Kwanini Mungu anaitwa Mungu na hakuitwa jina lingine? Kama Shetani ni mharibifu kwanini aliachwa hai?

Majina na sifa hubadilika kulingana na mahali na mahitaji ya nyakati lakini kiasili kitu ama mtu ni yuleyule
Wewe jina lako na hapa na jina lako asilia haliondoi uhalisia wako

Wewe kama baba fulani
Wewe kwa jina la cheo chako
Wewe kwa jina la ubin wako nk nk

Nini kinafanya mti uitwe mti?
Ni mizizi yake?
Ni matawi yake?
Ni shina lake?
 
kwanini naye aliitwa YESU, na katika biblia YESU anajina jingine anaitwa EMMANUEL yaani MUNGU MWENYE NGUVU,why JESUS
1. Kristo ni mrithi wa hili jina
Waebrania 1:1-4
Imeandikwa hivi:
“Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. Yeye kwa kuwa ni mng'ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu; amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao.”
Kwa mistari hii ya mwanzo ya waraka wa waebrania tunaona ya kuwa Yesu Kristoamewekwa na Mungu Baba yake “kuwa mrithi wa yote”. Na katika mambo aliyopewa kuyarithi ni pamoja na JINA HILI LA YESU – NDIYO maana imeandikwa “amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao” (waebrania 1:4)
Kwa hiyo ni wazi kwamba huyu mwana wa Mungu alipewa jina hili la Yesu kwa kuwa yeye MRITHI WA YOTE ya Baba yetu mungu aliye mbinguni
................................
...............................................
........................................................
Unaweza ukawa unajiuliza inakuwaje jambo hili. Lakini kabla ya kuendelea kusita, nadhani utakubaliana na mimi ya kuwa mtu hawezi kurithi kitu chake, bali anarithi kitu kisicho chake. Pia, mtu hawezi kurithi Jina Lake, bali anarithi jina lisili lake. Kwa hiyo biblia inapotuambia ya kuwa Baba amempa Mwana wake urithi wa Jina lake, ina maana ya kuwa hapo mwanzo jina la Yesu lilikuwa ni la Mungu Baba hadi alipoamua kumpa jina hilo motto wake kama sehemu ya urithi wake! Ndiyo maana yesu Kristo alisema, “
Kwa maneno mengine alitaka tujue ya kuwa jina la Yesu Kristo si “jina lake mwenyewe.” Lingekuwa “jina lake mwenyewe” angepokelewa, lakini kwa kuwa jina la Yesu Kristo alilokuja nalo ulimwenguni ni “jina la Baba yake” hawakumpokea.
Nadhani sasa unaweza ukaelewa kwa nini ina hili la Yesu Kristo linaitwa ni jina lipitalo majianyote mbinguni, duniani na hata chini ya nchi (wafilipi 2:9-10). Jina la Yesu Kristo ni jina lipitalo kila jina kwa kuwa ndilo jina la Mungu Baba pia. Mungu Baba angekuwa na jina jingine kuliko hili, biblia isingesema hata mbinguni jina la Yesu Kristo liko juu ya majina yote.
 
Watakwambia aliachwa kwa makusudi.

Kuna wasabato humu ungewapa tag wangekupa vifungu hadi ukasema inatosha. Na atheist pia wapo na wana hoja
Nimeshakaa na wasabato,na mashahidi wa Yehova macho kwa macho,uso kwa uso,hoja kwa hoja,hawakuweza kunijibu,kwakuwa mipaka yao ipo katika maandiko ambayo ndio mwisho na mpaka wao wa kufikiri,uwezo wa mwisho wa kufikiri wa binadamu umetiwa mipaka na maandiko.
 
uwezo wao unalingana, na wote waliumbwa na muumba mmoja, ndio maana shetani anauwezo mkubwa ata wa kuumba pia kiumbe chake na kinaishi milele sio kama Mungu anaumba mtu hasiyeishi milele anakufa.

HAWA NI MARAFIKI ILA WANATUCHORA TU, HAUWEZI KUZUNGUMZA NA ADUI YAKO, MUNGU ANAZUNGUMZA NA SHETANI.
 
