Kwanini Rais Samia amesema hataki mabango, Je hii ndiyo demokrasia?

Mabango yalitumika vibaya sana katika utawala wa jiwe
 
Kauli yoyote Ile inaweza kutafsiriwa vibaya. Mfano kauli Kama hiyo ya kutobeba Mabango mtu yeyote mwenye akili timamu anakuwa ameelewa maana yake maana rais alisema bango litaondoka na mteule wake maana yake wananchi wasikilizwe na kutatuliwa Kero zao na viongozi wa chini.

Kuna watu hubeba bango wakitaka rais awasaidie kumuondoa mtendaji wao wa kijiji au mwenyekiti wa kamati ya shule.
 
Hii nchi ngumu sana.
mbona rais kayaeleza hayo kwa kirefu sana kwenye hutba yake ile ya kua kwann hataki kuona mabango,
Hii nchi kubwa sana kuna maeneo rais hawez kufika so hao nao watatatuliwa lini kero zao na kuna mkuu wa wilaya huko,mkurugenz,mtendaji kata na wote wanalipwa mishahara kwa kodi zetu.
Ukituongoza wabongo fanya uwezalo t hatuna jema sisi.
 
Bango litaondoka na mteule wa rais hata kama mbeba bango ana kisasi binafsi na mteule ambacho hakihusiani na utendaji wa mteule?
 
Kazi za Wakuu WA Mikoa na Wilaya ni zipi kama wananchi watakuwa Hadi wamsubiri Rais ndipo shida zitatuliwe?. Hiyo ndio maana ya kauli ya Rais. Kawaweka huko karibu na wananchi ili wawatatulie shida zao., Sio ujambazi kama WA Sabaya Makonda na kina Jerry Muro.
 
Naomba tuweke thread moja kubwa ya kurekodi kwa video maneno yote ya rais.

Naona maneno yake mengi mazuri tu yanapotoshwa, ama kwa makusudi, ama kwa hila.

Tukiweka hii thread itasaidia kuwezesha kila mtu kuhakiki rais alisema nini, na ripoti potofu za alichosema zinapotosha wapi.

Kwa sasa watu wengi wanachangia ripoti potofu kama ziko sahihi.

Hii ni mara ya pili katika siku chache naona maneno ya rais yanapotoshwa.
 
Bango litaondoka na mteule wa rais hata kama mbeba bango ana kisasi binafsi na mteule ambacho hakihusiani na utendaji wa mteule?
Ukitaka yote hayo uwekwe wazi basi jua Rai's anaweza maliza masaa sita akifafanua Jambo moja
 
Ukitaka yote hayo uwekwe wazi basi jua Rai's anaweza maliza masaa sita akifafanua Jambo moja
Hujajibu nililouliza na ulilojibu sijauliza.

Na kazi ya rais kufafanua hata masaa sita hayatoshi.
 
Hivi mbona kauli yake inaeleweka tu, au mnatafuta tu vya kuongea[emoji848][emoji848][emoji848]
 

Unfortunately that’s the kind of world we live in now.

Mtu anazusha tu uzushi wake mtandaoni and people take it and run with it.

And very few people even seem to care to check the veracity of it.

Hata videos nazo ni za kuwa nazo makini sana. Maana zinaweza kuwa edited in way na kumfanya mtu aonekane anasema kitu flani ilhali si kweli:

Mfano, kuna clip nimeiona majuzi inayomwonyesha aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Mwanza, yule Chalamila.

Ile clip naamini imehaririwa na kupachika footage nyingi be iliyounganishwa na footage nyingine ili ionekane jamaa anahimiza watu waende kumpokea Samia na mabango ya matusi!

Sasa sina hakika kama hiyo ndo sababu ya yeye kutenguliwa kwenye nafasi yake au la, ila kusema ukweli ile clip imehaririwa kumchafua yule jamaa.

Ni muhimu sana kuwa makini siku hizi.

Kuna nukuu nyingi sana kwenye mtandao ambazo huwa zinakuwa attributed kwa Rais Mugabe na wapo watu wanaoamini kweli kuwa alizisema yeye!

