Kwanini TPDC wanalipwa mshahara mkubwa kiasi hiki?

Kwanini TPDC wanalipwa mshahara mkubwa kiasi hiki?

Kama ana Upper Second mwambie anitafute nimuunganishie akaanze hata kujitolea TPDC au PURA maana Mkurugenzi Mkuu wa PURA Eng.Sangweni ni mshkaji wangu anaweza akamsaidia,na uzuri pale ukipata nafasi ya kujitolea kisha nafasi zikaja kutangazwa official unachukuliwa kirahisi,na wao huwa wanatangaza wenyewe hawapitii PSRS
Hizi za TPDC na PURA zinazotangazwa PSRS je? Idhini si imetoka kwao? maana mwajiri ndio anapeleka maombi PSRS
 
Kila taasisi au shirika la serikali lina ajiri kupitia PSRS, hawa TPDC si kazi zao zilitangazwa huko utumishi hivi karibuni?
Labda kama wameanza siku za karibuni kupitia PSRS,lakini muda mwingi walikuwa wanaajiri wao direct,na si kweli kwamba kila Taasisi/Shirika la Serikali linaajiri kupitia PSRS,leo hii TANESCO wametangaza nafasi 5 au 6 lakini maombi unatuma kwa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO direct na sio PSRS
 
Labda kama wameanza siku za karibuni kupitia PSRS,lakini muda mwingi walikuwa wanaajiri wao direct,na si kweli kwamba kila Taasisi/Shirika la Serikali linaajiri kupitia PSRS,leo hii TANESCO wametangaza nafasi 5 au 6 lakini maombi unatuma kwa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO direct na sio PSRS
Hizo hapo,maombi ni direct kwa Mkurugenzi Mkuu TANESCO
Screenshot_20221212-094856.jpg
 
Hakika nifanikiwa kuingia Ikulu kwa njia yoyote ile 2030, lazima nikuteue kuwa Waziri Mkuu, au kama utakosa vigezo vya kielimu, basi nitakuteua kuwa Waziri wangu wa Elimu.

Yaani wewe ni Mgogo wa kwanza nchini kuwa na tabia kama za Marehemu Edward Moringe Sokoine. Wagogo wenzako wengine waliobakia, akili zote zimehamia tumboni.
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji120][emoji120]
 
Wakati nipo pale Staff hasa wa Idara ya Explorations walikuwa wanabadilishia mabegi Airport,yaani mfanyakazi anatoka safari ya kikazi mfano Norway na Dubai,anatua na Emirates saa 9 mchana ana check out,Mkewe anakuwa nje pale kamletea Begi lingine la nguo anabadilisha,anachukua nguo hizo alizoletewa,ana-check in kisha anageuza na Emirates hiyohiyo saa 11 jioni kwenda Calgary Canada huko au kokote kwenye kazi nyingine za Shirika,ndio maana pale Wafanyakazi walikuwa wanachukua VISA za mwaka mzimamzima kuepusha usumbufu
Dah, watu wanakula maisha ahse. Maninaa
 
Nilifanya kazi TPDC enzi Mkurugenzi Mkuu akiwa Yonna Kilagane,Mwenyekiti wa Bodi alikuwa General Mstaafu Robert Mboma,Mkurugenzi wa Masoko akiwa Dismas Fuko, Mkurugenzi wa Exploration Halfan Halfan ambaye baada ya kustaafu Mama Samia kamteua kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya TPDC hapohapo,enzi Ofisi zipo Upanga kabla hatujahamia Mkapa Tower.
Uzuri wa TPDC upo kwenye kuwajali wafanyakazi wake kitaaluma,maana ukipelekwa kusoma Masters au PhD Ulaya unalipwa mpaka Pesa ya Pedi inakuwa kwenye Bajeti yako.Wakati huo Eng.Modestus Lumato alikuwa Ofisa wa kawaida na sasa hivi ni Mkurugenzi Mkuu wa EWURA,wakati Eng.Charles Sangweni alikuwa Ofisa wa kawaida na sasa hivi ni Mkurugenzi Mkuu wa PURA.
Bwana MPWAYUNGU uliza swali lolote kuhusu TPDC nitakujibu
Mmmh,Watu Wana enjoy mema ya nchi
 
Kama ana Upper Second mwambie anitafute nimuunganishie akaanze hata kujitolea TPDC au PURA maana Mkurugenzi Mkuu wa PURA Eng.Sangweni ni mshkaji wangu anaweza akamsaidia,na uzuri pale ukipata nafasi ya kujitolea kisha nafasi zikaja kutangazwa official unachukuliwa kirahisi,na wao huwa wanatangaza wenyewe hawapitii PSRS
mkuu na mimi huwezi kunifanyia mpango nmesoma electrical nna upper second Ila npo tu kitaa nasugua benchi
 
Nilishatoka hapo Mkuu japo nina connection na Senior Staff wengi wa pale,kimsingi ni panono ndio maana kuna staff wawili Frola Salakana na Braison Kunyalanyala walihamishwa pale kwenda Idara nyingine za Serikali,kwa kuona kwamba pale wametolewa kwenye mrija wa Asali walikataa kwenda kuripoti huko walikohamishiwa wakafungua mpaka Kesi CMI[emoji1787][emoji1787]sijui hata Kesi yao iliishiaga wapi lakini waligoma kuhama wakawa wanakaa nyumbani tu,hatari sana
Umetaja hadi majina duh 😃
 
ila mishahara ya Tanzania inatakiwa kufanyiwa review watu wote mna degree moja mfano accounts ya halmashauli analipwa kidogo wa TRA au Bot au TCRA anampita mara kumi hii sio sawa wakati nature ya kazi ni moja
Hayo mashirika kama TPDC ni wazalishaji wakati halmashauri ni walaji, so hawawezi kuwa sawa na ni haki yao kulipwa hivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mishahara ya namna hii ni balaa na ni mitamu

Hyo 5 mil mwalimu anahangaika kuikopa bank na mpaka anamhonga afisa mikopo,afu kuna dogo anaikunja kwa mwezi na class alikuwa wa kawaida tu,
Elimu wanalingana?

Masomo waliyosoma yanalingana ugumu?

Kuna masomo huyo mwalimu mwenyewe aliyakimbia hata digrii akiambiwa kachukue hii wako wachache akakimbia mbio kuwa mimi siwezi

Pili huyo wa TPDC akitishia kuacha kazi na mwalimu akitishia kuacha kazi serikali itataka kumbembeleza yupi asiache kazi mwalimu au huyo mtaalamu wa TPDC?

Kupima kazi ipi muhimu waambie wote waandike barua ya notice masaa 24 kuacha kazi uone nani atajibiwa haraka kuwa kwenda zako.Mwakimu atakuwa wa kwanza kujibiwa kuwa ombi lako limekubaliwa
 
Back
Top Bottom