Kwanini tunalazimishwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa tupo Awamu ya Sita wakati Kiuhalisia bado tupo Muhula wa Pili wa Awamu ya Tano?

Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pil
 

Another Harebrained.
 
Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pil
Tufanye raisi wa sita. Mambo ya awamu kwanza hayapo kwenye katiba, katiba inaeleza vipindi vya miaka sio awamu. Awamu ni jina lililetwa nafikiri 1985 kama sikosei na ccm.
 
Awamu Ya Sita Na Rais Wa Sita Ni Kitu Kimoja.
Nyerere Amekaa Madarakani Muda Mrefu Kuliko Marais Wetu Wote ila Bado Kipindi Hicho Chote Kinahesabika Ni Awamu Ya Kwanza. Hata zile awamu 44 za marekani sio kwamba Maraisi wao wote wameongoza miaka 8 hapana. Kuna baadhi wameongoza miaka 2 wakafariki na akija Rais mungine Inahesabika ni Awamu Nyingine.

KATIBA Inasema Hivi:
Endapo Magufuli Angeongoza Miaka Mitatu Afariki Basi Samia Angemalizia Awamu Ya Magufuli. Ila Kwa Vile Magufuli baada Ya Uchaguzi wa 2020 Kaongoza Chini Ya Miaka Mitatu Basi Samia Anakuja Na Awamu Yake. Kwa faida Zaidi Nikwamba Endapo Uchaguzi Ujao Mama Samia Akihijataji Kutetea Kiti Chake Katiba Inamruhusu Kufanya Hivyo ila Akishinda Huo ndio Utakua Muhula Wake Wa Mwisho(2030).
Swali: kama Samia Anamalizia Awamu Ya Tano Inamaana Hadi 2025 Itakua Ameshatawala Miaka Kumi Kwa Mujibu Wa mtoa Mada. Na Kwa Mujibu Wa katiba Yetu Kiongozi Akishatawala Miaka Kumi Haruhusiwi Kugombea Tena, sasa je Iweje Mama SAMIA katiba Imruhusu Kugombea 2025 Wakati Atakua Ameshatimiza Miaka 10 Kiuongozi? .
 
Hivi vichwa mnabebea akili ama maji?
Easy katiba katika ibara ya 37 (5) na ibara ya 40 umetoa maelezo mazuri Sana.
Sasa sijui kwa Nini awamu ya tano hamuelewi Kama Isha Isha. Seee kwa kindali
 
Kusema hii awamu ni ya sita, ni sawa na kuamini kuwa baada ya Rais wa awamu ya 5 kufariki, na awamu ikafa

Kitu ninachoona anataka kujenga legacy yake, hataki kuwa kivuli cha rais wa awamu ya 5

Ukweli ni kwamba, hii ni awamu, muhula, au kwa lugha ya malikia ni 5th term

Sent from my M2004J19C using JamiiForums mobile app
 
Kwaiyo ni Rais au sio Rais na kama ni Rais ni Rais wa ngapi!
Tatizo CCM walijimilikisha nchi kuwa ni lazima waongoze miaka kumi na wakatumia Rais mfano wa tano kuita awamu ya sita lakini hakuna sheria inatambua hilo ila kiuhalisia JPM alikuwa Rais wa 5 nchi hii na Samia anakuwa ni Rais wa 6 nchi hii maana huwezi kusema Mama Samia ni Rais wa 6 Tanzania awamu ya 5. Ni juu yako kumwita Rais wa 6 au kama wanavyotaka awamu ya 6, Mama Samia anaelewa mchezo wa CCM wao kumwita awamu ya 5 ili 2025 waje waseme sasa tuchague mwingine lakini kuwa awamu ya sita basi inampa nguvu ndani ya chama CCM kumpa bila kupingwa 2025 kipindi cha pili kama wanavyopenda wao CCM japo hata sio katiba ya CCM ni utamaduni wao tu.
 
