Kenya formula ni hiyo hiyo lakini pesa wakiiba Kenya wanawekeza ndani ya Kenya. KAMA kweli viongozi wetu wezi pesa wanawekeza wapi mbona wachovu tu na hawahami nchi wao na watoto wao?80% mifukoni mwa watawala, 20% tunajengea madarasa na madaraja.
Mwafrika uroga Ili afurahishe nafsi Mzungu uroga Ili apate atakacho.Uko sahihi hakuna mzungu anayezuia teknolojia kugunduliwa Africa kuna mzungu mmoja alisema nasikia mna teknolojia ya kuruka na ungo Kama usafiri wa anga akasema si mfungue Viwanda vya nyungo muuze na muanze safari za kusafirisha abiria kwa njia ya anga mshindane kibiashara na ndege za Wazungu? Teknolojia hiyo Africa tunayo na hakuna mzungu kazuia Sasa mbona hatuitambui commercialize? Tuandike kama wao Fly KLM au fly Swiss air sisi zetu Tuandike fly Ungo the best and fastest flight in the world?
Kisichofunga ndoa na kuzimuJe chama kipi kitaleta maendeleo?
Nchi nyingi sana zimepata maendeleo kwa njia ya misaada.Mkuu 'FM WOLLE', kukusaidia kupata jibu sahihi kwa swali lako, nami ningependa nikuulize wewe na wasomaji wako wengine swali, ambalo kama mnaweza kulijibu kwa usahihi, basi swali lako nalo litakuwa limepata jibu:
Kuna nchi ngapi duniani ambazo zilishapata maendeleo kutokana na misaada?
Usikimbilie kujibu hili swali bila ya tafakuri makini juu yake, kama kweli nia yako ya kutaka jibu ya swali lako ni halali.
| Continent | Country | 2012 | 2013 | 2015 | 2019 |
|---|---|---|---|---|---|
| WORLD | [TOTAL] | 97,462.6 | | 152,727.7 | 167,800.3 |
| AFRICA | [TOTAL] | 46,003.5 | | ||
| ASIA | [TOTAL] | 25,970.5 | | ||
| MIDDLE EAST | [TOTAL] | 11,258.7 | | ||
| AMERICAS | [TOTAL] | 7,782.4 | | ||
| Asia | Afghanistan | 6,725.0 | 5,265.95 | 4,237.29 | 4,284.41 |
| EUROPE | [TOTAL] | 5,439.9 | | ||
| Asia | Vietnam | 4,115.7 | 4,084.7 | 3,157.36 | 1,094.63 |
| Africa | Ethiopia | 3,261.3 | 3,826.2 | 3,233.71 | 4,809.97 |
| Asia | Turkey | 3,033.1 | 2,740.5 | 2,145.22 | 824.90 |
| Africa | Congo, Dem. Rep. | 2,859.3 | 2,572.2 | 2,599.04 | 3,025.53 |
| Africa | Tanzania | 2,831.8 | 3,430.2 | 2,582.24 | 2,153.14 |
| Africa | Kenya | 2,654.0 | 3,236.2 | 2,464.18 | 3,250.97 |
| Africa | Côte d'Ivoire | 2,635.6 | 1,262 | 653.06 | 1,201.23 |
| Asia | Bangladesh | 2,152.0 | 2,669.1 | 2,570.1 | 4,482.60 |
| Africa | Mozambique | 2,096.9 | 2,314.1 | 1,814.74 | 1,907.78 |
| Asia | Pakistan | 2,019.0 | 2,174.1 | 3,747.5 | 2,170.74 |
| Africa | Nigeria | 1,915.8 | 2,529.4 | 2,431.5 | 3,517.32 |
| Africa | Ghana | 1,807.9 | 1,330.5 | 1,768.69 | 936.32 |
| Africa | Egypt | 1,806.6 | 5,505 | 2,499.43 | 1,740.59 |
| Middle East | Syria | 1,671.5 | 3,626.7 | 4,889.74 | 10,249.81 |
| Asia | India | 1,667.63 | 2,435.68 | 3,174.35 | 2,610.58 |
| Africa | Uganda | 1,655.1 | 1,692.5 | 1,628.2 | 2,100.01 |
| Africa | South Sudan | 1,578.0 | 1,447.4 | 1,674.83 | 1,885.27 |
| Africa | Morocco | 1,480.3 | 1,966.1 | 1,481.43 | 757.86 |
| Middle East | Jordan | 1,416.9 | 1,407.9 | 2,151.85 | 2,797.18 |
| Middle East | Iraq | 1,300.7 | 1,541.4 | 1,482.94 | 2,211.90 |
| Americas | Haiti | 1,275.1 | 1,170.5 | 1,045.86 | 726.46 |
| Africa | Malawi | 1,174.6 | 1,125.8 | 1,049.38 | 1,206.22 |
| Africa | Burkina Faso | 1,158.5 | 1,040.11 | 996.99 | 1,148.81 |
| Europe | Serbia | 1,089.8 | 783.2 | 312.48 | 570.70 |
| Africa | Senegal | 1,080.1 | 982.8 | 879.12 | 1,443.88 |
| Africa | South Africa | 1,067.1 | 1,292.9 | 1,420.27 | 971.48 |
| Africa | Tunisia | 1,017.0 | 713.6 | 474.54 | 984.03 |
| | ||||
| Africa | Mali | 1,001.3 | 1,391.3 | 1,204.13 | 1,863.21 |
| Africa | Zimbabwe | 1,001.2 | 811 | 788.29 | 974.89 |
Ndio kipi kitaje?Kisichofunga ndoa na kuzimu
Kile kinachoendelea kuwepoNdio kipi kitaje?
