Kwanini TPDC wanalipwa mshahara mkubwa kiasi hiki?

Kwanini TPDC wanalipwa mshahara mkubwa kiasi hiki?

Kuna madereva wa hazina wao per diem kwa siku ni laki tatu unachota tu unakuta safari ya siku 90 unalipwa cash...hahahahahaha ndo maisha sasa jiulize madereva wale wa site na hawa wa lami 24 hrs tofauti nayo...usiangalie ukubwa wa kazi ishu ni kwamba taasisi yenyewe tu inajipangia mishahara na ni baraka toka kwa wakubwa
Pia udereva una madaraja hauwezi kufananisha maslahi ya VIP na PSV.
 
Yani kuna ugumu gani wa kazi kwenye hili shirika? Maana anayeanza kazi tu anakomba mpaka million tano kwa mwezi. Ni mshahara wa mwaka mzima wa mwalimu.

Inamana kazi yao inaendana na kiwango cha mshahara? Dogo kaingizwa juzi tu kimagumashi hana hata miaka mitatu tayari kashusha Prado mpya zero kilometer pale Port. Nishauri serikali siyo nawaonea donge, ila wajaribu kupunguza hiki kiwango, haiwezekani mshahara wa mwalimu yeye anapiga kwa siku moja tu.

Nataka kujua kwa lipi hasa mpaka wapewe pesa ndefu kiasi hiki, yani unakaa miaka mitano tu kazini tayari salary slip inasoma million nane [emoji849].

View attachment 2443725
Nakukubali sana jembe langu mpwayungu village . Riziki hupangwa na Mungu na wala usisikitike fulani anapopatwa na mazuri, wala usifurahi fulani anapopatwa na mabaya.
 
Nilifanya kazi TPDC enzi Mkurugenzi Mkuu akiwa Yonna Kilagane,Mwenyekiti wa Bodi alikuwa General Mstaafu Robert Mboma,Mkurugenzi wa Masoko akiwa Dismas Fuko, Mkurugenzi wa Exploration Halfan Halfan ambaye baada ya kustaafu Mama Samia kamteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TPDC hapohapo,enzi Ofisi zipo Upanga kabla hatujahamia Mkapa Tower.
Uzuri wa TPDC upo kwenye kuwajali wafanyakazi wake kitaaluma,maana ukipelekwa kusoma Masters au PhD Ulaya unalipwa mpaka Pesa ya Pedi inakuwa kwenye Bajeti yako.Wakati huo Eng.Modestus Lumato alikuwa Ofisa wa kawaida na sasa hivi ni Mkurugenzi Mkuu wa EWURA,wakati Eng.Charles Sangweni alikuwa Ofisa wa kawaida na sasa hivi ni Mkurugenzi Mkuu wa PURA.
Bwana MPWAYUNGU uliza swali lolote kuhusu TPDC nitakujibu
Wewe kweli ni muandamizi Enzi hizo hata sisi tuliofanya field hapo tulikuwa tunapewa vijisenti
 
Okay..

Huko ukiwaambia nchi ngumu hawakuelewi..wanakuona umechanganyikiwa maana asali ni ya kutosha
Kabisa kiongozi Kuna jamaa angu yupo pale wizara za madini nianag'aa kama diamond anamatumizi ya hovyo minimum Kwa siku sio chini ya laki tano mpka Sita, yani hiyo pesa ni every day
 
ACHA wivu.

Tafuta kazi kwenye mamlaka yoyote upige pesa.
Regulatory authority mfano....

