#COVID19 Kwanini Rais ameamua kujificha nyuma ya kamati ya Corona? Anaogopa nini kuwambia Watanzania wajiandae na AstraZeneca? Anaogopa nini?


Inawezekana hatuelewani.

"Wote tunajua hata influenza za kawaida tu zinawaua wazungu kuliko hata Corona.... So sio jambo jipya kwa mafua hatari kma swine au bird flu kuua sana nchi za magharibi. Otherwise wangekufa wengi zaidi if wasinge weka sheria kma za lockdown au wasingekua na medical facility nzuri"

Hebu fafanua vizuri ulichokieleza hapo juu.
 
Side effects za Astrazeneca ni zipi?
 
Wewe ndio una safari ndefu possibly elimu na exposure ndogo sana.

Chanjo inayopigiwa kelele ni ya Oxford na ambayo imeshadungwa watu million 17 ulaya pekee na waliopata madhara hawafiki 100 ambayo ni chini ya 0.00001 sasa inatosha kudiscredit hiyo chanjo?

Then unajua kwamba ARVs na chemotherapy (wagonjwa wa kansa) zinaua zaidi kwa watumiaji. Ni lini sasa tutasitisha kuwapa wagonjwa wa kansa chemotherapy na ARVs kwa wenye VVU au wwe uchungu wako ni Chanjo hii tu.

Nilichogundua waTZ wengi hatuna exposure, hatusomi tafiti/vitabu (Lugha changamoto), Elimu changamoto... Ndio maana tunaropoka tu vitu bila kujiridhisha kwanza.
 
Elimu yangu sina uhakika kama ni sahihi au la maana ni mitahala hii hii ya wazungu iliyochini ya necta.. Ngazi nilizofika pengine ni ndoto zako kufika hapo sio busala sana kusema sana. Kuhusu exposure niliyonayo iko beyond ur bars.. Pia si vema sana kujinadi.

Tukirudi kwenye hoja mama.

Kwanza umekosea sehem ya uchungu wangu kwa ARVs na CHEMOTHERAPY kimsingi mabadiriko hayaanzi kama mwanga uingiapo jichoni baada ya kulifumbua.

Tunaanza na lililopo na sio kosa tulilofanya mkuu, hivyo kuanza kuweka doubt juu ya hiz chanjo n mwanzo mzuri kwasabb ni kweli zinamdhara.

Umesema 17mil ya watu wamepat hiyo chanjo which is not ni above 50mil... Waliopata madhara ukisema hawazid 100 n uongo kwan hakuna takwimu rasmi. Arafu kwa namna tu hali ilivyo ni ngum sana kupata uhakika wa data hizo kwasababu zimezingilwa na utata na siri sana.

Mwisho.
Chanjo hizi hazijatibu mtu aliyekitandani hazijamponya aliyeugua chanjo hizi hazijaleta uhakika wa kupunguza speed ya maambukizi na ikiwa waliopata chanjo wako salama kwann waanze kupta mashaka ya kuchangamana na wengine...??? Which means uhakika wa hiyo vaccine ni mdg mno kufanya kaz vema. Pia kusema waliokufa n wachache embu fikiria idadi hiyo ndogo ikakuangukia ww na wazaz wako hilo ndilo ttzo kubwa
 
Hili suala!! Linahitaji tafiti Kweli za kisayansi, Ila maamzi yake yanahitaji Hekima kuliko huo utafiti wa kisayansi
Hivi kweli kwa hali ilivyo, tunahitaji huo utafiti? mbona kama tayari tupo kwenye utafiti na matokeao tunayaona. utafiti unaonyesha maisha yaendelee, corona ni ugonjwa kama magonjwa mengine ambayo yanaweza kukupata na ukafa. Hakuna athari kubwa zilizoonekana kwetu, watu wanaendelea na shughuli zao kama kawaida, hawavai barakoa, hakuna lockdown, wala social distance na kila kitu kipo owkey. Hatuhitaji kamati wala babaake kamati.
 
Unataka tuweke lock down, huo ndio utaalam unaotaka, hao wenye lock down wanakufa wengi zaidi ya Tz sasa nini faida ya lockdown ? SSH ana tatizo, tena ni KUBWA.
Unajuaje kwamba wanakufa wengi zaidi kuliko Tz wakati Tanzania hawajatoa takwimu za gonjwa la Corona tangu April mwaka jana?.
 
Mama anaficha tu makucha. Covid tumeishinayo tangu wakati wa kipenzi chetu... Nini hasa asichokijua huyu mama, hiyo kamati ina jipya gani? Yani mapema sana mambo yameanza kuwa kiza. Kweli mwanamke ni mwanamke tu! Wapiga vigelegele muda sio mrefu mtaanza kutafuta leso kufutia machozi.
 
Kenya wanaofuata COVID19 protocols wako wapi?
Je hamsikii hosptali na mfumo wa afya ulivyozidiwa?
Mbona bongo tunaishi na vizuri tu na maisha yanaendelea kama kawaida?
Tunataka maisha gani zaidi?

Hujaenda Muhimbili wewe.. achilia mbali hospitali zingine. Mimi nimeshuhudia Muhimbili, wodi ya Mwaisela. Pale ni corona tupu.! Ukiwa confirmed kuna wodi maalum kabisa iko opposite na Kanisa unapelekwa (nyumba ya chini ina bati la kijani).. pale ndio wagonjwa wa corona wanakuwa isolated kabisaa. Hali si nzuri. Mko nyuma ya keyboard mnaongea utopolo. Watu tumepoteza wapendwa wetu, nyie mnasema nini?! Mama katumia busara sana kuanza na kamati, kumaliza mzizi wa fitina.
 
