Kwanini nchi nyingi za Afrika wanatumia lugha za wakoloni kama lugha za taifa, hivi hawaoni aibu?

Kwanini nchi nyingi za Afrika wanatumia lugha za wakoloni kama lugha za taifa, hivi hawaoni aibu?

Kutumia lugha ya mkoloni kwa shughuli mbali mbali hasa zisizoepukika kwa sasa, mfano masomo ya sayansi, sioni kama ni shida sana.

Shida yangu ni lugha ya mkoloni kufanywa kuwa ndio lugha ya taifa na inatumika mtaani hadi na wauza nyanya, ambao wangezweza kutumia lugha yao wenyewe kwenye masuala kama hayo.

Niwapongeze Kenya kwa kukifanya kiswahili kuwa lugha ya taifa lao, sina hakika juu ya Uganda,DRC kama wanampango juu ya kufanya kiswahili lugha ya mataifa yao. Bila kuisahau mikoa ya kaskazini magharibi mwa Tz, ya Rwanda na Burundi.

Hebu oneni hata aibu jamani, seriously..
.........Wewe unaishi kwa kutumia kila kitu kilichotoka kwa wakoloni, huoni aibu?
 
mkoloni gan ww !! kuna mkoloni alikua naongea kiswahili zaidi ya wafanya biashara wa asia n wabantu??
Hahahahaaaa!!! Sijui unaelewa nini kuhusu lugha, hususan ya Kiswahili. Lakini ni dhahiri shahiri kwamba umechelewa sana kaka. Mpaka leo kuna wamissionari wa kizungu wanaongea kiswahili zaidi ya wasukuma wa kibantu. Tena lahaja yake imenyooka zaidi ya wabantu wote wa Kariakoo. Hahahahaaaa!!
 
Nadhani hakuna aliyebisha juu ya uliyoyaandika. Sasa nenda uingereza halafu zungumza kiswahili, maana kwa maelezo yako wao ndio wamekitunga. Halafu tupe mrejesho.
Kiingereza ni kiswahili cha dunia. Hakuna namna ya kukikwepa. Ukiondoka nje ya mipaka ya Tanzania [emoji1241], kiswahili hakina thamani yoyote.

Tujivunie kiswahili tukiwa humuhumu mwetu. Siyo zaidi
 
Sio kweli kiswahili hakina asili ya uarabuni Bali kina asili ya mwambao ilikua lugha ya biashara ambayo iliweza kuunganisha watu wengi wafanyabiashara wa utumwa, pembe za ndovu n k walikua wanatumia kiswahili kwenye kuwasiliana

Mjeruman ndo alikipa kipaumbele sana kipindi Cha utawala wake sababu alivutiwa na jinsi ilivyokua inaunganisha watu,
Maneno mengi ya kiswahili asili ni Bantus+Hindus+Arabs
 
Tunawekana sawa tu. Hata kiswahili chenyewe aliyekirasimisha ni mkoloni. Yeye ndiyo alikitoa kwenye alphabeti za kiarabu na kukileta kwenye a, e, i, o,u na konsonati. Yeye ndiye alikinyambua na kutengenezea aina saba za maneno.....sijui nomino, vidamshi, vihangaya etc. Mkoloni alikopy kutoka kiingereza "seven parts of speech". Na alihakikisha makosa yaliyotokea kwenye kiinngereza, hayajirudii kwenye kiswahili. Mojawapo ya kosa kubwa la Engish waliloepuka ni neno kuandikwa tofauti na kutamkwa tofauti. Mfano, unaandika 'road' unatamka 'rod'. Huu ujinga waliufuta kwenye kiswahili. Ndiyo maana mzungu akija leo unaweza ukamuandikia kiswahili akakisoma utadhani anajua kitu. Wakoloni walikipanga kiswahili bana. Wale wa lingua nadhani tunaelewana.
Ni moja ya lugha zinazofundishika kiundani. Luhga nyingi ukiondoa ya malkia na baadhi ya luhga za ulaya, ukianza kujifunza unaanza na irabu kama siyo consonati then unaanza kutiririka na maneno. Huwezi kuzama deep kama kiswahili mpaka kwenye ma-adjustebo na ma-molankoyi huko.
Mkoloni ndiyo alikiunda kiswahili ili kifundishike. Na alianza kukifundisha upya. Na kwa wamatumbi ilikuwa ni lugha mpya. Kwenye kuandika ndiyo walianza kujifunza upya kabisaaaa, kama wameletewa kichina. Kumbuka kiswahili cha mwanzo kwenye maandishi kilitumia alphabeti za kiarabu.
Na kwa taarifa tu, wajumbe wa baraza la kiswahili kutoka Congo. Walijitoa kwenye baraza la kiswahili la Afrika mashariki na kati baada ya Shaban Robert kuchaguliwa kuwa mjumbe wa baraza la kiswahili. Na huo ndio ulikuwa mwanzo wa kiswahili kulegalega fasi ya Congo. Ikumbukwe kuwa baraza la kiswahili enzi za mkoloni lilikuwa na wazungu watupu, hasa makasisi wa kimisionari. Wawakilishi wa kutoka Congo hawakuamini kama mtu mweusi anaweza kuwa mtaalamu wa kiswahili, hivyo walipinga uteuzi wa Shaban Robert na wakajitoa.
Mafather wa kimissionari ndio waliandika hizi kamusi zote za kiswahili. Kiufupi wao ndio walizitunga. Na kiswahili kilitengenezwa, kilisimamiwa na mkoloni mpaka kikakaza na kikasimama. Mkoloni alikuwa anaenda kufuta mpaka lahaja zote na kubaki na moko. Toka Lamu mpaka Kampala kiswahili ni lahaja moja tu, sikumbuki alichagua lahaja ipi, ila alitaka akomae na lahaja moja tu. Na mkoloni angeweza coz alishaweza.
Kwakusema hayo basi, itoshe kusema 'ajabu ya mvita kuota mvinde'. Hichi kiswhili tunachojipigia upatu leo.....ni zao halali la mkoloni. Na nachelea kusema mnyonge myongeni laki credit zake tumpe.