Tungekuwa ni watu makini (tuliomo JF) huu ungekuwa ni mjadala mahsusi, tena wenye ushahidi wa tarakimu kuonyesha matumizi makubwa kwa watumishi hawa.Tatizo fedha nyingi zinazopatikana iwe kwenye makusanyo ya kodi au Misaada na mikopo kutoka nje zinaishia kwenye kuhudumia tabaka dogo la watawala(rulling class)
Hebu fikiria kwenye jimbo au Wilaya moja kuna
1.Mkuu wa Wilaya
2.Mkurugenzi
3.MBUNGE
4.Katibu Tawala
5.Mwenyekiti wa Halmashauri na Madiwani
Hapo hujaenda Serikali kuu,tunatumia fedha nyingi kuhudumia kikundi cha watu wachache kuliko kuhudumia wananchi walipa kodi na tozo wa nchi hii
Mkuu, usifikiri hilo la "Development Assistance" ni jipya na kwamba hata sisi wengine hatulijui. Tunalijua sana, ila hatukubaliani na wewe juu ya misaada hiyo kuleta maendeleo ndani ya nchi hizo unazotutolea kama mfano.Nchi nyingi sana zimepata maendeleo kwa njia ya misaada.
Ujerumani iliharibika vibaya wakati wa vita kuu ya pili, misaada ya "Marshall plan" iliwezesha nchi kurudi haraka; jambo muhimu lilikuwa "rasilmali ya kibinadamu" yaani idadi kubwa ya mahandisi na wanasayansi waliokuwepo, na wafanyakati wenye uzoefu wa kutenda kazi kwa umakini, (pamoja na kukosa utamaduni wa rushwa) lakini kwa viwanda na miundombinu vilivyoharibika, misaada hiyo ilikuwa muihimu.
Ukipenda kuona nchi zilizopokea viwango vikubwa vya misaada, angalia orodha chini. Kuna nchi zinazotumia pesa hiyo kwa manufaa yao, nchi nyingine ni hodari kumeza kila kitu bila kuendelea kweli.
(Nataja tu zile zilizopokea zaidi ya bilioni $ kwa mwaka)
Official Development Assistance received in millions of US dollars[2]
Continent Country 2012 2013 2015 2019 WORLD [TOTAL] 97,462.6 152,727.7 167,800.3AFRICA [TOTAL] 46,003.5 ASIA [TOTAL] 25,970.5 MIDDLE EAST [TOTAL] 11,258.7 AMERICAS [TOTAL] 7,782.4 Asia Afghanistan 6,725.0 5,265.95 4,237.29 4,284.41EUROPE [TOTAL] 5,439.9 Asia Vietnam 4,115.7 4,084.7 3,157.36 1,094.63Africa Ethiopia 3,261.3 3,826.2 3,233.71 4,809.97Asia Turkey 3,033.1 2,740.5 2,145.22 824.90Africa Congo, Dem. Rep. 2,859.3 2,572.2 2,599.04 3,025.53Africa Tanzania 2,831.8 3,430.2 2,582.24 2,153.14Africa Kenya 2,654.0 3,236.2 2,464.18 3,250.97Africa Côte d'Ivoire 2,635.6 1,262 653.06 1,201.23Asia Bangladesh 2,152.0 2,669.1 2,570.1 4,482.60Africa Mozambique 2,096.9 2,314.1 1,814.74 1,907.78Asia Pakistan 2,019.0 2,174.1 3,747.5 2,170.74Africa Nigeria 1,915.8 2,529.4 2,431.5 3,517.32Africa Ghana 1,807.9 1,330.5 1,768.69 936.32Africa Egypt 1,806.6 5,505 2,499.43 1,740.59Middle East Syria 1,671.5 3,626.7 4,889.74 10,249.81Asia India 1,667.63 2,435.68 3,174.35 2,610.58Africa Uganda 1,655.1 1,692.5 1,628.2 2,100.01Africa South Sudan 1,578.0 1,447.4 1,674.83 1,885.27Africa Morocco 1,480.3 1,966.1 1,481.43 757.86Middle East Jordan 1,416.9 1,407.9 2,151.85 2,797.18Middle East Iraq 1,300.7 1,541.4 1,482.94 2,211.90Americas Haiti 1,275.1 1,170.5 1,045.86 726.46Africa Malawi 1,174.6 1,125.8 1,049.38 1,206.22Africa Burkina Faso 1,158.5 1,040.11 996.99 1,148.81Europe Serbia 1,089.8 783.2 312.48 570.70Africa Senegal 1,080.1 982.8 879.12 1,443.88Africa South Africa 1,067.1 1,292.9 1,420.27 971.48Africa Tunisia 1,017.0 713.6 474.54 984.03 Africa Mali 1,001.3 1,391.3 1,204.13 1,863.21Africa Zimbabwe 1,001.2 811 788.29 974.89
