#COVID19 Kwanini Rais ameamua kujificha nyuma ya kamati ya Corona? Anaogopa nini kuwambia Watanzania wajiandae na AstraZeneca? Anaogopa nini?

#COVID19 Kwanini Rais ameamua kujificha nyuma ya kamati ya Corona? Anaogopa nini kuwambia Watanzania wajiandae na AstraZeneca? Anaogopa nini?

Mapumbafu sana haya,yako selfish sana.Hivi hata Mpango hayakumuona,na jiwe je?Mim nimepigwa week tatu usiombe ikuguse
Hili la Corona lipo, na lipo ili tukabiliane nalo, umeandika Kwa uchungu Sana mkuu, naheshimu mawazo yako Isipokuwa matusi

Licha ya hivyo, umejiuliza pia kwamba kunaambao wamepoteza Maisha Yao Kwa sababu ya chanjo za majaribio?

Unadhani wanaumia Kwa kiasi gani ndugu za hao wafiwa??

Swala hili la Corona, ni swala lenye utata mkubwa sana, angalia nchi jirani hapo, wameagiza chanjo, baada Tu ya chanjo kuingia, Leo hii mitungi ya oxygen haotoshi mahospitalini

Huoni kwamba hili suala linautata??
 
So we unachotaka ni nini sasa?? Maana unalalamika bila kusema nini unataka
Watu wambiwe tatizo lipo na wachukue tahadhali zote huku maisha yakiendelea,laiti kila mmoja angetikiswa na hili jambo tungapata somo,collective effort,both internal and external zinahitajika kukabiliana hii changamoto.Watanzania hatuambiliki mpaka yatupate hata mimi nilikua nachukulia kirahisi sana km ilivyokua kwa jiwe lakin imenipa somo
 
Hili la Corona lipo, na lipo ili tukabiliane nalo, umeandika Kwa uchungu Sana mkuu, naheshimu mawazo yako Isipokuwa matusi

Licha ya hivyo, umejiuliza pia kwamba kunaambao wamepoteza Maisha Yao Kwa sababu ya chanjo za majaribio?

Unadhani wanaumia Kwa kiasi gani ndugu za hao wafiwa??

Swala hili la Corona, ni swala lenye utata mkubwa sana, angalia nchi jirani hapo, wameagiza chanjo, baada Tu ya chanjo kuingia, Leo hii mitungi ya oxygen haotoshi mahospitalini

Huoni kwamba hili suala linautata??
Ok but watu kupoteza maisha wakati wa kujitibu ni tofauti na kutokuchukua hatua,ikumbukwe kuwa ni chanjo na tupo kwenye majaribio.Hivi hujawahi kuona dawa inatibu kwa fulani na mwingine inamletea matatizo hata kufariki?Mhim hapa ni hatua za ndani na nje zichukuliwe na kwa bahati nzuri kwetu ni kwamba tuna nafasi ya kujua ip chanjo nzuri kwakua zimeishaanza kufanyiwa majaribio na wenzetu,hivyo suala la Rais kuunda kamati ya wataalam ni jambo jema sana ktk kukabiliana na hii changamoto.
Bro nimepoteza ndugu na marafiki hvyo ninapoona watu wanaleta mzaha nakasirika sana.Dhana ya siamini mpaka inipate ni hatari
 
Kwenye suala la Corona lazima tukubali Magufuli alichemka big time.

Hakuna mtu mwenye akili timamu angekubaliana na Magufuli kwa jinsi alivyoishughulikia korona.

Huwezi kuwa dogma ukajifanya Tanzania haina korona wakati Dunia nzima ina korona eti mungu ametusaidia, huyo mungu alishindwa nini kumsaidia korona isimuue?

Nakubaliana na mama, shughulika na korona kitaalam.
Hakuna korona bali kuna changamoto za upumuaji,kama ipo mbona Philip aliyezushiwa kifo cha Corona alitoka live na kuikana tena na kuwakoholea watu bila balakoa mbona hawakupata hiyo corona.Kumuelewa Jiwe kwenye Marketing ya Corona Unahitaji IQ kubwa.
 
Kuna wakati mnadhani mama sio wa Lumumba?

Upinzani wa TZ haujawahi kuwa serious..[emoji16]
Majitu ya lumumba hayawez kubali ushauri Mungu wao aliwazoesha vibaya, too bad mungu wao kafa [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Magufuli alikuwa sahihi 100% suala la corona. Nashangaa watu wanaishabikia corona kama Mungu vile. Malaria inaua kila dakika, mamilioni kwa mwaka, watu kimya, corona yenye kuua mia hata elfu haiwezi watu kilele kibao. Pelekeni hizo nguvu kwenye malaria basi.
 