1. TPDC.
2.TRA.
3 TANAPA.
4.NEMC.
5. TCRA.
6. TANZANIA PORT AUTHORITY
NK.......

USITAMANI MALI YA JIRANI YAKO, WALA CHOCHOTE ALICHONACHO JIRANI YAKO.....
KUTOKA 20
Namba sita hapo wenye hela ni watu wa certificate na diploma imagine na degree yangu ya electric natumia harrier ambayo niliuziwa na shemeji yangu kwa milioni 8 (ni kama alinipa tu) ila kuna dogo wa operation Ana diploma Ana prado [emoji3]

So unaweza kupata kwenye mamlaka lkn bado ukawa njaa kali tu

Kuna jamaa anafanya kazi LITA Ana uhakika wa kukunja laki kila siku

•Jamaa wa ikulu asiponipeleka MSATA nitamloga
 
Mzee Mpwayungu hii dunia haina usawa. Cha muhimu ni kupambana tu usikose basic needs. Waalimu kwa kweli wana wakati mgumu. Hela yao ni ndogo ila ukirudi nyuma utaona wengi wao hawakufanya vizuri form 4 au 6 tofauti na waliosoma Petroleum Engineering. Hiyo kozi inachukua vipanga tupu waliosoma sayansi wakati hata division 3 ya 13 unaweza ingia Education UDSM. Kingine pia ajira za hao watu ni chache hivyo kitendo cha kwenda kusomea Petroleum Engineering walichukua risk kubwa mno. Ikumbukwe hata kwenye biashara sehemu yenye risk kubwa ndo kuna hela kubwa.

Waalimu pia wanafaidika na muda mwingi wa likizo kwenye mwaka. Ile miezi wanafunzi wanayofunga pia automatically waalimu wanapata likizo tofauti na fani zingine. Nawashauri waalimu wasikate tamaa wajiongeze kwenye ujasiriamali maana muda wa ziada wanao mwingi. Pia wasikae mbali na Chama Cha Mapinduzi kwasababu nyakati za uchaguzi wanawapaga madili.
 
Nilifanya kazi TPDC enzi Mkurugenzi Mkuu akiwa Yonna Kilagane,Mwenyekiti wa Bodi alikuwa General Mstaafu Robert Mboma,Mkurugenzi wa Masoko akiwa Dismas Fuko, Mkurugenzi wa Exploration Halfan Halfan ambaye baada ya kustaafu Mama Samia kamteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TPDC hapohapo,enzi Ofisi zipo Upanga kabla hatujahamia Mkapa Tower.
Uzuri wa TPDC upo kwenye kuwajali wafanyakazi wake kitaaluma,maana ukipelekwa kusoma Masters au PhD Ulaya unalipwa mpaka Pesa ya Pedi inakuwa kwenye Bajeti yako.Wakati huo Eng.Modestus Lumato alikuwa Ofisa wa kawaida na sasa hivi ni Mkurugenzi Mkuu wa EWURA,wakati Eng.Charles Sangweni alikuwa Ofisa wa kawaida na sasa hivi ni Mkurugenzi Mkuu wa PURA.
Bwana MPWAYUNGU uliza swali lolote kuhusu TPDC nitakujibu
Sawa, nikwavigezo gn walivyozingatia kuwapa mshahara mkubwa wafanyakazi wake, maana naona kama hiyo ni oversalary
 
kuna watu Tanzania ni watumishi wa umma na wengine humo humo serikalini ni kama deiwaka tuu sio sawa kabisa kuna taasisi wameshia wekewa mpunga wa mwisho wa mwaka huko halmashauli ni mwendo wa salary to salary
Naishangaa sana serikali haijui kuwa maisha yamebadilika, kumlipa mwalimu laki tano Kwa maisha ya sasa ni fedheha, lakini unakuta mtu yupo TPDC anagongwa million 7 Sasa unajiuliza Hawa wanapewa pesa ndefu hivyo wana hadhi kiasi gani cha kumpita Mara kumi mtumishi wa halmashauri
 
Mfano:-
  • Una 100,000/= unataka uigawe kwa watoto wako 100 (walimu); kila mtoto atapata 1,000
  • Mtu mwingine naye ana 100,000, akaigawa kwa watoto wake (25); kila mmoja atapata 4,000
Hii inamaanisha wingi wa wafanyakazi, unapunguza mgao wa kila mmoja.
Yeah sure, bora umelitambua hili
 
Back
Top Bottom