Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kama NSSF wakiruhusiwa na kuachwa watimize huo ubaguzi waliouanza, kila mwajiri atakuwa na haki ya kuajiri "wa ndani". Kila halmashauri inaweza kutumia huo mwanya, na kila mwajiri anaweza kutumia huo mwanya. NSSF lazima waambiwe kuwa hilo ni shirika la umma na linaendeshwa na kodi za watanzania wote, na linachangiwa michango na watanzania wote!! Hawana haki ya kuwatenga baadhi ya watanzania!! Napoendekeza wajitokeze mawakili kufungua kesi mahakamani kupinga UBAGUZI huu!!
Pia,..Ungefunguliwa uzi maalumu kwaajili ya hii mada, itasaidia.
 
Nimefungua uzi kule kwenye jukwaa la siasa (maana ndiko waliko wanasiasa wanataka kuwatenga wengine kwenye ajira). Uzi wenyewe unasema:

HUU UBAGUZI WA NSSF HAUKUBALIKI: Kutangaza nafasi za ajira kwa watu "wa ndani" humo NSSF. Rais SAMIA ingilia kati, unachonganishwa na wananchi!!​

Naomba wadau wote waliopo kwenye uzi huu tutumie uzi huo kwa nguvu zote kupinga huu ubaguzi. Kila mmoja atie neno hapo, ili ndani ya siku chache kuwe na mamilioni ya views na malaki ya posts zinazopinga ubaguzi kwenye ajira. Nina uhakika watalazimika kubadili msimamo!!
 
Ni kweli ndio maana mashirika na taasisi za Serikali zimekuwa ni mzigo kwa Serikali hii ni kutokana na Manpower iliyopo kuwa imeingia hapo za kwa vigezo vya uwezo bali ni kujuana pia hakuna anayeweza kumchukulia mwingine hatua kwa sababu ya kujuana huko, mwisho wa siku ni haya mashirika kuperform chini ya kiwango ili hali kulipana mishahara minono na marupurupu ndio kipa umbele.
Serikali inatakiwa kulitazama jambo hili kwa upana sana , hili la NSSF limeshtua sana, inatia shaka hata huo usaili wa TRA wa wiki ijayo unaweza kuwa ni kutimiza taratibu tu watakaopata ajira ni haohao waliopo TRA wanaojitolea.

Fikiria tu kwamba , mwezi wa kwanza vijana takribani 700 walifanya oral upande wa Tax management officer kati ya hao 184 ndio walioitwa kazini, kwa hiyo inaonesha vijana wengi kati ya idadi hiyo walikuwa data base ya utumishi, sasa swali ni kwanini isengetumika busara kwa hizi nafasi za sasa 206 za tax management officer kuwapa vijana waliokuwa data base ya utumishi ,kisha wakati ujao ndio hawa TRA wangeendelea wenyewe na mchakato wao wa kuajiri., ukizingatia kuwa hawa vijana waliingia data base mwezi wa kwanza na TRA wametangaza kazi mwezi wa tano, takribani ni miezi 3 tu ambayo kwa life span ya data base ilikuwa bado sana.

Ndio maana nikiitazama hii hali naona kuna jambo nyuma ya pazia.

Nampongeza sana Mh. Rais Dr. Samia Hassan kwa kufungua fursa za ajira nyingi sana kwa vijana kipindi hiki cha uongozi wake, ila changamoto hii aitazame kwa jicho jingine kabisa kama kuna watu wanamshauri ndivyo sivyo ni vema akapingana na mawazo yao maana itamharibia kazi yake nzuri aliyoianzisha ya kufungua fursa za ajira kwa vijana.

Jambo muhimu ni kuwa ajira zitangazwe watu waombe wakashindane , atakaeshinda apate nafasi lakini siyo kama ilivyojitokeza hili la NSSF limeta taswira mbaya sana kwa taifa.
Suala la viongozi wakubwa na wakurugenzi kufai waajiri wenyewe ni kwamba kwanza wanandg zao wanashindwa kuwapachika katika kazi, pua kulega kwa Psrs mara kuvuja paper mara kuchelewa mchakato nayo sababu nyingine kubwa, ila hapa tulipo fikia saizi ndio zama za fungulia mbwa yaani hapa saiz kiukweli pagumu kwa watu wa chini kupenya huko.Mwenye uwezo wa kuweka sawa hili ni kiongozi mkuu, kama magu aliweka sawa gii issue bora na yeye alikaushia vibali kuliko vibali vitoke kazi ziishie kwa watu wa kupenyezewa
 
