Elections 2010 Kwanini ni vigumu kuiba kura katika Uchaguzi Wetu - Tusitafute visingizio

Elections 2010 Kwanini ni vigumu kuiba kura katika Uchaguzi Wetu - Tusitafute visingizio

ni wazi hili suala la wizi wa kura ( rigging of election results) lipo mfano
  1. kenya
  2. zimbabwe
  3. zanzibar
  4. ongezea...
ndio maana hata kibaki na akina odinga waliamua kukubaliana kuwa na serikali ya mseto huko kenya; hali kadhalika zimbabwe na zanzibar tumeona hayo na akina komred mugabe na tsvangirai huko zimbabwe na karume na hamad huko zanzibar wamekubaliana kuwa na serikali ya mseto kutokana na usugu wa wizi wa kura.

inavyoonekana upande wa serikali unakuwa na 100% ya wizi wa kura na upinzani 0% ya ushindi na hapo kwa sababu ya wizi wa kura na hapo ndipo 'busara' inapotumika to save the nation.

tumekuwa tukishuhudia usaliti kwa upande wa upinzani kwa kurudi au kujiunga na chama tawala wakati wa mchakato wa kufikisha majina ya wagombea kwa kila chama. chama tawala kimekuwa kikituhumiwa kuwaghilibu wapinzani japo nacho kimekuwa kikikanusha malengo hayo.

hoja inayojengwa imelala kwenye hiyo ya ghiliba; kwamba kuna uwezekano kwamba kwa kuwa chama tawala kina uwezo mkubwa wa kifedha, kama inavyoonekana kwenye uwezo wake wa 'kuvasha' akina mama, vijana na akina baba kwa sare zilizosambaa nchi nzima, kinaweza kuwa nunua mawakala wa upiga ji kura na hivyo , wizi wa kura ukafanikishwa kwa nadharia hiyo.

hivyo, ni wazi wizi wa kura upo na kuna uwezekano katika hayo wanayodai wakuu wengi ikafanyika na ndio maana mimi nalikataa kwa nguvu zote suala la kulinda kura siku ya uchaguzi kwa kuwa hiyo, kwa mtazamo wangu, ni wajibu wa moja kwa moja wa wakala wa upigaji kura.
 
mzee mwanakijiji.
kwanza nashukuru kwa hii thread yako, imenielimisha sana, wengi wetu tumakalia kusema kura zitaibwa lakini seriously hakuna hata mmoja anaesema ZINAEBWAJE? kimantiki. so idea imebaki kuwa too hypothetical kiasi kwamba kwa mimi mpiga kura kwa mara ya kwanza najazwa tu hofu za kufikirika lakini sijathibitishiwa kiuhalali kwamba hicho kitu hufanyika. so wale ambao mmeshapiga kura hapo kabla like 2005, tuelezeni kimantiki huo wizi ukoje kiuutaaalam, na si kusema mara masanduku darini,tiki ya huku inahamia huku nk. asanteni.

Matokeo yanaibiwa kwa njia nyingi. Kwa sasa hatuwezi kujuwa wataiba vipi lakini kama ya Tunduma ni ya kweli then wanaweza kuwa na njia mpya wanaoijuwa wenyewe na ambayo haijatumika before. Haiwezekani wakawa wanatumia staily ileile kila siku lazima wae wanakuja na mbinu mpya.

Hivi hukuona kilichotokea Kenya when Chairman alipotangaza matokeo tofautina ya returning officer??? Wewe hukuona muda gani ulitumika kutangaza matokeo kule Zimbabwe??

Kwa hiyo MMKJ asitekegee kuwa ufundi walioutumia 2005 bado watautumia leo. Sasa kama MKKJ alikuwa observer kwenye uchaguzi na hakuona dosari hiyo haina maana kuwa hakukuwa na wizi, hawaezi kuiba sehemu ambayo ina obsevers na hatuwezi kuwa na observes 50,000 kwa hiyo huko wasiko ndiyo huko kunakoweza chakachuliwa!!
 