Sio kwamba hawaelewi basi tu hawataki kuelewa. mchezo uko hivi na Mama Samia anaelewa siasa za CCM wasiompenda, wanataka kulazimisha awamu ya 5 ili ikija 2025 wasiweze kumpa kijiti automatic za miaka mingine 5 kwa kusema awamu ya 5 inaishia hapa tufanye mchakato mpya wa kutafuta Rais ndani ya CCM na kama JPM angekuwa hai ndio ingekuwa hivyo kuna watu walishaota hiyo siku na JPM alishawahi kuwaonya na Mama juzi kawaonya, sasa Mama kuwa awamu ya 6 inafanya kama reset kwa maana 2025 kwa utamaduni wa CCM atapewa automatic sasa shida wale waliokuwa wanakimbilia hiyo nafasi wanaona itabidi mpaka 2030 mbali sana na umri utakwenda hii ndio siasa chafu na uhakika Mama anawajuwa hawa ndio maana akawaonya mnaotaka 2025 acheni haya tutayaongea. Hii ndio nyuma ya haya yote ndio maana Mama anawakumbusha hii awamu ya 6.
 
How comes mtu atumie ilani ile ile ya mwenzake halafu useme awamu ni tofauti? msilazimishe haya mambo.
Wapi ime define awamu ni ilani? unataka kusema Ilani ya mwaka 2015 ni ileile ya mwaka 2020? basi kama ni hivyo Magufuli alikuwa hii awamu ya 6 maana ilani ya 2015 ilikuwa nyingine na iliisha 2020 akaja na ilani mpya. hapa hakuna cha awamu wala nini ni lile onyo la JPM alishwahi kuwaonya walioanza mchakato wa 2025 akawataja na majina na juzi Mama kawaonya 2025, sababu ni kuwa wanataka kusema 2025 tufanye mchakato mya kutafuta mgombea CCM kuna watu wamesha invest sasa mama ka reset hii ni awamu mpya Rais mpya na tamaduni za CCM 10 years watu wameinvest 2030 wanaona mbali, ngoja Mama achukue kijiti mwenyekiti utaona panga litakavyopita mbona wanajulikana.
 
Jamani mbona mnajitoa ufahamu kwa makusudi, hili ni bunge la 11 sio la 5 ni bunge la 11 kwa maana kila baada ya miaka 5 uchaguzi japo Nyerere alitawala na kupita na mabunge matano. kwa hili ndio itabidi ujiulize wewe mbona bunge hili haliitwi la tano linaitwa Bunge la kumi na moja.
Wanaotetea na Kumtetea Rais Samia Suluhu Hassan kuwa yuko katika Awamu ya Sita waje pia kutuambia je, na hawa Wabunge nao ni wa Awamu ya Tano ( iliyokuwa ya Hayati Rais Dkt. Magufuli ) au nao ni wa Awamu tunayolazimishwa kuwa ni ya Sita?
 
Ni watu kutoelewa tu. Awamu huhesabika kutokana na mabadiliko ya Viongozi. Awamu sio fungu la Uongozi wa miaka 10. Hayati Mwalimu Nyerere alikuwa Rais wa awamu ya kwanza kwa kipindi cha miaka 20+

Mzee Ali Hassan Mwinyi aliongoza awamu ya pili kwa kipindi cha miaka 10 pia. Hayati Mzee Mkapa awamu ya tatu miaka 10, Mzee Kikwete awamu ya nne miaka 10, Mzee Magufuli awamu ya tano miaka mitano na miezi michache. Mama Samia Suluhu Hassan awamu ya 6 miaka....

Muhimu ieleweke kwamba awamu hubadilika kadri Uongozi unavyobadilika..
Mwendazake angeongezewa muda kama kelele kadhaa zilivyokuwa zinataka angehesabika kwa awamu mbili??
 
Tatizo kubwa kuna wana CCM bado wanateseka Mama kuwa Rais maana hawajawahi kuwaza alivyochagulia kwa makamu wa Rais kama mgombea mwenza na kushangilia hawakuwaza kama hili linaweza kutokea na labda hata katiba hatukujuwa kama huyu number 2 anaweza kuwa number 1 sababu huwa tunachukulia maisha for granted. Nadhani chaguzi zijazo makamu wa Rais itakuwa issue.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…