Nimefungua uzi kule kwenye jukwaa la siasa (maana ndiko waliko wanasiasa wanataka kuwatenga wengine kwenye ajira). Uzi wenyewe unasema:

HUU UBAGUZI WA NSSF HAUKUBALIKI: Kutangaza nafasi za ajira kwa watu "wa ndani" humo NSSF. Rais SAMIA ingilia kati, unachonganishwa na wananchi!!​

Naomba wadau wote waliopo kwenye uzi huu tutumie uzi huo kwa nguvu zote kupinga huu ubaguzi. Kila mmoja atie neno hapo, ili ndani ya siku chache kuwe na mamilioni ya views na malaki ya posts zinazopinga ubaguzi kwenye ajira. Nina uhakika watalazimika kubadili msimamo!!
Safi sanq mkuu
 
sisi tunawalalamikia Nssf lakini ukweli ni kwamba Nssf kajilipua kuwa liwalo na liwe ,ila alichofanya Nssf ndicho taasis nyingi inatekeleza behind the scene

umasikini ni laana wazee nchi imegeuka kuwa ya kundi la watu wa tabaka na ukanda fulani
 
sisi tunawalalamikia Nssf lakini ukweli ni kwamba Nssf kajilipua kuwa liwalo na liwe ,ila alichofanya Nssf ndicho taasis nyingi inatekeleza behind the scene

umasikini ni laana wazee nchi imegeuka kuwa ya kundi la watu wa tabaka na ukanda fulani
Inaumiza sana mwanangu Mfwende ,we mwenyewe nadhani unajua Madudu uliyoyaona kwenye zile kazi za majeshi .
Tegemeo la wengi ilikuwa ni huku kwenye huku PSRS ,sasa nako wahuni wanavuruga na kutaka kutengeneza mifumo yao ya kihuni .
Hii trend mbovu kichizi mazeee ,
Zinatengenezwa tabaka hapa
Mbaya sana hii
 
sisi tunawalalamikia Nssf lakini ukweli ni kwamba Nssf kajilipua kuwa liwalo na liwe ,ila alichofanya Nssf ndicho taasis nyingi inatekeleza behind the scene

umasikini ni laana wazee nchi imegeuka kuwa ya kundi la watu wa tabaka na ukanda fulani
Na kajilipua kwa sababu anajua kuna vigogo viko nyuma yake!! si kwa jeuri hii. Lakini Mungu wetu ni mkubwa na ni mwenye haki, huu ubaguzi hautafanikiwa!
 
Kuna watu naona wanalalamikia watu wengine kujitolea. Watu kujitolea sio kwamba wanapenda bali hali ya maisha inapelekea mtu kuamua kujitolea, Just imagine mtu kaomba kazi privates zaidi ya 80 anakosa, anaamua kuomba kazi Serikalini anakosa, wakati huo huo anahitaji kujitimizia mahitaji yake madogo madogo. Mtu huyu inafikia hatua anaamua kwenda kujitolea tu kwa Taasisi au shirika lolote litakalomkubali ili aweze kuondokana na aibu ya kukaa mtaani bule au aibu ya kuomba sabuni au mafuta kwa ndugu.
 
Kuna watu naona wanalalamikia watu wengine kujitolea. Watu kujitolea sio kwamba wanapenda bali hali ya maisha inapelekea mtu kuamua kujitolea, Just imagine mtu kaomba kazi privates zaidi ya 80 anakosa, anaamua kuomba kazi Serikalini anakosa, wakati huo huo anahitaji kujitimizia mahitaji yake madogo madogo. Mtu huyu inafikia hatua anaamua kwenda kujitolea tu kwa Taasisi au shirika lolote litakalomkubali ili aweze kuondokana na aibu ya kukaa mtaani bule au aibu ya kuomba sabuni au mafuta kwa ndugu.
Watu hawa lalamiki juu ya kujitolea wanacho lalamika ni namna gani hizo nafasi za kujitolea zinavyotolewa, umesha wahi kwenda kuomba nafasi za kujitolea kwenye hayo mashirika ukakubaliwa? ukienda kuna majibu mawili makuu utayapata
1. Nafasi ya kujitolea hakuna
2. Nenda kaandike barua utuletee (hapo ni pale umemkuta aliyekupokea siku hiyo ni muungwana), unaileta barua unakaa kusikilizia majibu ,siku, majuma, miezi , miaka inakatika , barua imetupwa kwenye dustbin habari inakuwa imeishia hapo.
 
