Kwanini Serikali haipigi marufuku uingizaji wa mitumba?

Kwanini Serikali haipigi marufuku uingizaji wa mitumba?

Hakuna nchi inayoweza kuendelea bila kulinda na kuendeleza viwanda vya ndani. Na njia kuu ya kulinda viwanda vya ndani ni kuzuia bidhaa cheap kutoka nje ya nchi.

Ndiyo maana China waliikataa Google, facebook nk. Ndiyo maana US waliipiga pini Huawei. Hili jambo mataifa karibu yote ya Afrika wanalichukulia poa, na ndiyo maana karibu bara lote masikini.

Viwanda vyetu vya mavazi haviwezi kuendelea iwapo tunapata nguo na viatu vya bei rahisi vya mitumba kutoka nje.

Ni sekta nyingi inatakiwa kudhibiti cheap imports, nimezungumzia mavazi sababu ndiyo huwa vitu vya kwanza kwa nchi inayoanza kuwa ya viwanda.

Kwanini Serikali haizuii mavazi ya mitumba ili tuanze kupiga hatua za maendeleo?
Njoo kweny wardrobe yangu utajifunza mtumba sio
akasambee maua ☺️☺️
 
Watu wa Dar ndio uendekeza mitumba, ukienda mikoani watu wamepiga spesho zao wala hawana habari na mtumba, waulize akina mama washona vyeleani wanavyonufaika na kushona vitenge, lkn wa dar wao upunguza matambala ya mitumba
Mimi sijasoma uchumi, lakini huwezi tu kuzuia import wakati hata hivyo viwanda vya ndani vichache vitatutengenezea nguo sio design nzuri.

Halafu kama maji na umeme tu shida kiasi hiki hivyo viwanda vitaendeshwa na nini?
 
Mimi sijasoma uchumi, lakini huwezi tu kuzuia import wakati hata hivyo viwanda vya ndani vichache vitatutengenezea nguo sio design nzuri.

Halafu kama maji na umeme tu shida kiasi hiki hivyo viwanda vitaendeshwa na nini?
Sio kwamba kuna upungufu wa nguo africa bali mkakati wa soko la nchi zilizoendelea, nchi yoyote africa ikijaribu kuzuia unafungiwa mikopo ya kimataifa nk, waulize Rwanda nin kilitokea baada ya Kagame kutangaza kuzuia hiyo mitumba. Wewe unaona unazuiwa hata kununua gari used kutoka nchi jirani lkn wanataka gari kama hilo ulinunue japan na kwingineko lkn sio africa au siku 1 ukipata hela yako vuka mpaka uende nchi jirani ukanunue pikipiki au gari kutoka kwa mtu halafu uone kama utaivusha mpaka itaozea mpakani, lkn gari hilo likiwa na doc za japan au ulaya ni siku 3 tu gari lako limesajiriwa nchini.
 
Sio kwamba kuna upungufu wa nguo africa bali mkakati wa soko la nchi zilizoendelea, nchi yoyote africa ikijaribu kuzuia unafungiwa mikopo ya kimataifa nk, waulize Rwanda nin kilitokea baada ya Kagame kutangaza kuzuia hiyo mitumba. Wewe unaona unazuiwa hata kununua gari used kutoka nchi jirani lkn wanataka gari kama hilo ulinunue japan na kwingineko lkn sio africa au siku 1 ukipata hela yako vuka mpaka uende nchi jirani ukanunue pikipiki au gari kutoka kwa mtu halafu uone kama utaivusha mpaka itaozea mpakani, lkn gari hilo likiwa na doc za japan au ulaya ni siku 3 tu gari lako limesajiriwa nchini.
Umenena vema sana mkuu.
 
Back
Top Bottom