Kwanini USA na EUROPE wamelitawala sana anga la ndege za abiria ulimwenguni?

Kwanini USA na EUROPE wamelitawala sana anga la ndege za abiria ulimwenguni?

ward41

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2022
Posts
749
Reaction score
2,533
Mashirika mengi ya usafiri wa anga ulimwenguni yanatumia sana ndege zinazotengenezwa na either Boeing ya Marekani au Airbus ya Europe. Ni kwanini? Ina maana nchi nyingine kama china, Russia, south Korea wameshindwa kuunda haya madude?

Hata mashirika yaliyoko china ndege zao ni either Boeing au Airbus. Wajuzi wa haya mambo tunahitaji elimu kutoka kwenu.

images (59).jpeg
images (60).jpeg
 
Asikwambie mtu, tecs za US na Ulaya ni za juu saana. Achana na ndege jaribu kucompare products zingine kama magari, mashine za ujenzi n.k utagundua vitu vyao ni jiwe haswa, hawanaga kurahisisha mambo.
 
Mashirika mengi ya usafiri wa anga ulimwenguni yanatumia sana ndege zinazotengenezwa na either Boeing ya Marekani au Airbus ya Europe. Ni kwanini? Ina maana nchi nyingine kama china, Russia, south Korea wameshindwa kuunda haya madude?
Hata mashirika yaliyoko china ndege zao ni either Boeing au Airbus. Wajuzi wa haya mambo tunahitaji elimu kutoka kwenuView attachment 2207265View attachment 2207267
Afu anakuja mtu anawabeza mabeberu, Ni hivi miaka ya 60 marekani alikuwa anatengeneza Boeing za kutosha, China Wana ka panga boy wanakaiza Xiang, kwa Africa Burundi ndo wanakamiliki[emoji3]
 
Mashirika mengi ya usafiri wa anga ulimwenguni yanatumia sana ndege zinazotengenezwa na either Boeing ya Marekani au Airbus ya Europe. Ni kwanini? Ina maana nchi nyingine kama china, Russia, south Korea wameshindwa kuunda haya madude?
Hata mashirika yaliyoko china ndege zao ni either Boeing au Airbus. Wajuzi wa haya mambo tunahitaji elimu kutoka kwenuView attachment 2207265View attachment 2207267
Beberu ni janja sana kwenye biashara! Ule mkasa uliyoikumbuga Boeing 737 ingekuwa ndo shirika la Boeing ni la wachina basi zimepigwa propaganda na uenda zingepigwa marufuku kwenye anga lao la Uraya na US!

Mrusi anazo ndege anatengeneza sijui anakwamaga wapi kujibrandi kwenye biashara zake! Nahisi pia Russia sehemu ambayo hajawekeza sana ni kwenye Social Welfare, angefanyia kazi hapa angeweza kuuza bidhaa zake nyingi maana kuhusu masuala ya Anga inaonekana Russia anategemewa sana huko US na Uraya hasa kwenye marocket yao ya anga za mbali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mashirika mengi ya usafiri wa anga ulimwenguni yanatumia sana ndege zinazotengenezwa na either Boeing ya Marekani au Airbus ya Europe. Ni kwanini? Ina maana nchi nyingine kama china, Russia, south Korea wameshindwa kuunda haya madude?
Hata mashirika yaliyoko china ndege zao ni either Boeing au Airbus. Wajuzi wa haya mambo tunahitaji elimu kutoka kwenuView attachment 2207265View attachment 2207267
Utamaduni wa mabeberu ndio sababu kubwa kuwa sehemu bora ya kuzalisha bidhaa zenye ubora ( compitetive culture ) tabia ya ushindani inachangia sana mabeberu kufanya tafiti na kuleta vitu Bora ambavyo vitashindana vizuri sokoni.

Sheria na taratibu za mabeberu zinawapa hati miliki wake wenye uwezo wakugundua formula za utengenezaji wa bidhaa muhimu za ushindani ( intellectual rights ). Nchi zenye elements za ujamaa kuna ubabaishaji na unafikili mwingi sana richa ya kuwa watu wake niwashindani
 
Ulaya kwenye magari na turbine engines za meli wako vizuri zaidi ya Marekani.

