Kwanini nchi za Magharibi zinaisaidia Ukraine silaha bila kificho lakini huzishutumu nchi zingine zinazoisaidia Urusi?

Kwanini nchi za Magharibi zinaisaidia Ukraine silaha bila kificho lakini huzishutumu nchi zingine zinazoisaidia Urusi?

Urusi mpaka inapewa msaada wa kifedha toka nchi za Magharibi halafu iwe tishio? Urusi ana nini cha pekee zaidi ya makombora ya nuklia?
Leo zaidi ya mwaka kaikalia Ukraine, hao wababe wanashindwa nini kumfurusha na kumng'oa kama walivyofanya kwa Hitler?
 
Kama kichwa cha thread kinavyoonesha, sishabikii vita ila inaonekana nchi za Magharibi na Marekani ni tishio sana kila anaemsaidia Urusi hufanya hivyo kisiri siri!. West hujiona wapo sahihi kwa Kila kitu na wanataka mtazamo/maadili yao uwe mtazamo wa dunia yote.

Hivi dunia haiwezi kuwepo bila vita Kila kona? Huyu anapigana na yule hawa wanapigana wenyewe Kwa wenyewe ili mradi tafrani.
Mkubwa mkubwa tu , na lazima fanya afanyavyo USA maana ni mkubwa
 
Leo zaidi ya mwaka kaikalia Ukraine, hao wababe wanashindwa nini kumfurusha na kumng'oa kama walivyofanya kwa Hitler?
Wakiingia vitani moja kwa moja, inaweza kusababisha janga la Dunia. Fahamu kuwa Russia ana silaha za nuklia, na Putin ni Rais dikteta ambaye ameua wapinzani wake wengi na amewaweka ndani wapinzani wake wengi.

Mtu katili hawezi kuona shida kuangamiza Dunia. Madikteta sifa moja kubwa waliyo nayo ni kutokubali kushindwa. Putin ana uhakika kuwa hayo mataifa ya Magharibi yakiingia vitani dhidi yake, lazima watampiga, na silaha pekee atakayoitegemea ni nuklia. Ndiyo maana mataifa haya ya Magharibi wameamua kutoa usaidizi wa silaha kwa Ukraine, na siyo wao kuingia vitani moja kwa moja dhidi ya Russia. Wanataka wamwangamize taratibu bila ya kuwepo kwa janga la Dunia. Nchi pekee imayoumizwa zaidi ni Ukraine maana uhai wa watu hauna mbadala.

Lakini kwa vyovyote vile, vita hii itaiumiza sana Urusi kwa miaka mingi. Haya mataifa ya Magharibi yanatoa ziada kuisaidia Ukraine, Russia anatumia kile ambacho kinahitajika sana kwaajili ya maendeleo ya watu wake. Angalia makampuni yalivyo mengi yaliyoondoka Russia, vijana wengi wenye ujuzi walivyomimbia Russia, silaha nyingi anazoendelea kuzitumia, n.k.
 
Urusi ndie aliyeanzisha vita vya kichokozi visivyo na mashiko kwa kuivamia Ukraine na kuteka maeneo ya Ukraine na kufanya uharibifu na ukatili mkubwa sasa uliona watu anasaidiwa mvamizi kumpiga mwasithiriwa
Kwa nini alianzisha vita
 
Wakiingia vitani moja kwa moja, inaweza kusababisha janga la Dunia. Fahamu kuwa Russia ana silaha za nuklia, na Putin ni Rais dikteta ambaye ameua wapinzani wake wengi na amewaweka ndani wapinzani wake wengi.

Mtu katili hawezi kuona shida kuangamiza Dunia. Madikteta sifa moja kubwa waliyo nayo ni kutokubali kushindwa. Putin ana uhakika kuwa hayo mataifa ya Magharibi yakiingia vitani dhidi yake, lazima watampiga, na silaha pekee atakayoitegemea ni nuklia. Ndiyo maana mataifa haya ya Magharibi wameamua kutoa usaidizi wa silaha kwa Ukraine, na siyo wao kuingia vitani moja kwa moja dhidi ya Russia. Wanataka wamwangamize taratibu bila ya kuwepo kwa janga la Dunia. Nchi pekee imayoumizwa zaidi ni Ukraine maana uhai wa watu hauna mbadala.

Lakini kwa vyovyote vile, vita hii itaiumiza sana Urusi kwa miaka mingi. Haya mataifa ya Magharibi yanatoa ziada kuisaidia Ukraine, Russia anatumia kile ambacho kinahitajika sana kwaajili ya maendeleo ya watu wake. Angalia makampuni yalivyo mengi yaliyoondoka Russia, vijana wengi wenye ujuzi walivyomimbia Russia, silaha nyingi anazoendelea kuzitumia, n.k.
Ngoja tuone mwisho nani ataibuka mshindi, combined west dhidi ya taifa maskini la urusi.
 
Kama kichwa cha thread kinavyoonesha, sishabikii vita ila inaonekana nchi za Magharibi na Marekani ni tishio sana kila anaemsaidia Urusi hufanya hivyo kisiri siri!. West hujiona wapo sahihi kwa Kila kitu na wanataka mtazamo/maadili yao uwe mtazamo wa dunia yote.

Hivi dunia haiwezi kuwepo bila vita Kila kona? Huyu anapigana na yule hawa wanapigana wenyewe Kwa wenyewe ili mradi tafrani.
Urusi itapewaje Silaha na humu Ndani Watu wanaishabikia kama taifa Kubwa lenye Silaha za Maangamizi?
 