Wakatabahu
Infopaedia.
Kongole kwa kutoa madini ila wangeacha alphabet za kiarabu ingekuwa unyama sana.
 
Saizi wataanza kusoma Kiswahili👇

Screenshot_20220211-190658.png
 
Safi sana, kama mimi nikivyomwambia jamaa anianbie ni waingereza wangapi huko UK wanazungumza kiswahili, maana alitaka kudai wao ndio wamekipangilia na wanahaki nacho [emoji23][emoji23]
Wapo wanaoongea, halafu Waingereza walitawala Dunia nzima, So Afrika Mashariki ilikuwa sehemu ndogo sana ya dola yao, na Kiswahili hakiwezi kufahamika kwa wengi UK ila kinafahamika

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
 
Wapo wanaoongea, halafu Waingereza walitawala Dunia nzima, So Afrika Mashariki ilikuwa sehemu ndogo sana ya dola yao, na Kiswahili hakiwezi kufahamika kwa wengi UK ila kinafahamika

Sent from my TECNO KC6 using JamiiForums mobile app
Sijasema hawapo wanaoongea, lakini kwa wanaodaiwa kukimiliki nilitegemea 99% wawe wanakiongea 🤷🏽‍♂️
 
Kongole kwa kutoa madini ila wangeacha alphabet za kiarabu ingekuwa unyama sana.
Yah!! Ingekuwa unyama ila sidhani kama kingeendelea kama kilivyoendelea sasa. Muarabu
Kongole kwa kutoa madini ila wangeacha alphabet za kiarabu ingekuwa unyama sana.
Asante sana mkuu. Unyama ungekuwa mwingi sana kaka. Ila tatizo kiswahili kisingekuwa kikubwa na hadhi kama iliyokuwa nayo leo. Na lunga nyingi za kaliba ya kiswahili mara zote zillishia kupotea.
Unajua lunga ni sauti za nasibu. Lakini kuitanua lugha na kuikuza si nasibu tena. Ni suala linalohitaji utashi wa kisiasa, madaraka na bajeti. Ndipo lugha inapopata hadhi na kuwa jabali. Pia kuitanua lugha inahitaji utaalamu na usimamizi. Najaribu kusema haya ili tuelewe safari kilikotoka kiswahili na kilivyofika hapa.
Post yangu ya kwanza, nimejaribu kumpa picha ya Kiswahili mtoa mada, ili aone hadhi ya leo ya kiswahili ni juhudi za jana za mkoloni, lakini ameamua kushupaza shingo. Hadhi ya kiswahili ndio ilimpa wazo la kudhani kiswahili chaweza kuwa lugha ya kimataifa. Credit ya hadhi hiyo ni ya mkoloni.
Tuachane na hilo, tuje kwanini mkoloni aliamuwa kubadili kiswahili toka herufi za kiarabu. Mkoloni alikuwa na plani yake mkononi na maono yake kichwani. Wakoloni wa kimisionari walitafuta lugha ambayo ingewafaa kueneza habari njema za Yesu. (na kweli, concept ya lugha iliwalipa sana. Kazi waliyoipiga ndani ya muda mfupi utadhani walifika Tanzania miaka 3,000 iliyopita). Waliona kutumia kiingereza ingewachukua muda sana. Au kilatini ndiyo mambo yangekwama kabisaaaa. Tukumbuke kwenye habari njema enzi hizo Kilatini ndiyo ilikuwa habari ya mjini kati. Waliona Kiswahili kina ubantu mwingi na kubwa zaidi