Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 301,577
- 754,412
Tulikuwa na kiongozi mwenye maono makubwa Mwalimu Nyerere.. Mpaka 1985 alikuwa tayari ameshaweka msingi mzuri wa viwanda vyama vya ushirika na mashamba makubwaNi kweli yametokea juzijuzi lakini lawama zangu nazitupa kwa wahenga kwamba ndio msingi wa haya yote kutokea sasahivi. Vijana wangekuoa bize na uzalishaji viwandani na mashambani wasingekuwa na huu upuuzi wanaouandika sikuhizi, na chanzo cha ukosefu wa ajira ni janga lililoandaliwa miongo kadhaa na hao wazamani. Wakaua viwanda, wakatuachia katiba ya ajabu, wakawa na nizamu ya woga mpk kizazi hiki kikaiga hvyohvyo. Wazungu wapo hapo walipo coz mababu na mababu walitengeneza njia kwa kuweza kuvuka bara na bara kwenda kuiba Mali sio Hawa wakwetu walipewa nchi unalipiwa Kila kitu na Kodi ya wananchi wetu lakini bado anaungana na mkoloni kumuibia tena nchi yake. Acha tu mada kama hizi ziwepo tupunguze stress zetu
Kwamba mashamba yatazalisha malighafi kwa ajili ya viwanda na vyama vya ushirika vitasimamia rasilimali watu, rasilimali vitu mauzo na manunuzi
Tayari tulishakuwa na viwanda, mashama na vyama vya ushirika karibia kila mkoa.. Vitu vingi tulitengeneza wenyewe kuanzia pini mpaka viwanda vya vipuri kwa ajili ya viwanda vyetu
Wakulima walikuwa na hakika ya kuuza mazao yao, wazalishaji viwandani walikuwa na hakika ya kuuza bidhaa zao.. Vyama vya ushirika vilikuwa na uhakika wa kuwaunganisha wazalishaji na wauzaji
Mashamba makubwa ya mkonge yako wapi leo hii?
Mashamba ya kahawa je?
Mashamba ya pamba?
Mashamba ya korosho, mtama, uwele mpunga nk?
Mashamba ya chai? Karanga?
Mashamba ya karafuu? Nknk
Shuleni tulikuwa tunajua kila zao linazalishwa mkoa gani
Viwanga vya mkonge Tanga?
Viwanda vya nguo Mwanza? Mwatex, Sunguratex?
Kitanda cha matairi Arusha
Kiwanda cha National battery na national radio? Dsm?
Viwanda vya vipuri Mang'ula Morogoro, Arusha na Moshi?
Kiwanda cha baiskeli Mwenge Dsm?
Viwanda mbalimbali Pugu road?
Viwanda vya national miling?
Spinning mabibo? Nknk
Hivi vyote vipo wapi?[emoji15][emoji25]
Vyama vya ushirika kila mkoa
KAUDO
KAUMA
Moshi
Tanga nknk
..n the like?
Taifa lilikuwa settled likienda kwenye mstari sahihi kabisa
Then what happened? What Nyerere built in 36 years in power was destroyed over few years by ascended presidents
Mashirika ya umma yakauliwa yote
Taasisi za fedha zikanyongelewa mbali.. Tukaletewa sime kali ya ubinafsishaji... Hapo ndio tulimalizwa kabisaa.. Mali za umma zikauzwa kwa bei ya kutupa...leo hii matajiri wakubwa wa Tanzania wanaoshindana na matajiri wa ulimwengu ukwasi wao ulitokana na upumbavu wa viongozi wetu
Naomba nisiandike zaidi nahisi uchungu mwingi moyoni..ndio maana nikimuona mtu anashadadia ccm...[emoji35][emoji34][emoji35][emoji34][emoji35]