Ok but watu kupoteza maisha wakati wa kujitibu ni tofauti na kutokuchukua hatua,ikumbukwe kuwa ni chanjo na tupo kwenye majaribio.Hivi hujawahi kuona dawa inatibu kwa fulani na mwingine inamletea matatizo hata kufariki?Mhim hapa ni hatua za ndani na nje zichukuliwe na kwa bahati nzuri kwetu ni kwamba tuna nafasi ya kujua ip chanjo nzuri kwakua zimeishaanza kufanyiwa majaribio na wenzetu,hivyo suala la Rais kuunda kamati ya wataalam ni jambo jema sana ktk kukabiliana na hii changamoto.
Bro nimepoteza ndugu na marafiki hvyo ninapoona watu wanaleta mzaha nakasirika sana.Dhana ya siamini mpaka inipate ni hatari
Mimi nadhani, timu itayofanya utafiti, ifanyie pia swala maambukizi ya Kasi Ikiwa Taifa linapoagiza chanjo, zikitua tu maambukizi nayo yanaongezeka Kwa Kasi!

Mf. Nchi jirani, Kwa tarifa za leo, inaonekana mitungi ya oxygen inaelekea kuzidiwa na wahitaji
 
Unataka tuweke lock down, huo ndio utaalam unaotaka, hao wenye lock down wanakufa wengi zaidi ya Tz sasa nini faida ya lockdown ? SSH ana tatizo, tena ni KUBWA.

Kupambana na Corona ni lockdown peke yake? Hakuna mtu anataka lock, bali njia nyingine za kisayansi zichukue nafasi. Mnatumia lockdown kama njia ya kubeba Utetezi wenu wa kiupotoshaji.
 
Magufuli alikuwa sahihi 100% suala la corona. Nashangaa watu wanaishabikia corona kama Mungu vile. Malaria inaua kila dakika, mamilioni kwa mwaka, watu kimya, corona yenye kuua mia hata elfu haiwezi watu kilele kibao. Pelekeni hizo nguvu kwenye malaria basi.

Kampeni ya malaria, ukimwi nk nazo zilivaliwa njuga, huenda ulikuwa hujazaliwa, waulize wazazi wako. Ni hivi, ushirikina sasa basi.
 
Wasalaam wana jamvi!

Nimeshangazwa sana na Mh Rais kusema ataunda kamati kuhusu swala la Corona ili baadae tuwe na msimamo kuhusu Corona!

Mimi kwenye hili nimejiuliza maswali hivi ni kweli Tanzania hatukuwa na msimamo kuhusu Corona? Huyu Rais si alikuwa Makamu wa Rais na Rais wake alishasema wazi kuwa Tanzania hakuna Corona na kama ipo ni ndogo sana?

Hii kamati anayounda anataka imwambie nini kipya asichokijua? Anataka aanze kutoa takwimu za Corona sasa anataka kamati imshauri?

Anataka aweke watu Lockdown sasa anataka kamati imshauri?

Anataka kulazimisha watu kuvaa barakoa sasa anataka kama imshauri?

Anataka kupokea chanjo ya Astrazeneca sasa anataka kamati imshauri?

Rais anaogopa nini kusema alikuwa hakubaliani na jinsi mtangulizi wake alivyo kuwa anaikabili Corona? Rais anaogopa nini kusema wamejiandaa kupokea chanjo ya AstraZeneca hivi karibuni?

Sidhani kama Rais anatakiwa kujificha nyuma ya kamati kwenye swala kama hili ambalo liko wazi!

Kuna kitu gani hajui ambacho anataka kamati imwambie?

Kwanini anajificha nyuma ya kamati anashindwa nini kuwambia watanzania wajiandae kudungwa Astrazeneca?

Kama Tanzania hatuna msimamo kwanini yeye havai barakoa? Hajui huo nao ni msimamo? Anataka ashauriwe nini?

Kwanini Tusiamini ana ajenda zake mkononi anataka azipitishe nyuma ya kamati ili watanzania waamini ni msimamo wa kamati kumbe ni msimamo wake?