hakina asili ya jamii yoyote ya Kitanzania. Lugha yenye asili ya jamii fulani ingesababisha upinzani wakati wa kueneza habari njema kwa jamii nyingine. (Pata picha ya hiyo vita, wachaga wameletewa injili kwa kihaya.......mi sipati hiyo picha). Kiswahili kikaonekana ndiyo lugha pekee inayokidhi vigezo vikubwa. Mambo mengine ya kiswahili mkoloni wa kimisheni aliona ni madogo madogo na yanarekebishika. Utaalamu wanao, madaraka ya mkoloni ni yao, fungu wanalo.....basi wamisheni wakaingia mzigoni kwa mara ya pili. Nasema mara ya pili sababu mzigo ulishaanza. Mzigo wa mara ya kwanza ulikuwa ni utafiti huo nilioelezea hapo juu. Utafiti wa kujua ni lugha ipi itawafaa.
Basi wakakichukua kiswahili. Kwanza wakaona kiswahili kwa upande wa maandishi, alfabeti za kiarabu hazifai. Kulingana na scope yao na mahusiano ya kibantu na kiarabu, waliona haiwezekani. Pia nadhani hawakuwa na utaalamu mwingi wa hizo arabic alfabeti japokuwa pia walitoa sababu za kifonetiki na muundo. Ndio maana hata kwenye alfabeti za kirumi hawakutumia Q na X kwenye kuunda maandishi ya kiswahili.
Mkoloni alikisimamia na kukitanua sana kiswahili. Kazi mojawapo ya Baraza la kiswahili la mkoloni ilikuwa ni kuunda misamiati na istilahi. Nadhani kiswahili ndiyo lugha iliyotanuka zaidi katika fani za sayansi na ujuzi mwingine ukilinganisha na lugha nyingine za barani Afrika. Ni uzembe wetu tu hatukuweza kukiendeleza kiswahili baada ya kuachiwa usukani. Kuna istilahi nyingi sana za kisayansi zimeshapotea na zinaendelea kupotea . Kwa scope ya mkoloni kiswahili kingekuwa ni lugha inayotumika kufundishia mpaka chuo kikuu. Pamoja na dini, mkoloni pia alihitaji nguvukazi yenye weledi.
Kuna watu wanasema kiswahili hakifai kufundishia elimu ya juu sababu hakijitoshelezi kwa misamiati na istilahi. Huo ni uongo mkubwa. Neno kama barakoa lilikuwa limeshapotea kama siyo Uviko kuja kulihuisha tena. Neno kama mpinimwendo=crank shaft halipo tena. Na kuna mengi mengine ya nyanja anuwai tukisema tuanze kuyakusanya hapa jamvini tuta-terminology za kila tasnia.
Istilahi zipo nyingi sana ila wenye nafasi ya kutoa maamuzi kuhusu kiswahili nao hawajui kiswahili. Tatizo la nchi zetu hizi, ukiwa kiongozi basi unajihisi unajua kila kitu. Na sisi hata kiongozi akiongea shombo hupigiwa makofi na vifijo. Kiswahili ni kipana kinahitaji utashi wa kisiasa na kimamlaka kiwe lugha ya Afrika. Mandeleo yote ya kiswahili leo hayakuja kwa nasibu, ni juhudi za watawala wa kikoloni. Tena kiswahili kimerudi nyuma sanasana baada ya mkoloni kuondoka.
 
Yah!! Ingekuwa unyama ila sidhani kama kingeendelea kama kilivyoendelea sasa. Muarabu

