Elections 2010 Kwanini ni vigumu kuiba kura katika Uchaguzi Wetu - Tusitafute visingizio

Elections 2010 Kwanini ni vigumu kuiba kura katika Uchaguzi Wetu - Tusitafute visingizio

I know the perception.. wanaibaje kura? Mawakala hawahesabu kura!
mawakala ndio vinara wakushiriki kuiba kura,na mwaka huu wakichagua mawakala njaa ndo wataumia sana,tena kuna mpango wa kupandikiza mawakala chama ndani ya upinzani,:A S thumbs_up:
 
hii ni imani ilijengeka.. watu wengi najua wanaingia kwenye kituo cha kupiga kura na wanatoka lakini hawajui nini kimetokea kabla yao au baada yao. KUtokana na imani hii nadhani kwa kweli Tume ya Uchaguzi lazima itoe tamko la maelezo ya jinsi kura zinavyopigwa na nini kinapaswa kufanywa au kufanyika maana naona watu wengi kweli wanaaminii wizi hutokea kwenye kituo cha kupigia kura. Hili wazo ni la hatari.

Kama wizi wa namna hii haupo, kwa nini CCm na serikali yake wanazuia watu wasikae kituoni kusubiri matokeo? kwa nini wapinzani wanasema kura zao zikiibiwa damu itamwagika, CCM inatuma jeshi kutoa tamko kuwa hakuna damu itakayo mwagika? hapa wana maana kuwa kura wataiba na hakuna atakaye sema fyoo maana jeshi litakuwa tayari kuwakabili!

M.M.Mwanakijiji, nisaidie kuniondolea hofu hii ya wizi kwa kunijibu ni kitu gani kinatokea unakuta mtu anagombea udiwani anakosa hata kura moja! kwamba hata yeye hakujipigia wala mkewe, wanaye au ndugu zake? Hii inawezekana je?

Kama hakuna wizi kwa nini CCM isikubaliane na vyama vingine na kutoa tamko la kulinda kura zao wote au kukana kujihusisha na wizi? Kama hakuna wizi, kwa nini Sisiem wasiwe vinara wa kuviondolea hofu ya kuibiwa vyama hivi vidogo kwa kukubali Tume ya uchaguzi iliyo huru ambayo hata wao wanaiamini?? Kama hakuna wizi, kwa nini CCM wana behave kama wakora ktk kipindi hichi? hawana uwazi, wateule wao wote unawaona wamekaa mkao wa kuchakachua tu?

kwa kweli mimi nimeichukia SISIEM si kwa sababu nimeona mbadala bali kwa sababu wanajitambulisha kama watu wa shari wanaodhani hii nchi iliumbwa kwa ajili yao pekee yao.

SHIME TUPIGE NA KULINDA KURA ZETU WANAMAGEUZI, ISIJE IKAWA MZEE MWANAKIJIJI AKAWA NAYE UMENUSISHWA ......NA SASA ANATUFANYA TUJISAHAU!!!!
 
Malafyale.. hilo tatizo halipo mwaka huu; matokeo yanatangazwa kila kituo na kila jimbo linatangaza rasmi.. hakuna haya ya takwimu za mawakala! Na as a matter of fact.. mawakala hawahesabu kura wao wanaangalia tu, sasa hawa mawakala wa Zanzibar walileta namba zao wote wakazijumlisha na zikapingana na zile za Tume ya Uchaguzi? How realiable was their tally?

