletewa Manzoki n.k kwenye ushirikina Simba ni jadi Yao kabla ata Mangungu.
Alikuwepo Mwenyekiti wa Simba marehemu Amir Bamchawi, uyu jamaa kipindi Cha uongozi wake Alifanya ulozi wa kufuru mbaya, Si kumbuki kwa hivi karibuni kama Kuna Kiongozi aliye wahi kufikia au kukaribia uwezo wake wa kichawi/ fitina pale msimbazi.

Uyu jamaa kwenye fainali ya 1993 kabla mpira hauja anza alitangaza njia ambazo watapita na kombe lao ili kulifikisha pale klabuni msimbazi.
Bahati mbaya Kiongozi mwenzake alimzidi akili na timu ikapoteza mechi.

Uyu Amiri Bamchawi anaweza kuwa the Greatest of all time in witchcraft based on football pale Msimbazi.

Jamaa ilikua siku inayo cheza Simba na ikatokea mvua imenyesha kabla ya mechi basi mara nyingi Simba ilishinda na yeye ni kama mu asisi wa Simba na mvua.

Kule Angola wakati Simba inakwenda kucheza nusu fainali ya pili ya kombe la CAF/ Abiola cup, mvua ilikua haijawahi kunyesha kwenye eneo lile kwa miaka kadhaa lakini siku ya mechi ya Simba dhidi ya Petro Atletico Aviacao kule Angola mvua kubwa ili mwagika.
Simba ikapata suluhu ya bila goli na kutinga fainali.
Kumbuka mechi ya Awali pale shamba la bibi mechi ili Isha kwa ushindi wa Simba wa goli 3- 1
Sawa tumekuelewa haya tuelezee kwa nini yanga kwenye derby iliyopita walipita mlango usio rasmi na mlimwaga maji uwanjani mkiongozwa na moloko pamoja na kocha wenu kiufupi hakuna team inayoshiriki league kuu Tanzania bara ambayo haifanyi uchawi .
 
Sawa tumekuelewa haya tuelezee kwa nini yanga kwenye derby iliyopita walipita mlango usio rasmi na mlimwaga maji uwanjani mkiongozwa na moloko pamoja na kocha wenu kiufupi hakuna team inayoshiriki league kuu Tanzania bara ambayo haifanyi uchawi .
Hilo hawezi kulisema Ila ingekuwa Simba angeanzisha thread Hadi 10
 
Mbona pamoja na hamasa ya uchawi bado wanakandwa? Haya mambo ni ya kupigwa vita kabisa,yanadumaza fikra.
Uchawi ni kucheza na saikolojia ya wachezaji wakiwa uwanjani, hakuna jipya. Kule ulaya na kwingineko walikopiga maendeleo ya kielimu nafasi ya uchawi na waganga imechukuliwa na psychologists, psychoanalysts na counselors, sisi hatuna watu hao badala yake jamii inawategea zaidi waganga wa jadi, wachungaji na mesheikh kutibu shida ya psychological. Na kama mtu atapiga marufuku waganga wa kienyeji idadi ya vichaa itaongezeka kwenye jamii. Kumbuka kuwa mganga wa kienyeji aliweza kuwaingiza wamatumbi kwenye vita na wajerumani wenye silaha za kisasa kabisa wakati wao wakiwa na mikuki na mapanga tu.

Mchawi/mganga anaweza kumuaminisha John Bocco, Shabalala, Kapombe, Saido, Mzamiru (wazee) na timu nzima ya simba kuwa wanaweza kuifunga Yanga, Al-Ahly, Barcelona na timu nyingingine zenye wachezaji vijana na wenye kocha mahili. Kwakutumia imani hiyo wanaweza ku fluke na kupata matokeo kwenye baadhi ya mechi na kuwachanga wafanya maamuzi kuhusu kuwaacha au kuwaongezea mpira kutokana na fluke zao uwanjani zinazotokana na jitihada na nguvu za mganga. Kwakiongozi na kocha anaeamini kwenye sayansi hawezi kufanyakazi kwa fluke bali ataangalia uwezo wa mchezaji unaotokana na umri wake, mazoezi na juhudi za uwanjani. Atafukuzia mbali wachezaji waliozidi miaka 30+ na kuwabakisha wachache tu kama mbegu (nahodha) ya generation mpya ya wachezaji wasioijua falsafa na tabia (culture) ya timu.
 