M.M Mwanakijiji,
Nataka kujua yale masanduku yaliyopo kwenye vituo vya kupigia kura nani anahusika kuyalinda na kuhakikisha hayana karatasi ambazo zimeshapigwa TICK?(Nimeyaona kwenye vituo)-Je,ni walewale watumishi wa serekali ambao wananjaa ndio wanapewa jukumu la kulinda?Hapo kuna nini mwanakijiji?
......Endapo hesabu ya idadi ya kura za mgombea zinakosewa kwa malaki halafu taarifa inatoka nani wa kutujulisha kuwa kuna kasoro?nani wa kufuatilia irekebishwe?
......Watu wote tunafika vituoni kupiga kura pamoja na wasimamizi wanaotoka katika vyama vyote,je kuna nafasi ya kukagua masanduku yote ambayo yatatumika kupigia kura ili kujihakiki wenyewe .
......Kama kuna masanduku ambayo yanatoka sehemu nyingine na tukaambiwa yametoka vituo vingine vya kupigia kura nani atakaye hakikisha kuwa ni kura halali?
......Kuhesabu kura siku zote inafanyika usiku na sio mchana kutokana na ukweli kazi huisha jioni sana,sasa kama wanataka kufanya umafya wa wizi wa kura usiku ni mtanzania gani ambaye atakuwa tayari kulinda magari yote yatakayokuwa yanaingia na kutoka vituoni?au ni haohao polisi?
......Hata hivyo njia naziona ni nyingi sana za kupindisha matokeo kirahisi sana.
......Mwanakijiji,nadhani unajaribu kuangalia kwahesabu za haraka haraka ni njia gani ambazo walikuwa wanatumia kupindua matokeo pamoja na njia rahisi ya mtangazaji wa matokeo ambaye hapingwi na kifungu chochote cha sheria endapo anamtangaza mtu hata kama hajashinda lakini anahesabika kashinda.
....Kwa mtazamo wako nina uhakika kwa kipindi hiki watanzania wameungana na watajaribu kwa njia zote hizi kuainisha njia za panya hili serekali iundwe kwa uhalali.
Thanks Mwanakijiji.
 
Wizi mkubwa hata hivyo unafanyika kwenye maeneo ambayo kuna upinzani mdogo sana wa chama kikongwe.ukizingatia kuwa kila kituo kina wapiga kura wasiozidi 500.so,kama kuna wapiga kura 350 waliopiga kura 250 kuna idadi ya kura hewa kama 250 ambazo watatumia kuziingiza kwa kila kituo na kubadili matokeo ya jumla.
 
jamani.. zinaibwaje? zamani ilikuwa rahisi kwa sababu sanduku linapakizwa kwenye baskeli kwenda kuhesabiwa sehemu nyingine.. siyo mnasema "wizi upo" kinadharia inawezekana lakini mtu aniambie unawezekana vipi? Wildcard anasema kuwa Zanzibar waliiba ah wapi!, kuna suala la Tume ya Uchaguzi kuingiliwa hilo limetokea Kenya na ninaamini ndilo lenye uwezekano mkubwa wa kutokea Tanzania mwaka huu..

Mzee Mwanakijiji,

CCM ni wajanja kuliko unavyofikiria. NInachofahamu mimi ni kuwa wizi wa kura unawezekana tu kama mawakala wamekula njama na CCM ili kupenyeza vikaratasi vya pembeni. Bila collusion haiwezekani. Hawa watu wana mapesa ya mchezo, just imagine uchaguzi mdogo wa Tarime walitumia zaidi ya laki 5, za nini kama si kuhonga? wanaweza wakamwaga kwa mawakala na kura zikachakachuliwa. Ni lazima tupate wazalendo wasiokubali kununuliwa, na ndivyo inavyokuwa katika majimbo kama Moshi Mjini, Karatu, Tarime. Sasa mimi nashauri hakuna kulala, Mzee usiwafanye watu wakabweteka kwamba hakuna wizi upo. Jana nilimsikia Dr Slaa Rais ajaye akisema kuwa kule Karatu walikamata karatasi bandia za kura. Wizi upo, mawakala wasituangushe.
 