Ukitazama kwa umakini utaona huyu mwana ni YESU,nayeitwa KRISTO anayeitwa EMMANUEL,mtu moja majina matatu ,amazing,lakini ukirudi katika MUNGU ni MUNGU tu hata ukirudi katika triinity utakuta ni MUNGU baba,Mungu Mwana,na Mungu Roho MTAKATIFU,Go deep Mwana anamajina halisi halali mengine,BABA nimeona ni hili Mungu na Roho mtakatifu ni hivyo hivyo,kwanini yeye ni hivyo hivyo MUNGU?
 
Jina lake halibadiliki kinachobadilika ni sifa tu kupitia jina lilelile kwa upande wa MUNGU,hii inaweza ikalingana na MTI jinsa ni MTI tu sifa pee hubadirika kama Mti wa Muembe,Mti wa machungwa Mti wa mpapai,nk,ipo sababu ya msingi ambayo MTI ulibatizwa jina hilo na sio GARI,,ni gani?
 
YWHN ndilo jina kuu zaidi
 
hilo ni suala la maana katika lugha husika,ukirudi katika uhalisia wa kuitwa hivyo na tukawa na tafsiri hiyo moja,yaani MUNGU mbaye ni GOD,ambaye ni SEBA nk,ningesemabasi kwanini LIITWA SEBA na sio ELIA,ndio hoja yangu
Hata angeitwa ELIA ungesema tena kwanini Elia na sio Seba.

Kwanini kiti kinaitwa kiti na sio Njubu?
 
Yote katika yote aidha alifeli au la ila tayari upo chini ya mamlaka yake. Hapo ulipo ningekuuliza " je unavyoona baba yako angefaa kuwa baba yako kwa jinsi alivyokulea?" pengine ungesema hapana...umezaliwa Afrika ila je ungelipewa nafasi ya kuchagua wapi ungependa uzaliwe pengine usingechagua Afrika ila pamoja na utashi wako ndo imekuwa ivo kutopendelea familia, nchi au bara ulipo ila tayari ishakuwa hivyo...hata dini pengine usingependa kujua chochote kuhusu dini yoyote au mfumo wowote wa maadili ila tayari upo ndani ya mifumo...you are already in the matrix, you can not change anything within. So kama upo ndani ya matrix tayari aidha sasa ukubaliane na mfumo au uupinge but are you powerfull enought to turn around your world?.... If you can not fight them, join them... jiunge na Mungu tu hata kama ka fail coz kutambua failure ya Mungu hakutakuepusha na demands zake juu yako.
 
Wewe kwanini uitwe majina uliyonayo na si mengine ni ipi?
 
MshA
M
MShana kwema Mzee
 
Mungu si Jina lake bali ni Title kama vile Rais ni Title, lakini tumepata Marais wenye majina tofauti. Rais wa sasa anaitwa Samia. Na vile vile Kuna Marais wengi ambao siyo Marais wa kweli wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; mfano Rais wa Chama Cha Wanasheria TLS (kwa sasa ni Sungusya).
The same applies for the Bible, for the Bible says there are many gods on earth (1 Corinthians 8:5) the Bible goes further to call Satan the god of this world (2 Corinthians 4:4). But the true God is only one Jehovah - Exodus 6:2&3 (Kutoka 6:2&3) hilo ndilo Jina alilomwambia mtumishi wake Moses. Na pia Yesu alipokuwa hapa Duniani alihakikisha anawaambia wanafunzi wake Jina hilo ( John 17:6&26)
Kulijua na kulitumia Jina hilo wewe binafsi wakati unasali kutakusaidia uokoke (Rom 10:13)
 
Unatumia kipimo gani kujua kichwa chenye ubongo wenye/usio na akili,tena kupitia maandishi tu?
 
Waarabu na Wazungu hakuna kitu walipatia Africa kama kuleta dini zao,
Ni vurugu mechi ambazo sio rahisi kuzishinda.
Wafia DINI ni watu wenye matatizo ya akili waliochangamka
 
Ahsante sana mkuu kwa detailed answer. Nimejifunza zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…