Uingereza walikuwa na Comet ndio ndege yao ya kwanza jet ya abiria na ndio ilianza duniani kama sikosei. De Havilland ndio waliitengeneza miaka hiyo wakiizidi Boeing. Boeing kilichowabeba ni tender za ndege za kijeshi faida walitoa hapo wakawekeza kwa abiria, pia wanakuwa na products ambazo ni dual use ndege inakuwa ya abiria inapewa version yake ya kuwa maritime patrol au anti submarine warfare.

Japan ilitakiwa iwe na uwezo mkubwa wa kutengeneza ndege hasa hawa akina Mitsubishi ila Marekani iliwawekea vikwazo vya miaka 7 kuanzia mwaka 1945 baada ya WW2. Huo muda ndio ulikuwa jet age ambaye hakutengeneza jet miaka hiyo aliachwa nyuma mno.

Ujerumani ilibidi iwe bingwa. Makampuni kama Messerschmitt na Focke-Wulf yalitoa fighter jets kwenye WW2 na zilisumbua. Wao ndio walitoa first jet fighter ikakamatwa na Wamarekani wakaenda kuisoma. Walikuwa vizuri kwenye aerospace engineering hadi rocket la kwanza walitengeneza wao zile V2 flying bombs. Vita iliwarudisha nyuma.

USSR walikuwa na mashindano na Westerns. Designers wao kupitia design and manufacturing bureaus kina KnAAPO na nyingine kupitia wanasayansi wao muhimu ambao wengi walishinda tuzo za Hero of Soviet Union, kina Mikoyan, Mikhail Gurevich, Tupolev, Pavel Sukhoi, Georgy Beriev, etc walikuwa wajuzi sana. Teknolojia ilishindwa kuungana kusaidiana, uchumi ukashuka, emphasis ikawa kwenye ndege za jeshi kuliko rais mwishowe soko la raia ndio kubwa kwahiyo wakashindwa. Hii consortium ya UAC ndio inawabeba hawa watengenezaji wa Sukhoi Superjet-100 ambazo ziko very reliant kwenye tech ya Western. Sanctions zinakuja hawaendi kokote.

UK walitelekeza sekta yao ya anga, wazungu waliokuwa watengenezaji wa spare parts ndio wakaungana kwenye Airbus ambayo mainly ni ya Ufaransa. Washiriki wengine ni UK, Spain, Italy, Germany na sijui kama kuna mwingine. Makampuni kama Aerospatiale na BAE Systems yaliunga juhudi hapo.

Mchina anakopi ila ni vigumu sana kukopi fly by wire systems na vigumu zaidi kukopi jet engines. Hizo wababe ni Rolls & Royce ya Uingereza, Pratt & Whitney ya Marekani. Wengineo ni kina Safran ya Ufaransa, General Dynamics ya US na Aviadvigatel ya Urusi ambayo inaachwa nyuma kwa sababu kadhaa.

Ndege hazina majaribio. Ukiharibu reputation leo kuja kuirudisha hata miaka 20 ni midogo, huwa zinapewa certificate kwa masharti sana hivyo kama hujui kitu usiwekeze hela nyingi mwishoni hakuna atakayenunua. Hata Marekani ilikuwa na McDonald Douglas ikapotea sokoni mpaka ikauzwa kwa Boeing. Ndio watengenezaji wa F-16
 
Afu anakuja mtu anawabeza mabeberu, Ni hivi miaka ya 60 marekani alikuwa anatengeneza Boeing za kutosha, China Wana ka panga boy wanakaiza Xiang, kwa Africa Burundi ndo wanakamiliki[emoji3]
Hata Rais XI akisafiri anatumia Boeing 747
 
Mkuu unastaili kusema "chukua daftari na peni uchukue notes"asante sana🙏🙏🙏
Ulaya kwenye magari na turbine engines za meli wako vizuri zaidi ya Marekani.