Sasa kama idadi kubwa ya familia moja moja hazina uchumi ulioimara kiasi cha kushindwa kujihudumia zenyewe hapo utasema idadi kubwa ya watoto siyo kikwazo? Familia zenye uchumi mzuri ndo zinaweza kujenga jamii yenye maendeleo na serikali Bora na siyo Bora serikali, hata hao tunaowatolea mfano, marehemu Mengi angalia idadi ya watoto na uchumi wa familia kama familia, hata maandiko yanasema chakula cha watoto huwezi kuwapa mbwa maana yake uwe na chakula kingi cha kushibisha watoto wako Ili ziada uwape wengine, kitu kinachoweza kuondoa umasikini ni Kila mtunza familia awe na kazi ya kuingiza kipato iwe hata kwa viboko serikali ndo kitu ilitakiwa kusimamia au kutengeneza katiba ya Kila mtu akifikisha umri wa kufanya kazi apewe kazi afanye kama ukiwa hujapata kazi kwa muda wa miezi mitatu baada ya shule upelekwe mashamba ya serikali mpaka ajira yako itakapopatikana.Sio kweli idadi ya watoto iwe kikwazo cha kutoendelea
The problems is how aid used.Aid never been a problem
Hapo ni suala la elimu ukiwapa elimu wote wakazalisha unakuwa na manpower ya kutosha.Sasa kama idadi kubwa ya familia moja moja hazina uchumi ulioimara kiasi cha kushindwa kujihudumia zenyewe hapo utasema idadi kubwa ya watoto siyo kikwazo? Familia zenye uchumi mzuri ndo zinaweza kujenga jamii yenye maendeleo na serikali Bora na siyo Bora serikali, hata hao tunaowatolea mfano, marehemu Mengi angalia idadi ya watoto na uchumi wa familia kama familia, hata maandiko yanasema chakula cha watoto huwezi kuwapa mbwa maana yake uwe na chakula kingi cha kushibisha watoto wako Ili ziada uwape wengine, kitu kinachoweza kuondoa umasikini ni Kila mtunza familia awe na kazi ya kuingiza kipato iwe hata kwa viboko serikali ndo kitu ilitakiwa kusimamia au kutengeneza katiba ya Kila mtu akifikisha umri wa kufanya kazi apewe kazi afanye kama ukiwa hujapata kazi kwa muda wa miezi mitatu baada ya shule upelekwe mashamba ya serikali mpaka ajira yako itakapopatikana.
Pamoja na jibu lako zuri, ambalo kimsingi naliunga mkono, sikubaliani nawe katika mlinganisho huo wa nchi za ulaya na hizi zetu, hasa Tanzania.
Tumepata uhuru takribani miaka sitini sasa. Ndio, tulianzia chini sana, na uwezo wetu ulikuwa mdogo sana, lakini muda huo ni muda mzuri na wa kutosha sana kuleta mabadiliko chanya kuliko haya tuliyofikia sasa hivi kama tungekuwa makini na kufanya mambo yetu kwa ueledi na uhakika zaidi.
Leo hii, hata yale mambo mazuri tuliyokuwa tumekwishayatimiza, ni kama tunarudi nyuma, kwa sababu hatuna tabia ya kuwa na kumbukumbu ya mazuri tuliyokwishafanya na kuyaendeleza ili tusigharimie tena kuyafanya upya. Ni kama serikali yetu haina kumbukumbu, pamoja na kwamba ni chama kilekile kinachounda serikali hizo. Wakati mwingine, serikali hiyo hiyo inarudia tena makosa yale yale yaliyofanyika huko nyuma.
Utapataje maendeleo kwa hali ya namna hiyo!
