Kwanini matumizi ya Mbolea za Kisasa katika nchi za Afrika ni lazima ikiwa nchi za Ulaya wanatumia Samadi?

Kwanini matumizi ya Mbolea za Kisasa katika nchi za Afrika ni lazima ikiwa nchi za Ulaya wanatumia Samadi?

Nimefanya utafiti katika kuongeza ufahamu kwenye mashamba ya vyakula na mazao mbalimbali yalimwayo na wazungu kitu nilicho gundua wao asilimia 100% wanatumia mborea ya samadi kutoka kwenye kinyesi cha ng'ombe,farasi na miti,pia na mabaki ya taka za majumbani hawatumii mborea za kutengeneza maabara je kwa nini sisi weusi watu wetu wanalazimishwa kutumia mborea za kutengenezwa kutoka maabala hii imekaaje ? wasomi mnao elewa mambo embu mtupe elimu katika hili asanteni
Wacha uongo kiongozi! Hebu soma hapa chini!
Screenshot_20240824-034016_Chrome.jpg
 
Hiyo ni biashara endelevu, ni kama mtu akianza kutumia ARV baada ya miezi kadhaa hawezi kuacha sababu Kinga asili zinapotea mwili unaanza kutegemea ARV's(Topic nyingine), tukirudi kwenye mbolea, hizo mbolea za viwandani kuna kitu zinafanya kwenye ardhi zetu taratibu, baada ya muda fulani bila hizo mbolea ardhi yetu itakuwa haistawishi mazao, hadi uweke hizo mbolea artificial.
Si taratibu, zikishatumika mara 1 tu basi hakuna zao lolote litalostawi wala kuota bila ya hizo mbolea artificial na hapo ndipo ujue wapi dunia ilipofikia.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Sio lazima kutumia mbolea za kisasa, unaweza kuendelea kutumia samadi.
 
Mkuu wakati tukijadili haya, wanaoyaanzisha hawalali pia. Wameweza kufanikiwa sababu sehemu kubwa ya viongozi ni vibaraka. Miaka ya nyuma kulikuwa na kuku wa wiki 3 anachinjwa!?,zile tikiti za kijani zilienda wapi!?,hujagundua sokoni Sasa hivi Kuna nyanya chungu kubwa kama ngumi na hazina siku nyingi!?,pilipili mwendokasi ukiikata ni kama teargas zilikuwepo!?,mifamo ni mingi sana,tunabadilishwa vitu taratibu, watu wapo maabara wanatengeneza mbegu za mchongo. Bahati mbaya sana wasomi wetu wa kilimo wamesinzia.
Acha kuwaonea wataalamu wa kilimo.Ni msomi yupi nchi hii mwenye nguvu kukiko wanasiasa? Nchi hii ujifanya mjuaji na kupinga maamuzi ya wanasiasa utaishia kutekwa. Ndio maana watu wanaangalia tu bora liende
 
Samadi ni kwa wakulima maskini au wale wa hobby tuu, hakuna serious commercial farming inayotumia samadi, bila modern agricultural machineries na mbolea za nitrogen wote mngekuwa mmekufa na njaa nyie, huo mchele mnaokula, ngano, sukari, mafuta etc 90% tunaagiza, mnafikiri vinalimwa na samadi? hata wakulima wetu wakiacha kutumia mbolea za viwandani watu watakufa njaa, Tanzania tunaagiza chakula kuliko mafuta ya petrol na sababu kubwa ni umaskini wa kutumia vitu kama samadi
 
Hawatumii mbolea za kutengeneza maabara, je, kwanini sisi weusi watu wetu wanalazimishwa kutumia mbolea za kutengenezwa kutoka maabara?

Wasomi mnao elewa mambo embu mtupe elimu katika hili, asanteni.
Hata vyakula kwenye mahoteli makubwa wako selective sana, nilishuhudia wakikataa kula kuku na beef wakisema zime tritiwa na madawa
 
Back
Top Bottom