Kwanini sauti ya Diamond Live ni mbaya lakini nzuri kwenye nyimbo tofauti?

Kwanini sauti ya Diamond Live ni mbaya lakini nzuri kwenye nyimbo tofauti?

Nasubiri thread Shardcole nae sijui atasemaje, kama umpendi mtu sema mimi sipendi full stop, sio unazunguka kama dawa ya mbu ya kuchoma, ina maana huyo diamond platnumz mziki kaanza leo, siku zote mlikuwa wapi mpaka muongee leo.
Unafiki mbaya sana Mkuu achana nae !! Anaanzaje kumponda mtu unayempenda kwa dhati? Hivi ajui kamsemo ka "Ukipenda huoni"?
 
Mimi sio mshabiki wa ali kiba hata kidogo, na wala cpendezwi na maringo yake na kujifanya kwake kuwa yeye ni mkuu. mimi ni shabiki wa diamond ndo mana nataka arekebishe pungufu ili, mana washabiki wake tunasemwa sana juu ya hili. najua akifanya mazoezi ataweza tu
Yaani unataka afanye mazoez ya kuongea??? Kha?? Mbona unamrudisha utoto wakati hatua iyo alishapita?
 
Jamani mi ni shabiki mkubwa na mzuri wa mziki wa bongo fleva, ila ili jambo linanipa wakati mgumu kuamini, huyu mkali wa bongo fleva diamond ana nyimbo kali sana ila kumekuwa na tofauti kubwa sana katika uwasilishwaji wa nyimbo hizo katika live performance na nyimbo tunazozisikia kwenye radio.

Diamond katika nyimbo ana sauti nzuri yenye base kidogo. Ila huyu jamaa sielewi kwanini akiimba live sauti inakua ingine kabisa yaani mbaya, mbona kina ben paul, banana, kiba king, rayvanny harmonise bela etc wakiimba live sauti inakua ile ile. au kuna ka application kwenye playstore anachokitumia kufanya sauti iwe nzuri studio.

Pia nafikiri sasa diamond aachie kina iyobo kucheza awapo jukwaani yeye afanye kazi moja tu ya kuimba, asijifanye michael jackson, na hii sasa ndo imekuwa weakness ya diamond ambapo mpinzani wake kiba anamfunikia.

Namshauri atafute mwalimu wa sauti na mziki wa live, vinginevyo hatutamuelewa . sauti ya jukwaani cjui ndo yake maana huwa mbaya, na akishindwa kabisa basi bana hata pua bwana

Kwaheri
Sijahudhuria matamasha mengi ya diamond platnumz, ila kuna kama mawili matatu nimewahi msikiliza pia nishawahi kuingia kwenye matamasha wakadha wakadha ya fiesta huku mikoani ingawa diamond platnumz hakuudhuri.

Ila kiukweli kabisa mimi ni shabiki mzuri wa diamond ila hilo swala la diamond kuwa na sauti mbaya wakati anaperform ni ukweli kabisa. Nakumbuka alikuja arusha triple A na mi nilikua miongoni mwa wahudhuriaji siku hiyo. Kwa kwl nilikua najiuliza mbona ladha ya mziki wa diamond platnumz ninaoujua mimi siuoni na nikaishia kukerwa na kile ambacho nlikua nikikisikia. Maana sauti ilikua mbaya mno, ingawa kwenye upande wa kucheza kwl huo upande alinikosha, Alicheza mno.

MTAZAMO WENGI
Diamond platnumz anatumia nguvu nyingi sana katika kucheza na kumpelekea kutumia pumzi kubwa sana ambayo inampelekea kushindwa kuimba sauti yake ama inaekaribia na sauti anaerekodia. Hvyo Kwa sasa anatakiwa kujua mashabiki wake wanaotegemea kusikiliza sauti yake kama mm siku ile arusha. Hvyo basi hakuna ulazima wa kila nyimbo anaeperform lazimwa ichezwe.

Pia nimehudhuria baadhi ya wasanii wa kibongo fleva kama ommy dimpoz, jux, v money, alikiba, jide hata man fongo ila sauti zao kwa stage ni nzuri sio kama ya chibu(ukweli).
 
hao uliowataja ni rappers sio vocalist kama diamond, Diamond yuko vizuri ila ajinoe zaidi katika vocal.Siko katika team zenu mi ni Team Tamadunu Muzik hahah Nikki Mbishi Songa One....
Haters gonna hate believers gonna believe
 
Haters gonna hate believers gonna believe
beliver can hate too, hawa jamaa wanawachanganya sana watanzania, anyway wiki hii tunatarajia kichupa cha ngoma ya Nikki Mbishi inaitwa Babu Talent shoot imefanyika kinondoni, support HipHop pia
 
Back
Top Bottom