Mwanakijiji,

Nakubaliana na maelezo yako kwamba, kuiba kura ni kazi ngumu ikiwa tu mawakala watakuwa wazalendo wa kweli. Lakini naomba nikwambie kwamba uchakachuwaji wa kura za Rais ni rahisi sana kufanyika na hufanywa na wasimamizi wa majimbo. Na ndiyo sababu kubwa ya tume kuzuia kura za rais zisitangazwe kwenye vituo vya kupigia kura ili kuwapa mwanya wasimamizi wa uchaguzi waweze kuchakachuwa. Tume ilibidi iweke utaratibu wa kura za rais kutangazwa au kubandikwa kwenye vituo vya kupigia kura sambamba na yale ya ubunge na udiwani! Vinginevyo wasimamizi wa majimbo wataendelea kuchakachuwa kura za rais kama kawa!! Nawashauri chadema wabuni mbinu makini itakayohakikisha kura za urais hazichakachuliwi na hawa wasimamizi wa majimbo! Wakiweza hilo ushindi kwa Dr. Slaa ni LAZIMA!
 
Kama "wenye authority" watafanya hivyo mnachosema watafanya kwanini watu waende kupiga kura? Kama mawakala wanaweza kuhongwa kirahisi hivyo na kubadilisha matokeo wakati ni kosa la jinai kwanini watu waende kupiga kura. Maana kila ninapowasoma ninaona kuwa ni hopeless case kwenda kupiga kura:

a. NEC watamtangaza wanayemtaka
b. Kura zitaongezwa kwa wagombea wa CCM vituoni
c. Mawakal wa vyama watakatiwa kitu kidogo ili wachakachue kura
d. Kura hazitolindwa vizuri.


Kama yote a - d yana ukweli (hasa ukisoma sentiments za watu hapa), ni wazi kuwa mpiga kura wa Tanzania hana sababu ya kwenda kupiga kura. Hiki ni kisingizio cha kuwapatia ushindi CCM kirahisi, na miye nina hofu wanaokieneza wana lengo hilo kabisa.. KUWAKATISHA TAMAA WAPIGA KURA WA UPINZANI WASIPIGE KURA KWANI KURA ZAO ZITAIBWA! CCM wanajua hili. Ni lazima tukatake.. KURA HAZIIBWI NA KILA MTU AKAPIGE KURA YAKE!!!! LETS CHANGE THE MESSAGE!

Offcourse this was your main message na umesomeka vizuri.

Si vizuri kurudia mambo lakini ndani ya CCM kauli waliyonayo ni ushindi ni lazima. Kama 'great thinker' chama tawala kinapoweka kauli mbiu ya namna hiyo maana yake ni nini? nini maana ya lazima?

Pili baadhi yetu ni wazoefu wa namna kura zinavyoibwa....tumekaa kimya muda mrefu kwenye hili tusionyeshe kura zinaibwa vipi ili tuendane na makusudi mema ya kupiga kura na kutimiza wajibu wetu.

Ni kweli kabisa wakati huu hata ukweli wa mambo unaweza kutumika vibaya na mdudu mtu akapita bila kupingwa.....hivyo umesomeka vyema MM...tukapige kura kana kwamba hakuna uchakachuaji.

Nakubaliana na wewe kwamba tuache mjadala wa uchakachuaji.....lakini elezea hilo........ isipokuwa unapodai kuwa watu waelezee wizi unatokeaje...kukaa kimya haimaanishi hatujui....lakini kama unaturuhusu tutaweka hapa vizuri na kurejea matokeo mbalimbali ya kweli na tutakupa sababu kwa nini karatu na kwingineko inakuwa vigumu wakati ubungo na kawe huwa ni kama kumnyatia kiziwi.

Na pia jaribu kutafuta maana ya neno 2010 hatudanganyiki uone kwa nini Shimbo alilazimika kuingilia kazi zisizomuhusu....
 
Wizi wa kura upo. Uchaguzi mdogo wa udiwani kata mojawapo Songea mjini wanachadema ilibidi wafanye kazi ya ziada kudhibiti wizi wa kura kutoka kwa manazi wa CCM. Na walishinda.

Hii habari nilisimuliwa na kiongozi mmoja wa Chadema mkoa wa Ruvuma miaka 2 iliyopita.