Mwanakijiji, nimekuelewa kuhusu matokeo ya kura za Urais pia kutangazwa vituoni hivyo kuondoa dhana ya wizi ktk vacuum itakayokuwapo between Vituo na Tume.

Pia ningependa mawakala wa vyama vyote vya upinzani washirikiane (ikiwezekana vyama vishirikiane kulipa mawakala) ili endapo mmoja atakuwa na kiu ama atashikwa haja (kubwa ama ndogo) wengine wawe macho.

Kwa ufahamu wangu kura zinaweza kuibwa kama ifuatavyo:

1:Vituo hewa:- Kura zitachakachuliwa katka hivi vituo bubu ambapo watatumika mawakala feki ambao watatia sahihi na kuthibitisha kuwa mgombea fulani kashinda.

2: Tume kuchakachua idadi ya matokeo halisi ktk vituo:- lengo hapa ni kutaka vyama husika vilalamike mahakamani wakati Rais atakuwa ameshatangazwa!. Sasa mtakapoenda mahakamani yataletwa masanduku yaliyochakachuliwa ili kuthibisha kuwa kura hazikuibwa!!.
 
MM unazungumziaje uwezekano wa 'vituo hewa' na mahesabu ya kura zake kuwasilishwa jimboni,?.

Pia unazungumziaje hali kama ile ya Kenya ambapo mahesabu aliyokuwa anapewa Kivuitu yalikuwa tofauti kabisa na yaliyokuwapo majimboni, na wapinzani walipokuwa katika jitihada za kulalamika, wakiwa wametuma helkopta maeneo mbalimbali kuwahisha karatasi 'orijino', "Mzee" akaapishwa ikulu?
 
... Wapiga kura tumpigie Dr.Slaa kwa wingi ili wizi wao ushindikane. Margin kati ya Dr.wa ukweli na wa kuchakachua iwe kubwa.

kweli inasikitisha sana kumbe kuna mtu kapewa tu udaktari hivi hivi kisa bembea ama jamani natamani kuna mwingine nilimsikia akisoma kozi ya maandalizi ya kujiunga na chuo kikuu huria cha Tz lakini ghafla naye ni DK siku hizi jamani nami natamani niwe raisi niweze kujipatia hizi chakachua shahada kwani ukibembea tu shahada

au vipi
 
Naweza perhaps nisizipende arguments alizozi-raise Mzee Mwanakijiji (kutopenda ni tofauti na kutokukubaliana mind you!)

Kwa hiyo kwa mtizamo chanya, hata kama sikupenda kusikia alichokisema huyu ndugu, mimi naona kuwa ametengeneza (kwa kujua au kutokujua) what I would refer to as a fantastic checklist ambayo wapinzani (hususani CHADEMA) wanaweza kuitumia ili kuepusha aina yoyote ya uchakachuaji (kama upo) katika ngazi ya vituo.

Ni checklist ambayo ikifanyiwa kazi itatoa solution si kwa uchaguzi huu tu bali hata kwa baadaye (nadhani ninaposema "baadaye" inaeleweka kuwa naongelea juu ya NEC kwani there's very little, if any, that can be done to undo what the present NEC can or cannot do).
 
Ujumbe umefika mwana kijiji, maana kama linalosemwa si kweli mbona hilo Container la vipodozi halijafunguliwa tuone ndani yake kuna nini?
Na hayo makaratasi yanapelekwa wapi? Uwazi na ukweli upo hapo? Tunaiomba serikali isifukuze watu vituoni kwa maji na mabomu ili washuhudie kura baada ya kuhesabiwa zimebandikwa kwenye vituo kama ulivyosema. CHADEMA na vyama vingine kwa vile wanao uzoefu wa majimbo mengine watumie hiyo experience kulinda hizo kura na kupata matokeo ya kweli. Muda huu vyama vipange mawakala waaminifu wa kusimamia vituo, ili kuwa na uhakika wa matokeo.

In the end, you're measured not by how much you undertake but by what you finally accomplish. Donard Trump.
 
