MADIBA MANDELA
JF-Expert Member
- Mar 2, 2014
- 503
- 398
Duh JF kweli naelimikaga sana tu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naunga mkonyo hoja.....ni kwel na sahihi
Ndiyo maana nilisema kwenye conclusion kuwa mwisho wa siku kila mtu ana mipango yake, wewe kama hauna idea ya ujasiriamali soma then pita, waachie wenye interest. Ndiyo maana kwenye hii forum kuna watu wanakuja na idea zao za kufuga bata, wengine machungwa
Mods Tafadhari usiunganishe uzi huu ili tufanye uchambuzi wa ki uchumi hapa na wadau.
Wiki iliyopita nili post uzi unaozungumzia ni jinsi gani utakuwa Middle Class, yaani kuteseka ki uchumi ,kama ndio kwanza unaanza maisha na unafuata fumula ya walio wengi, yaani kununua gari then kujenga nyumba
Ebu tuanze uchambuzi.
Kwa upande wa gari.
Bei ya chini kabisa ya gari used ni Tsh Milioni 5 au 6 mafano Vitz.
Tuweke kiwango cha chini kabisa cha matumizi ya mafuta kwa siku ambapo utatumia lita 5 hadi 6. Kwa siku utatumia 6X2,250=13,500/- kwa siku. Kwa mwezi itakuwa 13,500X30=405,000/-
Kwa mwaka 405,000X12-=4,860,000. Ukiweka Service na gharama zinginezo kama road license, bima, oil nk inafika milioni sita hadi saba kwa mwaka. Milioni saba ni sawasawa na kusomesha watoto 5 katika English medium school . Piga hiyo hesabu kwa miaka 5 utapata habari yako, na ndani ya miaka kama ingekuwa ni biashara ingekuwa mbali, au kukitokea makosa itakufa pia
Kwa upande wa Nyumba.
Nyumba ya kuishi utatumia milioni 40 au 50 kujenga nyumba ambayo itakusaidia ku serve kodi ya 150,000 kwa mwezi wakati kwa kutumia M40 ungetengeneza asset inayozalisha M1.5 kwa mwezi.
Nyumba ya kupangisha ni Idea nzuri lakini tathmini inaonesha nyumba ya kupangisha inatumia miaka 10 hadi 15 kurudisha hela, inategemea na mahali ilipo.
Kwa mambo kama haya ndiyo maana utakuta mtu kila mara analia kuwa haoni hela yake inakwenda wapi, lakini kasahau kuwa anahudumia gari.
Watu wengi hatuna utamaduni wa kuweka kumbukumbu ndiyo maana siku ile watu walisema maisha hayana fumula, wengine wakasema nanunua ndinga kwanza mambo mengine baadae. Tatizo liko hivi ukianza na gari, uje nyumba then uhamie kwenye business itakuwa ni too late kwako hasa ki umri, uzoefu unaonesha kwa watanzania waliowengi tunajenga nyumba kwa taratibu sana kutokana na kipata, leo unapata laki 1 unanunua bati 9, mwezi ujao siment mifuko 5.
NB: Mimi naona ni bora ukawekeza kwenye vitu vinavyozalisha kwanza then Gari na Nyumba vitakuja baadae, yaani vi hudumiwe na biashara zako, lakini siyo mshahara wako.
Hayo ni maoni, vinginevyo kila mtu ana malengo yake
Paragraph number 1 pumba tupu, hope utakuwa na vitz...............Mimi nakubaliana na wewe mkuu,ila inategemea unaishi mkoa gani,kwa mkoa kama Dar gari ni kitu cha lazima aisee otherwise hata ufuatiliaji wa miradi yako utakuwa mgumu.Jambo la kuzumgumzia hapo kwenye gari ni kuhusu kununua gari ambalo ni economy na si kutaka sifa kununua gari la CC nyingi na luxury wakati huna kipato cha ziada.
Ukianza biashara ukiwa kijana unajifunza mengi sana kuliko kusubiri mpaka umalize kujenga japo si kila mtu atajenga nyumba kwa muda mrefu,kama hela ipo jenga fasta umalize then uingie kwenye biashara mazima ukiwa kwako stress free.
Anyway topic hii ina mambo mengi ambayo ni variable from mtu na mtu,1.mazingira 2.Ability to take calculated risk 3.business knowledge 4.kipaumbele cha mtu kutokana na changamoto aliyonayo.5.opportunity available.n.k.but kwa mtizamo wangu, cash flow is first thing,yaani kufanya vitu ambayo vitaongeza mzunguko wangu wa fedha kwanza,na hapa ndo tunapotofautiana,mwingine anaona aanze na biashara bcz anaujuzi na uzoefu fulani kwake risk is very low,but some people bcz hana ujuzi na uzoefu wa biashara the best ni kutumia mshahara kujenga na kuridhika na kidogo,but financial freedom start with investment that will insure positive cash floww then spending but not all can afford this.