Lakini kwa upande mwingine nakubaliana nawe Mwanakijiji kwamba watu waende kupiga kura siku hiyo bila kukosa. Binafsi nimewahamasisha watu walioko kwenye network yangu wasiopungua 20 wamchague Dr wa ukweli Slaa.
 
Mwanakijiji hujui wizi unavyofanyika; ngoja tukujuze

1)Wizi wa kuwanunua mawakala katika vituo vya kupigia kura
Hapa mara nyingi zile kura za watu ambao hawakujitokeza, zote hupigiwa chama fulani kwa makubaliano ya kifedha

Kubadilisha kura zote ndani ya sanduku na kuweka nyingine zenye tiki ya chama husika
(Hapa lazima mtu kutoka nje alete hizo kura mpya na ndiyo dhana ya kuambiwa ukishapiga kura nenda nyumbani)

Kuharibu kura za chama kimojawapo kwa kuongeza tiki ya pili
Kwa kuwa katika hatua hii ni makubaliano ya wasimamizi wa kituo na mawakala, fomu zote hujazwa baada ya wizi huo kufanyika

2)Wizi wakati wa kusafirisha masanduku kwenda jimboni

Baada ya kura kuhesabiwa na mawakala kupewa nakala ya matokeo, huo siyo mwisho. Masanduku hupelekwa kwenye kata ambapo kura za diwani hujumlishwa na kutangazwa; lakini kura za rais na mbunge hazifanyiwi kazi pale, masanduku hubaki yamefungwa tu lakini hupelekwa kwa msimamizi wa jimbo kwa majumuisho na uhakiki.

Wizi hapa hutokea njiani wakati wa kuyasafirisha kwani huwa hayana wakala wa chama chochote. Mawakala mara nyingi hawakubaliwi kuyasindikiza kwa visingizio kuwa si kazi yao au gari limeshajaa masanduku.
Humo njiani, hasa usiku kura ndani ya masanduku huondolewa na kuchomwa moto na kuwekwa kura nyingine. Msimamizi wa sanduku la kituo husika hutafutwa (kwa kweli kuwa anajua mpango mzima) na kutengenezwa fomu nyingine za matokeo, na wakala wa chama husika huitwa na kuweka saini kwenye fomu mpya ya matokeo na ile ya zamani huharibiwa. Kwa saini za mawakala wa vyama vingine, huwekwa saini za kufoji.

Wakati wa kujumlisha matokeo ukifika ni wazi kutakuwa na fomu mbili tofauti za matokeo ya kituo hicho; moja ni ile iliyojazwa kituoni (ambayo huwa ndiyo sahihi) na ile ambayo imejazwa njiani baada ya kuchakachua. Kwa vyovyote vyama vitabishana juu ya fomu ipi ni sahihi, kila chama kikivutia upande wake – suluhu ni kufumgua tena lile sanduku na kuona exactly kuna nini ndani. Na kwa kuwa kura zilishabadilishwa njiani, fomu ya chama husika itaonekana kuwa na matokeao sahihi na hata kama kutakuwa na utofauti bado, kura zitakazotambuliwa ni zile zitakokuwa kwenye sanduku – zilizochakachuliwa. (nadhani umenielewa)

3)Wizi mezani: Hapa ni mabavu ya dola tu hutumika na kutangaza kuwa Fulani kashinda,Utakuta FFU na Polisi wamejaa na magari ya maji ya upupu yamewekwa standby kabla ya matokeo kutangazwa. Ukiona dalili hizo ujue kuwa dola inajiandaa kutoa matokeo yasiyowaridhisha wananchi (Hii sijui njia ya kuidhibiti)



Njia za kudhibiti wizi huo:

Kwa kuwa kila karatasi ya kupigia kura huwa ina namba, na kwa kuwa kila msimamizi wa kituo hukabidhiwa vitabu hivyo kwa namba; yafuatayo yafanyike

