Kwanini tunapenda kuigana?

Waingereza wana msemo wao mmoja "imitation is the sincerest form of flattery".

Mimi nina tatizo tofauti kidogo na wewe, sitaki kuonekana naiga.

Halafu jirani zangu huwa kama wananijua nataka kufanya nini.

Kuna wakati nilikuwa nataka kununua Range Rover Evoque,nikasema Evoque imekaa kama mtu mwenye kibiongo, ninunue Sport. He, ile najikusanya kusanya na kuangalia reviews, jirani yangu mmoja si akanunua Range Rover Sport!

Nikasem asinunui tena, nikinunua itakuwa kama naiga.

Akahama.

Akahamia mwingine.

Akawa na Mercedes Benz SUV.

Nikasema mimi nitanunua ya tofauti, sedan.

Sijakaa vizuri boyfriend wake akawa anakuja na Mercedes Benz AMG 65.

Nikasema isiwe tabu, nakwenda kivingine, tusifanane kabisa.

Nikaishia na BMW X5.

Sasa hivi naona kuna jamaa mwingine naye ana BMW X5, najikusanya niende na Porsche Macan maana naona ndiyo gari ambayo mtaani hakuna.
 
Duh....
 
Mnaweza kutumia material sawa na nyumba zisifanane. Usawa ninaouzungumzia ni ule mtu anachukua ramani yako anaenda kujenga vile vile kama wewe.
Ktk nyumba ndo nakataa kbsaa sitataka kuiga kbsaa....yaani zinafanana hadi kero...shida nyumba sio nguo kuwa itaisha yaani kila siku unaiona jinsi inavyofanana na ya Joni au Ally. Mbaya kuna wale watoto watukutu wakiingia tuu wanasema mama hii kama nyumba yetu unatamani umzame kibao cha kama kile cha mwinyi lakini unakumbuka uliomba ramani kwa baba yake
 
Hadi mtoto anagundua nyumba kama yao!
 
hata katika biashara ukianzisha kitu kila mtu naye anataka kufanya.usitulaumu akili zetu kama feni zilizo simama wanataka ujaribu uwe chambo wakiona kizuri nao wana jaribu wakisikia kibaya kutoka kwako nao wanakalia kukucheka
 
Ukitaka ramani labda ukachoree nje ya tz, hapa bongo watu watakuchorea kwa gharama afu wataenda iuza.
 

Hahahaa mbinguni tu wote tutakua sawa haki ya nani
 
Ili uendane na wakati, si vibaya kuiga vile vizuri..maisha yamebadilika hivyo tunatakiwa kuendana na wakati.

Ukiona kizuri, unaweza kuiga + ubunifu = utafika mbali kimaendeleo
 
This is my positive spin on it.

In full disclosure, I gotta be honest that at some point copycatting used to bother me. It used to annoy me big time.

But then I came to the realization that if you truly want your ‘own’ things then you might as well move to an island all by yourself and make everything for yourself that nobody else has.

Ha! Well...how about that now?!

So I changed my opinion on it. Now I don’t look at it as negatively as I did.

Now I take it as affirmation of my style, my taste, and my swag.

That they dig it and they wanna be like me. Nothing wrong with it, whatsoever.

If anything it’s gonna make me be more creative so I can maintain my ‘uniqueness’ [for lack of a better word].

So copy me all you want. It’s flattering.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…