Kwanini taarifa nyingi za miaka elfu iliyopita ni za kubuni au hazijulikani kiuhalisia? Je, kuna kizazi kilipotea?

Kwanini taarifa nyingi za miaka elfu iliyopita ni za kubuni au hazijulikani kiuhalisia? Je, kuna kizazi kilipotea?

mlinzi mlalafofofo

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2008
Posts
725
Reaction score
1,282
Uwepo wa wewe na mimi ni ushahidi tosha kuwa dunia imekaliwa na binadam kwa MUDA WOTE tokea alipoumbwa binadam wa kwanza.

Kama dunia imekuwa na watu muda wote maana yake watu hao walikuwa wakisimuliana habari za matukio yaliyokuwa yanatokea wkt wao wakiwepo na habari hizi waliwapasia vizazi vyao ikaendeleea ivyo hata kwa vizazi vya leo hii.

Sasa mbona leo hii habari nyingi za matukio ya miaka elfu uko nyuma ni kama za kubuni au za watu kuhisi? Mfano mzuri ni maandiko ya vitabu vitakatifu. bado kuna mengi tu ya humo yanabishaniwa hata leo hii juu ya usahihi wake.

Inakuwaje bado kuna habari zisizo hakika wkt tunajua mwanadam amekuwepo wakati wote? Je, inawezekana kuna yamebuniwa tu na kundi au watu fulani tu kwa faida yao? Au wakuu nyinyi mnaonaje?

Tia neno hapa.
 
Habari na elimu muhimu za zamani zimefichwa na watu wachache, wanazitumia kwa manufaa yao.

Mfano Library of Alexander (Egypt) ilichomwa moto na wakaficha baadhi ya vitabu.

Mfano mwingine ni stargate iliyokuwa imefichwa na sadam husein, USA walipo vamia direct walienda kuichukua na kuipeleka kwao kwa matumizi yao binafsi.
 
Kuna uwezekano civilization huwa inafika ukomo, dunia inakaa bila viumbe janja janja kama binadamu hata kwa miaka milioni kadhaa ikijisafisha ndipo inaruhusu kuibuka kwa viumbe wengine janja janja.
 
Habari nyingi na ukweli upo , ila wanaficha makusudi ...Kama unashangaa hilo leo hata waokufa kweny ajali tunapewa idadi tofauti .

Ukweli utabki kuwa ukweli milele ndiyo maana kuna watu wanhoji ....SIku zote utadanganya ila watu wakitumia akili lazima watagundua dosari .


Unapopanga kudanganya lazima kuna sehemu utaleta ukakasi , kiprotokal sio rahisi kueleza habari za miaka elfu nyumba ukaenda sawa kama ni muongo lazima kuna sehemu utakamwa.
 
Maandishi yanaandikwa na binadamu ambao hawajakamilika so lazima utaona baadhi ya makosa.
Kikubwa Ni kuangalia Kama maandishi hayo yamebeba dhima ya habari lengwa, inakutosha.
 
Kuna uwezekano civilization huwa inafika ukomo, dunia inakaa bila viumbe janja janja kama binadamu hata kwa miaka milioni kadhaa ikijisafisha ndipo inaruhusu kuibuka kwa viumbe wengine janja janja.
Theory nzuri kama ilivyo kwenye ujenzi wa pyramid za misri zimejengwa kwa ufasaha na watu wa zamani mpaka tunabaki kujiuliza kama alijenga ni binadamu au Aliens
 
Theory nzuri kama ilivyo kwenye ujenzi wa pyramid za misri zimejengwa kwa ufasaha na watu wa zamani mpaka tunabaki kujiuliza kama alijenga ni binadamu au Aliens
Mkuu umetoa mfano mzuri sana wa izo pyramids. licha ya ukubwa wote ule pyramid lakini mpaka kesho hakuna historia iliyonyooka ya ni nani waliozijenga na walizijenga vipi. bado kuna stori tu kibao za kubahatisha.
 
Uwepo wa wewe na mimi ni ushahidi tosha kuwa dunia imekaliwa na binadam kwa MUDA WOTE tokea alipoumbwa binadam wa kwanza.

Kama dunia imekuwa na watu muda wote maana yake watu hao walikuwa wakisimuliana habari za matukio yaliyokuwa yanatokea wkt wao wakiwepo na habari hizi waliwapasia vizazi vyao ikaendeleea ivyo hata kwa vizazi vya leo hii.

Sasa mbona leo hii habari nyingi za matukio ya miaka elfu uko nyuma ni kama za kubuni au za watu kuhisi? Mfano mzuri ni maandiko ya vitabu vitakatifu. bado kuna mengi tu ya humo yanabishaniwa hata leo hii juu ya usahihi wake.

Inakuwaje bado kuna habari zisizo hakika wkt tunajua mwanadam amekuwepo wakati wote? Je, inawezekana kuna yamebuniwa tu na kundi au watu fulani tu kwa faida yao? Au wakuu nyinyi mnaonaje?

Tia neno hapa.
Hata miaka 1000 ijayo watakao soma historia ya Mzee Mwinyi kwamba alikuwa anakwenda shule peku wataona ni uongo tu
 
ushahidi mkubwa ni wa mtu kuona tukio live na kisha mtu uyo kusimulia uzao wake au jamii yake. nje ya hapo habari husika inakuwa ni ya kubumba tu.
Kweli kabisa ila kazi inakuja kwa aliyesimuliwa naye akisimulia atasimulia alivyo elewa na kuna baadhi ya details atazisahau au kuona hazina umuhimu, baada ya muda story inaanza kwa tofauti na ilivyokuwa
 
Back
Top Bottom