Asante sana mkuu. Unyama ungekuwa mwingi sana kaka. Ila tatizo kiswahili kisingekuwa kikubwa na hadhi kama iliyokuwa nayo leo. Na lunga nyingi za kaliba ya kiswahili mara zote zillishia kupotea.
Unajua lunga ni sauti za nasibu. Lakini kuitanua lugha na kuikuza si nasibu tena. Ni suala linalohitaji utashi wa kisiasa, madaraka na bajeti. Ndipo lugha inapopata hadhi na kuwa jabali. Pia kuitanua lugha inahitaji utaalamu na usimamizi. Najaribu kusema haya ili tuelewe safari kilikotoka kiswahili na kilivyofika hapa.
Post yangu ya kwanza, nimejaribu kumpa picha ya Kiswahili mtoa mada, ili aone hadhi ya leo ya kiswahili ni juhudi za jana za mkoloni, lakini ameamua kushupaza shingo. Hadhi ya kiswahili ndio ilimpa wazo la kudhani kiswahili chaweza kuwa lugha ya kimataifa. Credit ya hadhi hiyo ni ya mkoloni.
Tuachane na hilo, tuje kwanini mkoloni aliamuwa kubadili kiswahili toka herufi za kiarabu. Mkoloni alikuwa na plani yake mkononi na maono yake kichwani. Wakoloni wa kimisionari walitafuta lugha ambayo ingewafaa kueneza habari njema za Yesu. (na kweli, concept ya lugha iliwalipa sana. Kazi waliyoipiga ndani ya muda mfupi utadhani walifika Tanzania miaka 3,000 iliyopita). Waliona kutumia kiingereza ingewachukua muda sana. Au kilatini ndiyo mambo yangekwama kabisaaaa. Tukumbuke kwenye habari njema enzi hizo Kilatini ndiyo ilikuwa habari ya mjini kati. Waliona Kiswahili kina ubantu mwingi na kubwa zaidi hakina asili ya jamii yoyote ya Kitanzania. Lugha yenye asili ya jamii fulani ingesababisha upinzani wakati wa kueneza habari njema kwa jamii nyingine. (Pata picha ya hiyo vita, wachaga wameletewa injili kwa kihaya.......mi sipati hiyo picha). Kiswahili kikaonekana ndiyo lugha pekee inayokidhi vigezo vikubwa. Mambo mengine ya kiswahili mkoloni wa kimisheni aliona ni madogo madogo na yanarekebishika. Utaalamu wanao, madaraka ya mkoloni ni yao, fungu wanalo.....basi wamisheni wakaingia mzigoni kwa mara ya pili. Nasema mara ya pili sababu mzigo ulishaanza. Mzigo wa mara ya kwanza ulikuwa ni utafiti huo nilioelezea hapo juu. Utafiti wa kujua ni lugha ipi itawafaa.
Basi wakakichukua kiswahili. Kwanza wakaona kiswahili kwa upande wa maandishi, alfabeti za kiarabu hazifai. Kulingana na scope yao na mahusiano ya kibantu na kiarabu, waliona haiwezekani. Pia nadhani hawakuwa na utaalamu mwingi wa hizo arabic alfabeti japokuwa pia walitoa sababu za kifonetiki na muundo. Ndio maana hata kwenye alfabeti za kirumi hawakutumia Q na X kwenye kuunda maandishi ya kiswahili.
Mkoloni alikisimamia na kukitanua sana kiswahili. Kazi mojawapo ya Baraza la kiswahili la mkoloni ilikuwa ni kuunda misamiati na istilahi. Nadhani kiswahili ndiyo lugha iliyotanuka zaidi katika fani za sayansi na ujuzi mwingine ukilinganisha na lugha nyingine za barani Afrika. Ni uzembe wetu tu hatukuweza kukiendeleza kiswahili baada ya kuachiwa usukani. Kuna istilahi nyingi sana za kisayansi zimeshapotea na zinaendelea kupotea . Kwa scope ya mkoloni kiswahili kingekuwa ni lugha inayotumika kufundishia mpaka chuo kikuu. Pamoja na dini, mkoloni pia alihitaji nguvukazi yenye weledi.
Kuna watu wanasema kiswahili hakifai kufundishia elimu ya juu sababu hakijitoshelezi kwa misamiati na istilahi. Huo ni uongo mkubwa. Neno kama barakoa lilikuwa limeshapotea kama siyo Uviko kuja kulihuisha tena. Neno kama mpinimwendo=crank shaft halipo tena. Na kuna mengi mengine ya nyanja anuwai tukisema tuanze kuyakusanya hapa jamvini tuta-terminology za kila tasnia.
Istilahi zipo nyingi sana ila wenye nafasi ya kutoa maamuzi kuhusu kiswahili nao hawajui kiswahili. Tatizo la nchi zetu hizi, ukiwa kiongozi basi unajihisi unajua kila kitu. Na sisi hata kiongozi akiongea shombo hupigiwa makofi na vifijo. Kiswahili ni kipana kinahitaji utashi wa kisiasa na kimamlaka kiwe lugha ya Afrika. Mandeleo yote ya kiswahili leo hayakuja kwa nasibu, ni juhudi za watawala wa kikoloni. Tena kiswahili kimerudi nyuma sanasana baada ya mkoloni kuondoka.
Katika yoote hayo, ni lipi ambalo limebishiwa au kupingwa?

Anyway, turudi kwenye mada, waAfrika tuone aibu kutumia lugha za kikoloni kwenye mamabo hata yasiyo ya kisayansi. Tutumie lugha zetu, hasa hasa za kiswahili, DRC na wengineo wabadilishe lugha za taifa toka za kikoloni na kuja kwenye kiswahiki chetu wa Afrika
 
Back
Top Bottom