Hivi nyie timu yenu unabadilisha uwanja wa kuingia, kuloga uwanjani mnaacha kuwajadili viongozi wenu wanaamini uchawi unarukia timu nyingine. Aliyesema huko wenye akili ni wawili hakukosea.
Aliekasema maneno ya wenye akili ni wawili ni mwanasimba mwenzenu manara wakati huo ni afisa habari wa simba sasa ajabu ni ipi hapo?lingekuwa jambo la kutisha endapo maneno hayo kayaongea mwana yanga
 
Badala ya kujadili timu lenu kuhusu mechi ijayo mnakaza mafuvu kwenye jambo lingine ndo maana mkapigwa 0-3 wiki 3 zote kusherekea goli 5 mkasahau mechi inayokuja

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi nilifurahi mno tulivyompiga simba 5 ila haikutakiwa tulikuze sana lile swala kiasi kile tukasahau kuwa tunashiriki mashindano muhimu mno nugazi alikuwa mtu smart sana kuliko huyu ali kamwe
 
Mimi nilifurahi mno tulivyompiga simba 5 ila haikutakiwa tulikuze sana lile swala kiasi kile tukasahau kuwa tunashiriki mashindano muhimu mno nugazi alikuwa mtu smart sana kuliko huyu ali kamwe
Mkuu ndo inavokuwaga, sidhani kwa zile sherehe kama waliifuatilia belouizdad jinsi wanavyocheza,na kujiona bora ...hata hiyo ya kujisahau inatokeaga sana Simba na timu zote kubwa. Nakuambia huu ushindi unaweza kuathiri hii hatua ya makundi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa tumekuelewa haya tuelezee kwa nini yanga kwenye derby iliyopita walipita mlango usio rasmi na mlimwaga maji uwanjani mkiongozwa na moloko pamoja na kocha wenu kiufupi hakuna team inayoshiriki league kuu Tanzania bara ambayo haifanyi uchawi .
Timu zote zinauamini uchawi kuwa upo kwenye jamii; Dini zote na vitabu vitakatifu vinasema hivyo; tamaduni zetu na mila zetu zinasema hivyo na tumekuzwa hivyo kwa kuaminishwa kuwa uchawi upo. baada ya simba kuwasha moto kwenye uwanja wa Orlando pirates na kuthibitishwa na CAF (evidence based) basi hakuna timu inayoiondolea simba uwezekano wa ulozi viwanjani (evidence based). Ndio maana timu nyingi za ligi kuu hivi sasa ziko tayari zipigwe faini lakini zisipitie mlango wa kaida dhidi ya mechi na simba.
 
Mkuu ndo inavokuwaga, sidhani kwa zile sherehe kama waliifuatilia belouizdad jinsi wanavyocheza,na kujiona bora ...hata hiyo ya kujisahau inatokeaga sana Simba na timu zote kubwa. Nakuambia huu ushindi unaweza kuathiri hii hatua ya makundi

Sent using Jamii Forums mobile app
Nikweli kumfunga mtani kuna raha zake ila jambo lilikuzwa mno mpaka ikawa kero hivi umechukua ubingwa wa ligi kuu mara 2 mfululizo halafu ushinde 5 usherehekee mwezi mzima kweli?umecheza final ya shirikisho halafu kwenye ligi ya mabingwa sawa uliweka lengo uishie makundi ila je ukiburuza mkia kwenye kundi napo sio fedheha? Tuna vijana wa ovyo mno kwenye yanga hasa huyu mpuuzi anaitwa alikamwe na privaldinho
 
Mkuu ndo inavokuwaga, sidhani kwa zile sherehe kama waliifuatilia belouizdad jinsi wanavyocheza,na kujiona bora ...hata hiyo ya kujisahau inatokeaga sana Simba na timu zote kubwa. Nakuambia huu ushindi unaweza kuathiri hii hatua ya makundi

Sent using Jamii Forums mobile app
CRB haikuwa na mchezaji hata mmoja kwenye timu yao ya taifa, wote walikuwa na fresh legs. Yanga kaka wachezaji wao wengi walitumika kwenye timu zao za taifa, walifika pale kwa makundi dakika za majeruhi kuweza kufanya recovery ya maana. Ndio maana wanayanga wako comfortable pamoja na matokeo ya 3-0. Tatizo labda litaanzia kwa matokeo na al-ahly. Kama ni lawama labda zimwendee gamondi kwa kushindwa kuwapanga wachezaji waliokuwa na fresh legs kama akina Fred Gift, Mauya, skudu, mkude, na wengine ambao wanalipwa mishahara Yanga pia na kuendele kuchezesha walewale wenye uchovu na maumivu madomadogo.

Simba watulie tu huu ni upepo wa kawaida kwenye mpira, hata man u na chelsea wanapitia njia hii ya msalaba kwa miaka mingi sasa, Liverpool walipitia njia hii ya gologota pia, simba ni nani kutoka mapovu hivi? Mangungu Mangungu, try again try again. Shida kubwa ni usajili mbovu na ushirikina. Onana kweli ni mchezaji wa kuichezea simba? ni kweli ngoma kaibiwa airport?

View: https://www.youtube.com/watch?v=_Rrrw9aEtUY
 
Aliekasema maneno ya wenye akili ni wawili ni mwanasimba mwenzenu manara wakati huo ni afisa habari wa simba sasa ajabu ni ipi hapo?lingekuwa jambo la kutisha endapo maneno hayo kayaongea mwana yanga
Manara yupo yanga na Kama mlimpokea mkijua ni mwanasimba inaonyesha jinsi gani alikuwa sahihi asilimia 100
 
Back
Top Bottom