Sad world.
 
Hapana utakuwa hujamuelewa vizuri.

Msikilize tena Mwanzo hadi mwisho utamuelewa vizuri.

Amesisitiza kero za wananchi kushughulikiwa na kutatuliwa na watendaji wa chini kwa kila ngazi badala ya kusubiri hadi pale Rais atakapokuwa akifanya ziara ndipo wananchi wamwambie na kutatuliwa kero zao.
 
naongezea alaisem mabango yawe kwa hishu za kitaifa tu sio kero.kero inaenda na mtu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ninachoona hapo ni wananchi kuminywa Uhuru wa kutoa kero zao, viongozi wengi ngazi ya mkoa au wilaya hawana kawaida ya kwenda vijijini kusikiliza kero za watu wao, kwa hiyo Kama amezuia mabango inamaanisha viongozi hawa watafanya juu chini Rais asione mabango ya wananchi.

Rais asingetoa tamko la kuzuia mabango ili ajue Kama kero za wananchi zinasikilizwa au hazisikilizwi.
 
Sawa.., hatuwezi kukuzuia kuona. Hayo ni maono yako
 
Sahihi kabisa. Ukiangalia uongozi wa awamu ya tano hata kama hakukuwa na bango mkuu alikuwa bado anauliza kuna kero gani hapa na kwa kweli kero hazikosekani kwa hiyo alitumia mabango au kero kwa kuzitatua papo kwa papo akiamini kuwa ndicho kwake kilikuwa kipimo cha uwajibikaji kwa wananchi sasa mama si mtu wa hulka hiyo yeye huenda na mfumo wake ndiyo maana ameona ili thamani ya uteuzi wa wawakilishi wake kwa wananchi ni pamoja na kutatua kero zao lakini sina shaka bado mabango tutayaona tu pamoja na angalizo alilolitoa
 
Hivi unaijua Tanzania hii? MA DC, Wakurugenzi na viongozi wengi ni Miungu watu, hawatatui mambo ya watu. Mnamkumbuka Yule DC kule Sumbawanga alishindwa maliza tu mgogoro wa mtu kuibiwa Ng'ombe. Mabango ni sehemu ya Wananchi kufikisha ujumbe kwa Mkuu wa Nchi.

Mimi maombi yangu kwa Viongozi, Wajue wameajiriwa na Wananchi. Wafanye kazi. Bila shitua shitua nchi yetu bado sana viongozi kuwajibika.
 
Wewe kama kiongozi utapata feedback wapi kama watendaji watendaji hawafanyi vyema? Mimi ofisini kwangu nikifanya kazi lazima mteja atoe feedback na ana wa copy wakubwa wote. Kiukweli imesaidia kuinua utendaji
 
Hata mimi nilimwelewa hivyo.
 
Wewe kama kiongozi utapata feedback wapi kama watendaji watendaji hawafanyi vyema? Mimi ofisini kwangu nikifanya kazi lazima mteja atoe feedback na ana wa copy wakubwa wote. Kiukweli imesaidia kuinua utendaji
Mkuu tunazungumzia li nchi hili la tanzania sio office hii mkuu hii nchi kubwa mno,,
rais hawez kufika kila sehemu,
Lazma tujenge utamaduni wa kila mtendaji kuwajibika eneo alipo.
Wewe t apo mkuu unaweza ukawa upo dar unaish magomeni gongolamboto hujakanyaga mwaka mzima.
lazma tujenge utamaduni wa uwajibikaji kila mtu katika eneo lake atimize majukumu yake.
Hili suala hata hayati magufuli amelisemea sana wat wawajibike katka maeneo yao,
Sio kila jambo mpaka rais ndo aje alishughulikie.
Kama wewe ni mtendaji uko kakonko kigoma jiulize niko huku kwa ajili gani,lazma ujihis natakiwa kutatua kero za watu.

Tukienda ivo kwamba kila kitu ad rais hatutafika popote milele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…