Kwanini Polisi walishindwa kuifichia aibu familia ya Mzee David Makerege? Yesu aliwaambia "asiye na dhambi miongoni mwenu awe wa kwanza kumtupia jiwe"

Kwanini Polisi walishindwa kuifichia aibu familia ya Mzee David Makerege? Yesu aliwaambia "asiye na dhambi miongoni mwenu awe wa kwanza kumtupia jiwe"

Naunga mkono hoja, wangeyaficha majina ya wote wawili at this stage kwa ajili ya kulinda heshima ya wanafamilia. Sababu ni kweli aibu ya si ya aliyekufa ila wanaobaki
 
Tatizo ni social network, and bad enough ni kwamba kila mmoja anataka awe wa kwanza kupost bila kujali athari ambazo wahusika watapata.

Nadhani ipo haja ya mamlaka kuchukua hatua kwa sababu habari zinaenzwa pasipo kujali chanzo mahususi cha habari husika na kimsingi habari nyingi zinazoanzia mitandaoni hasa ile isiyo jali reputations na newworthness.

Ninaamini katika taaluma inayohitaji umakini ni hii ya uandishi wa habari ingawa ndo tauma iliyojaa makajanja ambao mwisho wa siku ndo hawa wanapoteza maana kabisa ya Habari.
Waandishi wa habari wana changamoto zao lakini Polisi pia hawakutumia busara katika hili mkuu.
 
Yaani polisi wasitoe taarifa rasmi kwa lengo la kulinda heshima/kumfichia aibu marehemu?

Unajua kuwa Mambo ya kisheria huwa hayana kupindisha?
Wanamtolea nani taarifa? Hana familia?
 
Wewe ndio umeharibu kabisa maana wengi hatumjui na wala hili tukio Mimi nilikuwa zilijui maana sijalisikia wewe umenijuza na picha umenionyesha niwalaumu polisi au wewe uliyeweka msisitizo?

Siku nyingine ukiona habari kama hii ilete bila picha. Kuhusu huyo Mzee kwa umri huo alitakiwa awe nyumbani anacheza na wajukuu kama Sisi wengine tunavyofanya.
 
Yesu aliwahi kusema kwamba "asiye na dhambi miongoni mwenu awe wa kwanza kumtupia jiwe mtu huyu"
Kwani wewe umefikiria hotelini na huyo binti walikuwa wanafanya mambo gani. Labda walikuwa na mambo yao mengine mbona polIsi hawajasema zaidi ya kufia hotelini na binti amekutwa chumbani.
 
Hata kibiashara pia jina la hotel or logde linaharibiwa kiasi navyoona..kuna lodge ile kuna mtu alifia ndani..haikaa poa sio?

Wafanye uchunguzi kimya kimya then ripoti wapatiwe viongozi wa familia..najua mitandao ipo lakini kasi ya kusambaa habari haiwezi kufananishwa na habari official kutoka Press ya RPC
Hivi unajua bongo wanavyozini, nenda leo pale pale ukipata room nakupa laki.
 
Back
Top Bottom