Sidhani kama ni uwizi wa kura bali ni kwa sababu ya katiba yetu inayosema kuwa NEC ikitangaza matokeo ya U-Rais HAYAWEZI PINGWA POPOTE PALE;kipengele hiki ndani ya katiba ni cha kishetani!

Wasiwasi wangu ni huu,majumuisho ya mawakala wa CHADEMA unaweza ukaonyesha labda uchaguzi ni too close to call na hata labda Dr Slaa akashinda kwa kura chache lkn majumuisho ya mawakala wa Dr Slaa yakitangazwa vingine na NEC na huku wakilindwa na sheria ya kshetani kama"wakitangaza matokeo hayapingwi"tutafanyaje?

CCM wanaweza wakafaidika na sheria hii ya kishetani maana NEC sio huru!

Mh jamani kwani sheria ya uchaguzi inasemaje kuhusu kutangazwa kwa matokeo??? Sasa kama mawakala wa vyama vyote walisaini na kukubali kuwa yaliyopatikana ni matokeo halali na vyama vyote kupata nakala ya matokeo hayo kutoka majimbo yote, sasa hata NEC ikitangaza vinginevyo, je wakienda mahakamani na vielelezo vyao watakataliwa kweli, eti kisa NEC ilishatangaza matokeo???? Mimi hili haliniingii akilini hata kidogo.
Halafu pili suala la kusema kura zinaibwa.. zitaibwa, mbona hamsemi zitaibwa kwa njia gani???
Mwanakijiji hapa ametoa kwa kirefu kabisa maelezo mazuri ya jinsi utaratibu wote wa kupiga na kuhesabu kura ulivyo, na kuonyesha ilivyokuwa vigumu kuiba kura, sasa mbona hamtaki kuelewa jamani??? Mambo mengine sio ya kuweka Imani tu kama vile tuko msikitini/makanisani jamani.
Mi nafikiri ingekuwa busara kama tukaendelea kuelimishana namna ya kusimamia hilo zoezi kwa kuwaelekeza mawakala wetu wawe macho wakati wote ili wizi usitokee. Hii kulalamika wizi upo.. sijui kura zinaibwa.. jamani tuliache hili, halina tija kwa Taifa letu.

Nawakilisha Oktoba 31
 
MM unazungumziaje uwezekano wa 'vituo hewa' na mahesabu ya kura zake kuwasilishwa jimboni,?.

Pia unazungumziaje hali kama ile ya Kenya ambapo mahesabu aliyokuwa anapewa Kivuitu yalikuwa tofauti kabisa na yaliyokuwapo majimboni, na wapinzani walipokuwa katika jitihada za kulalamika, wakiwa wametuma helkopta maeneo mbalimbali kuwahisha karatasi 'orijino', "Mzee" akaapishwa ikulu?

Eeeh sasa huo ndo wizi na matokeo yake si uliyaona?? Na likitokea kama hilo kuna sehemu nyingi tu ambazo mgombea/chama kitakachodhulumiwa wanaweza kwenda kushitaki. Na matokeo ya hali hiyo hayaishii tu ndani bali hata kimataifa yanaharibu mahusiano.
Nafikiri Tanzania hatujafikia huko kwani Demokrasia ipo juu. Kama ikiandaliwa mipango madhubuti wizi hautatokea.
 
Uchakachuaji wetu wa matokeo huwa sana sana ni kughushi fomu ya matokeo na kumtangaza mgombea ambaye wapigakura walimkataa. Kwa kufanya hivyo wanakuwa wasimamizi na mawakala wameshirikiana katika kupika matokeo kwa manufaa yao wenyewe ya kuhongwa. Hata wewe hili umeliona kama ulivyosema hapa chini:-


Njia mbadala ya kuchakachua matokeo ni ile ya kuingiza kura za bandia baada ya kura kuhesabiwa kwenye vituo. Hili zamani kwetu uwezekano ulikuwa haupo lakini sasa lawezakana sana baada ya NEC kufuta utaratibu wa wapigakura kuwepo mita 200 kutoka kwenye eneo la kupiga kura.

