Kwanini tunatafsiri mshale wa saa kinyume na inavyoandikwa - hii inatokana na nini?

Kwanini tunatafsiri mshale wa saa kinyume na inavyoandikwa - hii inatokana na nini?

Siku kwa mujibu wa mfumo wa kimagharibi inaanza saa sita za usiku, wich is weird.

Katika mfumo wa Kiswahili siku inaanza saa moja asubuhi.

Tatizo tunachanganya mifumo, tunatumia mfumo wa kimagharibi ambao siku inaanza saa sita usiku lakini tukisoma kiswahili tuna soma saa kwa mfumo unaofuatisha siku inayoanza saa moja asubuhi.

Saa ya Kiswahili inatakiwa kuonesha saa moja pale ilipo 1. Nishawahi kuona saa iliyokuwa set hivyo.

Sadly, aliyefanya hivyo ni mzungu aliyependa Uswahili.

Na mimi kamwe huwezi kuta saa yangu nimeset kizungu.

Mwenyewe nishazoea fresh. Coz hakuna logic ya kuset masaa yetu kizungu wakati kiuhalisia tupo kinyume na mzunguko wao wa masaa na kuanza kwao kwa siku.
 
I have a question, kama hapa Tz(ingawa haifuatwi na wengi) siku huisha saa moja jioni(jua linapozama) na siku huanza saa moja asubuhi(jua linapochomoza), huu muda kati ya saa moja ya jioni na saa moja asubuhi inakuwa ni siku gani hasa? Na tarehe yake ni ya siku iliyoisha au inayofuata?

Kwani mkuu siku si ina masaa 24?
Yaani kuanzia 1 asubuh hadi saa 1 asubuhi tu tunakamilisha masaa 24 yaani ndo inakua siku 1.

So kuanzia 1 jioni hadi 1 asubuhi bado tupo kwenye siku ileile hadi kukuche ndo tunabadili tarehe. ( ikiwa hufuati ile ya Saba za usiku ndo kubadilisha tarehe kama wengi walivozoea)
 
Siku kwa mujibu wa mfumo wa kimagharibi inaanza saa sita za usiku, wich is weird.

Katika mfumo wa Kiswahili siku inaanza saa moja asubuhi.

Tatizo tunachanganya mifumo, tunatumia mfumo wa kimagharibi ambao siku inaanza saa sita usiku lakini tukisoma kiswahili tuna soma saa kwa mfumo unaofuatisha siku inayoanza saa moja asubuhi.

Saa ya Kiswahili inatakiwa kuonesha saa moja pale ilipo 1. Nishawahi kuona saa iliyokuwa set hivyo.

Sadly, aliyefanya hivyo ni mzungu aliyependa Uswahili.
sure: i think tunafanya maisha yetu magumu bila sababu, kuna wakati
ukifanya hivyo watu wanakutazama kama layman hivi. ni kama kuzungumza kwenye simu kisha ukutamka ni ''dipu'' badala ya ''nibipu''
japo siku hizi nimeamua kwenda moja kwa moja kutumia saa 24, badala ya matumizi ya pm na am.
 
sure: i think tunafanya maisha yetu magumu bila sababu, unajua mimi nilipokuwa primary niliona mtu akiandika kwa kufuata namba zilivyo, lakini wenzangu wakawa wanamcheka sana, anaonekana asiyejua kusoma saa.
ukifanya hivyo watu wanakutazama kama layman hivi. ni kama kuwa na simu na kutamka ni ''dipu'' badala ya ''nibipu''
japo siku hizi nimeamua kwenda moja kwa moja kutumia saa 24, badala ya matumizi ya pm na am.

Jambo lingine linalochangia ni kutaka kwenda sawa na ulimwengu wa nje ya utamaduni wetu.

Hatuwezi kuwa kisiwa.

Kwa mfano, unaweza kuepuka mfumo wa kimagharibi ukiwa kwako, lakini kwenye mtandao wa internet huwezi kuuepuka.
 
Saa 1 inaandikwa 7,2=8,3=9 sasa tofauti ni sita kwa kila masaa yaani 7-1=6 ambayo ni namba ya yule mnyama 666.Tafakari!
 
Hata mimi nilisikia hivyo.
Yani ukichukua zile namba ukitoa namba za saa halisi unapata common difference ambayo ni 6

what is the use of that 6 in their rituals???? coz ili kuthibitisha kwamba walitaka ije common difference (6) ni lazima utoe sababu ya kuwa hiyo sita inatumika katika nn na uoneshe kwamba ni jinsi gan ilivyomuhimu katika mambo yao
 
Mwanahisabati yeyote duniani hajawahi fundishwa kwamba 1ni7,2ni8,10ni4 wala 3ni9.Hata wewe ulipoingia Darasani kwa mara ya kwanza ulifundishwa moja ni moja 2n2 na 12ni12.Hata hesabu zoote duniani zinafanyika na zinatumika kiivyo.
1+1=2
hakuna 1 + 1= 14
never happen,
kwaio wee soma saa yako kama ulivyofundishwa kuhesabu.
 
I have a question, kama hapa Tz(ingawa haifuatwi na wengi) siku huisha saa moja jioni(jua linapozama) na siku huanza saa moja asubuhi(jua linapochomoza), huu muda kati ya saa moja ya jioni na saa moja asubuhi inakuwa ni siku gani hasa? Na tarehe yake ni ya siku iliyoisha au inayofuata?

are you serious? really???
 