Pili, sisi haitulazimu tena tukagundue kurudumu upya. Kuna mambo mengi sana tunayotakiwa kugezea tu yalivyofanywa na wengine ili nasi tufaidike nayo. Hata kama ikilazimu kubadili kidogo ili yalingane na hali yetu ilivyo, isingekuwa vigumu na kutuchukua muda mrefu namna hii kuleta mabadiliko ya maisha ya wananchi wetu.
Jambo ninalojua ni moja. Tunakosa kiongozi mwenye dira na usimamizi wa dira hiyo ili kutufikisha kwenye hayo anayoamini nchi yetu inayahitaji.
Chukulia mfano wa kilimo na elimu tu, maeneo mawili ambayo mimi naamini yangeweza kutubadilisha haraka sana kama nchi kama yangewekewa mkazo unaostahiri. Sisemi kamwe hapa kwamba mengine yote yataachwa, lakini haya mawili yawe na kipa umbele cha ziada katika uongozi wa kiongozi shupavu na imara ndani ya miaka kumi.
Kilimo ambacho wananchi wetu wengi ndiko wanakopatia ridhiki yao, wakapata mbegu bora, vitendea kazi na ushauri mahususi juu ya kazi zao; na serikali ikafanya kila iwezalo kuwasaidia kutafuta soko la mazao yao..., hali itakuwaje ndani ya miaka kumi?
Elimu yetu inaonekana kama tunarudi kinyumenyume. Tunakuwa na wasomi wengi, lakini thamani ya wasomi hawa inakuwa haijionyeshi katika jamii. Ni hawa hawa wahitimu wetu ndio tunaowategemea wasaidie kuleta mabadiliko ndani ya jamii zetu. Lakini sasa angalia tunavyokwenda, hata mashirika ya Vodacom na Tigo hawawezi kabisa kupata watu ndani ya nchi hii wa kuendesha vikampuni hivi, baada ya miaka sitini ya kufundisha watu wetu wenyewe?
Mkuu Bepari2020, nakumbuka mara ya mwisho tulikutana kule kwa Kagame na Rwanda yake. Pamoja na kwamba hatukuweza kukubaliana katika yale mambo huko, leo hii nitakubali katika hili moja la yeye kuwa na dira, basi.
Umetolea mfano wa nchi za Ulaya, sijui utasemaje kuhusu nchi kama Malaysia, Vietnam na nyingine ambazo nazo zimeibuka kutoka kwenye umaskini miaka kadhaa baada ya kuwa huru.
Maelezo yako mazuri sana tena mnoo ila umesahau " Mfumo wa Elimu Tanzania ni tofauti na hizo Nchi "" Elimu ndio kila kitu. Watanzania hawana makosa tatizo viongozi ( Sera ) wetu na dira au Sera zao.Hili la kuwaza viongozi Kila wakati si kweli mabilionea wakina Billy gates waliogundua. Microsoft hawakusaidiwa au kupewa dira na kiongozi yeyote awe wa serikali au yeyote au dira ya nchi akili zao ziiamka za wao kama wao
Wagunduzi wa Internet, simu, magari nk wote hakuna cha serikali wala nini
Wenzetu kwa asilimia kubwa huamini kuwa hatima ya maisha yao imo mikononi mwao wao wenyewe kama individuals sisi sababu tuko wavivu hatutaki kubeba responsibility hatima zetu tunasukumia viongozi! !!! Hivyo tunasababisha bongo zetu kulala sababu tutakuwa tumekabidhi viongozi ndio wawaze kwa niaba yetu ambao nao Ni bongolala kama sisi hawana tofauti sana na sisi! ! !! Mjinga akikabidhi mijinga kiongozi awaze kwa niaba yake matokeo yake yatakuwaje? Ndipo tulipo tuamke! !!!
Sasa Mungu aliumba ubongo kwenye kichwa cha kila mtu wa nini? Je ni kutumia tu kujua Choo kiko wapi au?
Kama elimu ni kila kitu mbona serikali na wazazi wamesomesha watoto nje ya nchi developed countries from kindergarten to university lakini bado wako hopeless hawana cha ugunduzi wowote pamoja na kulipia tuition fees mamilioni?Maelezo yako mazuri sana tena mnoo ila umesahau " Mfumo wa Elimu Tanzania ni tofauti na hizo Nchi "" Elimu ndio kila kitu. Watanzania hawana makosa tatizo viongozi ( Sera ) wetu na dira au Sera zao.
Amesema mdau mmoja hapo juu "tungeboresha kilimo na Elimu tungekuwa tumemaliza kila kitu.""
Development is a personal struggle. Mara chache kuna kurithi utajiri. Lakini zaidi personal ambition ndiyo chanzo cha utajiri.Kama elimu ni kila kitu mbona serikali na wazazi wamesomesha watoto nje ya nchi developed countries from kindergarten to university lakini bado wako hopeless hawana cha ugunduzi wowote pamoja na kulipia tuition fees mamilioni?