Yaani Influenza zimewasumbua sana nchi zenye baridi kwa miaka mingi yaani hata mafua nadhani unakumbuka mafua ya nguruwe, mafua ya ndege yalikua powerful huko kuliko Africa!! Lakini haimaanishi hawakuweza kucontrol so hizi kejeli za kusema ''wao wanakufa ilihali wana MADAWA kuliko sisi'' hazifai.

Kama issue ni wao kuwa na MADAWA/Sayansi kuliko sisi ila bado wanakufa..... eti waafrika tuna kinga sana au tuna Mungu sana ni uongo sana kwa sababu mbona VVU,Malaria, inatuua sisi kuliko wao? Ndio nakuuliza hyo kinga ipo kwenye corona tu au magonjwa mengine?

Lastly wwe ndio umedai wao wanakufa sana so nikahoji..... Takwimu zenu zipo ili kujustify hilo? Ama mnasema wao wanakufa sana compared na nchi gani ya Afrika ambayo inapima kwa percentage za ulaya/US?
 
Unaongea haya huangalii implication ya kukataa chanjo say ikitokea huwezi safiri nje ya nchi kama hauna chanjo (Yellow fever/ kipimo cha Ebola kipindi fulani) je mmejiandaaje kama taifa? Yaani what is our contingency plan?

Tuwe kama nchi iliyopata uhuru..... Then ww unakuta ni Professor kabisa wa medicine na unaongea hivi!! Funny enough nkikuuliza takwimu za covid fatalities TZ hauna wala hujawahi kwenda Aga Khan pale kufanya Exit poll!!

Weird
 
Side effects za Astrazeneca ni zipi?
Zipo nyingi tu na zina vary kwa condition ya mtu.... Kama tu ambavyo mimi binafsi nikitumia Ampixicilin huwa naharisha mfululizo na kukojoa kila sekunde tena hata wiki 3 baada ya kumaliza dozi!! Ssa ingekua ndio chanjo inafanya hivo si mngekuwa mnapovuka hapa!!

Kila dawa ina side effects hata Chanjo ya yellow fever ina madhara (Nmedungwa multiple times) ila mbona hamsitishi kuigawa?? Hivi kweli side effects ama vifo kwa watu 0.00001 vina justify kuikataa chanjo?

Well hapo juu nimesema Side effects za chemotherapy zimeua sana mbona hazipigwi marufuku pale ocean road? Kwanini kelele ni kwa AstraZeneca pekee?

I hope unaelewa hoja yangu.... Tuepuke double standards
 
mama anaweza kuwa kweli kwenye hili swala anaenda kumkosoa mtangulizi wake lakini nyuma ya pazia kuna influence kubwa sana ya hao mabeberu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kupingana na mabeberu kunahitaji moyo wa chuma hasa mkuu, mama hilo haliwezi na ameshaminywa kidogo ndio maana tunaona mambo kama haya ,chanjo ameshakubali na masharti kibao ameshapewa ni swala la muda tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mamayo! Wewe ulimpima ukaona alikuwa na corona???Uingereza wenyewe wamechemka kuweka watu Lockdown wameamua kufungua na wamekubali kuishi nao ugonjwa sasa Mwendazake alikosea wapi?
 
Hao unaosema wana double standards ni nani kwa sababu habari za Astrazeneca tumesikia kwenye nchi nyingi tu tumeona wengine wamezikata kabisa wengine wamesitisha kwa kwenye umri chini ya miaka 60,sasa sijui hayo unayoyaeleza wewe hayo mataifa hawayajui au vp.
 
Kila kiongozi wa nchi ni lazima afuate ushauri wa wataalamu wa tiba na afya
Dunia nzima tunaona wakipata ushauri kwa wataalamu

Nae Rais Samia ni lazima apate ushauri pia
Ataamua baada ya wataalamu ingawa imeanza kupungua katika baadhi ya nchi na wengine kudhibiti sana na sasa kupungua kiasi chake
Sidhani kama watu watafungiwa ndani ila tunaweza kutangaziwa tu kuwa ugonjwa upo na tujichunge kwa kuvaa [emoji40] na kupunguza misongamano
Najua Africa haujauwa sana ila vifo vipo
 
Mama ni mwanadiplomasia mzuri...
Hataki kuweka wazi kutokubaliana na mtangulizi wake kwakua anajua kuna mabaki ya misukule ya mzee itaanza kumzongaa....

Sasa anawatafuta taratibu...

Twende na Mama
 
Hadi sasa Mama Samia havai barakoa,mwanzo tulisema ni kwa sababu ya Jiwe ila sasa Jiwe hayupo ila bado Mama samia havai barakoa wala hata kusisitiza tu watu wavae barakoa.

Anamuogopa nani?

Yan na yeye anakosea, mkuu kosa ni kosa halibagui aisee yan iko hivyo yan magu alikosea na mama anakosea ivyo ivyo sasa nashindwa hata kuelewa yani
 
Labda nikuulize unakubali kwamba wazungu corona inawasumbua sana kuliko sisi kama ilivyo kwa mafua ambayo umekubali yanawasumbua sana wazungu kuliko sisi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…