Watu hawa lalamiki juu ya kujitolea wanacho lalamika ni namna gani hizo nafasi za kujitolea zinavyotolewa, umesha wahi kwenda kuomba nafasi za kujitolea kwenye hayo mashirika ukakubaliwa? ukienda kuna majibu mawili makuu utayapata
1. Nafasi ya kujitolea hakuna
2. Nenda kaandike barua utuletee (hapo ni pale umemkuta aliyekupokea siku hiyo ni muungwana), unaileta barua unakaa kusikilizia majibu ,siku, majuma, miezi , miaka inakatika , barua imetupwa kwenye dustbin habari inakuwa imeishia hapo.
Mimi kupata INTERN nilipitiaTAESA . Nilifanya Interview nikapangiwa INTERN pale TRA, nikakomaa kwa miaka miwili. Mkataba ulipoisha tukaondolewa wakapatiwa vijana wengine nafasi ya INTERN. Ilikuwa mwaka 2020 hadi 2022. Ni utaratibu mzuri sana ambao unawapa vijana kuongeza CV yao.
 
Kuna watu naona wanalalamikia watu wengine kujitolea. Watu kujitolea sio kwamba wanapenda bali hali ya maisha inapelekea mtu kuamua kujitolea, Just imagine mtu kaomba kazi privates zaidi ya 80 anakosa, anaamua kuomba kazi Serikalini anakosa, wakati huo huo anahitaji kujitimizia mahitaji yake madogo madogo. Mtu huyu inafikia hatua anaamua kwenda kujitolea tu kwa Taasisi au shirika lolote litakalomkubali ili aweze kuondokana na aibu ya kukaa mtaani bule au aibu ya kuomba sabuni au mafuta kwa ndugu.
Usilolijua ni kwamba hizo nafasi za kujitolea kwenye baadhi ya taasiosi, ni neno tu kujitolea lakini kuna posho ya kueleweka tu!! Na huwezi kuipata nafasi hiyo ya "kujitolea" bila connection. Na kujitolea huko ni hatua ya mwanzo tu ili kuhalalisha ajira hapo baadaye!! Ndiyo maana kuna makelele ya vigogo kutaka "wajitoleaji" wapewe kipaumbele!! Je ni lini ulisikia tangazo la kazi za mikataba au za kujitolea huko NSSF?
 
Watu hawa lalamiki juu ya kujitolea wanacho lalamika ni namna gani hizo nafasi za kujitolea zinavyotolewa, umesha wahi kwenda kuomba nafasi za kujitolea kwenye hayo mashirika ukakubaliwa? ukienda kuna majibu mawili makuu utayapata
1. Nafasi ya kujitolea hakuna
2. Nenda kaandike barua utuletee (hapo ni pale umemkuta aliyekupokea siku hiyo ni muungwana), unaileta barua unakaa kusikilizia majibu ,siku, majuma, miezi , miaka inakatika , barua imetupwa kwenye dustbin habari inakuwa imeishia hapo.
Umesema kweli kabisa!!
 
Mimi kupata INTERN nilipitiaTAESA . Nilifanya Interview nikapangiwa INTERN pale TRA, nikakomaa kwa miaka miwili. Mkataba ulipoisha tukaondolewa wakapatiwa vijana wengine nafasi ya INTERN. Ilikuwa mwaka 2020 hadi 2022. Ni utaratibu mzuri sana ambao unawapa vijana kuongeza CV yao.
Watu walioingia huko kwa jinsi yake ni wachache sana dhidi ya wengi walioingizwa huko kwa connection. Na nyie wachache hutumiwa kuwafumba watu macho!! Lakini hata hivyo, hoja ya msingi ni kutaka kuwatenga waombaji wengine walio nje ya NSSF kwa sasa!! Hao ma-intern wasiepushiwe ushindani kwa kuwatenga na kuwazuia waqombaji wengine!!
 
Suala la viongozi wakubwa na wakurugenzi kufai waajiri wenyewe ni kwamba kwanza wanandg zao wanashindwa kuwapachika katika kazi, pua kulega kwa Psrs mara kuvuja paper mara kuchelewa mchakato nayo sababu nyingine kubwa, ila hapa tulipo fikia saizi ndio zama za fungulia mbwa yaani hapa saiz kiukweli pagumu kwa watu wa chini kupenya huko.Mwenye uwezo wa kuweka sawa hili ni kiongozi mkuu, kama magu aliweka sawa gii issue bora na yeye alikaushia vibali kuliko vibali vitoke kazi ziishie kwa watu wa kupenyezewa
Dah ila mama ktk hili kashauriwa vibaya so sad kwa kweli
 
Back
Top Bottom