Sio kweli umekaririshwa au mahaba...
Nimekaririshwa na nani, au mahaba ya nini! Huo ndiyo ukweli. Marais wengi wa Marekani wanaingizwa madarakani na makampuni yao ya kuzalisha na kuuza silaha.

Na silaha hizo hutumika katika vita mbalimbali duniani. Wamefanya hivyo Vietnam, Korea, Iraqi, Syria, Afghanstan, Cossovo, na hata sasa wanaunga mkono mgogoro wa Urusi na Ukraine kwa kuisaidia silaha Ukraine.
 
Kama kichwa cha thread kinavyoonesha, sishabikii vita ila inaonekana nchi za Magharibi na Marekani ni tishio sana kila anaemsaidia Urusi hufanya hivyo kisiri siri!. West hujiona wapo sahihi kwa Kila kitu na wanataka mtazamo/maadili yao uwe mtazamo wa dunia yote.

Hivi dunia haiwezi kuwepo bila vita Kila kona? Huyu anapigana na yule hawa wanapigana wenyewe Kwa wenyewe ili mradi tafrani.
Akili yako haina akili, Kwamba wewe hujui kuwa Ukraine imevamiwa? Na kwa mjibu wa Umoja wa maazimio ya Umoja wa Mataifa nchi inayovamiwa inapaswa kusaidiwa silaha ili kujilinda? Na vile vile kwa mjibu wa maazimio ya Umoja wa Mataifa kumsaidia Mvamizi ni kosa , na Bwana Vikwazo atakuwekea Vikwazo?

Nakuomba ondoka kwenye itikadi za kijamaa, ili uondokane na Kuishi kwenye Propaganda. Na uanze Kuishi kwenye Ukweli.
 
Kama kichwa cha thread kinavyoonesha, sishabikii vita ila inaonekana nchi za Magharibi na Marekani ni tishio sana kila anaemsaidia Urusi hufanya hivyo kisiri siri!. West hujiona wapo sahihi kwa Kila kitu na wanataka mtazamo/maadili yao uwe mtazamo wa dunia yote.

Hivi dunia haiwezi kuwepo bila vita Kila kona? Huyu anapigana na yule hawa wanapigana wenyewe Kwa wenyewe ili mradi tafrani.
Umeandika kifupi sana, na karibu majibu yote ukayatoa humo humo kwenye andiko hilo fupi, na hapo hapo ukajibu swali lililomo kwenye kichwa cha mada.

Jamaa (West) walikuwa na 'project' yao ambayo ilistukiwa.

Sasa waliyekuwa wamemweka mbele (Ukraine) katika utekelezaji wa 'project' yenyewe wanazidi kumsurubu wenyewe kwa kumpa vijisilaha ambavyo havitaweza kubadili matokeo, lakini akiendelea kusurubiwa! Wakati huu Ukraine alitakiwa awe kwenye mazungumzo ya kumaliza vita.
 
Nimekaririshwa na nani, au mahaba ya nini! Huo ndiyo ukweli. Marais wengi wa Marekani wanaingizwa madarakani na makampuni yao ya kuzalisha na kuuza silaha.

Na silaha hizo hutumika katika vita mbalimbali duniani. Wamefanya hivyo Vietnam, Korea, Iraqi, Syria, Afghanstan, Cossovo, na hata sasa wanaunga mkono mgogoro wa Urusi na Ukraine kwa kuisaidia silaha Ukraine.
Hebu tafakari bro kilicho sababisha Marekani aende Huko Iraqi, Syria, Afghanstan, Cossovo ninini???[emoji101][emoji101]

Sent from my vivo Y67 using JamiiForums mobile app
 
Marekani ni Taifa la uovu na uharibifu.
kilicho sababisha Marekani aende Iraqi, Syria, Afghanstan, Cossovo ninini???[emoji101][emoji101]
Kuondoa uovu wa ma-dictetor au kupeleka uovu??
 
kilicho sababisha Marekani aende Iraqi, Syria, Afghanstan, Cossovo ninini???[emoji101][emoji101]
Kuondoa uovu wa ma-dictetor au kupeleka uovu??
Ungekuwa unafahamu unafiki na u double standard wa Taifa la Marekani na Marais wake, hata usingeuliza hili swali lako.
 
kwa hiyo wewe mtoa mada, nchi yako ikivamiwa ikaomba misaada na kusaidiwa, je watakaokusaidia watakuwa wanafanya kosa?.. 🤔🤔🤔
 
Urusi ndie aliyeanzisha vita vya kichokozi visivyo na mashiko kwa kuivamia Ukraine na kuteka maeneo ya Ukraine na kufanya uharibifu na ukatili mkubwa sasa uliona watu anasaidiwa mvamizi kumpiga mwasithiriwa
Unaweza kutwambia alianza kwa sababu gani. Tungekuwa tuaongea kwa kuweka ushaabiki pembeni, ukweli ungekuwa una tamalaki. Kibaya zaidi tunaangalia tukio Wala hatufuatilii chanzo chake.
 
Unaweza kutwambia alianza kwa sababu gani. Tungekuwa tuaongea kwa kuweka ushaabiki pembeni, ukweli ungekuwa una tamalaki. Kibaya zaidi tunaangalia tukio Wala hatufuatilii chanzo chake.
Kwanza tuanzie hapa hii ni vita vya Putin na Ukraine alianzisha kwa sababu anachuki na Ukraine baada ya kibaraka wake Putin kufurumushwa kwa maandamano na Putin anataka kuiteka Ukraine na kumpandikiza kibaraka wake mwingine
 
Back
Top Bottom