Nafikiri sababu siku inaisha saa sits za siku. Kwa hiyo hesabu inaanzia saa saba za siku Yaani 1.00 am. Kwa hiyo saa moja asubuhi 7.00 am ni muda mrefu sana baada ya siku kuwa imeanza.
 
Mwenye thina uhakika but kuuliza si ujinga!
Hizo hesabu ulizoziweka mbona ukiikusudia nö yoyote inakuja hivyo hivyo?
mfano, nö 4
5-1=4
6-2=4
7-3=4
8-4=4 na kuendelea....
...
Au mimi thijaelewa!
Embu alieelewa hasabu za jamaa na mahusiano yake ktk mpangilio wa usomwaji saa.

Ni kweli hukuelewa.
Saa mbili kwenye uso wa saa inaonesha 8. chukua 8-2=6
saa moja utaonekana 7. toa 7-1=:6.
10-4=6
12-6=6
nadhani umeelewa sasa!
 
Masaa unayoyahesabu wewe ni ya kiarabu vile wao huanza siku saa 12 asubuhi. Watu wa magharibi siku huanza baada ya saa 6 usiku na ndio utaratibu duniani kote. Pia kiarabu wiki huanzia jumamosi wakati wamagharibi siku huanza jumatatu.

Hii yakwako inaleta mantiki nakubaliana na wewe kabisa.
 
Duh... This is "Unkwepable" hata ukibadili mfumo wa saa mifumo mingine kama ya Internet hatuwezi kubadili....

Bora tuendelee hivyo hivyo tulivyozoea make haiathiri chochote....
 
Jambo lingine linalochangia ni kutaka kwenda sawa na ulimwengu wa nje ya utamaduni wetu.

Hatuwezi kuwa kisiwa.

Kwa mfano, unaweza kuepuka mfumo wa kimagharibi ukiwa kwako, lakini kwenye mtandao wa internet huwezi kuuepuka.

Mkuu hapo umenena!
 
Na hii ni kwa kiswahili tu. Kwani lugha chache nimazojua wakiona mshale kwenye 2 wanasoma 2 na waelewa cha kufanya kwa muda huo. Shida ni sie tukiona mshale kwenye 2 tumasoma kinyume
 
Wakuu musichanganye mambo ni hivi sisi (watz)mambo/vitu vingi tunafuata uingereza ambapo saa lnaanzia saa 6 usiku.
 
I have a question, kama hapa Tz(ingawa haifuatwi na wengi) siku huisha saa moja jioni(jua linapozama) na siku huanza saa moja asubuhi(jua linapochomoza), huu muda kati ya saa moja ya jioni na saa moja asubuhi inakuwa ni siku gani hasa? Na tarehe yake ni ya siku iliyoisha au inayofuata?

Siku inaanza saa moja asubuhi na juisha saa kumi na Mbili asubuhi tena......one day= 24hrs
 
Mbona jibu liko wazi hapo.Ni kutokana na utamaduni/mapokeo? wa waliovumbua hizo saa na si vingievyo.Kumbukeni tamaduni hizo na mapokeo zimetufanya tunapoandika katika baadhi ya lugha maandishi hutokea kulia kwenda kushoto na katika lugha nyingine maandishi hutoka kushoto kwenda kulia ,lakini katika hili hatuhoji kulikoni iwe hivi?na sisi tunaojiuliza kwa nini saa 1 isomeke 7 hatujiulizi kwa nini neno batil katika lugha moja maandishi hutoka kulia kwenda kushoto na kwenye lugha nyingine maandishi hutoka kushoto kwenda kulia
 
wana JF ningeomba hapa mnijuze wale mnaoelewa hilijambo kwa undani zaidi manake najiuliza sijui ni utumwa ama nini?, manake siielewi hii, kukuta saa inaandikwa nane(8) lakini inasomwa mbili(2), ama inaandikwa kumi(10) lakini inasomwa nne(4). huu utaratibu wa kusoma saa ndivyo sivyo ulitokana na nini?.

pia je na wazungu (waingereza) ama hata wamarekani huko makwao wanasoma hivyohivyo mishale ya saa?. ama wanafuata mtindo huo wa namba.ningeombwa wenye kuelewa chanzo mtujuze.


View attachment 137430

mimi mtu yeyote atakuwa sahihi pale ambapo saa itakuwa imeandikwa saa (8) yeye akasema ni saa (2). Kwa nini nasema hivyo?
Hii inatokana na sababu kuwa ni saa (8) tokea siku mpya ikiwa imeanza yaani baada ya saa (6) mchana au usiku.
Na atakaye sema saa (2) yuko sawa kwa sababu ni saa (2) baada ya jua kuchomoza au kuzama.
Kwa maana hiyo basi unakuta saa inasema saa (8) asubuhi. Sisi tunatafsiri kuwa ni saa (2) asubuhi, tukiwa na maana kuwa ni masaa (2) tokea jua lichomoze.
Vivyo hivyo ukikuta kwenye saa imeandikwa saa (8) usiku. Mtu akikuambia ni saa (2) usiku yupo sawa kwa sababu anamaanisha ni masaa (2) tokea jua lizame.
Naamini nimeeleweka.
 
Back
Top Bottom