Uingereza walikuwa na Comet ndio ndege yao ya kwanza jet ya abiria na ndio ilianza duniani kama sikosei. De Havilland ndio waliitengeneza miaka hiyo wakiizidi Boeing...
 
Ulaya kwenye magari na turbine engines za meli wako vizuri zaidi ya Marekani.

Uingereza walikuwa na Comet ndio ndege yao ya kwanza jet ya abiria na ndio ilianza duniani kama sikosei. De Havilland ndio waliitengeneza miaka hiyo wakiizidi Boeing. Boeing kilichowabeba ni tender za ndege za kijeshi faida walitoa hapo wakawekeza kwa abiria, pia wanakuwa na products ambazo ni dual use ndege inakuwa ya abiria inapewa version yake ya kuwa maritime patrol au anti submarine warfare.

Japan ilitakiwa iwe na uwezo mkubwa wa kutengeneza ndege hasa hawa akina Mitsubishi ila Marekani iliwawekea vikwazo vya miaka 7 kuanzia mwaka 1945 baada ya WW2. Huo muda ndio ulikuwa jet age ambaye hakutengeneza jet miaka hiyo aliachwa nyuma mno.

Ujerumani ilibidi iwe bingwa. Makampuni kama Messerschmitt na Focke-Wulf yalitoa fighter jets kwenye WW2 na zilisumbua. Wao ndio walitoa first jet fighter ikakamatwa na Wamarekani wakaenda kuisoma. Walikuwa vizuri kwenye aerospace engineering hadi rocket la kwanza walitengeneza wao zile V2 flying bombs. Vita iliwarudisha nyuma.

USSR walikuwa na mashindano na Westerns. Designers wao kupitia design and manufacturing bureaus kina KnAAPO na nyingine kupitia wanasayansi wao muhimu ambao wengi walishinda tuzo za Hero of Soviet Union, kina Mikoyan, Mikhail Gurevich, Tupolev, Pavel Sukhoi, Georgy Beriev, etc walikuwa wajuzi sana. Teknolojia ilishindwa kuungana kusaidiana, uchumi ukashuka, emphasis ikawa kwenye ndege za jeshi kuliko rais mwishowe soko la raia ndio kubwa kwahiyo wakashindwa. Hii consortium ya UAC ndio inawabeba hawa watengenezaji wa Sukhoi Superjet-100 ambazo ziko very reliant kwenye tech ya Western. Sanctions zinakuja hawaendi kokote.

UK walitelekeza sekta yao ya anga, wazungu waliokuwa watengenezaji wa spare parts ndio wakaungana kwenye Airbus ambayo mainly ni ya Ufaransa. Washiriki wengine ni UK, Spain, Italy, Germany na sijui kama kuna mwingine. Makampuni kama Aerospatiale na BAE Systems yaliunga juhudi hapo.

Mchina anakopi ila ni vigumu sana kukopi fly by wire systems na vigumu zaidi kukopi jet engines. Hizo wababe ni Rolls & Royce ya Uingereza, Pratt & Whitney ya Marekani. Wengineo ni kina Safran ya Ufaransa, General Dynamics ya US na Aviadvigatel ya Urusi ambayo inaachwa nyuma kwa sababu kadhaa.

Ndege hazina majaribio. Ukiharibu reputation leo kuja kuirudisha hata miaka 20 ni midogo, huwa zinapewa certificate kwa masharti sana hivyo kama hujui kitu usiwekeze hela nyingi mwishoni hakuna atakayenunua. Hata Marekani ilikuwa na McDonald Douglas ikapotea sokoni mpaka ikauzwa kwa Boeing. Ndio watengenezaji wa F-16
Umeeleza vizuri sana ila pia kuna promotion na propaganda nazo zinafanyika sana kwenye hili siko ulimwengu umeaminishwa kua ndege bora ni za ulaya tuu nyingine mbovu.....hata Boeing au Airbus wapate ajali itaonekana ni sababu nyingine sio ubora....ila kampuni nyingine utasikia ni ubora mbovu
 
Back
Top Bottom