Sasa ndg. Rutashubanyuma haina maana basi ya kuwa na mawakala vituoni, kama tukisema wapiga kura wote wajae ndani ya chuma cha kuhesabia kura. Tena ndugu ni bora kufanya kazi na watu 10 kuliko na watu 100 maana hapo uwezekano wa kuiba kura ndo mkubwa zaidi na fujo kutokea. Watu wachache ni rahisi kwa wao wenyewe kuangaliana na kuhakiki zoezi zima linavyokwenda.

Hoja yako ya kuingiza kura za bandia, nafikiri Mwanakijiji aliieleza vizuri sana tu, pitia tena hoja zake upate ufafanuzi. Labda kukukumbushia tu... Tangu masanduku ya kupiga kura yafike kituoni, mawakala wanahakiki kila hatua mpaka yanapofungwa baada ya zoezi la upigaji kura kwisha, sasa hizo kura bandia zinaingizwa wapi??? Labda ndumba zifanyike...
 
Malafyale.. hilo tatizo halipo mwaka huu; matokeo yanatangazwa kila kituo na kila jimbo linatangaza rasmi.. hakuna haya ya takwimu za mawakala! Na as a matter of fact.. mawakala hawahesabu kura wao wanaangalia tu, sasa hawa mawakala wa Zanzibar walileta namba zao wote wakazijumlisha na zikapingana na zile za Tume ya Uchaguzi? How realiable was their tally?

Hilo linafanyika kila uchaguzi. hata mi nilibandika matokeo ya kituo nje mwaka 2000.
 
Thanks Mwanakijiji. Hata mie naamini baada ya kushuhudia mchakato wa upigaji kura, uhesabuji wake na utangazwaji wa matokeo. Si rahisi kura kuibwa bila njama kufanyika kwa pamoja na timu nzima ya usimamiaji katika kila kituo, yaani msimamizi, mawakala wa vyama, na waangalizi. Kinachoweza kufanyika ni kwa Chama kimoja kuamua kuwanunua watu wote hao ili kutoa hesabu tofauti ya matokeo ya kura katika kituo na kwa raha zao wanasign kuridhia uchakachuaji huo. Lakini kama kuna pingamizi kura haziibiki kirahisi hivyo. Cha msingi kila chama ama mgombea anatakiwa aweke wakala wake mwaminifu katika kila kituo ili kulinda kura.
 
Kura zinaibwa kama zilivyoibwa mamilioni y EPA, Kura zinaibwa kama zilivyoibiwa hela katika kilimo kwanza, Kura zinaibiwa kama alivyoangushwa Mangula katika kiti cha Uenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa, Kura zinaibwa kirahisi kama JK alivyobandika picha yake kabala hajabalehe akiwa na mama yake katika mabango ya kampeni za CCM, kura zinibwa kama cheo cha Umakamu mwenyekiti wa CCM bara kilivyoibiwa toka kwa Pius Msekwa na kupewa mrithi wa ujinga wa baba ridhi1, kura zinaibwa kama Kigwangwala alivyopewa nafasi ya kugombea ubunge huku Selelii aliachwa,kura zinaibwa kama Jk alivyokubali kirahisi ofa ya kufanyiwa Birthday na vijibwakoko vya radio ya mawinguni akilipwa fadhila za kufanikisha kuupora mradi wa watu wa malaria no more bila aibu. Bado unataka tu kujua kura zitaibwa vipi? Zitaibwa kwa kuwa NEC imezidiha idadi ya wapiga kura toka milioni kumi na mbili mpaka milioni 19 ili kura zingine hewa wapewe watu fulani, kura zitaibwa kwa kuwa zimeagizwa kompyuta maaluma ambazo zitatumika kutuma kura katika server kubwa ambazo watendaji wasiojua hata kushika Mouse wanafundishwa hii leo pale Ubungo Plaza lengo ikiwa waseme watendaji wameshindwa kutumia teknolojia uchaguzi haukufanikiwa kama ilivyopangwa wakati Rais ameshatangazwa na ku,nuka kuwa mwiko kupinga matokeo
 
Mzee mwenzangu unazeeka vibaya,unapoteza hii dhana ya UZEE DAWA,VILEVILE KUWA KIBARAKA WA CCM,KUMEKUCHAKACHUA KABISA.POLE.

