Kwanini Tanzania hakuna daily briefing juu ya Corona virus pandemic?

Kwanini Tanzania hakuna daily briefing juu ya Corona virus pandemic?

Wanaochukulia maisha simple tu ni wapuuzi na hawajali afya zao na za wale wanaowazunguka. Ni lini serikali imetangaza corona imeisha watu waache kuchukua tahadhali?

Yaani wewe kila siku unaambiwa uchukue tahadhari unapuuza eti kwa kuwa hautangaziwi takwimu mpya. Watu kama hawa ni wa kuwapima vyote, corona na akili.

Sent using Jamii Forums mobile app

Iko wazi mkuu, muamko umepungua sana kwenye jamii. Ile kunawa mikono na kuvaa barakoa imepungua. Kama wewe ni mfatiliaji na "mzururaji" mzuri utaelewa kile nachomaanisha.

Mimi kuchukua tahadhari zote wakati wengine wanachukulia simple tu bado haitoshi kunihakikishia usalama wangu. Mwanzoni kwenye vituo vya bodea boda ,bajaji na kwenye maduka kulikuwa na ndoo za maji na sabuni, watu walikuwa hawapati huduma bila kunawa mikono. Ila kwa sasa zile ndoo nyingi ukikagua utakuta hazina maji, sabuni hakuna, pia watu hawanawi mikono tena kwea sana kama sharia ili ndio wapate huduma.

Tuliweza kudhibiti huu ugonjwa na kupunguza madhara kwa kuwa mwanzoni tulichukua tahadhari kwa hali ya juu. Na hilo limeleta matokeo chanya ndio maana hadi sasa hali iko vizuri. Ila kwa sasa kuna kujisahau kidogo na kulega lega, kitu ambacho sio kizuri maana ugonjwa bado upo. Msisitizo na uelemishaji uendelee kwa kiwango kile kile kama awali.
 
Mkuu ebu tupe hiyo sheria inayokataza mikutano ya hadhara ya vyama vya Siasa.Hii itasaidia kuachana na hao wapiga kelele
Sasa hiv takriban nchi zote zinazuia shughuli za mikutano nadhani unalitambua hilo mkuu kama mbowe anataka kuitisha mkutano nahisi afanye hivyo baada ya corona kuisha
 
[emoji15][emoji15][emoji15]
34567890-.jpg
EYSLdRMWoAYYDUj.jpg
 
Nauliza hili swali sababu kama wananchi tunataka kufahamu ukweli juu ya hili janga. Tunataka waziri wa afya, au msemaji mkuu wa serikali kila siku awe anatoa taarifa zilizo rasmi.

Mbona nchi za wenzetu ambazo zimekumbwa na hili janga kila siku lazima watoe taarifa rasmi kuhusu maambukizi,waliopona na waliofariki.

Au hapa Tanzania ndio kusema mambo yanaenda kimya kimya? Maana watu kila kukicha ni kutishwa tu na habari ambazo sio rasmi.

Mara tunasikia watu wanazikwa usiku, mara tunasikia rubani wa Tanapa alikufa kwa Covid-19,mara kuna maiti imekaa siku mbili mtaa wa Lumumba. Lakini hatusikii serikali ikikanusha wala kuwaambia ukweli wananchi.

Kwa jinsi hili janga lilivyo serious ilipaswa waziri wa afya au msemaji wa serikali angekuwa kila siku anakaa na wanahabari na kutoa takwimu na taarifa rasmi.

Lakini mtu mmoja ambae anamiliki jarida la mtandaoni (Pambazuka) anapoachiwa awe anaandika habari za uongo kuwa watu wanazikwa usiku kimya kimya ni jambo baya maana watu hofu inazidi kwa wananchi.

Inatoka habari kuwa madereva wanne watanzania wamepimwa huko Uganda na kukutwa na ugonjwa wa Covid-19. Hofu inazidi kuwa kubwa kwa wananchi.
Hivyo ili kuondoa hofu lazima mtupatie taarifa rasmi,kama nchi tupo wapi?

Maambukizi ni mengi? Yamepungua? Na wanaopona ni kiasi gani? Hii iwe kila siku na mruhusu kupigwa maswali na waandishi wa habari kama Andrew Cuomo gavana wa New York anavyofanya kila siku. Maana hatulali ni hofu tu.
Vipi bado mnataka data?
 
Briefing sio kama hazipo , zipo na wanapatiwa mabeberu huoni kama wametoa mihela juzi, nchi hii ina siri sana
 
IMEKUJA UTI IKO HAPO CONCO ukiipata unakata moto.... Mungu akatupe wepesi
 
Back
Top Bottom