Kwanini serikali imebariki magari ya viongozi wa serikali kuwa namba feki? Mwanzo nilizani ni uhuni wa madereva kumbe wanapewa wabandike feki

Kwanini serikali imebariki magari ya viongozi wa serikali kuwa namba feki? Mwanzo nilizani ni uhuni wa madereva kumbe wanapewa wabandike feki

Hii kitu imekuwa very common halafu wanasumbua sana barabarani, muda mwingine unakuta hayo magari yako na vibinti vidogo vya chuo kwenye mahotel na lodgings
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dah .
Ngojeni niwaeleshe, Gari yoyote inayoingia nchini lazima isajiliwe kwa plate number za kawaida.. zile tunazozijua za T454 EGF(mfano).. alafu kisha ndiyo kama za serikali zinapewa Hizo namba zao za STM,. Kwahyo zile za serikali ubandikwa wakati tayari hizi gari zina plate no. Za kawaida za mfumo wa nchi..
siyo lazima gari la serikali liwe na namba za kawaida kwanza ndipo lipewe namba za STM. Yanaweza kusajiliwa moja kwa moja na namba za serikali.
 
Unakuta gari jipya kabisa halafu usajili T.... AAM

😅
 
Naungana na wewe kwa asilimia mia. Unajua hawa jamaa wanatoa majibu yao uchwara humu wanafikiri huko serikalini wanafanya kazi wenyewe na hakuna watu wengine wenye uelewa zaidi yao.
Kweli kabisa
 
Elimu elimu elimu

Shida ya wabongo huwa hawana tabia ya kuuliza vitu yeye akishashiba ugali wake,mpe kichwa cha habari tu story nzima ataimaliza yeye.

Gari zote za serikali huja na namba za kiraia kupitia wizara ya ujenzi kisha namba hizo husajiliwa tena kwenye taasisi/wizara husika kwa namba husika.

Swala la kubadili namba limeruhusiwa kisheria endapo mhusika/mwenye cheo mfano mkuu wa mkoa hayumo ndani ya hyo gari hivyo dereva hutakiwa kubadili namba na kuweka namba iliyokuja na gari ama namba inayotambulika na ofisi.

Na pindi mhusika anapopanda plate namba yenye cheo chake huwekwa kwenye gari husika kutambulisha ni gari ambayo imembeba fulani.

Japo mfumo huo ni tofauti kidogo na jeshi au polisi ambako wao huwa hawaweki namba za kiraia bali za jeshi then mhusika anapopanda huwekwa initial kama nyota nk ili kutambulisha kwenye gari kuna fulani
Umeandika uongo kwa confidence kubwa mno na umechanganya mambo

Gari za serikali haziji kwa namba za kiraia. Zina usajili wake, huo usajili wake ndio utabadilika kulingana na matumizi ya cheo. Mfano mawaziri wao watakua na utambulisho wao, wakuu wa mikoa nao watakua na utambulisho wao Kama unavyoinaga RC DSM, RC DOM n.k. lakini ule usajili wa kiserikali(STN 5736, STM 3855 n.k) unabaki kama ulivyo

Huyo hoja yake ilikua ni kutoka namba za serikali na kuwekwa za kiraia na sio kutoka namba za cheo husika(RC DSM) na kuwekwa namba za kiserikali
 
Si kila cheo kina mamlaka ya kupeperusha bendera ndo maana plate no inatumika kuonyesha ni mtu gani aliyebebwa na ana mamlaka gani.

Refer tukio la Nape.
Alivyoenguliwa akiwa mlimani city gari ileilibidi usiku ule ule irudi wizarani dodoma lakini ikiwa na plate no za kawaida sababu hapakuwa na waziri tena
Uongo huu. Haliwezi kuwa na plate namba za kawaida, litakua na plate namba za serikali mfabo STM 3422 n.k kutoka iliyokua ya cheo chake W HTHM
 
Asilimia 90 ya magari hasa mashangingi ya serikali yana namba mbili mbili?

Yaani ni hivi namba Moja utakuta inasoma vizuri tu STL/SU/W/NW/DFPA n.k lakini ukitazama kuna namba nyingine FEKI huwa inafichwa na kutumika kwenye gari ile ile ikisomeka kwa namba za kawaida kama magari mengine T ....AKZ / BPA/ CAG/DAF n.k

Serikali ituambie imebariki mambo hayo ya kihuni kwa faida gani?

Je sheria ya usalama barabarani inatambua matumizi ya namba mbili kwenye gari moja?

Katika mpango wa kupunguza utekaji na matumizi mabaya ya mafuta magari ya serikali; TAMISEMI haioni ni wakati sahihi kuyapaka rangi za taasisi kulingana na nembo zao?
Tafuta kazi ya kufanya
 
Back
Top Bottom