Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Habari wakuu,naomba kuuliza hivi ikiwa mtu umefanya interview za post ambazo zilikuwa za mikataba na nyingine za permanent halafu placement zikatoka ukawa umepata ile ya mkataba vp kuhusu placement za permanent bado nitaitwa au hapo imekaaje maana Kuna placement za permanent zilitoka baada ya kupata hii ya mkataba na jina halikuwepo
 
Bandiko bora kwa mwaka wote wa 2024
 
Wewe oral uliionaje? Wanasema maandishi mekundu siyo mazuri
 
Oral niliifanya tu vizuri,na mpaka sasa status inasoma selected for oral interview both web na app, wasiwasi wangu ni kuwa isije ikawa kwa vile nimepata hii ya contract wakaninyima zile za permanent
Hii sio rahisi
 
Mkuu umeongea point kweli lakini Utumishi hakutabiriki ,Kuna watu najua wamepata Kazi Sababu walikua darasani vizuri GPA nzuri,wengine wanajua kujieleza vizuri ,kujiamini kwingi.na wengine Wana hizo sifa zote lkn hawajapata,na wengine Ni God's grace tu
 
Wakuu nimeshafanya oral interview,
Kwenye web status bado iko SELECTED FOR Oral interview then kwenye app Status inasoma NOT SELECTED for oral interview. Hii inamaanisha nini?
Haya mambo ya status ni pasua kichwa sana
 
Mkuu ni either upende au usipende ila ukweli ni huo hakuna God's Grace hapo, ni vile tu hujui wengine walifanya vipi kwenye kujibu na huwezi kuona matokeo yao

Ukweli ni kwamba watu wengi wanafanya vibaya interview za Oral na wenye unafuu wengi hupata kazi kupitia hiyo opportunity

Utumishi wakisema wanataka watu 50, watachukua watu wao 50 au ata na zaidi haijarishi matokeo yao yatakuwaje, watachukua hadi Wenye mark's 30 ilimradi tu lengo litimie

Kama hujawahi kujua basi ujue, kuwa wengi ambao wanafanikiwa katika haya maisha kwenye kila nyanja ni wale wasiowekeza Akili na nguvu kubwa kwenye mambo ya Imani Imani za Mungu Bali ni wale wanaowekeza kwenye kufanya na kuwa competent

Mimi nimepata kazi kupitia utumishi sio kwamba nilifanya vizuri bali nilikuwa na unafuu kwa sababu interview ilikuwa Ngumu sana kusema ukweli

Wapo ambao nawajua nawewe najua unawajua tangu tuko vyuo waliwekeza nguvu kubwa kwenye kusali sana ili wafanye vizuri kwenye masomo yao na wawe vizuri kwenye Mambo mengine ila ndio hao hao waga Wana wanaongoza kwa kudisco na wanaoshinda Bar na club watoboa

Tatizo tumelelewa na kuamini vitu ambavyo havina msaada sana kwenye maisha yetu ya kila siku, Mambo za kuambiana ohhh ridhiki mafungu saba, ohhh Mungu waga Hawai wala hachelewi, ohhh Mungu anajua kama angenipa Mie basi nisingedumu pale

Brother hizo ni lugha ambazo zinatumika Kwa Maskini Tu ili kujifariji, wekeza Nguvu,Muuda,Akili,Maarifa na connection katika Mambo yako na lazima tu utajitofautisha na walio wengi

Na kwakuwa wengi wetu waga sio wakweli katika kuelezea njia za mafanikio basi huishia kusema ni Mungu tu, ata kama ulipewa mchongo husemi husemi ukweli, kama kwenu waga mnafanya matambiko ni kheri ukafanye hayo kuliko kukaa kulia na Mungu

Mwisho wa siku ndugu yangu haya ni mawazo yangu tu, na wala sio sheria kusema lazima iwe kweli, bali tunajaribu kupeana uzoefu wa hapa na pale kama kuna sehemu utaona unafaa unaishi nao, kama mtu ataona ni pumba basi fresh akakeshe Kanisani na awe swala 5

DUNIA haijawahi kuwa FAIR na haitokuja kuwa FAIR
 
Ajabu nyie mkiona mtu katokea Database mnahisi alifanya vibaya oral kumbe huyo ndo alieongoza na akawekwa pembeni ili kusubiri mchakato wa maandalizi akale Asali yake
Sio kweli, haiwezekani chaguo la kwanza ichukue wa alama ndogo kuliko chaguo la pili.

"Orodha ya majina haya pia inajumuisha baadhi ya wasailiwa waliokuwa kwenye
kanzidata (Database) kwa kada mbalimbali ambao wamepangiwa vituo vya kazi baada ya
nafasi kupatikana."

"Kwa wale ambao majina yao hayapo
katika tangazo hili watambue kuwa hawakupata nafasi/hawakufaulu usaili, hivyo wasisite
kuomba kwa mara nyingine nafasi za kazi zitakapotangazwa."
 
Mkuu kuna sehemu nimesema anachukuliwa mwenye alama ndogo na mwenye alama kubwa anaachwa?

Jitajihidi kuelewa hoja yangu, nasema kuwa sio kila anaetoja database alifanya vibaya, wanaotoka database na kwenda kwenye Taasisi wengi wao wanakuwa walifaulu vizuri sana ila kutokana na maandalizi ya Taasisi kuwa yanachukua muda mrefu hupelekea kuwekwa pending ila kazi washapata

Nyie mkiona mtu anatokea Database mnadhani wote hawakufanya vizuri ila kumbe wengi wao ni waliofanya vizuri ila kuliko placement yake itoke mwezi wa 1 alafu kazini aende kuanza mwezi 4 wanaona wamuweke Kwanza benchi kusubiri mchakato ukamilike

Nimetolea mfano wafanyakazi wapya Halmashauri wanakaa hadi zaidi ya Mwaka/miaka ata Hela zao za kujikimu hawapewi, ila kwa Taasisi waga ni tofauti, kuna budget ya hela za kujikimu,na wengine Makazi na usafiri bila kusahau mishahara yao

Acheni kuishi Kwa kukariri kuwa wanaotoka kwenye placement wa Kwanza ndio waliofanya vizuri kwenye Oral kuliko watakaokaa database, wanaotoka database na kwenda kwenye Taasisi kubwa wanakuwa walifanya vizuri ila wakasubirishwa Tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…