Ni kweli sana Mkuu, japo kwa kuongezea nadhani raha ya kanzi data itakuwepo pia kama nafasi uliyoomba inaweza kupatikana kirahisi kwenye taasisi nyingine.
Kuna baadhi ya nafasi kulingana na alichosomea mtu, hata akikaa kwenye kanzi data ni mpaka taasisi hiyo hiyo au inayofanana na hiyo ipate tena nafasi. Hapo sasa ndio changamoto.
Nadhani miongoni mwa maboresho wangefanya mtu akishaingia kwenye kanzi data, sifa zinazoangaliwa iwe ni vyeti vyake vinamruhusu kupangiwa kazi gani na sio lazima iwe ni nafasi kama ile aliyoomba ikamfikosha Oral.
Ndugu mchambuzi na mwanasheria wetu wa thread na Jf kiujumla, uliyejikita kwenye masuala ya psrs
Mwifwa ukipata nafasi naomba kwa niaba ya wengine utupe somo kuhusu kanzi data kwa vigezo vya psrs.