1)Kila chama kipate nakala ya namba za vitabu vya kupigia kura vilivyopelekwa kila kituo
2)Mawakala waelekezwe kunukuu namba za vitabu kwenye kituo kabla upigaji kura haujaanza na msimamizi awadhibitishie kuwa hivyo ndivyo vitabu alivyopokea toka msimamzi wa jimbo
3) Iwe ni lazima kwa kila wakala kusaini fomu ya matokeo kituoni na kama ana malalamiko yoyote yale ajaze kwenye fomu ya malalamiko (unajua mkiachia wa CCM pekee akasaini, hata ikijabadilishwa anatafutwa huyo mmoja anasaini na mchezo unakuwa umeisha)
4) Wakati wa kuhesabu kura, iwe vituoni au wakati wa kuhakiki katika ngazi ya jimbo (ambako huwa ndipo matokeo huwa yameshachakachuliwa), kila sanduku la kura lihesabiwe peke yake na ihakikishwe kuwa namba za karatasi zilizozomo zinaoana na namba alizokuwa amekabidhiwa msimamizi wa kituo na mawakala wawe wametoa taarifa kwa vyama vyao juu ya namba zilizotumika kwenye vituo vyao.
5) Kwa kuwa mawakala ndio wameaminiwa na vyama vyao, wayasindikize masanduku ya kura hadi jimboni pale uhakiki na utangazaji unapofanyikia. Kuyasindikiza hadi kwenye kata na kuishia hapo hutoa mwanya kwa watendaji wa kata kushirikiana na CCM kuyabadili. Sanduku lolote litakalowasilishwa bila mawakala litengwe na lihasabiwe tofauti na kama litakuwa na kura tofauti na fomu za mawakala, likataliwe - Nakumbuka hii ilifanyika Temeke wakati Mrema akigombea. Ni marufuku mawakala kusafiri tofauti na masanduku yao - magari yabebe masanduku kidogo na mawakala.


6) Mwakala wapewe elimu ya kutosha na wajue kuwa wanamuwakilisha mgombea, wasiwe tayari kununuliwa –kuna thread nzuri humu yenye kipeperushi juu ya elimu.
 

Attachments

mmh.. Jamani mnataka wote tuanze kuimba "kuna wizi wa kura" wakati kiakili haikubaliki hata kivitendo? Hakuna mtu hata mmoja ambaye amewahi kuonesha kura zinavyoibwa ambaye siwezi kuonesha ni kwa jinsi gani hilo atakalopendekeza haliwezekani. Nimeweka ushahidi wa kiakiil kuwa kama kuna maeneo ccm wangeweza kweli kuiba kura na walikuwa na sababu ya kufanya hivyo ni moshi mjini na karatu.. Kwanini hawakuiba?

Anayejua kura zinaweza kuibwa tanzania kituoni aseme basi nimsikilize.. I'm open minded. Ila tusiwatafutie watu kisingizio.. Ushindi na kushindwa katika hili uko mikononi mwa chadema na miye nawasupport kwa asilimia 100 kushinda lakini siyo kwa kulilia "tutaibiwa kura". Ushindi utakuja kwa kupata kura nyingi period! Now.. Go and get them! Washawishi watu wapige kura, wasihi watu waichague chadema n.k lakini hilo la wizi ... Miye kwa kweli simo..

naomba tuchukue muda kumwelewa mwanakijiji, anauliza mbona kila mara moshi mjini cc, wanashindwa kuiba kura? Mbona kwa zitto walishindwa? Mbona tarime walishindwa. Kilichofanyika huko mwaka 2005 na katika uchaguzi mdogo ndicho kinachotakiwa kufanyika mwaka 2010 na hoja ya kura kuibiwa itashindwa kufanya kazi. Hebu tujiulize ni nini kilfanyika katika majimbo hayo ambayo chadema ilipata ushindi?
 