Wasalaam!
Poleni wakuu, tumempoteza rais wetu na misimamo yake, wafuasi tumebaki! Tuzingatie tu kwamba kila zama na kitabu chake! Tuteseke zetu kwa miaka minne, kama wale wenzetu waloteseka kwa miaka 6!
Wasalaam!
 
Hakuna korona bali kuna changamoto za upumuaji,kama ipo mbona Philip aliyezushiwa kifo cha Corona alitoka live na kuikana tena na kuwakoholea watu bila balakoa mbona hawakupata hiyo corona.Kumuelewa Jiwe kwenye Marketing ya Corona Unahitaji IQ kubwa.
Yeye mbona hakuchomoka kwenye hiyo corona?
 
Kenya wanaofuata COVID19 protocols wako wapi?
Je hamsikii hosptali na mfumo wa afya ulivyozidiwa?
Mbona bongo tunaishi na vizuri tu na maisha yanaendelea kama kawaida?
Tunataka maisha gani zaidi?
Hamtaki maisha zaidi, mtupishe kwanza kwa hii miaka minne tuirudishe Tanzania duniani! Kwa anaye ona hawezi aende tu, huko nchi ya malaika ambapo malaika mkuu anaongoaza na kule hakuna corona wala lockdown, hata hospital za kuzidiwa hazipo! Mfumo wa afya haujazidiwa kama Kenya kule!
 
tukisema mnatumia makalio kufikiri mnachukia.

kwa akili zako za kuvukia barabara magu angefariki kwa corona ungethubutu kumwona samia,mama janet,na waliokuwa walinzi wa jpm wakiwa hawavai barakoa???au walichanjwa???vipi yeye hakuchanjwa akafariki??

siasa sio upumbavu,fanyeni siasa kama taaluma nyingine.
Mama Janeth hukumuona amevaa barakoa? Ama wewe macho yako yako kwenye makalio?
 
Mpendwa wetu alikua ni rais mnajim
Dunia nzima hili jambo limetesa sana
Ila Magu alielewa hii kitu imetokana vp

M/mungu alitaka kuwakumbusha watu wake kwamba wamemsahau vya kutosha hivyo haraka wamrudie

Ile Magu kutamka hadharani kua hili tuna mwachia m/mungu , bas hapo mungu akatupa kinga
Na nan ni mbora wa kinga isipokua ulinzi toka kwa mungu???????

Bas Hakimu Mfawidhi , jiandae hutokuja kusikia watu 800 wamekufa kwa siku kisa korona
Kama NYC, hutokuja kuona jiran zako wanakufa kama kuku.

Hili jambo ni mungu tu anatulinda.

NB: kinyume na msimamo wa mpendwa wetu
Tujiandae na mengi
Kwani ni mungu yupi huyo wa hayo mambo yenu ya kinajimu unamzungumzia hapa? Mnazuia taarifa za watu 800 wamekufa badala ya kuzuia watu 800 kufa?!
 
Ni wapi kusikokuwa na Corona?
Ni nani mpaka sasa kaidhibiti Corona?

Habari ya Udoct na Uprof achana nao, na punguza jaziba hazisaidii!!

Kama unaona zinasaidia, toa faida moja wapi tuone

Hii kauli ya “nani kaidhibiti corona?” ni ujinga mwingine mkubwa mlioletewa na Jiwe. Kwa akili finyu, kudhibiti ni sawa na kumaliza. Ni magonjwa mangapi bado yapo duniani lakini tunasema yamedhibitiwa? Dunia inapambana na Covid-19 sisi tumekaa pembeni kama mashabiki au wanga kusubiri washindwe. Wakipata tiba imara eti ndio tuanze kulilia msaada!

Kuna nchi zimefanikiwa kushusha kiasi na kasi ya maambukizi na vifo vinavyotokana na Covid-19 na wanazo takwimu za kuthibitisha. Wanapitisha maamuzi kisayansi. Sisi tumekana na kuficha takwimu na kuendekeza kauli za kijinga kama “changamoto ya upumuaji”, “mtaani kwenu nani kafa kwa corona?”, “hakuna tiba ya corona”, “hatutaki chanjo”, “corona ni hofu tu”, nk.

Acha Mh SSH aturejeshee SANITY kwa kufanya mambo kwa akili.
 
Ni wapi kusikokuwa na Corona?
Ni nani mpaka sasa kaidhibiti Corona?
New Zealand
Screenshot_2021-04-08-14-58-47-1.png


Shida yenu hamna takwimu mmekalia propaganda za lumumba.
 
Back
Top Bottom