Sina uhakika na mtazamo wa kisiasa wa MMKJ. Lakini natofautiana na wewe kwenye hii mada kwa kuwa alichofanya ni kuuweka wazi utaratibu ili kila mtu ajue kinachotokea.

Ninatazamia ajitokeze mwingine atakayesema 'naye amewahi kuwepo kwenye mchakato' na alishuhudia au hakushuhudia wizi wa kura.

Nionavyo mimi tatizo huwa lipo kwenye kura za urais. Tatizo lipo pale zinapotangazwa, lazima tukumbuke kuwa mara nyingi wakati tume inapotangaza matokeo haya sio kila mtu huwa anafanya hesabu ya jumla kujua chama chake kimepata kura ngapi. Na kama ilivyosemwa, miaka ya nyuma kura za urais zilikuwa hazitajwi majimboni, jambo ambalo lilikuwa likiwapa Tume uhuru wa kutangaza matokeo ya urais bila kuthibitishwa na waangalizi wa vyama katika vituo vya kupigia kura katika mchanganuo wa jimbo kwa jimbo.

Hili la waangalizi ndiyo hapo kura zinapopotea. Si rahisi, kwa vyama hivi vya upinzani kupata wasimamizi WAKWELI katika vituo vyote vya kupigia kura. Wataweza kwa vituo vichache lakini SI VYOTE. Ili waweze vituo vyote, maandalizi yake yalihitaji muda mrefu ili kuweza kufanikiwa.

Na ndiyo maana, ilikuwa rahisi kwa wapinzani kushinda majimbo kadhaa kutokana na kuweka nguvu ya mawakala bora maeneo hayo.

Waungwana, tuangalie mchango huu wa MKJJ kiundani na si kudandia kishabiki.
 
jamani.. zinaibwaje? zamani ilikuwa rahisi kwa sababu sanduku linapakizwa kwenye baskeli kwenda kuhesabiwa sehemu nyingine.. siyo mnasema "wizi upo" kinadharia inawezekana lakini mtu aniambie unawezekana vipi? Wildcard anasema kuwa Zanzibar waliiba ah wapi!, kuna suala la Tume ya Uchaguzi kuingiliwa hilo limetokea Kenya na ninaamini ndilo lenye uwezekano mkubwa wa kutokea Tanzania mwaka huu..

Mzee Mwanakijiji,

Nimewahi kushiriki kuhesabu kura mara mbili na ukweli ni kwamba wizi wa kura upo na unafanyika. Nimewahi kukutana na mbinu mbili;

1. Umegusia suala la posho kwa wasimamizi wa vituo. Vyama vingi vya upinzani economic base yao si nzuri na hivyo malipo kwa wasimamizi inakua ni hela kidogo tu. Wasimamizi wa vyama kwa sababu tu ya njaa yao huwa wanakubali kuhongwa na hivyo kuruhusu matokeo yasiyo sahihi kutangazwa.

2. Mbinu ya pili ni ile ya kufunga idadi ya kura 80 badala ya 100 zinazotakiwa kwa kila fungu. Kwa yule wanayetaka ashinde zikifika kura 80 wanafunga as if ni kura 100 na kwa yule wanayetaka ashindwe, wanazipeleka mpaka 120. The idea behing hapa ni kuhakikisha kuwa idadi za kura walizopata wagombea zije ku-tally na namba ya kura zote zilizopigwa. Hii nayo inafanyika pale wasimamizi wa vyama wasipokuwa makini au wanapokubali kurubuniwa kwa pesa.

Sasa Mzee mbinu hizo zikitumika si wizi wa kura huo?

Tiba
 
Jamani siku moja Profesa Lipumba alisema alipopiga kura kwenye kituo fulani alipigia CUF(URAIS,UBUNGE NA UDIWANI)lakini matokeo yalipotoka Mbunge na Diwani hawakupata hata kura moja,sasa tuite hiyo ni nini kama sio wizi?Au mimi sielewi nini maana ya neno WIZI?
 
Back
Top Bottom