naomba tuchukue muda kumwelewa mwanakijiji, anauliza mbona kila mara moshi mjini cc, wanashindwa kuiba kura? Mbona kwa zitto walishindwa? Mbona tarime walishindwa. Kilichofanyika huko mwaka 2005 na katika uchaguzi mdogo ndicho kinachotakiwa kufanyika mwaka 2010 na hoja ya kura kuibiwa itashindwa kufanya kazi. Hebu tujiulize ni nini kilfanyika katika majimbo hayo ambayo chadema ilipata ushindi?
Obvious mbinu iko Rahisi Hayo Majimbo yalikuwa au yana wabunge/wagombea wakweli na wachapakazi... so this tell us that what matters is putting competent aspirants. Wizi wa Kura ni Strategy ya CUF ambayo ilishindwa all the way. CHADEMA yaweza iga kama inaona it is a working strategy.
 
Anachosema mwanakijiji ni kuwa...Jukumu letu watanzania ambao tumejiandikisha kupiga kura ni kwenda kutumia haki yetu ya kupiga kura siku ya Jumapili tarehe 31 Oktoba; Period!
Hofu ya kuibiwa kura iliyopo miongoni mwa wanajamii ni kubwa na ndio itakayopelekea wananchi wengi waliojiandikisha kukata tamaa ya kupiga kura. Kuna watu wengi sana, hususan vijana ambao walikosa kujiandikisha, kwa kuwa waliona hamna maana yoyote ya kufanya hivyo kwani kwa mtazamo wao hata wangejiandikisha na baadaye wakapigia kura vyama vya upinzani, CCM itashinda tu (kwa hofu hiyo hiyo ya kuibiwa kura)

Na sasa kuna baadhi ya wengi waliojiandikisha wameshaanza kuwa na hofu ya kuibiwa kura na kuona kwamba hata siku ya uchaguzi ukifika hawataenda kupiga kura kwani CCM itashinda tu, na hata kama watapigia kura upinzani, CCM wataiba kura na kuwa washindi.

Hii hofu ni mbaya na ndio maaana Mwanakijiji anasema kazi yetu sisi tuliojiandikisha ni kwenda kupiga KURA siku ikifika.

Well said! Hakika wewe umemwelewa Mwanakijiji kama mimi nilivyomwelewa!
 
offcourse this was your main message na umesomeka vizuri.

Si vizuri kurudia mambo lakini ndani ya ccm kauli waliyonayo ni ushindi ni lazima. Kama 'great thinker' chama tawala kinapoweka kauli mbiu ya namna hiyo maana yake ni nini? Nini maana ya lazima?

Pili baadhi yetu ni wazoefu wa namna kura zinavyoibwa....tumekaa kimya muda mrefu kwenye hili tusionyeshe kura zinaibwa vipi ili tuendane na makusudi mema ya kupiga kura na kutimiza wajibu wetu.

Ni kweli kabisa wakati huu hata ukweli wa mambo unaweza kutumika vibaya na mdudu mtu akapita bila kupingwa.....hivyo umesomeka vyema mm...tukapige kura kana kwamba hakuna uchakachuaji.

Nakubaliana na wewe kwamba tuache mjadala wa uchakachuaji.....lakini elezea hilo........ Isipokuwa unapodai kuwa watu waelezee wizi unatokeaje...kukaa kimya haimaanishi hatujui....lakini kama unaturuhusu tutaweka hapa vizuri na kurejea matokeo mbalimbali ya kweli na tutakupa sababu kwa nini karatu na kwingineko inakuwa vigumu wakati ubungo na kawe huwa ni kama kumnyatia kiziwi.

Na pia jaribu kutafuta maana ya neno 2010 hatudanganyiki uone kwa nini shimbo alilazimika kuingilia kazi zisizomuhusu....

mimi naona mnkj tumemuelewa kuwa kwa kulalama lalama kuwa kuna wizi wa kura kunawakatisha tamaa wapiga kura. Al of us should be positive. Lakini vile vile ni lazima tukubali mwisho wa uwezo wetu. Kwa sasa nashiriki katika kufanikisha kampeni za mgombea mmoja wa chadema na kubuni mikakati ya kulinda ya ulinzi wa kura.

