Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

usiwe na hofu mkuu huo mkeka wa wizara ya kilimo bdo haujatoka kabisa. Some individual are too pessimistic and negative mentality. Jiandae na usahili pasipo kusahau Mds za mchumi taasisi ya bunge nazo hazijatoka.
Benge nafasi zipi hizi ambazo bado? Kama ni MWANDISHI RASMI WA TAARIFA ZA BUNGE, KATIBU, UGAVI, DAKTARI, MADEREVA n.k tulishafanya written & oral wale waliobahatika walishaitwa kazini wiki tatu baada ya usaili . ..waliwai sana nadhan walikuwa na uhitaji mkubwa
 
Hata kama nina shida ya kazi ila nikipangiwa wilaya ya Bahi naacha kazi hapo hapo.
 
Hata kama nina shida ya kazi ila nikipangiwa wilaya ya Bahi naacha kazi hapo hapo.
Jobless wewe ujui mbinu za kivita...ngoja nikupe mbinu sasa ukipangiwa popote nenda ila ukifika kule make mishahara yako ya miezi kadhaa zen tumia hiyo chapaa kutafuta uhamisho. Kuipata ajira sio issue simpo kama unavyodhan . Pia hata ukiwa umepata ajira bado unaruhusiwa kuomba kazi mpya zinazotangazwa na PSRS cha msingi barua ipitie kwa mwajiri wako....na ndio maana tunapoenda kwa saili tunakutana na watu wana ndiga wengi wale ni watumishi wa umma sema wanataka kuchange channel toka channel ya kawaida (tamisemi) kwenda HD (MASHIRIKA YA UMMA) ili wakarambe asali huko na uzir wake ukishakuwa mtumishi wa umma unaruhusiwa kuomba hata kama una umri mkubwa ila usizidi 45. Ndio maana zile ajira za TPA (Bandari) miaka mwisho 21 ila watumishi wa umma hata kama una zaidi ya 21 unaruhusiwa ila isizidi 45. So usiache kwenda Bahi
 
😂😂😂Ndo qkipangiwa huko lazima aanze kulia
Ni kweli Kuna sehem ni ngumu sana,ila inabidi ufocus tu..penye Nia Pana njia unajua..binafsi siwezi kuachia kazi niliyoisubiri kwa kufunga na kusali kwa muda mrefu kizembe tu hapana..ukishaingia kwenye mrija wa asali mbona unatoboa tu mbele kwa mbele kama injili🤣
 
Kupata check namba ndiyo kipengele,ukishapata mambo mengine yanawezekana kabisa.wakurugenzi unaowaona Leo kwenye majiji usifkiri walianzia hapo
Nimeajiriwa kitambo sana ila nimesema tu, hata kama ningekuwa na shida ya ajira huko nisingeenda, wangapi wamekataa kazi kwa kuona mazingira sio wezeshi?

Njaa zenu ndio hufanya mnaparamia kila kazi, mkishapata mnaanza kulia na kushinda kwa waganga.

Pambania kesho yako katika ndoto kubwa, hizi ajira za zinazohusishwa na kila wilaya unaweza kuziepuka kabisa.

Nchi hii kuna maeneo unaenda kufanya kazi ambapo kiuhalisia SERIKALI au KAMPUNI inafaa ikulipe na fedha zingine za mazingira magumu kazini. Hizo wilaya mm nikiwa Rais nchi hii nawapa na posho ya mazingira magumu.
 
Kumbe upo kwenye ajira tayari 🤣🤣🤣hongera
 
Sio rahisi kihivyo, ukiingia ndio utanielewa, kuhama sehemu moja kwenda nyingine hasa kwa watu walioko Dunia ya Giza kama hizo wilaya na kule Uvinza, Kibondo + Buhingwe ni ngumu kuhamishwa.

Hata kama una njaa, weka malengo yako ya kugombania kazi nzuri. Ukijipanga na ukisoma unaweza kufaulu mitihani ya utumishi.

Tangu kusoma kwangu, sijawahi kuomba kazi kwenye Halmashauri yoyote ile, sikutaka na nilipambana na mashirika ambayo mostly utakaa sehemu kidogo yenye unafuu wa mshahara na mazingira yako.

Mfano. MWALIMU WA BUHIGWE AU KONGWA anafanana na Mwalimu wa Dar au mikoa iliyoendelea kiasi? Kwann hawa wasipewe posho ya mazingira magumu? Vumbi, ukame, maji shida, umeme mtihani, usafiri mashaka nk, kwnn hawa wanaoishi zama za kale za mawe wasionwe na serikali kwa kuwapa posho ya mazingira magumu kutokana na utayari wao wa kulitumikia taifa wakiwa huko kusikonoga CHAI?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…