Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

PSRS huwa wanasema usiache kufuatilia placement na mwaka 2021 walileta kanuni ya kukaa database kwa mwaka mzima.

Yeye kwa kutojua hilo ndio ikawa sababu ya kuacha kufuatilia.

Unasema placement yao ya kwanza ilitoka septemba 2021, muda wake wa kukaa database ulikuwa unaisha septemba 2022 na bahati nzuri akapata nafasi mapema(April 2022)
 
Asante kwa ushauri
Kanuni hii hapa(24).

Uzito wa kanuni hii ni "kutoripoti bila sababu"

Sasa mimi namshauri aende PSRS akiwa na nyaraka zake zote na awe na hiyo PDF ya placement, akawaeleze hii shida yake, ajitahidi kuwaeleza namna ambavyo hakuweza kuipata barua kwa wakati kupitia anwani aliyoiandika.

Endapo watamuelewa, watamjuza kama nafasi yake ishajazwa au la. Kama imejazwa, automatically hii kanuni ya 24 itamhusu.

Kama ataangukia kwenye hii kanuni, akawaombe wampe nafasi ya kuendelea kuomba kazi zingine zitakazoendelea kutangazwa.

Pia ajaribu kuwaomba kuhusu kukaa database ingawa muda wake ulishaisha.

Kila la kheri kwake.
 
Habarini? Hivi utajuaje kwamba upo kwwenye Kanzidata baada ya oral?
Masahihisho:
Kanzidata unaingia baada ya placement kutoka uliyoifanyia oral ila unatakiwa uwe umefaulu hiyo oral na ukakosa nafasi.

Jibu:
Hauwezi kujua kama upo kanzidata, wanaojua ni PSRS tu, wewe utajua kama ulikuwa kanzidata endapo ukipata nafasi na ukaona jina lako kwenye placements.
 
Hapo ndo unatakiwa utumie multiple choice skills

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Je kwenye pdf ya placements za april jina lake lipo?? Au psrs walituma barua kwenye posta yake, bila kuweka jina lake kwnye pdf ya placements kwenye website yao??
 
Nao utumishi si wawe wanawapigia watu simu hao wanaopata kupitia data base
Ngoja jamaa aje aseme hapa kama hakuona jina kwenye pdf af akakuta barua kwenye posta miezi kadhaa mbele, tuone kama psrs kweli walikosea....au ni vile tu jamaa alipitiwa na hakufuatilia pdf za placement nafasi ikampita hivi hivi.
 
Ngoja jamaa aje aseme hapa kama hakuona jina kwenye pdf af akakuta barua kwenye posta miezi kadhaa mbele, tuone kama psrs kweli walikosea....au ni vile tu jamaa alipitiwa na hakufuatilia pdf za placement nafasi ikampita hivi hivi.
@little finger njoo utoe clarification kuhusu hili swala.
 
Ngoja jamaa aje aseme hapa kama hakuona jina kwenye pdf af akakuta barua kwenye posta miezi kadhaa mbele, tuone kama psrs kweli walikosea....au ni vile tu jamaa alipitiwa na hakufuatilia pdf za placement nafasi ikampita hivi hivi.
Mkuu angeona jina kwenye PDF si angeenda kuchukua barua, hajui kama PDF ilitoka au lah

Kilichotokea ni kwamba alikuja kukata tamaa ya kuangalia pdf za placement, kumbuka interview kafanya june 2021 na anasema hajawahi kupigiwa simu
 
Mkuu angeona jina kwenye PDF si angeenda kuchukua barua, hajui kama PDF ilitoka au lah

Kilichotokea ni kwamba alikuja kukata tamaa ya kuangalia pdf za placement, kumbuka interview kafanya june 2021 na anasema hajawahi kupigiwa simu
placements za psrs zote ziko kwnye ARCHIVE yao kwenye website, chakufanya mwambie achambue pdf moja baada ya nyingine(jina kwa jina) from sept 2021 mpaka April 2022 aone kama atakuta jina lake, akikuta jina aisee ataambiwa yeye mzembe, asipokuta that means psrs ndio walikosea...af alichokaje jamaa? yani placement inatoka sept 2021 na anajua kabsa database ilikua miezi 6, anashindwa ku view pdf's tu mpaka april? Alizingua hapo kwenye kuchoka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…