Kwa kweli i wish all of us had joined chadema 3 years ago, insted of just being mere spectstors. Tukajenga mtandao wenye kuweza kuhimili trust ambayo watanzania wanaionyesha kwa chadema.
 
jamani, matokeo ya kura yakibadilishwa mtu anaweza kwenda kufungua kesi kwani masanduku yale hayatupwi. Kwamba kuna uwezekano wa kuwa na ukiukwaji wa taratibu hilo lawezekana lakini massive rigging sasa hivi nimesema ni "ngumu mno"... Tusiwatishe watu kuwa kura zao zitaibwa. Kura wakapige kwa wingi kwani hiyo ndiyo njia pekee ya kuzuia uwezekano wa wahalifu kuchakachua upigaji kura.


Masanduku huwa yanahifadhiwa bohari, je kuna usalama gani apo?
 
Mwjj naomba unijibu haya maswali.

a)Ushawahi kusimamia uchaguzi?
b)Lini ilikua mara yako ya mwisho kupiga kura tz?
 
Mwanakijiji.
Kura zinaibiwa sana, mimi binafsi nilishuhudia mwaka 1995 kwenye uchaguzi mkuu. wakati huo nilikuwa Dodoma. Augustine Mrema alipata kura nyingi sana kata ya Kikuyu kwa sababu ya shule ya Mazengo, kwa macho yangu nilishuhudia kura hizo zikihamishwa wakati huo polisi akiwa ndani ya chumba walichokuwa wakitumia kuhesabu kura. Hata Aliyekuwa mbunge wa Dodoma mjini Hashim Saghaf alifaidika na hiyo operation chafu.
Anyway, kwa kifupi kura zinaibwa sana.
 
Haiwezekani mtu yuleyule aliyakuwa kinara wa kushabikia chama hewa kilichobuniwa na CCM cha CCJ leo aje atufundishe ikiwa kura huwa zinaibwa au laa
 
Nami nakubaliana na mwanakijij Chadema inatakiwa kuwa makini na wanchokisema ni vigumu sana kuiba kula kama waonavyo cha msingi kuwashawishi watu wapige kura kuliko watwaone sasa wakapige kura za nini wakati wataiba haha

Hebu tuangalie baadhi ya hoja zako kwa kifupi tu...................Kwanza umejijibu mwenyewe kuwa wizi wa kura yawezekana sasa maandishi mengi ni ya nini?

[/B]Kinachofanyika na ambacho huwa kinafanyika ni kuwanunua mawakala wa vyama vya upinzani jambo ambalo ndilo liliigharimu Chadema karibu viti vyote vya Tukuyu na vinginevyo wakati wa By-elections isipokuwa jimbo la Tarime. Kwa hiyo hoja yako hii hapa chini siyo ya kweli hata kidogo:-



Kama CCM iliweza kuwarubuni wagombea wa vyama vya upinzani kuwapelekea fomu walizozichukua kugombea ubunge na udiwani kwa malipo yanayosadikiwa kati ya Tshs 20-50milioni kwa ubunge na Tshs 0.5 hadi 2 milioni kwa udiwani watashindwa kuwarubuni mawakala ambao wengi wao ni njaa tupu?

Kuhusu kuwa na mawakala vituo vyote wala siyo suluhisho kwa sababu kama mawakala siyo waaminifu watarubuniwa tu.

Baada ya mawakala kurubuniwa watasaini matokeo ambayo hayashahibiani na hesabu za kura na yule ambaye hastahili atakuwa amechaguliwa kuwa kiongozi haramu.

