Kwanini sehemu ya mbele ya uume inaitwa kichwa?

Tulikuwa na kiongozi mwenye maono makubwa Mwalimu Nyerere.. Mpaka 1985 alikuwa tayari ameshaweka msingi mzuri wa viwanda vyama vya ushirika na mashamba makubwa
Kwamba mashamba yatazalisha malighafi kwa ajili ya viwanda na vyama vya ushirika vitasimamia rasilimali watu, rasilimali vitu mauzo na manunuzi
Tayari tulishakuwa na viwanda, mashama na vyama vya ushirika karibia kila mkoa.. Vitu vingi tulitengeneza wenyewe kuanzia pini mpaka viwanda vya vipuri kwa ajili ya viwanda vyetu
Wakulima walikuwa na hakika ya kuuza mazao yao, wazalishaji viwandani walikuwa na hakika ya kuuza bidhaa zao.. Vyama vya ushirika vilikuwa na uhakika wa kuwaunganisha wazalishaji na wauzaji

Mashamba makubwa ya mkonge yako wapi leo hii?
Mashamba ya kahawa je?
Mashamba ya pamba?
Mashamba ya korosho, mtama, uwele mpunga nk?
Mashamba ya chai? Karanga?
Mashamba ya karafuu? Nknk

Shuleni tulikuwa tunajua kila zao linazalishwa mkoa gani

Viwanga vya mkonge Tanga?
Viwanda vya nguo Mwanza? Mwatex, Sunguratex?
Kitanda cha matairi Arusha
Kiwanda cha National battery na national radio? Dsm?
Viwanda vya vipuri Mang'ula Morogoro, Arusha na Moshi?
Kiwanda cha baiskeli Mwenge Dsm?
Viwanda mbalimbali Pugu road?
Viwanda vya national miling?
Spinning mabibo? Nknk
Hivi vyote vipo wapi?[emoji15][emoji25]

Vyama vya ushirika kila mkoa
KAUDO
KAUMA
Moshi
Tanga nknk
..n the like?
Taifa lilikuwa settled likienda kwenye mstari sahihi kabisa
Then what happened? What Nyerere built in 36 years in power was destroyed over few years by ascended presidents

Mashirika ya umma yakauliwa yote
Taasisi za fedha zikanyongelewa mbali.. Tukaletewa sime kali ya ubinafsishaji... Hapo ndio tulimalizwa kabisaa.. Mali za umma zikauzwa kwa bei ya kutupa...leo hii matajiri wakubwa wa Tanzania wanaoshindana na matajiri wa ulimwengu ukwasi wao ulitokana na upumbavu wa viongozi wetu

Naomba nisiandike zaidi nahisi uchungu mwingi moyoni..ndio maana nikimuona mtu anashadadia ccm...[emoji35][emoji34][emoji35][emoji34][emoji35]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…