Kwanini unapaswa kununua bond au Hati fungani ya NMB?



Mkuu bonds sio hisa
hakuna swala la kuangalia mambo yanaenda au la
ni unawakopesha wewe pesa kwa riba kwa mda fulani
mda ukifika wanakulipa

ninavyofahamu hakuna kujitoa ...wala kuongeza wala kupunguza
unawapa mda ukifika wanakulipa chako....
 
Quarterpin, je katika mahesabu yao wanajali kuhusu kushuka kwa thamani ya ela yetu, nikiweka kwa mfano mil 20, kwa kasi jinsi ela yetu inavyoshuka 20ml ya leo si sawa na 20ml ya baada ya miaka ya miaka 3.
 

1. Iwapo utahitaji fedha ulizowekeza katika hati fungani kabla ya muda wa kukomaa, itakupasa kuuza hati fungani yako katika soko la hisa la Dar-es-Salaam (DSE) kupitia wakala. Kisha utalipwa fedha zako pindi tu hati fungani yako itakapouzwa kwa mwekezaji mwingine.

2.Huwezi kuongeza wala kupunguza.
 
Quarterpin, je katika mahesabu yao wanajali kuhusu kushuka kwa thamani ya ela yetu, nikiweka kwa mfano mil 20, kwa kasi jinsi ela yetu inavyoshuka 20ml ya leo si sawa na 20ml ya baada ya miaka ya miaka 3.

Unaponunua hati fungani ya NMB, unakuwa umeikopesha benki fedha zako, gawio lako baada ya miaka mitatu litakuwa kwa kiwango kile kile cha riba mlichokubaliana.
 
Ni wazi sasa wengi wetu sasa tumeelimika kupitia mada nyingine za hati fungani za NMB (NMB BONDS)ni kupitia mada hizo maswali maoni uchambuzi na hata kuchagiza kwa namna yake vilijitokeza
Wengi waliongelea kuhusu faida kidogo ipatikanayo kwenye hatifungani, lakini naamini kabisa hawakutafakari kuhusu gharama za uendeshaji kodi bima nk za hatifungani
Si kila mmoja wetu ni mfanyabiashara au anaweza kufanya biashara, kwahiyo unaweza kuwaza faida nono unayowaza kupata kwenye biashara fulani lakini bila kutafakari yafuatayo
-kodi za pango
-gharama za uendeshaji
-mishahara ya wafanyakazi
-kodi mbalimbali
-risk mbalimbali
-muda wa ufuatiliaji
Na wakati mwingine hasara au mzigo kuchelewa kutoka kwa wakati
Ukija kuyajumuisha haya yote na faida unayopata utajikuta faida ni ndogo kuliko matarajio yako
Kuna wengi wetu pia wameweka pesa zao nyingi tu bank huku Zikiwa zina makato ya kila mwezi na gharama nyinginezo. .HUKU NI KUPOTEZA
Hivyo basi kwa mkakati huu waliokuja nao NMB wa hatifungani ni wazi utakuwa ni mkombozi kwa watu wengi hasa
wafanyakazi wa kaliba zote
Wafanya biashara kubwa za kati na ndogo ndogo
Watu wa jinsia zote
Wenye kupata pesa za msimu nk nk
Pesa yako ya kunulilia hatifungani inakuwa salama huku ikizalisha
Unakuwa huna pressure hata msimu Unapokuwa chini
Unakuwa huna gharama za uendeshaji
Unakuwa una uhakika wa faida isiyoyumba
Huhitajiki kulipa kodi mbalimbali wala mishahara ya wafanyakazi
Kimsimgi unakuwa na faida yako murua isiyokuletea headache yoyote
Kwasasa NMB ni Benki inayofanya vizuri sana kwahiyo uhakika wa pesa yako unakuwa si wa mashaka mashaka
Hujachelewa bado unayo nafasi ya kununua hatifungani za NMB
 

Kaka mshana jr umeelezea vizuri na ninaimani bandiko lako litawatoa watu wengi gizani kwa maana kununua hati fungani ya NMB ni tofauti na kuweka fedha zako Benki ambapo utakuwa unakatwa monthly charges and sorts. Bond ni kwamba unaikopesha benki ya NMB fedha zako kwa muda na riba ya 13%.
 
Asante nafikiri kwa picha inaweza kuwa rahisi zaidi kwa mtu kuelewa dhana nzima ya hatifungani za NMB
 
Hizo bond wanaweka watu wenye hela ngingi ambazo hawajui wazitumiaje.
Sasa ww na mshahara wako wa 1m unataka ukanunue bond?!.. utachekesha..
 
Mkuu bonds sio hisa
hakuna swala la kuangalia mambo yanaenda au la
ni unawakopesha wewe pesa kwa riba kwa mda fulani
mda ukifika wanakulipa

ninavyofahamu hakuna kujitoa ...wala kuongeza wala kupunguza
unawapa mda ukifika wanakulipa chako....
Kujitoa kupo,
Bond hii itasajiliwa ktk solo la Hisa la Dar es salaam na huko unaweza uza kama utahitaj hela yako kabla ya maturity date

Lakin si kama ukiona mambo hayaendi kama ulivyo andika sababu kwenye bond makubaliano mliyoingia awali ndo yanafuatwa hata kama itakuwaje
 
Hata uwe na 100m usiwekeze kwenye bond, bora uchek issue zingine.
Ni mpaka uwe na mipango thabiti na uhakika wa kurudisha msingi na faida...wengi wamepoteza pesa nyingi kwa kufanya biashara na uwekezaji mwingine kisha wakaishia kutapeliwa kuibiwa au kupata hasara
 
Nadhani somo zaidi linahitajika hasa mlengwa wa hili jambo (kipato cha kati na matajiri) anatakiwa alishwe taarifa za kushibisha ili aridhike na kuiona faida ya kuingia kwenye mfumo huo
Lakini naomb niwe muwazi hili jambo halimsaidii masikini hapa namaanisha mwenye kipato kisichozidi mil.20 kwa mwaka huu si uwanja wake kabisa
 
Habarini wakuu poleni na majukumu.... Asee kuna hili tukio la NMB kuuza hatifungani lililoisha mwezi June mpaka leo roho inanisuta kwa kutowekeza hata kamtaji kadogo katika hatifungani hiyo... Kwani ilikua na riba ya 13% ulikua ni moja ya uwekezaji mzuri kwa kweli kwa ambaye anafedha bank kuliko kuziweka katika current accounts..
 
Hata hivyo soon interest za mabenki zitakwenda huko kwa sababu ya Liquidity problem kwenye mabenki kufuatia serikali kupanda 500B kwenye mabenki.
 
Hati fungani hizihizi za 13%[/QUOTE]
Hati fungani hizihizi za 13%[/QUOTE]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…