Kuhusu kutokuwepo hukumu kwenye mahakama zetu kuhusiana na matokeo ya kura kuchakachuliwa ulioiibua kwenye mada yako:-


Tatizo la hii hoja yako ni kuwa si maeneo yote yenye kero za wizi wa kura mahakama ilikwisha kuyapokea na kuyayafanyia kazi na hivyo kumaanisha ya kuwa mahakama hapa haitusaidii sana kuelewa sakata hili. Mahakama hushughulikia hoja zilizopo machoni pake na kamwe haishughulikii hoja ambazo hazijalalamikiwa. Kwa lugha nyingine ili upate uhimili wa kimahakama katika hoja zako inabidi uthibitishe ya kuwa maeneo ambayo tunahofu ya kura kuibiwa yalikwisha kushughulikiwa na mahakama zetu kupitia malalamiko kadha wa kadha ambayo ungeliyataja.

Labda kuongeza ufahamu wetu kwenye hilo ningependa kutoa mfano wa jimbo la uchaguzi la Starehe nchini Kenya. Jimbo hilo aliyeshinda mwaka 2007 alikuwa ni Askofu Magreth Wanjiru wa ODM lakini mpinzani wake Bw. Kamana wa PNU alikwenda Mahakamani kubisha ya kuwa matokeo yaliyotangazwa hayakuheshimu kura zilizopigwa na akaomba uhesabuji wa kura urudiwe. Hili ombi mahakama zetu hazijawahi kulisikiliza na kwa hiyo huwezi ukasema ya kuwa hakuna uchakachuaji wa kura kwa vile mahakama hazijathibitisha. Mahakama haziwezi kuthibitisha mambo ambayo hayajalalamikiwa.

Mahakama kuu ya Kenya iliagiza "recount" na matoeko yake Kamana Maina akaonekana kumbe ndiye aliyepaswa kutangazwa na msimamizi wa uchaguzi kuwa ni mshindi lakini asiyestahili ndiye aliyetangazwa mshindi yaani Askofu Magreth Wanjiru. Huyu Askofu alikwenda kuwa Naibu Waziri wakati ni kihiyo tu. Hii ndiyo hali halisi ya chaguzi zetu na ndiyo maana viongozi tulionao ni wabovu na wala siyo wananchi hawajui kuchagua viongozi wazuri ila mfumo uliopo unaruhusu uchakachuaji wa matakwa ya wananchi.

Wizi wa kura wa kutoheshimu matokeo ndiyo ulio mkubwa hapa nchini na hata hapa Arusha ninaamini ya kuwa Bw. Lema alimshinda wa CCM aitawaye Felix Mrema jimbo hili mwaka 2005 na endapo kura zingelirudiwa kuhesabiwa kingelikuwepo kilio na kusagaga meno kwa CCM. Lakini Bw. Lema hakwenda mahakamani kwa sababu ambazo zipo nje ya mada hii, hivyo sitazijadili.

Wizi wa pili ambao safari hii huenda ukatumika ni kumwongezea mgombea kura na hili wasiwasi umeongezeka kutokana na NEC kutuzuia wapigakura kulinda kura zetu tukiwa mita 200 kutoka kwenye vituo vyetu vya kupiga kura!!!!!! Wanasema twende nyumbani na tutajulishwa matokeo tu. Sasa tutajuaje ya kuwa baada ya sote kuondoka mawakala na wasimamizi wakashirikiana kubadilisha kura ndani ya maboksi ya kura ili kumbeba mgombea ambaye tayari ameshindwa uchaguzi? Hata ukienda mahakamani na maboksi yaliyochakachuliwa bado utajikuta umeshindwa tu.

Hili linawezekana kwa sababu NEC haina watumishi wa kudumu na inategemea watumishi wa umma kutoka serikali za mitaa. Tumeona jinsi wakurugenzi wanaotenda haki kama yule wa hapa Arusha Bw. Mbuya CCM imembughudhi kwa kutofanya yale ambayo wao wanataka. Sasa itakapokuja kuchakachua matokeo kwa kubadilisha kura ndani ya maboksi ya kura tuwategemee hawa makuhani wa CCM kutenda haki jamani? Let us be fair and reasonable on this...........

