Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Endelea kuwa na subira. Kama placement zilianza April mwishoni(hapo tuhesabu ni early May) muda wa data base utadumu hadi May/June mwanzoni mwaka huu. Kwa hiyo database yako bado ipo active sana.

Muda ukifika utapata nafasi, nina imani oral uliifanya vizuri.

Kundi langu tuliloenda Oral kwa pamoja hadi sasa tushapata nafasi wote ingawa kwenye Oral tulikuwa tunapambania nafasi 1, ila wengine walikuja kuanza kuchomolewa kutoka data base.
 
Wanahitajika 10, oral tumeitwa 160 sema neno
 
Wanahitajika 10, oral tumeitwa 160 sema neno
Wote ambao walifaulu oral watapata nafasi kwa muda wao.

PSRS wanapoita watu wengi oral huku nafasi zikiwa chache sio kwamba wanataka kuwapotezea watu muda, hapana.

Hapo inakuwa ni Advantage kwa pande zote mbili(PSRS na Jobless). PSRS wataokoa muda wa kusaili mara kwa mara kwa nafasi zile zile kwa kuweka hao akiba ili waje kuwapangia nafasi baadae. Jobless wanakuwa wanaokolewa pia kwenye ishu ya muda na gharama za kwenda kufanya usaili tena.

Kwahiyo pindi ukiitwa kwenye usaili, kuwa na malengo 2 hata kama nafasi ni 1.

Lengo la kwanza, kafanye usaili ili upatw hiyo nafasi kwa muda huo.

Lengo la pili, kafanye usaili ili ubaki database endapo lengo la kwanza likikwama. Kukaa database ni ushindi kulinganisha na yule aliyeogopa kwenda kufanya kisa nafasi ni 1 na akaamua kutoenda ili asipoteze muda na pesa.

Mimi nilijiwekea hayo malengo 2 hasa lengo la pili baada ya kukandwa saili za mwanzo(saili 3). Bahati nzuri nikaangukia kwenye lengo la kwanza, pia hata kama ningekwama kwenye lengo la kwanza ningekuwa nishatimiza lengo la pili hadi sasa maana tayari kundi letu lote tushapangiwa kazi
 
Ubarikiwe...
 
Mkuu ubarikiwe Sana Sana sana binafsi napata nguvu Sana ninapoona comment zako. kwenye huu Uzi mkuu uwepo wako ni wamuhimu Sana, ubarikiwe Sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…