Kwanini nyumba ikifika hapa inakuwaga ngumu kumalizia?

Kwanini nyumba ikifika hapa inakuwaga ngumu kumalizia?

Tafizo binadamu mbwembwe nyingi mnoooo. Mara sijui choo cha million tatu tile 120.000 per sqm. Wewe jenga kwa uwezo wako basi.
Pagumu kupau tuu kwenye ujenzi maana inahitajika hela ya mkupuo.
Kwengine kote easy tuu.
Uita fundi maikl anatemgeneza chumba kimoja baada ya miezi mitatu akuja kutegeneza chingine
Hii point nimeichukua
 
Nguvu ya kuanzia msingi hadi kwenye lenta inakuwaga ya kasi san,a kuanzia hapo hadi kumalizia wengi hurudi nyuma nini shida?

View attachment 3086249
Siyo hatua zote ni ngumu kumalizia. Hatua ngumu hapo ni kuweka paa tu kwa sababu inahitajika hela za pamoja ili kuweka paa tofauti na huko nyuma ulikuwa unaweza kujenga boma kidogo kidogo na hakuna madhara. Ila hauwezi kuweka nusu paa japo watu wanafanya.

Ukiishapaua, hatua zinazofuata pia unaweza kuzifanya kidogo kidogo mfano kuweka madirisha machache au plasta baadhi ya vyumba, nk.
 
nenda kiwandani au dukani wekeza bati utashinda tu
 
Mimi fundi alinipigia kuwa tatumia mbao mia mbili...lakini mpaka anamaliza kupaua nilitumia mbao zaidi ya miatatu....
Nikimuuliza vipi mbona ulikadiria kidogo akaishia kucheka,akasema "boss ningekuambia mbao mia tatu usingekubali tuanze kazi"...
Ujenzi ni process kwani unapanga hiki mara kinatokea kingine....
Bahati nzuri kuhusu bati nilikua nanunua mdogo mdogo huko nyuma,nilinunua bati nyingi hadi nyingine zilibakia😂😂

Fundi aliekadiria bati alizidisha makadirio.
NILICHOJIFUNZA
Vijana wengi tunaishi kwa matumaini ya kuwa na pesa nyingi huko mbeleni lakini inaweza kuwa si kweli...
Kama una kiwanja anza kujenga na hizo hizo laki mbili zako unazopata.
Punguza matumizi yasiyo na ulazima.
Nikipiga thamani ya nyumba yangu hadi sasa ni kama milioni 50 lakini sijawahi shika hata milioni 10 cash na wala sijajenga kwa mkopo na sidaiwi na mtu yoyote....
Kujenga ni process na inahitaji uvumilivu
 
Mimi fundi alinipigia kuwa tatumia mbao mia mbili...lakini mpaka anamaliza kupaua nilitumia mbao zaidi ya miatatu....
Nikimuuliza vipi mbona ulikadiria kidogo akaishia kucheka,akasema "boss ningekuambia mbao mia tatu usingekubali tuanze kazi"...
Ujenzi ni process kwani unapanga hiki mara kinatokea kingine....
Bahati nzuri kuhusu bati nilikua nanunua mdogo mdogo huko nyuma,nilinunua bati nyingi hadi nyingine zilibakia😂😂

Fundi aliekadiria bati alizidisha makadirio.
NILICHOJIFUNZA
Vijana wengi tunaishi kwa matumaini ya kuwa na pesa nyingi huko mbeleni lakini inaweza kuwa si kweli...
Kama una kiwanja anza kujenga na hizo hizo laki mbili zako unazopata.
Punguza matumizi yasiyo na ulazima.
Nikipiga thamani ya nyumba yangu hadi sasa ni kama milioni 50 lakini sijawahi shika hata milioni 10 cash na wala sijajenga kwa mkopo na sidaiwi na mtu yoyote....
Kujenga ni process na inahitaji uvumilivu
Kweli
 
Nguvu ya kuanzia msingi hadi kwenye lenta inakuwaga ya kasi san,a kuanzia hapo hadi kumalizia wengi hurudi nyuma nini shida?

View attachment 3086249
Sababu ni kuwa kuanzia hapo, vitu vingi ni lazima ufanye kwa mara moja.. mfano, huwezi kupiga kenchi au kupaua kwa kidogo kidogo, au kupiga rangi mara nyingi kazi hizo zikianza inabidi umalize hivyo zinahitaji hela nyingi kwa wakati mmoja.
 
Mwisho wa yote, hiyo kazi imenyooka sana. Heshima kwao mafundi.
 
Back
Top Bottom