Mwisho kauli yako hii ya kutubeza wale wenye hofu na kuchakachuliwa matokeo kuwa hatujui utaratibu wa upigaji kura hapa nchini zinakera kwa sababu kwanza hutujui lakini umekuwa mwepesi sana kutuhukumu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Kweli hili limenishangaza sana na kunisikitisha mno........ We are doing this for ourselves but for the benefi of our posterity and nothing less......Tungeweza kunyamaza na kusema watajijua kwani ugali mezani si upo lakini kama una kiona mbali lakini hukitumii kwa manufaa ya wenzio hata kama wewe hupati kitu machoni pa Mwenyezi Mungu wamchukiza.....Ndiyo maana tunajitolea kuelimisha umma ambao ndiyo ulitugharimia sana kuipata elimu hii.......................Kwa siku zijazo kauli kama hii uitafakari kabla ya kuitoa.....


hayo maeneo machache ambaye vyama vya upinzani vimefanya vizuri ni kuwa vina mtandao mkubwa wa kulinda matokeo yao na wapiga kura walikuwa hawazuiwi kuwa mita 200 nje ya vituo vya kupiga kura kama itakavyokuwa safari hii.

Uchaguzi lazima uthibitiwe na wapiga kura siyo wasimamizi, mawak
 
mzeePunch uwa unaskiza habari wap?? hapo tunakataa iyo habari yako... hivi kwann nyie watu mnataka kufanya JF kawa ya kihuni??hiyo ishu ya gari ni nyingine ambayo dokta slaa aliisema ikiwa uku maeneo ya tunduma tena mpakani..
hivyo usiPotoshe UMMA
 
Maelezo mazuri kwa uhamasishaji tuende kupiga kura lkn kwa wizi wa kura upo tena wa kutisha,

  • Jimbo la magogoni znz,uchaguzi mdogo uliofanyika hivi karibuni,wakati wa kuhesabu kura hafla umeme ulizimwa unguja nzima,hafla waliingia ffu na gari lao,wakaingia ndani then wakatoka,inasemekana walitoka na sanduku la kura,kwa maana hiyo walibadilisha.
  • Jimbo la rahaleo nakumbuka,mgombea mmoja wa ccm,alisema lirudiwe mara mbili kuhesabiwa,mara ya tatu,akaling'ang'ania sanduku,huku yule wa Cuf nae akawa hakubali,mara polisi wakaingia wakam-beba yule wa cuf,hakuonekana kwa muda mrefu,viongozi wa cuf walimfatilia sana walishindwa..
  • Jimbo la kiembe samaki, mansur alikuja na gari la wapiga kura feki,huku likilindwa na ffu,wakapiga kura then wakaondoka na wakati wa kuhesabu kura mawakala wa Cuf woote walitolewa nje..
  • hivi sasa znz ktk daftari baada ya kupewa vyama vya upinzani, Cuf wamegundua takriban kura zao kama alfu sabiini watu wamekatwa hawamo,na kuna kura hewa karibu alfu tisiini,habari za ndani lkn.
  • Dar hakuna asiejua uchaguzi ulopita ccm walivofanya uzushi kweye karatasi tena kwa habari za ndani wameshirikiana na taifa moja kubwa duniani.
TAHADHARI: SAFARI HII HATA KALAMU NINA WASI WASI NAZO,NAWAUSIA WATANZANIA WENZANGU TUCHUKUENI KALAMU ZETU.. TUSIWAAMINI HAWA MAFISADI.
 
Mada hii ingeletwa na mtu mwingine kama MS kungejaa matusi hapa au shutuma kwamba katumwa. Kaileta Mwanakijiji JF wamesalimu amri. Double standard!!
 
Back
Top Bottom